Hapa unachanganya umiliki na uana habari, huyo DJ ni mmiliki na sio mwanahabari, na lengo la msingi la Clouds Radio ilikuwa ni kutoa burudani, habari zilikuja baadae sana!. Mmiliki wa Media kubwa kabisa nchini, IPP Media, ni Mzee Mengi na sio mwana habari!. Mmmiliki wa Media ya pili kwa ukubwa Tanzania, Sahara Media, ni Antony Diallo, sio mwanahabari!, Mmmilikiwa media ya tatu kwa ukubwa nchini, AMG, ni Shabir Abji, sio mwanahabari!. Wamiliki wengine karibu wote wa vituo vyaredio na TV sio wanahabari!. Wanahabari wenye redio zao ni Abdalah Majura na Ahmed Kipozi, hizo redio zao wewe unazikia?.
Pasco