Mkuu nimecheka hadi machozi.Dah ilikua form 2 nilisema kwa cube members wangu kuna kiatu cha jamaa mmoja Wa form six kinanuka ,wakaenda kunisemea ,kumbe jamaa alikua mtabe na anaheshimika kindakindaki ,muda Wa jioni unaingia kaanza kunitafuta dormitory ,nlienda kulala juu ya mti mpaka asubuhi nikanyoosha kwa headmaster kwa usalama wangu ,asubuhi naona jamaa anakuja kwenye office ya headmaster huku anapiga mluzi halafu katabasamu
Headmaster mwenyewe anazima fegi kwa jamaa akaniombea msamaha ,kweli jamaa akawa kaka wangu Wa shule hakuna aliyenionea Tena ,sema ndio hivyo kumfulia, anakupa sh 50 umletee mkate,soda na change ibaki ,ukiletewa nido sijui na blueband unanyoosha moja kwa moja kwake