uaminifukazi
JF-Expert Member
- Oct 22, 2014
- 1,481
- 928
Hawa Wafu Fm kiboko yao Sugu tuu.
Huyo Sugu kaishia kusanda na kuwatosa vinega wenzie baada ya kulambishwa mshiko na Ruge... kawaulize Vinega watakwambia.. hawana hamu na huyo mchumia tumbo.
Hawa Wafu Fm kiboko yao Sugu tuu.
kuitetea clouds fm ni mpaka uwe na mafuriko ya uwehu kichwani.
Hapa hatuangalii nani alitenda kosa hapa tunaangalia nini kilifuatia baadae! Iwe Clouds ndio wakosaji au hapana, ukweli bado unabaki pale pale kwamba ni Jay Dee mwenyewe ndie alikataza nyimbo zake kupigwa; tena hakukataza kiuungwana, na full kejeli na kujitapa kwamba anaanzisha radio yake... miezi inapita, hiyo radio hatuioni.... watu mkaanza kudanganyana kwamba EFM ndo radio ya Radio! But in addition, wimbo unaozungumziwa hapa ni Alikufa kwa Ngoma ambayo ni ya Mwana FA, Mwana FA na Jay Dee nao hawapo kwenye good terms! Imeshatokea si mara moja wala mara mbili msanii kufuta mistari ya msanii aliyekuwa amemshirikisha kv tu they're no longer in good terms! Hili lilitokea kwa Zay B Vs Nature na hata Diamond na Kiba, bifu lao lilianzia huko... wakafutiana mistari ambayo walishirikiana! So, what if hata Mwana-FA mwenyewe hayupo ready kusikia sauti ya Jide kwenye nyimbo zake??kwa nn aliongea hayo??? kosa ni la nani?? ukiona mtu kafikia hatua ya kutoa kaulo hizo lazima ujipime ulichomkosea mlalamikaji huenda walimfanyia kitu mbaya sna dada wa watu.
Hilo la siasa hata mie nimeshapata kulisema kwenye posts za nyuma... unajua kuna watu kibao sio watu wa burudani wengine wameijua burudani baada ya kuja mjini na hata wale waliokulia mjini kuna wengine wamekuja kuijua burudani baada ya kutoka kwenye vifungo vya wazazi wao... baada ya kumaliza shule na labda kuingia chuo mwaka wa kwanza ndipo wakaanza kufunguka macho! Hawa wote huwa wanachanganya siasa na burudani kv burudani sio ada yao na haipo kwenye damu zao!! Hawa ni wale ambao wala hawafahamu pale Billz watu wanatimba kila leo bila kujali kwamba mmiliki ni mwenyekiti wa chama fulani cha siasa! Lakini hawa watu waliokurupukia burudani ukubwani, kama Billz ingekuwa inamilikiwa na mtu yule wasiyemuunga mkono kisiasa, kila siku hapa tungeona posts kuhusu Billz! Wengi wao bifu lao na Clouds lilianzia kwa Kibonde ambae kwa asili huwa achgui cha kuongea... hajali kama utachukia au hautachukia! Sugu nae alipoingia kwenye bifu na Clouds, nao wakaingia waziwazima....... Jide alipoingia kwenye bifu, nao wote wakamfuata... kwa mara ya kwanza tukashuhudia vituko vya karne kusikia Jide akiitwa kamanda!#Nazdaz tatizo la hawa vijana wa fb ni kupenda kushadadia mambo wasiyoyajua. Muda wote wanawaza siasa tu matokeo yake wanapeleka siasa hata kusikostahili. Kulalama na kulalamika ndo imegeuka kuwa jadi ya Mtanzania. Basi wameamua kuchagua maisha ya kulalamika ni bora wakawa wakweli kwa kila upande badala ya hizi ngonjera za double standards tunazoziona humu kila siku.
FidQ alikua na kipindi pale EATV sijui kimeishia wapi lakini nakumbuka kwenye wimbo wake kachana ukweli kuwa, HAKUNA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI, BALI KUNA UHURU WA MWENYE CHOMBO CHA HABARI. KAMWE IPP HAIWEZI KUMPINGA MENGI. Nadhani hakumlenga mengi kama mengi bali alimtolea mfano kuwa vyombo vya habari vipo kwa ajili ya wamiliki wake na sio wananchi. Kwahiyo hizi ngonjera za kuwa mnakuja hapa kushambulia MEDIA Moja ni vyema mkaachana nazo kwani huu ni mfumo na sio suala la mtu binafsi. Na utakapoamua kulielezea ni bora ukawaambia wamiliki wote wa vyombo vya habari kuanzia IPP,CLOUDS GROUP, SAHARA, UHURU, MAGIC,TIMES,MAWIO, TANZANIA DAIMA, NIPASHE nk.
Utoto unaozungumzwa ni wa ku-mute kipande alichoimba Jay Dee kwahiyo lazima tuangalie source ni kwanini imetokea hivyo!Mada inahusu utoto unaofanywa na clouds ila watu wanajadili beef la clouds na Jay dee.
#Nazdaz tatizo la hawa vijana wa fb ni kupenda kushadadia mambo wasiyoyajua. Muda wote wanawaza siasa tu matokeo yake wanapeleka siasa hata kusikostahili. Kulalama na kulalamika ndo imegeuka kuwa jadi ya Mtanzania. Basi wameamua kuchagua maisha ya kulalamika ni bora wakawa wakweli kwa kila upande badala ya hizi ngonjera za double standards tunazoziona humu kila siku.
FidQ alikua na kipindi pale EATV sijui kimeishia wapi lakini nakumbuka kwenye wimbo wake kachana ukweli kuwa, HAKUNA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI, BALI KUNA UHURU WA MWENYE CHOMBO CHA HABARI. KAMWE IPP HAIWEZI KUMPINGA MENGI. Nadhani hakumlenga mengi kama mengi bali alimtolea mfano kuwa vyombo vya habari vipo kwa ajili ya wamiliki wake na sio wananchi. Kwahiyo hizi ngonjera za kuwa mnakuja hapa kushambulia MEDIA Moja ni vyema mkaachana nazo kwani huu ni mfumo na sio suala la mtu binafsi. Na utakapoamua kulielezea ni bora ukawaambia wamiliki wote wa vyombo vya habari kuanzia IPP,CLOUDS GROUP, SAHARA, UHURU, MAGIC,TIMES,MAWIO, TANZANIA DAIMA, NIPASHE nk.
Clouds ni media kipuuzi sana.
Hivi hii redio bado ina wasikilizaji?
Wanajishushia hadhi sana,Kampuni kubwa kuwa na beef na msanii? Ni Kichekesho sana.
Hivi clouds fm ni kitu gani hicho!?
nshamalizana nao hawa, wajinga sana, hii sio mara ya kwanza, siwapi audience yangu.
Clouds FM wajinga sana...!! Nawachukia mpaka basi..
Ni takataka fulani hivi ya makelele
Mnapata wapi muda ya kusikiliza radio ya wapuuzi wa design hii??
bahati mbaya hata sisikilizi redio
hii ndio bora radio fm na sio radio bora
Wananikera sauti zao hasahasa hicho kipindi, wanajifanya sauti za kidhungu
Hivi hii redio bado ipo hewani?
Mtu mwerevu mwenye akili zake timamu hawez kuiskiliza clouds wala kuitizama.. Cause imejaa mitoto ya uswaz iliyokosa nizamu
Hofu yangu ni kwamba, wote nyinyi na wengine kama nyinyi mchango wenu ni sawa na tone la maji kwenye bahari! Si tu kwamba mnajifanya hamuisikilizi wakati mnaisikiliza lakini hata msipoisikiliza, effect take is almost negligible coz', wakati nyie mnajidai hamuisikilizi, there're millions outta there wanaoisikiliza including hao wasanii mnaojifanya kuwatetea!! By the way, Clouds FM ni nini hasa?Hawa Wafu Fm kiboko yao Sugu tuu.
Superbrands has launched programmes in over 88 countries including all the key global markets. These programmes aim to identify those brands that are performing above and beyond others within the market. At the heart of each programme is an independent and voluntary council of leading experts comprising individuals with a deep appreciation of the "brandscape" in the country being examined.
The council comprises luminaries from the marketing and communication industries plus notable figures from local and international blue chip companies and media organisations. Only those brands highly rated by the council are invited to join the Superbrands project. Each country has its own local panel to ensure that only the most deserving of brands attain the credential and feature in the project. More http://superbrandseastafrica.com/about-us/
Hebu kwenda huko, wewe??!! Ndio maana wala sikujisumbua kukuweka kwenye hiyo list hapo juu kv nafahamu unanogesha genge tu hapa!!!sisikilizagi
Mmesahau ishu ya rama dee na clouds
Maisha ni kuchagua nadhani clouds FM ndo wamechagua aina hiyo ya maisha na sidhani kama wanavunja sheria ingekua kuna kitu hakipo sawa TCRA wangeingilia kati wao ni taasisi binafsi na wana aina yao ya maisha hivyo tuwaache tu kumbukeni Magic FM kwa muda mrefu walikua hawapigi nyimbo za Diamond mpaka pale walipomaliza tofauti zao pia East Africa Tv n Radio kama sio IPP kwa ujumla kuna wakati nao walikua hawachezi nyimbo za ally kiba audio mpaka video so to me sioni tatizo lolote usipopigwa huku utapigwa kule pia dunia ni kubwa huwezi kumfurahisha kila mtu
Kucheka chela tu
Ukabila wenu pelekeni IPP huko kwa wachaga. Pale Clouds hakuna ukabila hizo chuki zako tu... leta fact kuthibitisha upuuzi wako.
Taja makabila ya presenters tunaowazungumzia hapa!Una Uhakika Ukabila Hamna Au Unataka Ujulikane Kuwa Umekomenti Thread
Habari Wanabodi,
Nipo nasikiliza Clouds FM kipindi cha xxl segment ya "Album Review".Leo wana Review album(2003) ya Mwana Fa ya "Toleo Lijalo" yenye nyimbo kama Wanapendana,Alikufa kwa ngoma etc.Kwenye wimbo wa alikufa kwa ngoma ameimba na Anaconda(Lady Jay Dee) cha kushangaza kwenye huo wimbo wakati wana review ikifika sehemu ya chorus ya jide wana-mute inasikika beat tu.Kitendo cha clouds FM kama taasisi kampuni nzima kuweka beef na msanii mmoja inajidhihirisha Clouds FM ni radio ya wahuni tu.
Clouds FM sio mara ya kwanza kufanya upumbavu huo,nakumbuka kipindi cha nyuma Inspector Haroun alienda nao tofauti,kipindi hiko wimbo wake wa "Buzi" ndio ulikuwa una-hit basi jamaa kila ikifika pale anapochana Inspector sauti wanaondoa inasikika beat tu.
Kwenye ngoma ya Ben Pol "Jikubali" kuna moja ya mstari unaimbwa "Nampenda Lady jay Dee,namzimia Zitto" ile sehemu ya neno Lady Jay Dee wanaisugua(Scratch) na ilo neno halisikiki kabisa.
Kwenye kuadhimisha miaka 15 ya Dully sykes,kwenye promo walikuwa wanapiga nyimbo za nyuma za Dully Sykes,kuna ngoma inahitwa Bijou inavyoanza ina neno "Okay mbili sifuri sifuri nne,P-funky kinywele kimoja" ilipoanza hapo kwenye P-funky wakaikata kabisa wakaipeleka mbele.
Kwa Mchezo huo wa kitoto unaofanywa na Clouds Media inaishushia hadhi sana hiyo kampuni,kitendo cha kampuni hiyo kufanya mambo ya utoto ni wadhi redio inaendeshwa na makanjanja na sio watu wenye ueledi.Clouds FM ikubali pia matakwa ya wasanii,kama msanii akikataa kufanya deal kwa sababu anaona haimfaidishi yeye ni haki yake kukataa na si kigezo cha kutopiga nyimbo zake.
Kuna watu watasema kwamba redio zipo zaidi ya 60 na TV zaidi ya 20 kwanini wasanii wailalamikie Clouds tu? Hapa tunacholalamika ni kufinya(mute) sauti yeyote iliyopo kwenye nyimbo alizoshirikishwa msanii walioenda nae tofauti.Kama wanapiga wimbo wa ben pol waachie wimbo kama ulivyo na si ku-mute majina ya watu waliotajwa wenye beef nao.
CLOUDS MEDIA ACHENI UTOTO.