Miaka miwili ya Rais Samia alifanya maamuzi ya busara kuruhusu chanjo ya UVIKO-19

kalacha mateo

Senior Member
Sep 27, 2021
118
237
Ikiwa ni miaka miwili tangu Rais Samia Suluhu aingie madarakani kuna mengi ameyafanya lakini kuruhusu chanjo ya UVIKO-19 nchini na yeye kuwa wa kwanza kuchoma chanjo mbele ya watanzania wote yalikua ni maamuzi ya busara na ujasiri.

Ilionyesha jinsi gani yeye ni kiongozi kwenye chochote atasimama mbele kwa ajili ya watanzania, lakini pili ni ishara ya kujali watanzania na afya zao. Baada ya Kuruhusiwa kwa chanjo ya UVIKO-19 watanzania waliochanja wakaanza kuruhusiwa kuingia kwenye mataifa mengine na wafanyabiashara kwa kiasi waliweza kurudi kwenye biashara zao.

Kuelekea #MiakaMiwiliYaMama tunajivunia kuwa na kiongozi anaejali wananchi wake.

Fqnt3d_WYAI29zR
 
Kwenye chanjo sijapinga ila sitapiga daima lbd nikifika akhera,wazungu walitengeneza movie chenzi type.
 
Back
Top Bottom