Kila mtu huitwa kivyake...

Sio lazima wawe pamoja...

Ikumbukwe Kila mtu hapa Duniani anakazi ambayo amepewa na Mungu kufanya.

Ndoa ni mambo ya Duniani tu.
Huyo siyo Mungu wa wa Kristo....
Hizo ni flavour za wasiojielewa.
Mungu ana utaratibu.
 
Hivi wewe unaijua nia na madhumuni ya WAWATA? Mbona mnapayuka msiyo yajua.....

WAWATA ni walezi wa kanisa na mara nyingi wamepewa kazi ya kuwalea vijana wa kiume wenye miito hasa ya upadre ndio maana wana majitoleo mengi kwenye hizi shule za mapadri.

Kwenye kanisa katoliki hamna mwenye kibali cha kuvunja ndoa hayupo si WAWATA, UWAKA au Padri.
Kwani ndoa huwa zinavunjika kwa KIBALI?
 
Technically dini ni Kwa Ajili ya wajinga ila Zina Msaada Kwa Serikali,kuleta utulivu wa jamii na mfumo wa ulaji Kwa wajanja ila Kwa sisi wenye akili tunajua no Utapeli 🤪🤪
Hivi binadamu ambaye mmekutana ukubwani mtakuwaje mwili mmoja sijui, khaa, hii dhana huwa naishangaa kweli. Ila watakuambia ni mambo ya rohoni.
 
"HII NDIO SABABU YA SHUSHO KUMUACHA MUMEWE"

"Kusema ule ukweli mimi niliondoka kwa mume wangu ili nianzishe kanisa langu, nilijiongeza ili ndoto zangu ziweze kutimia maana kama ningeendelea kuungana na mume wangu sehemu moja ningeendelea kudidimia. Siku hizi hakuna mambo ya mke na mume ni mwili mmoja!! hiyo haipo utapotea ndugu yangu, wewe na mume wako au na mke wako hamuwezi kuwa sawa, hiyo haipo kila mtu ana njia zake"

"Na mimi siogopi watu nasema ukweli, haya ninayoyasema ndiyo yapo kichwani kwangu, huyu ndio mimi, kwanini niendelee kudanganya watu. Kwanza mimi licha ya kuwa Mchungaji lakini sipendi watu waniite Mchungaji Christina Shusho, sipendi na sitaki"- Ameyasema Christina Shusho Mwimbaji nguli wa muziki wa Injili.

Una Maoni Gani Kwake...!!

Huyu anamuacha mume akaanzishe “Kanisa lake”, SIYO LA YESU KRISTO. Maana Kanisa la Yesu Kristo linafundisha Injili ya Kristo asemaye: “kwa hiyo mtu atamwacha baba na mama, na kuambatana na mkewe, nao wawili watakuwa mwili mmoja?. Ndiyo maana si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi alichounganisha Mungu mwanadamu asikitenganishe” (Mt 19:5-6). Huyo Shusho anayakana maneno ya Injili ya Bwana. Kanisa lake litafundisha Injili gani? Tamaa ya dunia ni hatari sana. Kuzingatia Injili ya Yesu ati ni kudidimia! Kwake kuikana ndiyo kutamwinua! Anataka kuupata ulimwengu wote kwa hasara ya nafsi yake. Sasa atashangaa kitakachomtokea kwa kumkana Bwana aliye ukweli, njia na uzima. Tumwombee.
 
Ndoa kama wakristo mnavyodai ni muunganiko wa mtu mume na mtu mke ili kuwa mwili mmoja. Hivyo huyo Shusho na mumewe walikuwa mwili mmoja na ndoto zake zilitakiwa ziwe ndio za huo mwili mmoja (ndoa).


Sasa kama ni mkristo anaetambua hilo basi kusema alimuacha mumewe kufukuzia ndoto zake ni utapeli wa hali ya juu huu.

Atupe sababu nyingine. Asitulaghai sisi wenye akili.
Kudanga tu hana jingine, sababu alizotoa ni very cheap.
 
Kipindi yupo na mume wake, mume aliumwa sanaa, watumishi wenzake wakamuombea ikagundulika Christina anataka kumtoa mume wake kafara
Akaulizwa akakana... mume akapona ndoa ikaendelea, alikua ni mwizi kwa mume wake
Ametembea sana na waumini wa kike kanisani kwa mume wake
...🙄🙄🙄....?
 
NGoja Diamond amkamue matako yale Anafikir ni mwenzie yule.
By the way shusho sio mzuri hata. Mtu kaolewa toka 19yrs anapigwa pumbu tu mpaka leo hii kuna kipya gani?

Nb.
Mwanamke hana uwezo wa kui control pesa wale fame. Atakusumbua tu akvipata hivyo vitu
 
Hamna mtu anayeweza muelewa Christina kwakuwa ukiitwa na Mungu Kuna vitu unatakiwa uache ..

Hata wanafunzi wa Yesu waliacha hata kazi wakamfuata Yesu...

Mambo ya Rohoni na mwilini ni tofauti kabisa...
MUNGU hakuwahi kuongea na mwanamke moja kwa moja ni aidha amtumie kama daraja kumfikia mwanaume wake au atamkutanisha na mwanaume kisha kazi iendelee.

Mpangilio ni huu, MUNGU>>>>MWANAUME>>>>> MWANAMKE>>>>>WATOTO.
Ukigeuza tu hiyo flow majanga yanaanza, mara ushoga, mara panya road, mara talaka, mara mauwaji ya wivu wa mapenzi, mara watoto wa nje ya ndoa, mara single mother.

Tuzingatie maagizo ya MUNGU sio maoni ya watu wanaojiita manabii.
 
Back
Top Bottom