Habari njema kwa majiji ya Roma, Madrid, New York, taarifa za leo zimeonyesha maambukizi na vifo kutokana na Covid 19 umepungua.
Na hii imetokana na lockdown katika majiji hayo pia na maeneo mbalimbali ya nchi hizo Italia, Spain na USA, hata kule Wuhan bila lockdown corona isingeisha.
Kuna kauli zinatumika na viongozi wa Tanzania kuwa hawawezi kutumia mbinu za mataifa yaliyoendelea kudhibiti Corona kwa kuwa Watanzania wengi ni masikini.
Na kauli hii inaungwa mkono na viongozi wa serikali, chama tawala na upinzani lakini.
Huko Uturuki Rais wa nchi hiyo alisema wananchi wachape kazi lakini kilichoripotiwa leo na madaktari wakinukuliwa na vyombo vya habari ni kuwa maambukizi katika taifa hilo yanaenda kwa kasi zaidi ilivyokuwa China, Italy, Spain na USA, yaani kiwango cha maambukizi huko Uturuki kinatisha.
Kule Brazil hivyo hivyo, tukija hapa Bongo unaambiwa lockdown haitawezekana, hebu tupeni mbinu mbadala ambayo mnafikiria kuwa inaweza kuzuia maambukizi, maana nahisi wiki mbili zijazo tutakuwa tunaongea lugha moja.
Kula USA mpaka chui ameambukizwa korona, huku kwetu mbwa, paka na ng'ombe wasipo ambukizwa tumuombe Mungu.
Sent using
Jamii Forums mobile app