Habari ndugu wanaJF,
Jana kwenye mkutano wa rais na wanahabari nilimsikia akiongea confidently kuhusu kuagiza na kuanza kutumia chanjo za covid. Ieleweke kwamba hizo chanjo zilitolewa kwa dharura bila conclusive data za kitafiti na baadhi ya madhara ya muda mfupi yaliyokwishatokea ni kuganda kwa damu (blood clots), kushuka kwa kiwango cha chembechembe nyeupe za damu zinazohusika na kuganda kwa damu 'platelets' na kusababisha tatizo linalojulikana kitaalamu kama 'thrombocytopenia' matatizo ya mzio 'autoimmunity' ambapo chembe chembe za kinga zinashambulia viungo vya mwili na hii ikitokea kwenye viungo muhimu kama figo, ini na ubongo inaweza kupelekea vishindwe kabisa kufanya kazi 'organ failure'.
Hivi karibuni shirika la kuthibiti magonjwa la marekani CDC limeripoti kuongezeka kwa cases zinazoonyesha athari kwenye misuli ya moyo 'myocarditis' na hata kwenye kiwambo kinachozunguka moyo 'pericarditis' kwa vijana na watoto waliochanjwa chanjo ya korona inayotumia teknolojia ya mRNA.
Pia, uchambuzi wa kitaalamu uliotolewa hivi karibuni umeonyesha ndani ya masaa 48 kibebeo cha chanjo inapodungwa mwilini 'lipid nanoparticles' kimeonekana hasa kwenye vifuko vya mayai kwa wanawake 'ovaries' na kwenye uboho wa mifupa 'bone marrow' jambo ambalo siyo la kawaida na linaweza kusababisha shida za uzazi kwa akina mama na matatizo ya kansa za damu 'leukemias' 'lymphomas' na ukizingatia hizi shida za kansa, madhara ya uzazi na hata mzio 'autoimmunity' zinaweza kuchukua muda mrefu hata miaka zaidi ya mitatu kudhihirika.
Je, wataalamu wamemshauri rais kwa kuzingatia utaalamu na up-to-date information zinazotolewa kuhusu madhara ya hizo chanjo? au wameamua tu kutoa ushauri unaoendeshwa na upepo wa ngoma inavyochezwa huko duniani kuhusiana na huu ugonjwa wa covid.
Mimi ningeshauri zitumike zaidi njia za kujikinga badala ya kuhimiza kampeni za chanjo ambayo ipo kwenye utafiti, kwa sababu ukishachanja hakuna namna ya kuondoa hiyo chanjo mwilini, kinachobaki inakuwa ni kupambana na madhara yanayoweza kutokea ndani ya muda mfupi, muda wa kati au muda mrefu.
Nawasilisha.
Jana kwenye mkutano wa rais na wanahabari nilimsikia akiongea confidently kuhusu kuagiza na kuanza kutumia chanjo za covid. Ieleweke kwamba hizo chanjo zilitolewa kwa dharura bila conclusive data za kitafiti na baadhi ya madhara ya muda mfupi yaliyokwishatokea ni kuganda kwa damu (blood clots), kushuka kwa kiwango cha chembechembe nyeupe za damu zinazohusika na kuganda kwa damu 'platelets' na kusababisha tatizo linalojulikana kitaalamu kama 'thrombocytopenia' matatizo ya mzio 'autoimmunity' ambapo chembe chembe za kinga zinashambulia viungo vya mwili na hii ikitokea kwenye viungo muhimu kama figo, ini na ubongo inaweza kupelekea vishindwe kabisa kufanya kazi 'organ failure'.
Hivi karibuni shirika la kuthibiti magonjwa la marekani CDC limeripoti kuongezeka kwa cases zinazoonyesha athari kwenye misuli ya moyo 'myocarditis' na hata kwenye kiwambo kinachozunguka moyo 'pericarditis' kwa vijana na watoto waliochanjwa chanjo ya korona inayotumia teknolojia ya mRNA.
Pia, uchambuzi wa kitaalamu uliotolewa hivi karibuni umeonyesha ndani ya masaa 48 kibebeo cha chanjo inapodungwa mwilini 'lipid nanoparticles' kimeonekana hasa kwenye vifuko vya mayai kwa wanawake 'ovaries' na kwenye uboho wa mifupa 'bone marrow' jambo ambalo siyo la kawaida na linaweza kusababisha shida za uzazi kwa akina mama na matatizo ya kansa za damu 'leukemias' 'lymphomas' na ukizingatia hizi shida za kansa, madhara ya uzazi na hata mzio 'autoimmunity' zinaweza kuchukua muda mrefu hata miaka zaidi ya mitatu kudhihirika.
Je, wataalamu wamemshauri rais kwa kuzingatia utaalamu na up-to-date information zinazotolewa kuhusu madhara ya hizo chanjo? au wameamua tu kutoa ushauri unaoendeshwa na upepo wa ngoma inavyochezwa huko duniani kuhusiana na huu ugonjwa wa covid.
Mimi ningeshauri zitumike zaidi njia za kujikinga badala ya kuhimiza kampeni za chanjo ambayo ipo kwenye utafiti, kwa sababu ukishachanja hakuna namna ya kuondoa hiyo chanjo mwilini, kinachobaki inakuwa ni kupambana na madhara yanayoweza kutokea ndani ya muda mfupi, muda wa kati au muda mrefu.
Nawasilisha.