Chuo Kikuu cha Dar (UDSM) chajadili Mkataba wa Bandari

bagamoyo

JF-Expert Member
Jan 14, 2010
21,305
24,200

Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Ndaki ya Sayansi ya Jamii​

Kitivo kikongwe cha chuo kikuu cha UDSM chajadili kwa pamoja na jamii nzima mkataba wa bandari



Mwenyekiti wa mjadala wa leo Dr. Ng'wanza Soko Kamata wa kitivo cha CoSS UDSM aliwakaribisha wote waliojumuika ukumbini na wale walioshiriki kwa njia ya Zoom mtandaoni.

Ndaki ya Sayansi ya Jamii UDSM pia hujikita katika kuchambua tafakuri zilizopo katika jamii na hili jambo la sakata la mkataba wa bandari linaloifikirisha jamii ya kiTanzania linaangaziwa kwa upana.

Video ndefu hapa juu inawakilisha tafakuri inayotuletea yote ya mjadala mpana na mkubwa uliowaleta washikadau wakiwemo wanazuoni waalimu wahadhiri waandamizi 9 wa chuo kikuu wakiwemo Dr. Ng'wanza Soko Kamata, Dr. Richard Bruno Mbunda, Prof. Issa Shivji, wanafunzi wa UDSM na wananchi wanajamii kupitia mtandao


Uchambuzi wa Profesa Shivji mazito yabainika mkataba wa bandari



Chini ya ndaki ya sayansi ya jamii CoSS College of Social Sciences leo wahadhari na wanafunzi wajadili kwa kina mkataba wa bandari na unaleta madhara gani kwa taifa.

Mchokoza mada Dr. Richard Bruno Mbunda pamoja na wahadhiri na wanafunzi wa chuo kikuu cha UDSM na mgeni mwalika profesa Issa Shivji wamejadili kwa kina mada ya mkataba wa bandari ambao imekuwa habari kuu isiyozimika katika vijiwe na mitandao ya kijamii.

Dr. Richard Mbunda anasema kuwa pamoja na Ofisi ya Katibu wa Bunge kuwa ni mshauri mkuu wa bunge lakini pia secretariat ya bunge kuonesha kwa mapendekezo mapungufu ya mkataba lakini kamati ya bunge husika, waziri na bunge zima liliamua kutoyatilia maanani maangalizo muhimu ya secretariat ya Bunge kuhusu mkataba huu usioupa haki ya sovereignty Tanzania

Ila leo ndaki hiyo ya chuo kikuu cha Dar es Salaam imeamua kurudia enzi ambazo chuo kikuu hicho kongwe kilikuwa hakiko nyuma kuandaa mihadhara ya kuchambua mambo mazito yanayoendelea katika jamii .

Profesa Issa Shivji ameamua kujikita zaidi katika mguso huo wa mkataba una maana gani hasa pia unatuletea nini mezani na kumuachi Dr. Richard Bruno Mbunda akijikita kisheria zaidi una mazuri na mapungufu gani.

Profesa Issa Shivji anasema mkataba huu ni treaty yaani mkataba baina ya nchi na nchi na nchi hiyo ni Tanzania na nchi nyingine ambayo ni ngumu kusema kama ni nchi au la.

Ila kuna jambo ambalo limejitokeza katika hilo maana katika treaty lazima kuwepo nipe na nikupe baina ya wawili katika mkataba. Hilo halipo bali haki zote amepewa Dubai huku wajibu wote amepewa Tanzania bila haki. Yaani mkataba umekuwa uwekezaji ingawa unaitwa ni mashirikiano.

Ila ushirikiano huo si wa kijumla bali ni wa bandari na mwekezaji ametajwa ni DP World siyo wawekezaji wa kijumla wa kuhesabika kwa namba makampuni au wafanyabiashara kutoka Dubai.

Jingine ni kuwa DP World inamilikiwa na serikali yaani ni state company. Maana yake kampuni ya serikali inaweza kuleta mgongano wa kidiplomasia tofauti kama ingekuwa kampuni ya binafsi kwani kampuni binafsi huwa haiwezi kuleta mgogoro wa kidiplomasia maana mambo yote yangeishia mahakamani ila kwa kampuni inayomilikiwa na serikali ni tofauti.

Hii ina maana 80% matayarisho shughuli na mapendekezo ya mradi (early project activities) huu mradi wa serikali ya Dubai kupitia DP World na serikali ya Tanzania yalikuwa yameshaandaliwa hata kabla ya mkataba uliopitishwa na azimio la Bunge la Jamhuri ya Muungano tarehe 10 June 2023 mjini Dodoma.

Hii ina maana mikono ilishafungwa na mkataba hata kabla ya IGA ya Dodoma na hiyo mikataba mingine midogo midogo imeshamalizwa kabla ya HGA . Host Government Government Agreements inayotajwa kuwa itafuatia.

Mfano suala la ardhi kwa sheria za Tanzania rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania katiba yetu inasema ni mdhamini / mwangalizi wa ardhi yote ili ndani ya mipaka ya nchi na kuwa mtanzania au mwekezaji akipewa umiliki wa miaka 33 au 66 au 99 Rais ana mamlaka ya kuichukua akiona inafaa kutumika kwa manufaa mapana ya jamii na nchi.

Lakini kwa mkataba wetu na DP World, hili la rais wa Tanzania ni mdhamini / mmiliki wa ardhi yote ya Tanzania amevuliwa mamlaka hayo na ameshanganganywa mamlaka hayo na mkataba huu wa aina yake wa bandari. Maana mkataba na Dubai unasema kuhusu ardhi upo bayana neno la kiingereza incumbrace (in property law) kuwa hakutakuwa na kikwazo chochote ...

Bandari ya Dar es Salaam haijathaminisha ili ijulikane serikali yetu imeshawekeza trilioni ngapi kabla DP World haijaingia mkataba. Hakuna mpango maalum wa kuelezea mapato yatagawanywa vipi baina ya Tanzania na DP World kutokana na mradi huu wa bandari.

Ajira za upande wetu zitakuwa za kada ya makuli ndiyo wataajiriwa pengine na wachache kwenye HR yaani utumishi lakini wataalamu wote watatoka nje. Kuhusu kazi za ndogo ndogo za kandarasi ku supply vitu kwa DP World itatolewa kuna masharti, vigezo na kanuni kibao ambazo wafanyabiashara wa Tanzania watashindwa kutimiza mfano standards, competitive market prices za kimataifa n.k Nani atakuwa mdhibiti kuhakikisha tenda ndogo kampuni za kitanzania zitawe kushinda kuuzia DP World vifaa, vipuri n.k mhadhara huu wa ndaki ya sayansi ya jamii CoSS unakuna vichwa wakiangalia mbele.

Muhadhara huu wa CoSS ndaki ya Sayansi ya Jamii ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam unaenda mbali na kuona nini kifanyike maana mkataba huu ni mgumu kunufaisha taifa hata ukifanyiwa marekebisho kupitia hatua za HGA host government agreement.

Muhadhara wa huu CoSS pia uliunganisha jamii nje ya chuo wachangiaji mada na maswali kupitia mtandaoni live na kuona yafuatayo yafanyike .

Bunge liamue kukataa azimio lake lenyewe la tarehe 10 June 2023 kuhusu mkataba huu. Bunge lina mamlaka hayo na haliwezi kuhojiwa na DP World wala jumuiya ya kimataifa. Maana Bunge linachanguliwa na wananchi wa Tanzania na pale wananchi wanapokataa mkataba huu baada ya kusikilizwa, wabunge ni wajibu wao kuandaa azimio lingine linalozingatia maoni ya wananchi kuwa wameukataa mkataba / makubaliano haya.

Muhadhara unafahamishwa kuwa nchi kadhaa zimeweza kuvunja mikataba ya aina hii na haikuonekana ni ajabu na kutolea mifano Ecuador ilifuta mikataba 26, nchi ya Bolivia ikaondoa mikataba 17 huku South Africa nayo mikataba 20 iliondolewa wakati India nayo ilifuata mikataba 58.

Hivyo serikali na kikao cha bunge lake baada ya Azimio la Bunge kupitisha mkataba wa bandari kutoa kauli ya unyenyekevu ipo sikivu na kuahidi kusikiliza kelele pia maoni ya wananchi wake pamoja na maoni ya washikadau kama wataalamu wa sheria, wahadhiri wa vyuo vikuu, vyama vya siasa n.k

Mhadhara wa watu-huru kupitia tafakuri ya kina unafikiri ni wakati sahihi wa Bunge kuitisha kikao cha dharura kukaa na kufuta azimio lake la tarehe 10 Juni 2023 na bunge kuishauri serikali kuanza mchakato mpya kumpata mwekezaji mwenye masharti ya manufaa hata kama katika mchakato huo mpya wa wazi shindani atakuwemo DP World na wengine ambao watashindanishwa ...
 
Walijadili ule mswada wa cyber crime pale Nkurumah Hall, lakini kilitokea nini?
Ule mswada si ulipitishwa wala hata yale marekebisho waliyoyataka hayakufanywa!

Maxence Melo alikuwepo ni shahidi!

Hata huu mkataba walivyojadili matokeo yatakuwa sawa na yale ya mswada wa cyber crime tu!
 
IMG_7396.jpg

IMG_7387.jpg

IMG_7381.jpg

IMG_7386.jpg
 
Ujenzi wa BWAWA la ufuaji umeme MWALIMU NYERERE ulipingwa na akina ndg.Tundu Lissu kwa kuwashirikisha CDU na "lobbying" zao pale BUNDESTAG kwa kigezo cha uharibu wa mazingira ya turathi ya dunia pale Selous....na pia matumizi mabovu ya fedha za umma TRILIONI 6.5...ila hayati JPM akafanikiwa kuutekeleza

Hakuna litakaloanzishwa likakosa WAPINGAJI.

#SiempreSSH
 
Hoja ya DP WORLD kumilikiwa na serikali ya UAE ni ya kushangaza sana.....

Hebu angalia hili ....

Arab Contractors ni kampuni binafsi lakini tulimuona Rais wa Misri mh.El Sisi akituma ujumbe mzito kuja na hao Arab Contracts kuingia mkataba nasi wa Trilioni 6.5 kujenga bwawa la kufua umeme Mwalimu Nyerere....

Hoja ni hii....

Haya makampuni pamoja na kuwa ni ya kibinafsi ila yana "affiliation" sana na maslahi ya SERIKALI na madola yao......unaweza kutoigopa ARAB CONTRACTORS isiyo na "mafungamano" na serikali ya Misri na kuiogopa DP WORLD waliodhihirisha mafungano na serikali yao na kubaki binafsi "kujichezesha mchezo wa kadenge"

Dunia imebadilika TUSIKARIRI TU....

Kule Urusi , OLIGARCHY walianzisha makampuni binafsi kwa "fedha ya hazina ya nchi ".....


#ChifuHangayaAnaupigaMwingi

#SiempreJMT
 
serikali ya UAE ni ya kushangaza sana.....

Dubai siyo nchi, mgogoro wake ni tofauti na ndiyo maana Arab Contractors ina udhamini wa nchi ya Egypt. Kukitokea jambo serikali ya Tanzania inaweza kuongea jambo na serikali ya nchi ya Egypt kidiplomasia kabla ya hatua za kisheria n.k

Je mgogoro ukitokea kati ya Tanzania na 'nchi' ya Dubai itawezekana suala likaanzia kwanza ngazi ya 'kidiplomasia' au itabidi kuomba kwanza utatatuliwe kwa udhamini wa UAE ? Maswali ni mengi

Tutazame mahusiano baina ya nchi ya UAE na Australia, mashirika ya kimataifa n.k Dubai haina mamlaka hayo wala kofia ya kuhesabika kama nchi mbele ya Jumuiya ya Kimataifa na Mikataba ya Kimataifa

IFAHAMU NCHI YA UAE / FALME ZA KIARABU
Wizara ya Mambo ya Nje ya Australia inaitambua Nchi ya United Arab Emirates ambayo ndani yake yapo majimbo saba : Abu Dhabi, Dubai, Sharjah, Ajman, Umm Al-Quwain na Fujairah huku jimbo la saba la Ras Al Khaimah ilijiunga na Shirikisho la UAE mwaka 1972. Huku mji mkuu wa nchi ya UAE ikiwa ni Abu Dhabi, mji uliopo ndani ya jimbo / emirate kubwa na tajiri zaidi ya nchi ya UAE .

Rais wa shirikisho la nchi ya UAE ni maulana sheikh Mohammed bin Zayed Al Nahyan. Kiongozi wa jimbo la Dubai maulana sheikh Mohammed bin Rashid Al Maktoum ni Makamu wa Rais pia ni Waziri Mkuu na Waziri wa nchi ya UAE

Mahusiano baina ya Australia na nchi ya UAE ni ya kirafiki, katika nyanja mbalimbali huku yakiendelea kukua.

Nchi ya UAE ushirikiano wake na Australia umewezesha nchi hiyo ya Australia kuwa ni mwekezaji mkubwa zaidi wa mitaji na biashara nchini UAE kuliko nchi yoyote ya Masharik ya Kati.


United Arab Emirates country brief

Overview

The United Arab Emirates (UAE) is situated in the Southeast of the Arabian Peninsula, bordering Oman and Saudi Arabia. In December 1971, the UAE became a federation of six emirates - Abu Dhabi, Dubai, Sharjah, Ajman, Umm Al-Quwain, and Fujairah, while the seventh emirate, Ras Al Khaimah, joined the federation in 1972. The capital city is Abu Dhabi, located in the largest and wealthiest of the seven emirates.
Since its Federation in 1971, the UAE has developed rapidly and is now noted for its modern infrastructure, international events and status as a trade and transport hub. In 2021, the UAE commemorated its Golden Jubilee, 50 years since federation.
The UAE will host the COP28 international climate summit in Dubai in 2023.

Political overview

The President of the UAE is His Highness (HH) Sheikh Mohammed bin Zayed Al Nahyan. The Ruler of Dubai, HH Sheikh Mohammed bin Rashid Al Maktoum, is the Vice-President, Prime Minister and Defence Minister.

The UAE's federal structure includes a Supreme Council (comprising the Rulers of each Emirate), a Council of Ministers and Federal National Council. Each Emirate is governed by its own Ruler, with its own local government, courts and police forces.

The Federal National Council comprises 40 members, half of which are appointed and half elected. Elections were last held in October 2019 and for the first time the UAE implemented a requirement for 50 per cent of total members to be women.

This requirement saw a significant increase in the number of female candidates. The Federal National Council has an advisory role and is a forum in which concerns of Emiratis are raised.

The UAE is a member of the Gulf Cooperation Council (GCC), the Arab League, the Organization of Islamic Cooperation, the United Nations (including UN Security Council member, 2022-23), the Organization of the Petroleum Exporting Countries, the Non-Aligned Movement and the World Trade Organization. The International Renewable Energy Agency, established in 2009, has its headquarters in Abu Dhabi.
On 15 September 2020, the UAE and Israel signed the Abraham Accords Peace agreement in Washington, DC.

Bilateral relations​

Bilateral relations between Australia and the UAE are friendly, multi-faceted and growing rapidly.

They are underpinned by extensive trade relations, and the UAE is Australia's largest Middle East trade and investment partner.

The two countries enjoy good defence, aviation, security and law enforcement cooperation, the latter underpinned by agreements on mutual legal assistance in criminal law matters and extradition.
Australia was among 192 participating countries at Expo 2020 Dubai, which ran from 1 October 2021 to 31 March 2022.

Expo 2020 provided a key platform for Australian companies to reengage with traditional partners and progress market diversification strategies, including the growth of exports into the Middle East and South Asia.

The Australian Ambassador to the UAE is based at the Australian Embassy in Abu Dhabi. Australia also has a Consulate-General/Trade Commissioner in Dubai.

State government offices representing New South Wales, Queensland, Western Australia, and Victoria are also based in the UAE.

People to people links​

People-to-people contacts have expanded rapidly on the back of the strong growth of direct air links. Prior to the COVID-19 pandemic restrictions, over 100 Emirates and Etihad flights per week operated between the UAE and Australia.

An estimated 15,000 Australians live and work in the UAE.

At the start of 2020, in response the severe Australian bushfire season, the UAE donated fire trucks and generators to several affected communities. On 16 January 2020, the Burj Khalifa, the world's tallest building which is located in Dubai, was lit up with the phrase ‘#mateshelpmates' as a sign of the UAE's support for bushfire response.

Economic overview​

The UAE is the Middle East's third largest economy, and one of the wealthiest countries in the region on a per capita basis. Its GDP in 2021 was estimated at US$410.2 billion, a real GDP growth rate of around 2.2 per cent.

The UAE has six per cent of the world's oil reserves and the seventh largest proven natural gas reserves. Petroleum exports were US$49.6 billion in 2019. In the medium term, oil and gas (which account for over two-thirds of exports and the bulk of government revenue) will continue to underpin the UAE's economy.

However, significant steps towards economic diversification have already been taken, with approximately 70 per cent of GDP now generated by sectors other than oil and gas. To celebrate 50 years of nationhood in 2021, the UAE launched 50 new economic initiatives to boost the country's competitiveness and attract US$150 billion in foreign direct investment over the next nine years.

Abu Dhabi, which has the vast majority of oil and gas reserves in the UAE, has made significant investments in establishing aerospace, nuclear power, defence, information technology (micro-processing), petrochemical and clean-tech industries – the latter most prominently represented by the multibillion-dollar initiative of Masdar City, a zero-carbon city outside Abu Dhabi.

Abu Dhabi is also investing heavily in educational institutions, and cultural and sporting attractions such as the Formula One racing track, Ferrari theme park, and the Louvre Abu Dhabi to diversify the economy away from oil and encourage tourism.

Dubai has also diversified into the exhibitions, events, ICT, re-export and financial sectors. Taking advantage of its position near the head of the Gulf, it has consolidated its historical reputation as a regional entrepôt. Dubai has developed luxury hotels, large port facilities (including Jebel Ali) and a range of free trade zones to attract both manufacturing and services industries.

The UAE population of 10.1 million (2022) depends substantially on its expatriate workforce, which made up about 88 per cent of the population in 2021. The UAE is also opening up utilities to greater private sector involvement. Several free trade zones across the country attract foreign investors, by offering full ownership and zero taxes.

The COVID-19 pandemic has had a significant impact on the UAE's economy, particularly due to the reduction in passenger numbers through air hubs, the reduction in tourist arrivals and the impact of COVID-19 measures on commerce. The UAE is expected to recover to pre-pandemic levels of economic activity over the next three years.

Trade and Investment​

On 17 March 2022, then Minister for Trade, Tourism and Investment Dan Tehan and HE Dr Thani bin Ahmed Al Zeyoudi, Minister of State for Foreign Trade, issued a joint statement announcing Australia and the UAE's intention to pursue a Comprehensive Economic Partnership Agreement (CEPA). DFAT consultations with stakeholders continue, and will inform the possible agreement and the Australian Government's approach to future negotiations.

The United Arab Emirates (UAE) is Australia's largest trade and investment partner in the Middle East. With $5.5 billion in two-way trade in 2021 (over $10 billion pre-COVID), the UAE is Australia's 18th largest export market globally for goods and services.

Exports to the UAE were worth $3.24 billion in 2021 and were dominated by red meat, transport services and machinery and automotive parts.

Australian imports from the UAE were worth $3.24 billion in 2021 (mainly petroleum products).

Services trade is an increasingly important component of the commercial relationship, including construction, financial and professional services, tourism and education. Education is seen as an area of potential growth, with several Australian institutions active in the UAE market, including: Wollongong University, which in 1993 was the first private university to establish a campus in Dubai; Murdoch University, which opened in Dubai in 2007; Curtin University, which opened in Dubai in 2018; the Australian International School Sharjah; the Victorian International School Sharjah; and a number of Australian institutions with partnerships with local institutions to deliver the Australian curriculum in-country.

Australia's commercial profile in the UAE is significant, with UAE-based Australian companies numbering over 300. Australian companies, institutions and capabilities are working in a range of industries, including steel trading, building, construction and financial services, banking services, materials and equipment, agricultural supplies and services, industrial minerals, dairy products, marine manufacturing, education and training services, sports and recreation, health services, livestock, oil field supplies, courier and freight services. Many companies use Dubai as a regional base, in view of its transport, financial and communications infrastructure.

UAE entities hold significant investments in Australia, including in the agribusiness, tourism, health and aged care and resources sectors.
In 2020, UAE investment in Australia was estimated at $11.6 billion according to ABS data.

The Abu Dhabi Investment Authority (ADIA), the world's fourth largest sovereign wealth fund, has invested in ports, the TransGrid electricity network and the Queensland Motorway project.

Other UAE sovereign wealth funds also have assets and are examining other investment opportunities in Australia.

Source : https://www.dfat.gov.au/geo/united-arab-emirates/united-arab-emirates-country-brief
 
Dubai siyo nchi, mgogoro wake ni tofauti na ndiyo maana Arab Contractors ina udhamini wa nchi ya Egypt.

Je mgogoro na 'nchi' ya Dubai suala la kidiplomasia utatatuliwa kwa udhamini wa UAE ?

IFAHAMU NCHI YA UAE / FALME ZA KIARABU
Wizara ya Mambo ya Nje ya Australia inaitambua Nchi ya United Arab Emirates ambayo ndani yake yapo majimbo saba : Abu Dhabi, Dubai, Sharjah, Ajman, Umm Al-Quwain na Fujairah huku jimbo la saba la Ras Al Khaimah ilijiunga na Shirikisho la UAE mwaka 1972. Huku mji mkuu wa nchi ya UAE ikiwa ni Abu Dhabi, mji uliopo ndani ya jimbo / emirate kubwa na tajiri zaidi ya nchi ya UAE .

Rais wa shirikisho la nchi ya UAE ni maulana sheikh Mohammed bin Zayed Al Nahyan. Kiongozi wa jimbo la Dubai maulana sheikh Mohammed bin Rashid Al Maktoum ni Makamu wa Rais pia ni Waziri Mkuu na Waziri wa nchi ya UAE

Mahusiano baina ya Australia na nchi ya UAE ni ya kirafiki, katika nyanja mbalimbali huku yakiendelea kukua.

Nchi ya UAE ushirikiano wake na Australia umewezesha nchi hiyo ya Australia kuwa ni mwekezaji mkubwa zaidi wa mitaji na biashara nchini UAE kuliko nchi yoyote ya Masharik ya Kati.


United Arab Emirates country brief​

Overview​

The United Arab Emirates (UAE) is situated in the Southeast of the Arabian Peninsula, bordering Oman and Saudi Arabia. In December 1971, the UAE became a federation of six emirates - Abu Dhabi, Dubai, Sharjah, Ajman, Umm Al-Quwain, and Fujairah, while the seventh emirate, Ras Al Khaimah, joined the federation in 1972. The capital city is Abu Dhabi, located in the largest and wealthiest of the seven emirates.
Since its Federation in 1971, the UAE has developed rapidly and is now noted for its modern infrastructure, international events and status as a trade and transport hub. In 2021, the UAE commemorated its Golden Jubilee, 50 years since federation.
The UAE will host the COP28 international climate summit in Dubai in 2023.

Political overview​

The President of the UAE is His Highness (HH) Sheikh Mohammed bin Zayed Al Nahyan. The Ruler of Dubai, HH Sheikh Mohammed bin Rashid Al Maktoum, is the Vice-President, Prime Minister and Defence Minister.
The UAE's federal structure includes a Supreme Council (comprising the Rulers of each Emirate), a Council of Ministers and Federal National Council. Each Emirate is governed by its own Ruler, with its own local government, courts and police forces.
The Federal National Council comprises 40 members, half of which are appointed and half elected. Elections were last held in October 2019 and for the first time the UAE implemented a requirement for 50 per cent of total members to be women. This requirement saw a significant increase in the number of female candidates. The Federal National Council has an advisory role and is a forum in which concerns of Emiratis are raised.
The UAE is a member of the Gulf Cooperation Council (GCC), the Arab League, the Organization of Islamic Cooperation, the United Nations (including UN Security Council member, 2022-23), the Organization of the Petroleum Exporting Countries, the Non-Aligned Movement and the World Trade Organization. The International Renewable Energy Agency, established in 2009, has its headquarters in Abu Dhabi.
On 15 September 2020, the UAE and Israel signed the Abraham Accords Peace agreement in Washington, DC.

Bilateral relations​

Bilateral relations between Australia and the UAE are friendly, multi-faceted and growing rapidly.

They are underpinned by extensive trade relations, and the UAE is Australia's largest Middle East trade and investment partner.

The two countries enjoy good defence, aviation, security and law enforcement cooperation, the latter underpinned by agreements on mutual legal assistance in criminal law matters and extradition.
Australia was among 192 participating countries at Expo 2020 Dubai, which ran from 1 October 2021 to 31 March 2022.

Expo 2020 provided a key platform for Australian companies to reengage with traditional partners and progress market diversification strategies, including the growth of exports into the Middle East and South Asia.

The Australian Ambassador to the UAE is based at the Australian Embassy in Abu Dhabi. Australia also has a Consulate-General/Trade Commissioner in Dubai.

State government offices representing New South Wales, Queensland, Western Australia, and Victoria are also based in the UAE.

People to people links​

People-to-people contacts have expanded rapidly on the back of the strong growth of direct air links. Prior to the COVID-19 pandemic restrictions, over 100 Emirates and Etihad flights per week operated between the UAE and Australia.

An estimated 15,000 Australians live and work in the UAE.

At the start of 2020, in response the severe Australian bushfire season, the UAE donated fire trucks and generators to several affected communities. On 16 January 2020, the Burj Khalifa, the world's tallest building which is located in Dubai, was lit up with the phrase ‘#mateshelpmates' as a sign of the UAE's support for bushfire response.

Economic overview​

The UAE is the Middle East's third largest economy, and one of the wealthiest countries in the region on a per capita basis. Its GDP in 2021 was estimated at US$410.2 billion, a real GDP growth rate of around 2.2 per cent.

The UAE has six per cent of the world's oil reserves and the seventh largest proven natural gas reserves. Petroleum exports were US$49.6 billion in 2019. In the medium term, oil and gas (which account for over two-thirds of exports and the bulk of government revenue) will continue to underpin the UAE's economy.

However, significant steps towards economic diversification have already been taken, with approximately 70 per cent of GDP now generated by sectors other than oil and gas. To celebrate 50 years of nationhood in 2021, the UAE launched 50 new economic initiatives to boost the country's competitiveness and attract US$150 billion in foreign direct investment over the next nine years.

Abu Dhabi, which has the vast majority of oil and gas reserves in the UAE, has made significant investments in establishing aerospace, nuclear power, defence, information technology (micro-processing), petrochemical and clean-tech industries – the latter most prominently represented by the multibillion-dollar initiative of Masdar City, a zero-carbon city outside Abu Dhabi.

Abu Dhabi is also investing heavily in educational institutions, and cultural and sporting attractions such as the Formula One racing track, Ferrari theme park, and the Louvre Abu Dhabi to diversify the economy away from oil and encourage tourism.

Dubai has also diversified into the exhibitions, events, ICT, re-export and financial sectors. Taking advantage of its position near the head of the Gulf, it has consolidated its historical reputation as a regional entrepôt. Dubai has developed luxury hotels, large port facilities (including Jebel Ali) and a range of free trade zones to attract both manufacturing and services industries.

The UAE population of 10.1 million (2022) depends substantially on its expatriate workforce, which made up about 88 per cent of the population in 2021. The UAE is also opening up utilities to greater private sector involvement. Several free trade zones across the country attract foreign investors, by offering full ownership and zero taxes.

The COVID-19 pandemic has had a significant impact on the UAE's economy, particularly due to the reduction in passenger numbers through air hubs, the reduction in tourist arrivals and the impact of COVID-19 measures on commerce. The UAE is expected to recover to pre-pandemic levels of economic activity over the next three years.

Trade and Investment​

On 17 March 2022, then Minister for Trade, Tourism and Investment Dan Tehan and HE Dr Thani bin Ahmed Al Zeyoudi, Minister of State for Foreign Trade, issued a joint statement announcing Australia and the UAE's intention to pursue a Comprehensive Economic Partnership Agreement (CEPA). DFAT consultations with stakeholders continue, and will inform the possible agreement and the Australian Government's approach to future negotiations.

The United Arab Emirates (UAE) is Australia's largest trade and investment partner in the Middle East. With $5.5 billion in two-way trade in 2021 (over $10 billion pre-COVID), the UAE is Australia's 18th largest export market globally for goods and services.

Exports to the UAE were worth $3.24 billion in 2021 and were dominated by red meat, transport services and machinery and automotive parts.

Australian imports from the UAE were worth $3.24 billion in 2021 (mainly petroleum products).

Services trade is an increasingly important component of the commercial relationship, including construction, financial and professional services, tourism and education. Education is seen as an area of potential growth, with several Australian institutions active in the UAE market, including: Wollongong University, which in 1993 was the first private university to establish a campus in Dubai; Murdoch University, which opened in Dubai in 2007; Curtin University, which opened in Dubai in 2018; the Australian International School Sharjah; the Victorian International School Sharjah; and a number of Australian institutions with partnerships with local institutions to deliver the Australian curriculum in-country.

Australia's commercial profile in the UAE is significant, with UAE-based Australian companies numbering over 300. Australian companies, institutions and capabilities are working in a range of industries, including steel trading, building, construction and financial services, banking services, materials and equipment, agricultural supplies and services, industrial minerals, dairy products, marine manufacturing, education and training services, sports and recreation, health services, livestock, oil field supplies, courier and freight services. Many companies use Dubai as a regional base, in view of its transport, financial and communications infrastructure.

UAE entities hold significant investments in Australia, including in the agribusiness, tourism, health and aged care and resources sectors.
In 2020, UAE investment in Australia was estimated at $11.6 billion according to ABS data.

The Abu Dhabi Investment Authority (ADIA), the world's fourth largest sovereign wealth fund, has invested in ports, the TransGrid electricity network and the Queensland Motorway project.

Other UAE sovereign wealth funds also have assets and are examining other investment opportunities in Australia.

Source : https://www.dfat.gov.au/geo/united-arab-emirates/united-arab-emirates-country-brief
Sawa...

Ni kweli si nchi....

Sasa akina prof.Shivji wanasema ni ya serikali....je ni serikali gani kama si miongoni mwa serikali zilizopo ndani ya UAE?!!!

Hapo ndipo ilipo hoja yangu......
 
Kundi kubwa, ndo maana nimesema walio wengi, na sio wotee.
Nlishaepusha longo longo km hii yako.
Sawa mimi nina longolongo

Kwa kuwa wewe umsomi ninaamini kabisa umefanya tafiti na kugundua kuwa ni "kundi kubwa" linalopinga huu mkataba na DP WORLD....

Karibu Nyamisati......nilikuambia kuhusu yale "mambo ya bahari" unayakumbuka?!!!
 
Yaan Serikali ifanye kuachana na huu mkataba, mbna rahisi tyuh.
Sio rahisi, walishatafuna pesa za watu.
Wabunge wamegharamiwa na DPW bila shaka kwani hapakuwa na tenda iliyotangazwa.

Mkataba huu una malengo mahususi yamejificha na tukiuvunja pia tuna walipa.

DPW ni ukoma akiingia mahali hata bila kufanya lolote ukivunja makubakiano ya awali unamlipa
 
Sio rahisi, walishatafuna pesa za watu.
Wabunge wamegharamiwa na DPW bila shaka kwani hapakuwa na tenda.
Mkataba huu una malengo mahususi yamejificha na tukiuvunja poa tuna walipa.
DPW ni ukoma akiingia mahali hata bila kufanya lolote ukivunja makubakiano ya awali unamlipa
Bora tumlipe then tuwe huru na rasilimali yetu, kuliko yeye aitawale ndo worse zaidi
 
Back
Top Bottom