Hapa hatuangalii nani alitenda kosa hapa tunaangalia nini kilifuatia baadae! Iwe Clouds ndio wakosaji au hapana, ukweli bado unabaki pale pale kwamba ni Jay Dee mwenyewe ndie alikataza nyimbo zake kupigwa; tena hakukataza kiuungwana, na full kejeli na kujitapa kwamba anaanzisha radio yake... miezi inapita, hiyo radio hatuioni.... watu mkaanza kudanganyana kwamba EFM ndo radio ya Radio! But in addition, wimbo unaozungumziwa hapa ni Alikufa kwa Ngoma ambayo ni ya Mwana FA, Mwana FA na Jay Dee nao hawapo kwenye good terms! Imeshatokea si mara moja wala mara mbili msanii kufuta mistari ya msanii aliyekuwa amemshirikisha kv tu they're no longer in good terms! Hili lilitokea kwa Zay B Vs Nature na hata Diamond na Kiba, bifu lao lilianzia huko... wakafutiana mistari ambayo walishirikiana! So, what if hata Mwana-FA mwenyewe hayupo ready kusikia sauti ya Jide kwenye nyimbo zake??
Kwamba ukiona mtu kafikia kutoa kauli hizo lazima ujipime, hakuna asiyefahamu kwamba Jide ni mtu aliyejaa majivuno, jeuri, dharau na maneno machafu! Jide ni mtu asieyechanganyika na wasanii wenzake lakini bado hilo halimzuii kuingia kwenye migogoro na wasanii wenzake! Katika hali ya kawaida, kv hayupo karibu na wenzake basi hata migogoro kwake isingekua imetokea! Napoteza muda kuongea mengi, lakini hivi karibuni tu tumeshuhudia anavyotumia social networks kusema maovu ya mumewe... mumewe ambae, pamoja na ukaribu wake na watu wa Clouds, lakini wakati wa bifu lao aliamua kusimama pamoja na mkewe! Kwahiyo mtu kama huyo ni ngumu kufikia conclusion kwamba walionza ukorofi ni Clouds! Leo hii Stara Thomas akiingia kwenye mgogoro na yeyote, lazima wadau watajiuliza, what's wrong lakini sio kwa Jide!