Clouds TV na propaganda ya vita kisiasa

Clouds TV na propaganda ya vita kisiasa

Mkuu Ngonani, tujitahidi tuwe na shukrani katika madogo ili tuweze kushukuru kwa makubwa!, Tangu kombe la dunia limeanza, kuna kituo chochote kimewahi kupeleka crew huko kombe linakochezewa?!. Badala ya kuilaumu Clouds, ulipaswa kuipongeza kwa hatua hiyo tuu ya kupeleka team Brazil! kutupatia hicho kidogo walichoweza!. Tuwe na appreciation japo kidogo!, ila pia sishangai, Watanzania wengi ni watu wa kulalamika na kulaumu tuu kutwa kucha!. Think positive, be positive!.
Pasco

Narudia tena wangechunguzwa kama kweli kilichowafanya wapeleke mtu Brazil ilikuwa ni mambo ya mpira. Watangazaji hao wanasikika sana kwa mambo yao ya unga mitaani. Afrika kusini wlikwenda kwa hilo hilo, tunaambiwa.
 
Hebu nisaidie ni kwa nini Clouds wameshindwa kuwa ni chombo cha habari!
Naomba ufahamu kwamba taaluma yako inakujenga ktk mtindo ambao unaweza kukufanya uweze mambo mengine nje ya taaluma. Mwalimu anajijenga kiakili kiasi kwamba anaweza kujenga hoja na kuwa mwanasiasa. Ni vigumu DJ au baharia kuwa reasonable kiasi cha kuwa mtu wa kujenga hoja.

Clouds wanatimiza matakwa ya mwajili na ndo maana mbali na taaluma, huwezi kuwasikia wakisema baya juu ya rafiki wa mwajili wao. ktk ITV hutasikia hata siku moja wakisema kinyume na Mengi. that is natural hata US ni hivyo. Sijui kama ulisikia mtangazaji aliyeachishwa kazi NBC wakati wa vita ya Iraq?
Mkuu Patriot, nahisi sijakuelewa?!, unauliza kama Clouds wameshindwa kuwa chombo cha habari?!, ama ndio unasema Clouds wameshindwa kuwa chombo cha habari?, tueleweshane sifa za chombo cha habari ni zipi, na Clouds kwenye sifa hizo, wameshindwa nini?!.

Kwa msio jua, hata channel o inayopiga muziki 24/7 ni chombo cha habari!.

Vyombo vya habari duniani kote vina majukumu matatu ya msingi,
  1. Kuhabarisha
  2. Kuelimisha
  3. Kuburudisha.
Chombo cha habari kinaweza kuyafanya yote matatu kwa pamoja, au kinaweza kufanya mawili au hata kufanya moja kati ya hayo na bado kikawa ni chombo cha habari!. Kwa maoni yangu Cloud ni chombo cha habari kamili gado!.

Pasco
 
Hapa unachanganya umiliki na uana habari, huyo DJ ni mmiliki na sio mwanahabari, na lengo la msingi la Clouds Radio ilikuwa ni kutoa burudani, habari zilikuja baadae sana!. Mmiliki wa Media kubwa kabisa nchini, IPP Media, ni Mzee Mengi na sio mwana habari!. Mmmiliki wa Media ya pili kwa ukubwa Tanzania, Sahara Media, ni Antony Diallo, sio mwanahabari!, Mmmilikiwa media ya tatu kwa ukubwa nchini, AMG, ni Shabir Abji, sio mwanahabari!. Wamiliki wengine karibu wote wa vituo vyaredio na TV sio wanahabari!. Wanahabari wenye redio zao ni Abdalah Majura na Ahmed Kipozi, hizo redio zao wewe unazikia?.

Pasco

Pasco hivi huyu Abdallah Majura Burembo wa CCM ndo huyo mwenye radio aliyekuwa Radio One baadae BBC?
 
Pasco hivi huyu Abdallah Majura Burembo wa CCM ndo huyo mwenye radio aliyekuwa Radio One baadae BBC?
No ni watu wawili tofauti, mmoja ni Abdallah Majura Burembo M/Wazazi CCM, mwingine ni Abdallah Idrissa wa Majura, alikuwa RTD-Radio One-BBC-Sasa anamiliki kituo chake cha redio!.
Pasco
 
kituo kimejaa mal*ya wake kwa waume.
Sasa hizi ni chuki!, bahati nzuri nimefanya RTD, nimeanzisha Radio Tumaini, nimeeanda DTV, nimeanzisha TVT na sasa ninajitegemea, hakuna kitruo chochote cha redio ambacho ni cha watakatifu!. Tena RTD ya enzi zile, isingekuwa "soo" ni mzunguko papo kwa papo!, tatizo la Clouds ni kituo cha kishua, mambo ya kishua au ya kizungu, kila kitu ni open hadi "on air!", huku wabongo tumezoea mambo ya kichini chini, kisiri siri, RTD "On Air" ni heshima adabu na full nidhamu!, lakini huko kwenye corridors, hadi chooni!. Ujana mbaya!, na haswa unaporukwa na akili kwa sababu ya ..., sitaki kabisa kukumbuka, kuanzia kwenye meza ya ofisi!, kwenye kiti cha ofisi!, kwenye ngazi!, kwenye corridor! hadi washroom!.
Kwa Watanzania wa kizamani, usiri ndio mpango mzima!, vijana wa kisasa ni uwazi kwa kwenda mbele!. Amini usiami wale wenye usiri ndio mtandao umeenea kuli hawa wa mambo hadharani!.
Sitetei mambo hayo, ila ndio ndio human nature na hizo ni moja ya huduma muhimu za kibinaadamu!.
Pasco
 
No ni watu wawili tofauti, mmoja ni Abdallah Majura Burembo M/Wazazi CCM, mwingine ni Abdallah Idrissa wa Majura, alikuwa RTD-Radio One-BBC-Sasa anamiliki kituo chake cha redio!.
Pasco

Asante sana kaka,ila kwa hili la Clouds mi huwa siwaungi mkono kasoro kipindi cha michezo mara moja moja huwa nawasikiliza lkn vipindi vingine vyote nilishaacha kuwasikiliza kwa sabab huwa wanaweka sana personal issues kam vile mambo yao ya disco,michapo n.k mpaka wanaboa.
 
Kwa nini utengeneze kitu cha hovyo ukisubiri mtu aende TCRA. Hawa jamaa siyo watu wa kuangalia tu. Nilisikia wakihusishwa na wauza madawa ya kulevya na kufanya ushirika nao. Wakati wa kifo cha mangwea mwingine alibanwa makofi hadhalani.

Kinachofanyika ni ule ushabiki wa kumusifia rais kila wakati wakajifanaya ni swahiba wao na sasa wanajaribu kurudi huko huko. Ni ukosefu wa seriusness ambao kwa ujumla pia ni madahala ya elimu ndogo ya wahusika. Huwezi kutoka kwenye uDJ ukawa mawanahabari wa maana, bila elimu.
Sawa kabisa, lakini suluhu ni kufuata taratibu ili waadhibiwe au kuchukuliwa hatua stahili. TCRA ndiyo mamlaka inayohusika. Ebu wapelekeeni malalamiko tuone hatua watakazochukua. Nimesoma humu JF kuwa wamesimamisha kipindi chao kimoja kwa uchunguzi, basi mkipeleka na mengine Yawezekana wakasimamisha kituo badala ya kipindi.
 
Sasa hizi ni chuki!, bahati nzuri nimefanya RTD, nimeanzisha Radio Tumaini, nimeeanda DTV, nimeanzisha TVT na sasa ninajitegemea, hakuna kitruo chochote cha redio ambacho ni cha watakatifu!. Tena RTD ya enzi zile, isingekuwa "soo" ni mzunguko papo kwa papo!, tatizo la Clouds ni kituo cha kishua, mambo ya kishua au ya kizungu, kila kitu ni open hadi "on air!", huku wabongo tumezoea mambo ya kichini chini, kisiri siri, RTD "On Air" ni heshima adabu na full nidhamu!, lakini huko kwenye corridors, hadi chooni!. Ujana mbaya!, na haswa unaporukwa na akili kwa sababu ya ..., sitaki kabisa kukumbuka, kuanzia kwenye meza ya ofisi!, kwenye kiti cha ofisi!, kwenye ngazi!, kwenye corridor! hadi washroom!.
Kwa Watanzania wa kizamani, usiri ndio mpango mzima!, vijana wa kisasa ni uwazi kwa kwenda mbele!. Amini usiami wale wenye usiri ndio mtandao umeenea kuli hawa wa mambo hadharani!.
Sitetei mambo hayo, ila ndio ndio human nature na hizo ni moja ya huduma muhimu za kibinaadamu!.
Pasco

Kwa hiyo Pasco,Clouds wakiwa exposed then unatafuta vivid example ya ku-justify huku ukijenga defence mechanism kwao??!!

Tangu mwanzo hulaani wala kukosoa uozo wao,bali kila post uko busy kuwa-shield na kuleta sababu linganifu cha kutetea!!!!
 
Last edited by a moderator:
Mimi nimeondoa Chanel na kufuta kabisa kwenye TV na radio yangu kituo hiki
 
Pasco, wanachofanya Clouds sio ushua bali ni ustaarabu wa kishenzi, kuna ya kuweka public na ya kuficha hasa kwa watoto.
 
Asante sana kaka,ila kwa hili la Clouds mi huwa siwaungi mkono kasoro kipindi cha michezo mara moja moja huwa nawasikiliza lkn vipindi vingine vyote nilishaacha kuwasikiliza kwa sabab huwa wanaweka sana personal issues kam vile mambo yao ya disco,michapo n.k mpaka wanaboa.
RTD ni redio ya taifa, hivyo focus yao ni issues za kitaifa na kutanguliza mbele maslahi ya taifa!. Radio Free Africa ni redio ya harakati za ukombozi barani Africa, focus yao ni uanaharakati!. Radio Tumsaini ni kuleta tumaini lililopotea, focus yao ni matumaini!. Radio Imani ni kujenga Imani!, Redio Upendo ni kuhamasisha Upendo, Praise Power kusifu na kutukuza!, etc, etc, Clouds Radio ni People's Station!, radio ya watu, mambo ya watu na personal issues kuhusu watu!..
Ukitaka mambo ya kitaifa sikiliza RTD, ukitaka mambo ya imani sikiliza Tumaini, Upendo, Praise Power au Radio Imaan, ukitaka mambo ya watu ndio usikilize Clouds Radio!.
Pasco.
 
Pasco, wanachofanya Clouds sio ushua bali ni ustaarabu wa kishenzi, kuna ya kuweka public na ya kuficha hasa kwa watoto.
Kwa ufahamu wangu ya kikubwa yanaanza saa 4:00 kwa loveness love au Diva!, watoto ambao hawajalala mpaka saa 4:00 usiku hao sio watoto hao ni wakubwa!.

Find out mtu aliyeishi Sweeden, kuanzia saa 6:00 usiku, adult movies ziko free to air!, nilishangaa nikamuuliza mwenyeji wangu, akaniambia kama kuna watoto wako macho at midninght!, hao sii watoto ni wakubwa hao!. Kesho yake kwenye supper markets na kwenye news stands kwenye streets adult magazine nje nje!, anayeuziwa must be 18 years!.
Pasco.
 
Kwa hiyo Pasco,Clouds wakiwa exposed then unatafuta vivid example ya ku-justify huku ukijenga defence mechanism kwao??!!

Tangu mwanzo hulaani wala kukosoa uozo wao,bali kila post uko busy kuwa-shield na kuleta sababu linganifu cha kutetea!!!!
Mkuu Mudy, ukishaamua kudhania, endelea tuu kudhania!, sio kwamba siikosoi Clouds ukitaka nitakuwekea hadi threads, ila mimi pia nina kitu kinaitwa "appreciation" kukubali hata mazuri kidogo!, hiyo imepelekea mimi humu jf kuitwa gamba simply kwa sababu kwa maoni ya wengi, CCM did nothing for this country, mimi nasema sii kweli!, pamoja na mabaya yote ya CCM, CCM did something!, no matter how little it is, it is not nothing!, it is something!.
Pasco!.
 
Huu uzi umenizindua pakubwa sana, sasa nimejua mengi

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
Huu uzi umenizindua pakubwa sana, sasa nimejua mengi

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums


Mkuu wengi hawaoni mbali kwani wamelala na danganya toto ya media!!
 
Bro !! anaemtunza hela mpiga zumar ndo anaechagua wimbo , ruge,kusaga mbona wana kadi za ccm ktambo

Kwa clouds is too much now,Reginald Mengi ni kada wa CCM na mfadhili pia lakini media zake hazifanyi upuuzi huu!!!
 
Mkuu Mudy, ukishaamua kudhania, endelea tuu kudhania!, sio kwamba siikosoi Clouds ukitaka nitakuwekea hadi threads, ila mimi pia nina kitu kinaitwa "appreciation" kukubali hata mazuri kidogo!, hiyo imepelekea mimi humu jf kuitwa gamba simply kwa sababu kwa maoni ya wengi, CCM did nothing for this country, mimi nasema sii kweli!, pamoja na mabaya yote ya CCM, CCM did something!, no matter how little it is, it is not nothing!, it is something!.
Pasco!.

Mkuu Pasco,Reginald Mengi alishawahi kushitakiwa na serikali/TCRA kwa kutumia zaidi ya nusu saa kuwatuhumu mafisadi papa ITV na pia alishawahi kuhojiwa media zake ndani ya bunge kuwa kwa nini kwenye taarifa za habari coverage ya Mengi huchukua dakika nyingi kuliko Kikwete??!!

Najua unayatambua fika sana hayo,sembuse sisi kuikosoa clouds??!! Au ndio wote unataka tu-appreciate tu kwa watawala na wenye noti hata kama wanakosea kisa wana mazuri pia??!!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom