Crazy things you did in secondary school

Siku ya Graduation pale Mazengo Sec mwaka 1985, kiongozi wa sherehe alikuwa mshikaji wangu Kasanga. Basi nilimfuata na Kisadolini changu na akanijazia Pilau.

Pilau la Mazengo miaka hiyo lilikuwa kali sana. Kwa wenyeji wa Dodoma watakuwa wanamkumbuka Mzee Mapilau na yale Mapipa yake (SHABA). Nilikula siku hiyo hadi nikawa siwezi kuhema. Jamaa walishangaa kuwa mbona hawaoni tumbo kutokea. Basi kutoka siku hiyo nikajulikana kuwa nina tumbo kama la Mamba, linafutuka pembeni.

Upuuzi wa Mazengo ilikuwa ni chooni. Utakuta mtu anapita koridoni na karatasi yake anaipekecha ili ilainike.... "pyeke pyeke pyeke..." na akitoka huko basi anapita kwenye ule mti nyuma ya bweni la Mwongozo na kujipigapiga na mtawi.

Hii ilikuwa inasaidia kuuwa ile perfume uliyoikwaa kule NYUMBA KUBWA. Ule mti ulikuwa na harufu moja kali sana na ukitoka hapo unanukia freshi. Mabinti wa Msalato, mlivumiliaje ile harufu??
 
Mhhh, miziki ya BLUES.

Hii nakumbuka miaka ya 90 ulizuka ugomvi mkubwa sana (tuko chuoni wakati huo). Jamaa alikuta mziki unalia na akasema "daa blues kali sana". Jamaa akamjibu kuwa hii siyo BLUES.

Blues ni miziki kama ya akina Erick Clapton, B B King, John Lee Hooker nk. Ni kosa kubwa sana lilikuwepo Bongo kuiita miziki yote slow kuwa ni Blues. Nafikiri jina zuri ilitakiwa iwe Soul au R & B nk. Ni sawa na Miziki ya Lingala. Jamaa alienda kwa Mcongo na kuomba BOLINGO. Mcongo akashangaa kwa vipi jamaa anamuomba MAPENZI???

Kwa hiyo mjihadhari next time msichanganye mambo kwa watu wasiyo Wabongo. Hii ni lugha yetu tu WATANZANIA.

Watu leteni story zaidi tufurahi. Mbona hatuoni za kwenye Train? Nikiwa Arusha Tech, nilikuja kukutana na kijana aitwaye KILLER. Huyu alikuwa akisoma ILBORU. Alikuwa akija kutembelea jamaa aliosoma nao Tanga School. Walimpa jina Killer kwa sababu alimtupa mtu dirishani wakati train linakwenda. Sijui kama ilikuwa kweli au lahh.
 
Sikonge, umenikumbusha mzee Shed!!

Kule paliiitwa beach bwana, kuna pafyumu ya kufa mtu, kuna jamaa alikuwa anavua nguo zote ili kuingia huko kutabaruki.

Duuu, Mzee Shedi siyo? Namkumbuka yule Mzee. Nakumbuka kuikamata Periodic Table ya Chemistry, watu walitumia majina ya pale na wakafanya ikawa rahisi kuikariri....
He He,
Lile BEDA Bovu CHONYA nipe Orange Fanta Nende
Na MGANYIZI alivuta Sigara Paketi Sita Cloroquine Arusha.
Nimesahau hizi Element ila Mganyizi nafikiri i Magnesium, Orange ni Oxygen, He ne he ni Helium na Hydrogen, Alivuta ni Alminium????
Ilisaidia sana, MSASA tukawa tunamtesa kwenye mtihani wa Chemistry. Ile baadaye tukawa na yule mama wa Kigeruman. Yeye na mumewe walikuwa walimu. Siku moja akafungua gas ya FeS??? Mhhh, harufu mbaya? Kakajua tunakacheka, kakatugeuzia kibao kuwa "hiyo harufu si ngeni kwetu kwani hata maharage yana Sulfer...." Wanaume akawa katushika pabaya.
 
Kwa wale waliopita Lutengano miaka ile ya themanini na ushee, najua watakumbuka kituko cha mwalimu mmoja ambaye siku hiyo alikuwa zamu na alikuwa akiwaita wale waliokosekana kwenye roll-call ya jana yake ili awapatie adhabu. Hata alivyomaliza kuwaita, wanafunzi kwa pamoja walipiga kelele kwa kusema.
"Mwalimu acha ujiko"

Kwa rafudhi ya nyanda za juu na kifua mbele mwalimu huyo alijibu.
"Na huyo Ujiko apite mbele...!"
 
Rum six mido pale Soweto (Ujamaa) palikuwa si pakwenda kwa wale nyoya (wenye baa nyekundu moja begani - fomu wani!!) wadau nadhani mtakuwa mnakumbuka kwamba Ujamaa ni bweni lililokuwa likiongoza kwa kutrotisha (kuwasumbua) fom nyonya miaka yote! Ikiwa pamoja na kumwagiwa bichi (maji machafu), kupigwa chaga usiku au kuingizwa lokani).

Lakini kilichonichekesha zaidi ni kumkumbuka UNYAMA UNYAMA (ticha wa mota vehicle) aliyekuja Soweto kuamsha watu alfajiri siku moja akiwa mwalimu wa zamu, halafu akasikia sauti ikitokea floor ya juu kabisa ikimwambia "Unakuja kutumbusua asubuhi yote hii kwa sababu nyumbani kwako hapakaliki, wakati wenzako wanachagua wake wazuri wa kuoa we ukachagua kipori, matokeo yake unashindwa hata kulala nyumbani kwako" UNYAMA UNYAMA akajibu "Wewe unaeongea hivyo kama kweli ni mwanaume na unajua wanawake wazuri kuliko mimi shuka hapa chini tuonane"

Kituko kilikuwa kitamu yaani mpaka ilibidi jamaa waigize siku graduu!!

Ebwana nimekumbuka mambo mengi sana,

Big up sana kwa mameni KABOTA, MAGERE, MSASA, KATUNZI, mzushi TETE, KAMEME, mchungaji ISHENGOMA.
 
Sikonge na Ngonalugali - wazee wa Complex, mmnenikumbusha mbali sana. BTW wale watoto wenu mlowaacha pale kijijini Kikuyu sasa ni wakubwa, mnapeleka matumizi wakulu??

Are you SCORPION OR blackscorpion?

See you if you get to know what I mean!

Mimi china batoto nje ya ndoa, nimuaminifu hata kabla ya kuoa. lakini teh teh, maana nimekumbuka vikuyu waliokuwa wakija kuomba na watoto wao wakidai wana baba waliosoma maeneo hayo.

Mliozaa kule nendeni mkachukue familia zenu!

Mimi bana dhambi yangu ilikuwa kuwahi parade ya Sudan!!!!!!!!!
 
Siku ya Graduation pale Mazengo Sec mwaka 1985, kiongozi wa sherehe alikuwa mshikaji wangu Kasanga. Basi nilimfuata na Kisadolini changu na akanijazia Pilau. Pilau la Mazengo miaka hiyo lilikuwa kali sana. Kwa wenyeji wa Dodoma watakuwa wanamkumbuka Mzee Mapilau na yale Mapipa yake (SHABA). Nilikula siku hiyo hadi nikawa siwezi kuhema. Jamaa walishangaa kuwa mbona hawaoni tumbo kutokea. Basi kutoka siku hiyo nikajulikana kuwa nina tumbo kama la Mamba, linafutuka pembeni.......
Upuuzi wa Mazengo ilikuwa ni chooni. Utakuta mtu anapita koridoni na karatasi yake anaipekecha ili ilainike.... "pyeke pyeke pyeke..." na akitoka huko basi anapita kwenye ule mti nyuma ya bweni la Mwongozo na kujipigapiga na mtawi. Hii ilikuwa inasaidia kuuwa ile perfume uliyoikwaa kule NYUMBA KUBWA. Ule mti ulikuwa na harufu moja kali sana na ukitoka hapo unanukia freshi. Mabinti wa Msalato, mlivumiliaje ile harufu??
hahahahahaha umenikumbusha mbaaaaali miaka yangu yote shuleni sikuwahi kutumia maji lakini cha ajabu nikirudi likizo situmii makaratasi.........kuna wakati magodoro unakuta limenyofolewa wamekwenda kujiswafia.
 
Siku ya Graduation pale Mazengo Sec mwaka 1985, kiongozi wa sherehe alikuwa mshikaji wangu Kasanga. Basi nilimfuata na Kisadolini changu na akanijazia Pilau. Pilau la Mazengo miaka hiyo lilikuwa kali sana. Kwa wenyeji wa Dodoma watakuwa wanamkumbuka Mzee Mapilau na yale Mapipa yake (SHABA). Nilikula siku hiyo hadi nikawa siwezi kuhema. Jamaa walishangaa kuwa mbona hawaoni tumbo kutokea. Basi kutoka siku hiyo nikajulikana kuwa nina tumbo kama la Mamba, linafutuka pembeni.......

Ahsante kwa kunivunja mbavu..LOL! :)
 
Upuuzi wa Mazengo ilikuwa ni chooni. Utakuta mtu anapita koridoni na karatasi yake anaipekecha ili ilainike.... "pyeke pyeke pyeke..." na akitoka huko basi anapita kwenye ule mti nyuma ya bweni la Mwongozo na kujipigapiga na mtawi. Hii ilikuwa inasaidia kuuwa ile perfume uliyoikwaa kule NYUMBA KUBWA. Ule mti ulikuwa na harufu moja kali sana na ukitoka hapo unanukia freshi. Mabinti wa Msalato, mlivumiliaje ile harufu??

hahahahahaha umenikumbusha mbaaaaali miaka yangu yote shuleni sikuwahi kutumia maji lakini cha ajabu nikirudi likizo situmii makaratasi.........kuna wakati magodoro unakuta limenyofolewa wamekwenda kujiswafia.


Sikonge wewe ni noma, kumbukumbu yako sio mchezo.
Kuna kipindi magazeti yanaadimika kabisa, inakulazimu kuchana daftari la mtu.

Form I walikuwa wanakera maana walikuwa wanashindwa kulenga shimo. Ndama wengine wakiingia wanapanga magogo hadi mlangoni. Hapo inabidi mtu uingie chaka.
 
Sikonge wewe ni noma, kumbukumbu yako sio mchezo.
Kuna kipindi magazeti yanaadimika kabisa, inakulazimu kuchana daftari la mtu.

Form I walikuwa wanakera maana walikuwa wanashindwa kilenga shimo. Ndama wengine wakiingia wanapanga magogo hadi mlangoni. Hapo inabidi mtu uingie chaka.
Hii topic tangu niianzishe mimi ni vicheko tu. Wakuu naona mmekumbuka mbali sana. Interesting to read em comments
 
Wakuu mmesahau? Form 1 a.k.a njuka, amoeba, mswaki, single cell etc. alikuwa anapewa pesa kama dola moja hivi, anaambiwa alete paketi kadhaa za sigara na change juu! Maskini walikuwa wanaleta.

Wakati mwingine kama Njuka hana pesa anaandikiwa barua kutuma kwa wazazi kuwa amevunja dining hall ikaangukia roll call kwa hiyo wamtumie pesa ya kulipia uharibifu huo.

Au kwamba wazazi walisahau kumnunulia ameoba au hydra hivyo wamtumie pesa haraka kabla hajafukuzwa shule!
 
Nakumbuka nikiwa Form 1, tulikuwa tunafanya mtihani wa kiingereza basi baada ya muda wa mtihani kuisha mwalimu akasema wote wekeni kalamu chini, mimi kuangalia nilikuwa nimejibu maswali kama matano tu kati ya kumi na tano , basi tulivyoambiwa kila mtu alete mbele karatasi tulizofanyia mtihani mimi niliificha ya kwangu sikuikusanya kabisa.

Siku mwalimu anarudisha makaratasi ya mitihani kwa wanafunzi na mimi nikamdai kuwa mbona mimi sijapata mtihani wangu, basi mwalimu alienda ofisini alitafuta bila kupata baade ikabidi anipe tu maksi akaniandikia 78%.
 
Nakumbuka nikiwa Form 1, tulikuwa tunafanya mtihani wa kiingereza basi baada ya muda wa mtihani kuisha mwalimu akasema wote wekeni kalamu chini, mimi kuangalia nilikuwa nimejibu maswali kama matano tu kati ya kumi na tano , basi tulivyoambiwa kila mtu alete mbele karatasi tulizofanyia mtihani mimi niliificha ya kwangu sikuikusanya kabisa. Siku mwalimu anarudisha makaratasi ya mitihani kwa wanafunzi na mimi nikamdai kuwa mbona mimi sijapata mtihani wangu, basi mwalimu alienda ofisini alitafuta bila kupata baade ikabidi anipe tu maksi akaniandikia 78%.

Mhh, hiyo ni hatari sana. Form 1 tu umeanza cheating......??
 
Wakuu mmesahau? Form 1 a.k.a njuka, amoeba, mswaki, single cell etc. alikuwa anapewa pesa kama dola moja hivi, anaambiwa alete paketi kadhaa za sigara na change juu! Maskini walikuwa wanaleta. Wakati mwingine kama Njuka hana pesa anaandikiwa barua kutuma kwa wazazi kuwa amevunja dining hall ikaangukia roll call kwa hiyo wamtumie pesa ya kulipia uharibifu huo. Au kwamba wazazi walisahau kumnunulia ameoba au hydra hivyo wamtumie pesa haraka kabla hajafukuzwa shule!


Mswaki?
Ninayokumbuka ni njuka na ndama.
 
Back
Top Bottom