Chama cha conservative cha Cameroon na CHADEMA

Chama cha conservative cha Cameroon na CHADEMA

Wapinge wakati mwaka 2005 na 2010 waliwapa Magari, Pikipiki, Baiskeli, na paunds za kutosha..

Wapinge waone kama mwaka 2015 watapata kitu tena

hii inazidi kunipa wasiwasi na umakini wa viongozi wa cdm.

Hivi kweli tukiwapa nchi si watahalalisha ushoga?. Ilikuwaje wakubali kufadhiliwa na shoga?
 
Hili la ushoga ni cheap political agenda furthered by ****** like membe. Kwanza kajichangaja eti halikuwa limezungumzwa ktk minisiterial levels mara kulikuwa na juhudi za Cameroon kulipenyeza, what's the fuss?

Take it or leave it, PERIOD.

Sawa hapa nyumbani hii ni desturi mpya na of coz mbaya, nakubali. Lakini ukitembea nchi za wenzetu huo kwao ndo utamaduni wao, so what? Twende kwenye hoja za msingi sio cheap and baseless grandios......things like:
- Kwa nini Tz ni maskini licha ya rasimali zote tulizonazo
- Kwa nini Utawala bora ni hadithi tuu, ndio chanzo cha ufisadi, uzembe na kukithiri kwa rushwa
- Iko wapi Katiba Mpya ambayo inatokana na wananchi na yenye kumilikiwa nao?
- Kwa nini vilaza kama Membe, Ngeleja nk ni mawaziri mpaka leo?
- Kwa nini hakuna la maana la kuijuvnia ktk miaka 50 ya uhuru?
nk, nk

Mods: plz do justice by purge this thread.
ukitembea nchi za wenzetu?????unamaanisha nini?hao ni wenzenu ktk lipi?kama binadamu au?kama ni wenzenu fateni na taratibu zao.any way nakukumbusha koma kusema wale ni wenzetu labda kama wewe ni mwenzao.sioni hata 1 la kujifananisha nao.civilized au?
 
Ritz, umewashika magwanda pabaya.

Wakitoa tamko la kupinga alichosema mfadhili wao si watakosa fadhila?
 
Vipi nyie mnaoongwa suti!! hamna hata aibu!! Loh!
 
Nasikitika kwamba baada ya mleta thread kuleta topic ambayo yaonyesha hana uelewa,na baadhi yetu kujaribu kumwelesha sasa yamegeuka malumbano ambayo mtu mweledi huwezi endelea kuchangia.
 
Ritz, umewashika magwanda pabaya.
Wakitoa tamko la kupinga alichosema mfadhili wao si watakosa fadhila?

Hebu muache kudanganya watu kwa sababu hao conservatives ni heri kuliko hao wengine. Imetokea tu kwamba kwa sasa hao ndio wanaongoza serikali lakini ingekuwa wa"liberali" hata wasingewabembeleza. Halafu kuna watu wanataka kutudanganya kwamba kuna sehemu duniani hakuna mambo ya ushoga, loo ! kweli ukipenda chongo utaita kengeza.

Hebu tembeleeni hapa;

ALWAAN - شبكة المثليات العربيات -

Umoja wa Mashoga Uarabuni. Nchi zinazowakilishwa ni Bahrain, Egypt, Iraq, Jordan, Lebanon, Morocco, Saudi Arabia, Syria, Tunisia, and the UAE.
 
Mkuu, fuatilia siasa za Uingereza ndio useme, sera za kukubali mashoga ni sera za Conservative..

Chama cha Labour kinapingana na sera za mashoga..

Hakuna sehemu yoyote kwenye katiba ya Uingereza mashoga wanaruhusiwa




Uingereza haina KATIBA!!
 
JAmani sometimes malumbano kabla ya kuyajengea hoja hayana mantiki kwa taifa.ni bora mtu kufikiri kabla ya kutoa hoja.chadema kama wanafadhiliwa na hao concervative nadhani haina maana kuwa masharti ni lazima kukubali ushoga.hivi kampuni ya bia kudhamini michezo ni lazima wachezaji wawe walevi? na kama ikiw ani lazima kulewa basi na mkataba ufe.the same to politics..sioni jambo gumu katika hili...tuwe wawazi zaidi kusemea hoja...mikataba ya madini inavunjwa hili lisiwezekane kuna nini????????
 
Unataka tamko gani? maana ni kama unamajibu tayari,unategemea CDM na umakini wake wakubali ujinga wa huyu cameron...?
 
JAmani sometimes malumbano kabla ya kuyajengea hoja hayana mantiki kwa taifa.ni bora mtu kufikiri kabla ya kutoa hoja.chadema kama wanafadhiliwa na hao concervative nadhani haina maana kuwa masharti ni lazima kukubali ushoga.hivi kampuni ya bia kudhamini michezo ni lazima wachezaji wawe walevi? na kama ikiw ani lazima kulewa basi na mkataba ufe.the same to politics..sioni jambo gumu katika hili...tuwe wawazi zaidi kusemea hoja...mikataba ya madini inavunjwa hili lisiwezekane kuna nini????????

Mimi ni nachojua serikali iliyoko madarakani inakuwa ina tekeleza 'manifesto' ya Chama killichoshinda uchaguzi mkuu. Hivyo maamuzi ya chama yana athiri moja kwa moja uendeshaji wa serikali husika pamoja na matamko yatolewayo na viongozi wa serikali hiyo. Mimi napata wakati mgumu kujua ni kwa jinsi gani serikali ya Conservative itazitaka serikali za nchi inazozifadhili zikubali "mambo ya kumfedhehesha mwanadamu kwa Mungu muumbaji" wakiti huo huo Chama hicho cha Conservative kilegeze masharti kwa vyama inavyovifadhili katika nchi hizo. Kama chama hicho kitakuwa kinalegeza masharti kwa vyama kinavyofadhili basi wasiwasi wangu utaongezeka juu ya Conservative kuwa kina mpango wa Kuhujumu mageuzi ya kistaarabu ya nchi husika kwa kuvirubuni vyama hivyo(vifadhiliwavyo) vionekane mamluki wake. Hivyo mleta hoja na haki ya kuhoji msimamo wa CHADEMA. Tanzania tunayoitaka ni ile iliyo huru kimaamuzi sio ile itakayokuwa kama ya" Wahuni wa Bengharz" ambayo ilipokea 'peremende' ili kuharibu jamii ya watu wake.
 
Kuna watu humu JF huchangia mada kama watu ambao hawajaenda shule, hii inasikitisha sana ukitilia maanani kwamba JF ni ya GREAT THINKERS. Kwanza kabisa naomba watu waelewe kwamba kufanya vizuri kwa kiongozi wa nchi basi ni kufanya vizuri kwa chama chake kinachoongoza nchi husika. Kumekuwa na malalamiko mengi sasa hivi nchini Uingereza zinazotolewa kwa Waziri Mkuu katika uendeshaji wa nchi na hii ni lawama kwa Conservative. Hata katika nchi ya Tanzania malalamiko yanayotolewa juu ya uendeshaji mbaya wa nchi inakwenda kwa CCM ambacho ni chama tawala.
Ukizungumzia suala la masharti ya misaada linalotolewa na serikali ya Uingereza kwa Tanzania na nyingine za Commonwealth ni lazima wautambue ushoga. Napenda niwaambie wana JF kwamba ni serikali ya Conservative ndio ilnayoshinikiza hili suala wala sio Labour, kwa mantiki hiyo katika suala hili ni chama cha Conservative ndio inayohusika. Tusipende kupindisha ukweli kwa sababu ya mapenzi yetu kisiasa.
Tukija katika hoja ya msingi ni kwamba suala linalozungumzwa linahusiana na misaada inayotolewa na Uingereza ambayo serikali yake inaongozwa na Conservative ambao ni watoaji wa misaada kwa CHADEMA. Hoja husika ina mahusiano na utoaji wa misaada ambayo CHADEMA hupewa na chama cha CONSERVATIVE. Swali ni je CHADEMA msimamo wao ni upi, kwa kuwa wafadhili wao wanaowapa misaada wanataka wautambue USHOGA kisheria? Wataendelea kupokea misaada na kukubali msimamao wa Conservative au watakataa kwa faida ya yao, wafuasi na wanachama wao; na nchi kwa ujumla? Hili sio suala la kuropoka kama alivyoropoka HAKI bin AMANI, Mchaka Mchaka na Chakaza, kuweni makini katika kuzungumzia jambo zito kama hili. Hili jambo linaambatana na DHAMBI KUBWA sana mbele ya siku ya hukumu ya MWENYEZI MUNGU lazima mtambue hilo. Labda watu hawa niliowataja ni sehemu ya wanaotaka kuipeleka nchi katika BALAA hili.

MWENYEZI MUNGU ATUEPUSHIE HILI BALAA NA CHADEMA KUWENI MAKINI KATIKA HILI MSIJE MKALIZALILISHA TAIFA.
 
Hili suala la ushoga naona limeishafika mbali sijui hatima ya nchi yetu na viongozi wetu watalichukuliaje ili kuliokoa taifa
 
@rizt, kwa maana hiyo nyie mko karibu na Labour party au? Kama jibu ndiyo basi tambua kuwa Labour party ndio waliokuwa madarakani wakati sheria inayoruhusu ndio za watu wa jinsia moja kupitishwa. Vyama vyote vikuu Uiengereza vinaunga mkono ushoga!

Wanabodi.

Chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema) kinatakiwa kiweke wazi msamamo kwa watanzania mahusiano yao na chama cha Conservative cha Uingereza..

Conservative ni wadhili wakubwa wa Chadema wanawapa misaada mingi sana Chadema.

Tunakumbuka 2005 na 2010 Chadema walipokea misaada mingi kutoka Conservative, Pikipiki, Magari, Baiskeli, pamoja na pesa..

Waziri mkuu wa Uingereza Davidi Cameron, kutoka chama cha Conservative, alitoa kauli kwenye mkutano wa nchi wanachama wa Jumuia ya Madola (CHOGM) uliofanyika Perth, Australia..

Nchi zinazoomba misaada kwao zitambue haki za mashoga kama moja ya masharti ya kupewa misaada hiyo..

Tunaomba viongozi wa Chadema walitolee maelezo jambo hili sababu kati ya wanaopokea misaada Chadema nao inapokea
 
Hili suala la ushoga naona limeishafika mbali sijui hatima ya nchi yetu na viongozi wetu watalichukuliaje ili kuliokoa taifa

Jambo hili sio la kufanyia masihara, kwa sababu linagusa mishipa ya fahamu ya uhuru na imani za watanzania na utamaduni wao. Hivyo suala hili hili lisiishie kwa CHADEMA na CCM kutoa misimamo yao juu yake bali vyama vyote ambavyo vinatarajia kuchukua uongozi wa nchi hii pamoja na mambo mengine vinatakiwa pia kutoa misimamo yao, ili wananchi tufanye maamuzi.
 
Ritz, kwa nini mwenyekiti wa chama chenu amehongwa suti na mwarabu? Je ndiyo sera ya chama chenu wanaume kuhongwa suti na wanaume wenzao wa kiarabu? Jibu tafadhali.
 
Uingereza haina KATIBA!!

Mkuu, kaa kimya unajiabisha ebu tufahamishe wanaongozwa na nini?

Hivi unajua kuwa Katiba yetu sehemu kubwa kuna vifungu kutoka kwenye katiba ya Uingereza..
Kila pumba pro cdm mnakubaliana kama hii
 
nenda democrat au GOP, nenda labor au conservatives vyote vinakubali na vina wanachama mashoga. Ni namna tu wanavyotaka ku-gain political advantages juu ya ushoga ndipo utaliona. Hivi Membe hajui kuwa ktk masuala ya ushoga Ulaya na Marekani hakuna vyama vyenye itikadi tofauti kimsingi?

Halafu mi sioni tofauti ya dhambi ya uzinifu na ushoga. Kama vile nisivyoona haja ya tofauti kati ya dhambi hizo na uuaji, ubakaji na ufisadi. Hivi hasa Membe na ccm wanataka kusema nini hapa?

Hajui pia ndani ya ccm wapo wanaojiuhusisha na ushoga? Tena viongn
 
Mimi ni nachojua serikali iliyoko madarakani inakuwa ina tekeleza 'manifesto' ya Chama killichoshinda uchaguzi mkuu. Hivyo maamuzi ya chama yana athiri moja kwa moja uendeshaji wa serikali husika pamoja na matamko yatolewayo na viongozi wa serikali hiyo. Mimi napata wakati mgumu kujua ni kwa jinsi gani serikali ya Conservative itazitaka serikali za nchi inazozifadhili zikubali "mambo ya kumfedhehesha mwanadamu kwa Mungu muumbaji" wakiti huo huo Chama hicho cha Conservative kilegeze masharti kwa vyama inavyovifadhili katika nchi hizo. Kama chama hicho kitakuwa kinalegeza masharti kwa vyama kinavyofadhili basi wasiwasi wangu utaongezeka juu ya Conservative kuwa kina mpango wa Kuhujumu mageuzi ya kistaarabu ya nchi husika kwa kuvirubuni vyama hivyo(vifadhiliwavyo) vionekane mamluki wake. Hivyo mleta hoja na haki ya kuhoji msimamo wa CHADEMA. Tanzania tunayoitaka ni ile iliyo huru kimaamuzi sio ile itakayokuwa kama ya" Wahuni wa Bengharz" ambayo ilipokea 'peremende' ili kuharibu jamii ya watu wake.

Mkuu, nashukuru sana kwa mchango wako wenye ujenzi kwa taifa letu..
Nimejifunza kitu kutoka kwako, mungu tuepushe na ushoga!
 
Demokrasia tunayoifikira tunaifuata hapa bado sana, ushabiki wetu wa siasa tunaufananisha kama ushabki wa Simba na Yanga, msimamo uliosemwa na Membe (pamoja na ukigeugeu wake mf. 'nchi haiwezi kuongozwa na DJ akimzungumzia Rajoelina, na waendesha pick ups NTC halafu kesho tunamuona JK akishikana mikono na NTC) ndio msimamo wa nchi, Tanzania ni zaidi ya vyama vya ccm, cuf na cdm, matamko ya vyama hivi kwa namna yoyote ile yanakuwa yanawahusu wananchama wao na si tanzania.

Unapotaka cdm watoe msimamo wao kwa kuwa tu conservative ni washirika wa cdm kwa jambo linalohusu nchi ni HOJA dhaifu sana na isiyo na mashiko yoyote kwa TAIFA Tanzania, nchi yetu ina itikadi zake na moja tu ni kuheshimu UTU wa mtu, watu wote ni sawa, sasa kama utaniambia itikadi na misingi ya Taifa hili inaweza kubomolewa kwa misaada au mapenzi ya vyama, nitakuelewa vinginevyo KIOJA chako kiko sawa sema kimekuja sehemu isyo sahihi.

PM wa UK alikuwa akizilenga NCHI na si vyama, kifupi ilikuwa ni kama anatuambia WATANZANIA wote kuwa kama hatutafanya wanayoona ni sahihi basi MISAADA yao wataipunguza.
Labda cha kujiuliza hapa, kama NCHI Tz, misaaada yao tunastahili kuipokea na je tunaihitaji kweli na kama tunaihitaji kweli ni isaada ya aina gani, je endapo tukiuvunja uhusiano nao kuna kitu gani tutafaidika na wao watapoteza nini.
Imani yangu ni kwa Tanzania nje ya vyama tunavyovishabikia ambavyo bila kujali ni kipi itikadi kwao na menejiment ni tatizo na kwa kuongozwa na watu wa aina hii tuliyonayo (madarakani na wanaosubiri kuingia madarakani) wanaofikiria matumbo na viuno basi si ajabu tukaendelea 'kufanywa' ombaomba na tunaowaamini kutuongoza.
Vyama tulivyonavyo bila kujali urafiki vinavyounda na vyama vya nje hatutakubali kuharibu TANZANIA yetu
 
Back
Top Bottom