Kilbark
JF-Expert Member
- Feb 25, 2008
- 572
- 170
Tuwe objective katika ku-critic ni kweli kwamba wamekopy na kupaste lakini unashauri nini? Mimi binafsi nawapongeza CLOUDS kwa sababu ni wachache sana wenye uthubutu na ni mfano bora kwa vijana wenye kiu ya mafanikio. Nikiri hawa jamaa wanajitahidi sana na naamini wataleta ushindani mzuri. Kuhusu EATV ukijaribu kuangalia nao kwa kiasi fulani wameiga mpangilio wa programu zao channel O. Na hakuna anayebisha, hata hivyo kwa sasa EATV wako hatua ya mbali ingawa sidhani kama wanagenerate revenues kutoka nchi nyingine za Afrika Mashariki pamoja na kwamba lengo lao ni kuteka soko la Afrika Mashariki. Hata hivyo safari bado ni ndefu. Tujiangalie wenyewe kwanza ndipo tuangalie wengine. CLOUDS na EATV kazeni buti nyinyi ni watanzania mafanikio yenu yanaiwakilisha Tanzania.