Fixed Point
JF-Expert Member
- Sep 30, 2009
- 11,304
- 12,753
- Thread starter
- #81
nakubaliana nawe kabisa kuhusu urafiki na undugu.... hapo nilitoa tu mfano.Uhusiano wa kidungu ni tofauti na urafiki. Huwezi ukaomba udungu kwa maana hiyo wazazi wataendelea kuwa wazazi bila kujali hali ya mtoto wao. Urafiki unaweza kufa wakati wowote. Lakini urafiki unakuja kulingana na kufurahisha/kuvutiwa na mambo fulani fulani anayoyafanya mwezio. Huwezi ukawa rafiki mkubwa wa changudoa, na unajua kabisa ni changudoa, halafu wewe unasema unafurahishwa na hali hiyo. Lazima utakuwa na element ya kutoona tofauti kati ya madhara ya uchangudoa na maisha kwa ujumla.
Rafiki hata wale ambao unafahamu wana tabia njema haimaanishi mnafanana kabisa tabia zenu, kuna vitu ambavyo hamfanani kabisa, lakini hiyo haimaanishi urafiki wenu utakufa sababu kuna baadhi ya vitu hamlingani......
hali kadhalika kama rafiki yako ni mwizi au changudoa. huweji jua urafiki wenu ulianzia wapi. labda wakati mnaanza hakuwa changudoa ila katikati ya safari basi inaibuka hiyo tabia ya uchangudoa.....
concern yangu hapa ni je uue urafiki na huyo mtu sababu sasa kawa changu? hata kama hakupeleki kweny hiyo biashara yao na wala hamuongei kuhusu hiyo biashara yake?
kuna siku (hii ilinisikitisha kidogo) kuna dada kamwambia best friend wake kuwa hawezi kuendelea na urafiki wao sababu tu yeye kaolewa na huyo shosti hajaolewa kwa hiyo akiendelea kuwa naye basi watu watafikiri na yeye ni muhuni tu (nadhani hapa alikuwa anamlenga mumewe).....
nilijiuliza maswali mengi na sikupata jibu. labda utanisaidia mtu kama huyu utamchukuliaje?