China sio nchi iliyoendelea

China sio nchi iliyoendelea

Sasa VoA ni kina nani? hio ni voice of America, hayo ni mawazo yao, Trump mzee wa makavu live amekiri China is developed country, sasa wewe na Trump nani anafahamu siasa za dunia yote hii?
Pinga point, usipinge nani katoa point.

That is ad hominem logical fallacy.

VOA wametoa sources hawajatunga hadithi yao tu.
 
Najua kuna siasa na viongozi wa China wanasema wao ni Develop8ng country kisiasa.

Lakini pia, IMF wanawaiita China developing country kwa viwango vyao vinavyoangalia mambo mengi sana.
Viongozi wa China hata kesho nchi ya 2 duniani kiuchumi, nchi ya 3 kwa nguvu ya jeshi duniani, nchi ya kwanza kwa PPP duniani wakitaka iwe termed ni developed country wanakuwa na hao IMF hawatopinga, ni suala la kimaslahi zaidi kwao kujiita developing country kuliko kumaanisha.

Sasa kama Taiwan ni developed, unajua vitu vingine inabidi ucheke tu,

Sawa mkuu nimekuelewa.
 
Pinga point, usipinge nani katoa point.

That is ad hominem logical fallacy.

VOA wametoa sources hawajatunga hadithi yao tu.
Nimepinga hoja, nauliza wewe unampinga Trump aliyeongoza US for 4yrs akisema China ni developed?
 
Nimeichukia marekani kwenye uzi upi hemu ntajie nione
Ntaisifia ikiwa inastahili kama haistahili siwezi isifia
Haya masuala ya kuabudu china na Americant yamekujaje tena
Uislamu ni kila kitu kijana yaani hakuna kitu utakitaja kisihusiane na uislam kwa namna moja ama nyengine hakuna
Eti uislamu ni kila kitu endelea kujifariji inarusiwa
 
Taja sector kuu za uchumi 10 duniani kisha niambie ktk hizo sector kama China haimo ktk top 3 ya kila sector.

Haya mambo ya developing vs Developed ni terms za kisiasa tu. International politics!

Nakuhakikishia, hakuna kinchi hata kimoja cha Ulaya kinachotia pua kwa China, siyo kiuchumi, Kijeshi, Kisayansi, Kitekinolojia, Kimiundombinu, Kienergy production, Kienergy consumption etc.
 
Najua kuna siasa na viongozi wa China wanasema wao ni Develop8ng country kisiasa.

Lakini pia, IMF wanawaiita China developing country kwa viwango vyao vinavyoangalia mambo mengi sana.
Mkuu IMF mwaka 2018 ilipeleka mapendekezo kwenye shirika la biashara duniani kuwa China iondolewe kwenye nchi inayo endelea iwekwe kwenye kundi la nchi zilizo endelea kwa sababu haina vigezo tena ya kukakaa kwenye kwenye kundi hilo.
Lakini viongozi wa China walicharuka na kupinga kutolewa kwenye nchi zinazo endelea.
Hivyo hiyo hoja yako ya viongozi wa china kufany siasa haina mashiko kwasababu hakuna kiongozi yeyote wa china ambaye alisha simama na kusema China imeendelea, bali viongozi wa China wenyewe ndo wanapinga nchi yao kuitwa nchi iliyo endelea kwa kuofia kupoteza baadhi ya faida za kibiashara na kiuchumi.
 
Taja sector kuu za uchumi 10 duniani kisha niambie ktk hizo sector kama China haimo ktk top 3 ya kila sector.

Haya mambo ya developing vs Developed ni terms za kisiasa tu. International politics!

Nakuhakikishia, hakuna kinchi hata kimoja cha Ulaya kinachotia pua kwa China, siyo kiuchumi, Kijeshi, Kisayansi, Kitekinolojia, Kimiundombinu, Kienergy production, Kienergy consumption etc.
Upo sahihi mkuu.
 
Viongozi wa China hata kesho nchi ya 2 duniani kiuchumi, nchi ya 3 kwa nguvu ya jeshi duniani, nchi ya kwanza kwa PPP duniani wakitaka iwe termed ni developed country wanakuwa na hao IMF hawatopinga, ni suala la kimaslahi zaidi kwao kujiita developing country kuliko kumaanisha.

Sasa kama Taiwan ni developed, unajua vitu vingine inabidi ucheke tu,

Sawa mkuu nimekuelewa.
Why are you rehashing a point that we have no dispute on?

Unajua kujenga hoja logically kwa kuangalia ambapo hatukubaliani na kuacha ambako tunakubaliana, kwa sababu hakuna point ya kuendeleza kusisitiza the political side of this, since it is known and agreed upon?
 
Nimepinga hoja, nauliza wewe unampinga Trump aliyeongoza US for 4yrs akisema China ni developed?
What are you trying to say?

Trump hajambi?

Unataka tumuOngelee Trump badala ya kuOngelea hoja za uchumi?
 
What are you trying to say?

Trump hajambi?

Unataka tumuOngelee Trump badala ya kuOngelea hoja za uchumi?
Inawezekana kwani we ulishakaa nae ukasikia amejamba? hilo ukiniuliza mie sifahamu awe anajamba ama kuharisha ila alishakuwa kiongozi wa US, amekaa white house, anaelewa siasa za dunia hii na anafahamu siri nyingi na mambo mengi, yani akiongea yeye na wewe nitamsikiliza yeye.

Tuandae uzi tuweke mdahalo kwa muda huu uwe unajiandaa kutafuta hoja.
 
China ni developing country, hata ukiangalia IMF standards za kuangalia vigezo, China imewekwa kuwa ni developing country.

GDP per capita ya China bado ni ndogo kuiweka kuwa proper developed country.

China inatisha kwa ukubwa wa uchumi, kitu ambacho ni tofauti na ubora wa uchumi. Mara nyingi watu wanachanganya haya mambo mawili.

Kwenye GDP per capita mwaka 2021, China imepitwa na Seychelles, nchi ya Africa.

GDP per capita 2021 (World Bank figures)

China $ 12,556
Seychelles $ 14,753
Kwenye nchi kumi bora ya nchi zinazo ongoza kwa GDP per capita Kuanzia Marekani na nchi kubwa zote za Ulaya hazimo kwahiyo tuseme hazijaendelea kisa kuzidiwa GDP per capita na akina Qtaar na UAE?

Utajiri una sifa zake na umasikini una sifa zake ,na siku zote mtu kuitwa tajiri sio razima ulingane na tajiri mwingine, huwezi kumuita Mo masikini kisa kazidiwa utajiri na Dangote,huwezi kumuita dangote masikini kisa kazidiwa utajiri na Billeget ,huwezi kumuita Billget kisa kazidiwa utajiri na Aron Musk.
China kwa miundo mbinu aliyo nayo , Teknolojia aliyo nayo,mfumo wa elimu alio nao,huduma za kijamii anazo wapa raia wake na nk... Inatosha kabisa kuwa na sifa za kuwa nchi iliyo endelea tofauti na hapo ni kuendeka ubishi tu.
 
Why are you rehashing a point that we have no dispute on?

Unajua kujenga hoja logically kwa kuangalia ambapo hatukubaliani na kuacha ambako tunakubaliana, kwa sababu hakuna point ya kuendeleza kusisitiza the political side of this, since it is known and agreed upon?
China ni developed country, tuache mbambamba.
 
Mkuu IMF mwaka 2018 ilipeleka mapendekezo kwenye shirika la biashara duniani kuwa China iondolewe kwenye nchi inayo endelea iwekwe kwenye kundi la nchi zilizo endelea kwa sababu haina vigezo tena ya kukakaa kwenye kwenye kundi hilo.
Lakini viongozi wa China walicharuka na kupinga kutolewa kwenye nchi zinazo endelea.
Hivyo hiyo hoja yako ya viongozi wa china kufany siasa haina mashiko kwasababu hakuna kiongozi yeyote wa china ambaye alisha simama na kusema China imeendelea, bali viongozi wa China wenyewe ndo wanapinga nchi yao kuitwa nchi iliyo endelea kwa kuofia kupoteza baadhi ya faida za kibiashara na kiuchumi.
Mimi nakwambia naelewa viongozi wa China wanafanya siasa kulazimisha China kuitwa nchi inayoendelea (but China is developing despite tgat), halafu na wewe unanipa mfano wa kuonesha hilo hilo, kwamba viongozi wa China wanafanya siasa, halafu unaniambia hoja yangu ya kwamba naelewa viongozi wa China wanafanya siasa haina mashiko?

Umeelewa hata hoja yangu ni nini?

Au umefanya assumption ukafanya hesabu za kugawanya kwa zero sehemu bila kujua?
 
Kwenye nchi kumi bora ya nchi zinazo ongoza kwa GDP per capita Kuanzia Marekani na nchi kubwa zote za Ulaya hazimo kwahiyo tuseme hazijaendelea kisa kuzidiwa GDP per capita na akina Qtaar na UAE?

Utajiri una sifa zake na umasikini una sifa zake ,na siku zote mtu kuitwa tajiri sio razima ulingane na tajiri mwingine, huwezi kumuita Mo masikini kisa kazidiwa utajiri na Dangote,huwezi kumuita dangote masikini kisa kazidiwa utajiri na Billeget ,huwezi kumuita Billget kisa kazidiwa utajiri na Aron Musk.
China kwa miundo mbinu aliyo nayo , Teknolojia aliyo nayo,mfumo wa elimu alio nao,huduma za kijamii anazo wapa raia wake na nk... Inatosha kabisa kuwa na sifa za kuwa nchi iliyo endelea tofauti na hapo ni kuendeka ubishi tu.
Hii ndio developing country?
main-qimg-2ba306fd3f0d2e3e1d0bf11a97bcbce2.png
 
Inawezekana kwani we ulishakaa nae ukasikia amejamba? hilo ukiniuliza mie sifahamu awe anajamba ama kuharisha ila alishakuwa kiongozi wa US, amekaa white house, anaelewa siasa za dunia hii na anafahamu siri nyingi na mambo mengi, yani akiongea yeye na wewe nitamsikiliza yeye.

Tuandae uzi tuweke mdahalo kwa muda huu uwe unajiandaa kutafuta hoja.
I will just point out the logical fallacy in this line of argument.

The logical fallacy here is "argument from authority".
 
Kiranga unatumia vigezo gani kusema China bado ni developing country ?
 
Kwenye nchi kumi bora ya nchi zinazo ongoza kwa GDP per capita Kuanzia Marekani na nchi kubwa zote za Ulaya hazimo kwahiyo tuseme hazijaendelea kisa kuzidiwa GDP per capita na akina Qtaar na UAE?

Utajiri una sifa zake na umasikini una sifa zake ,na siku zote mtu kuitwa tajiri sio razima ulingane na tajiri mwingine, huwezi kumuita Mo masikini kisa kazidiwa utajiri na Dangote,huwezi kumuita dangote masikini kisa kazidiwa utajiri na Billeget ,huwezi kumuita Billget kisa kazidiwa utajiri na Aron Musk.
China kwa miundo mbinu aliyo nayo , Teknolojia aliyo nayo,mfumo wa elimu alio nao,huduma za kijamii anazo wapa raia wake na nk... Inatosha kabisa kuwa na sifa za kuwa nchi iliyo endelea tofauti na hapo ni kuendeka ubishi tu.
Kwa nini unaishia kwenye kumi bora? Umepataje standard ya kusema uchukue kumi bora tu, na si 11 au 9 bora?

Hizo metrics ukizotaja China zinawafukia Wachina wangapi na wangapi haziwafikii? Nchi haiwi nchi iliyoendelea kwa kuwa na mifumo mizuri mijini tu au sehemu fulani tu ya nchi. China ni nchi kubwa na ina watu wengi sana masikini, mnaelewa hili?
 
Mimi nakwambia naelewa viongozi wa China wanafanya siasa kulazimisha China kuitwa nchi inayoendelea (but China is developing despite tgat), halafu na wewe unanipa mfano wa kuonesha hilo hilo, kwamba viongozi wa China wanafanya siasa, halafu unaniambia hoja yangu ya kwamba naelewa viongozi wa China wanafanya siasa haina mashiko?

Umeelewa hata hoja yangu ni nini?

Au umefanya assumption ukafanya hesabu za kugawanya kwa zero sehemu bila kujua?
Inapaswaujibu hoja zake, kwa nini viongozi wa China wanakataa nchi hio kuwa kwenye kundi la developed country.
chinae.PNG
 
Back
Top Bottom