Lizarazu
JF-Expert Member
- Aug 23, 2015
- 6,331
- 7,885
Mkuu huyu jamaa ni miongoni mwa wale wanaosoma wakiamini maisha yao yako kwenye makaratasi(yaani vyeti) na akiharibu hapo basi tena hana njia nyingine ya kumtoa kimaisha, na ndio maana unaona anajasifu GPA kwa sababu amesoma kama ametumwa na nzengo hadi kuipata hili asije akawa omba omba mtaani.... Hajui kwamba kuna watu wamemaliza mwaka juzi na first class lakini hadi leo bado wanafundisha twisheni sababu ya kukosa ajira zinazohusiana na taaluma zao, na hapo hapo kuna watu wamemaliza na Pass tu mwaka huu tayari sasa hivi wapo makazini wanakula mishaara.Hahahaaa mtu mzima kujisifia GPA ni aibu watu wanajisifia pesa na mishemishe kwenye maisha
Tafuta pesa GPA yangu naijua mimi hata nikikwambia hutaamini na wala hatujuani
We kila kukicha tafuta hela, saivi waza kupata hela nyingi sana
Achana na GPA narudia tafuta helaaaa
GPA yangu ipo kwenye vyeti kazi nilishapata ila tatizo sijapata pesa za kunifanya niridhike
Tatizo langu ni pesa tuuu
Nawewe tafuta helaaaa
Huyu mleta maada ana mengi ya kujifunza kuhusu life lilivyo kwa sasa.