Chama cha conservative cha Cameroon na CHADEMA

Chama cha conservative cha Cameroon na CHADEMA

@rizt, kwa maana hiyo nyie mko karibu na Labour party au? Kama jibu ndiyo basi tambua kuwa Labour party ndio waliokuwa madarakani wakati sheria inayoruhusu ndio za watu wa jinsia moja kupitishwa. Vyama vyote vikuu Uiengereza vinaunga mkono ushoga!

Mkuu, JF sio sehemu ya porojo weka ushahidi wa maneno yako tuone wabunge wangapi wa Labour, walipiga kura na wabunge wa ngapi wa Conservative, walipiga kura..
 
Ili suala ni suala zito na nyeti, CDM hawawezi kukwepa kutoa tamko. Bila kujali CDM kuwa wao si serikali kwa sasa lakini conservatives ni maswahiba wa CDM hivyo serikali yao kushinikuza ushoga kunaleta picha kuwa hata vyama wanavyovifadhili navyo vinashinikizwa kukubali sera hiyo.
Kuna uwezekano MOU ya CDM na CONSERVATIVES haijazungumzia suala la sera ya ushoga lakini kwa sasa Conservatives wameweka wazi bila kukubali ushoga kama sehemu ya haki za binadamu upati ufadhili hivyo ni wazi CDM lazima watuambie wanasimamia wapi ktk hili. Serikali imejibu lakini CCM kama chama haijajibu? NCCR hapa ningependa ajibu JAMES MBATIA, ajibu Hoja hii maana chama chao kina shutumiwa sana kwa tatizo hili, kuwa viongozi wao wawili wanahusika na kushiliki ktk ushoga.CUF, TLP na vyama vyote vitoe matamko yao wazi.

Lakini CDM ni lazima wajibu maana wao na CONSERVATIVES ni maswahiba HIVYO UKIMYA WAO unaweza kutufanya tutafsiri tuonavyo sisi kuwa ni sahihi. TSHAVANGIRAI wa ZIMBABWE(upinzani) kaweka wazi wao wanaukubali USHOGA , COMRADE MUGABE(utawala) kasema Piga ua USHOGA aka USENG..., aka UPUNGA NK labda afe ndio utakuwa tambuliwa ZIMBABWE lakini akiwa hai wasahau
 
Demokrasia tunayoifikira tunaifuata hapa bado sana, ushabiki wetu wa siasa tunaufananisha kama ushabki wa Simba na Yanga, msimamo uliosemwa na Membe (pamoja na ukigeugeu wake mf. 'nchi haiwezi kuongozwa na DJ akimzungumzia Rajoelina, na waendesha pick ups NTC halafu kesho tunamuona JK akishikana mikono na NTC) ndio msimamo wa nchi, Tanzania ni zaidi ya vyama vya ccm, cuf na cdm, matamko ya vyama hivi kwa namna yoyote ile yanakuwa yanawahusu wananchama wao na si tanzania.

Unapotaka cdm watoe msimamo wao kwa kuwa tu conservative ni washirika wa cdm kwa jambo linalohusu nchi ni HOJA dhaifu sana na isiyo na mashiko yoyote kwa TAIFA Tanzania, nchi yetu ina itikadi zake na moja tu ni kuheshimu UTU wa mtu, watu wote ni sawa, sasa kama utaniambia itikadi na misingi ya Taifa hili inaweza kubomolewa kwa misaada au mapenzi ya vyama, nitakuelewa vinginevyo KIOJA chako kiko sawa sema kimekuja sehemu isyo sahihi.

PM wa UK alikuwa akizilenga NCHI na si vyama, kifupi ilikuwa ni kama anatuambia WATANZANIA wote kuwa kama hatutafanya wanayoona ni sahihi basi MISAADA yao wataipunguza.
Labda cha kujiuliza hapa, kama NCHI Tz, misaaada yao tunastahili kuipokea na je tunaihitaji kweli na kama tunaihitaji kweli ni isaada ya aina gani, je endapo tukiuvunja uhusiano nao kuna kitu gani tutafaidika na wao watapoteza nini.
Imani yangu ni kwa Tanzania nje ya vyama tunavyovishabikia ambavyo bila kujali ni kipi itikadi kwao na menejiment ni tatizo na kwa kuongozwa na watu wa aina hii tuliyonayo (madarakani na wanaosubiri kuingia madarakani) wanaofikiria matumbo na viuno basi si ajabu tukaendelea 'kufanywa' ombaomba na tunaowaamini kutuongoza.
Vyama tulivyonavyo bila kujali urafiki vinavyounda na vyama vya nje hatutakubali kuharibu TANZANIA yetu

Umezungumza mambo mengi mazuri na yenye mashiko lakini ni vyema tukakubaliana kuwa CDM na CONSERVATIVES ni marafiki, na katika urafiki huo CDM huwa anafadhiliwa na CONSERVATIVES katika kuendesha harakati za kisiasa hapa nchini. Kama huo ndio ukweli CONSERVATIVES kupitia serikali yake imeweka wazi kuwa bila Nchi zetu kukubali haki za binadamu kwa kujumuisha USHOGA kuwa ni sehemu ya haki za binadamu hivyo itambuliwe kisheria ktk nchi zetu wao kama serikali ya Uingereza hawatotoa ufadhili kwa nchi zetu. Kumbuka uhusiano wa CDM na CONSERVATIVE si wa Cameron na Freeman au na Dk Slaa bali ni uhusiano wa vyama hivyo lazma kutakuwa na MOU inayoongoza ushirikiano huo au urafiki huo. Hivyo majibu ya CDM yatatuweka wazi kuhusu kilichomo ktk MOU yao kama inahusisha kutambuliwa kwa USHOGA kama sehemu ya msingi ya haki za binadamu au la. Pili kama ktk MOU hawajazungumzia sera au mambo ya haki za binadamu ni wazi CDM wanapaswa kutueleza nini msimamo wao kuhusu mwenendo wa sasa wa swahiba wao CONSERVATIVES maana kama leo wanazishini kiza nchi kukubali USHOGA ni wazi kesho wataamia kwa vyama wanavyoshirikiana navyo nao watambue ushoga. KUMBUKA kwa sasa hapa DUNIANI hakuna ushirikiano usio na manufaa kwa pande zote mbili. (labda shirikiano zinazoandaliwa na mafisadi wetu wa TZ waitwao na chama chao MAGAMBA) lakini ushirikiano wowote ni lazima unufaishe pande zote kama sio sasa basi baadae, hivyo kama CONSERVATIVES hawanufaiki sasa kwa ushirikiano wao na CDM wanatumaini baadae CDM wakishika DOLA wao lazima watanufaika na opportunity za kiuchumi na kijamii zilizopo TZ hivyo CONSERVATIVES uwasaidia CDM ili wajekushika DOLA ili uhusiano wao ulete faida na kwao pia ktk kushirikishwa ktk shughuli za kiuchumi hapa TZ ambapo watafaidika kutoa ajira kwa wananchi wao, kupata soko la bidhaa zao na kama CDM watakuwa wasaliti kwa nchi yao basi wao CONSERVATIVES wanufaike na Rasilimali zetu.

Hivyo kama ufadhili wao kwa CDM unalengo la kuwasaidia washike DOLA na kwa sasa CDM ni chama MBADALA wa CCM hapa BONGO ni wazi ushirikiano wa CDM na CONSERVATIVES unagusa si maslahi ya wanachama wa CDM bali na WATZ kwa ujumla maana matokeo ya uhusiano wao yakiwa mazuri tutanufaika wote na yakiwa mabaya tutaumia pia bila kujali sisi ni wana CDM au la. Na sharti la kukubali USHOGA lina athiri nchi kwa ujumla si chama pekee hivyo kusema Kuwataka CDM wajibi hatuwatendei haki si kweli. WATOE MAJIBU ILI TUELEWE MSIMAMO WAO JE WANAKUBALI USHOGA AU LA? KAMA WANA UKUBALI KAMA MARAFIKI ZAO CONSERVATIVES WATUAMBIE KAMA HAWAUKUBALI KAMA WATANZANIA WENGI WASIVYO UKUBALI WATUAMBIE. KIUFUPI URAFIKI UNAGHARAMA ZAKE NA UWA HAZIKWEPEKI HIVYO KUTOA MAJIBU NI SEHEMU YA GHARAMA ZA URAFIKI WAO HIVYO NI LAZIMA CDM WALIPE HIYO GHARAMA
 
Mkuu, fuatilia siasa za Uingereza ndio useme, sera za kukubali mashoga ni sera za Conservative..

Chama cha Labour kinapingana na sera za mashoga..

Hakuna sehemu yoyote kwenye katiba ya Uingereza mashoga wanaruhusiwa

Kaka umeshajibiwa vizuri sana lakini inaonekana una asili ya ubishi usio na msingi hata kwa mambo yaliyo wazi. Hapo kwenye red; hivi Cameroon alikuwa anaongea kama kiongozi wa chama chake ama kama Mkuu wa Serikali ya Uingereza? Hivi alikuwa anaongelea sera za chama au sheria za nchi kutambua haki za mashoga? Hebu tumia akili bro.

Well, hebu tuliangalie suala hilo kwa mtazamo tofauti: ANC cha Afrika ya Kusini ni chama rafiki (wa damu, kufa na kuzikana) wa CCM na vyote ni vyama tawala na tena vikiwa na udhibiti wa mabunge ya nchi zao. Miaka michache iliyopita, Afrika Kusini ilitambua na kuingiza katika sheria zao "Haki za Mashoga" likiwa taifa la kwanza na pekee Afrika kufanya hivyo! Mbona hatujasikia CCM ikitangaza kuvunja "urafiki" na ANC? Tafadhali, hebu tumia akili kidogo.

Mimi naamini kabisa, kwa mtiririko wa mambo unavyoenda, CCM (CCM kama taasisi) ndicho chama kitakachoingiza nchi hii katika ushoga na si vinginevyo.
 
Ushoga kwa watu wanaomwamini Mungu na haki za binadamu ni kosa kubwa sana. Hivyo viongozi chadema muwe makini na tamko kuhusu ushoga mkikosea chama kitapoteza wanachama
 
Wanabodi.

Chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema) kinatakiwa kiweke wazi msamamo kwa watanzania mahusiano yao na chama cha Conservative cha Uingereza..

Conservative ni wadhili wakubwa wa Chadema wanawapa misaada mingi sana Chadema.

Tunakumbuka 2005 na 2010 Chadema walipokea misaada mingi kutoka Conservative, Pikipiki, Magari, Baiskeli, pamoja na pesa..

Waziri mkuu wa Uingereza Davidi Cameron, kutoka chama cha Conservative, alitoa kauli kwenye mkutano wa nchi wanachama wa Jumuia ya Madola (CHOGM) uliofanyika Perth, Australia..

Nchi zinazoomba misaada kwao zitambue haki za mashoga kama moja ya masharti ya kupewa misaada hiyo..

Tunaomba viongozi wa Chadema walitolee maelezo jambo hili sababu kati ya wanaopokea misaada Chadema nao inapokea

ubatili mtupu, kwani ni kwa nini jamii yetu inachukia ushoga?-hata mmi nachukia sana tena sana na nikiona shoga au hata nikisikia uwepo wao napata kichefuchefu.
Lakini huwa najiuliza na naomba wan jf tujiulize, hivi ni nini hasa msingi wa sisi kuuchukia ushoga?
Ni mafundisho ya dini zetu? Ni maagizo ya vitabu vyetu vitakatifu?
Kwamba tunaogopa dhambi?
Tunaogopa kumkosea mungu wetu mkuu?
Na ufisadi je?
Uzinzi je?
Uwongo je?
Wizi je?
Udikteta?
Ubinafsi je?
U sisi tu je?

Yeye aliye msafi na awe wa kwanza kurusha jiwe.

Ushoga si haramu zaidi kuliko hayo mengine,
ccm na serikali yake haina haki ya kupinga ushoga kwa nguvu zake zote.

Ukichukia dhambi moja na ukakumbatia zingine inakuwaje?

Nadhani hizo nchi za magharibi zilijiuliza sana maswali haya kabla ya kutoa huo uhuru wa mashoga.

Naomba nieleweke kwamba mimi siungi mkono na wala sitaunga mkono ushoga.

Hivi kwa mfano shoga akikuuliza swali hili, ipi ni haramu zaidi kwa jamii ushoga na uzinzi utajibu vipi?
Ufisadi na ushoga?
Mbona mafisadi na wazinzi serikali zetu zinawapenda?
Jamii zinawafanyia sherehe mafisadi na akina membe hawasemi?

Serikali na wananchi wengi wayatendayo kila siku hayana tofauti na ushoga.
Kwanini mashoga wanyimwe haki wakati mafisadi wananyenyekew na kuheshimiwa?
Ni ubatili mtupu.
 
Mkuu, fuatilia siasa za Uingereza ndio useme, sera za kukubali mashoga ni sera za Conservative..

Chama cha Labour kinapingana na sera za mashoga..

Hakuna sehemu yoyote kwenye katiba ya Uingereza mashoga wanaruhusiwa

Hivi wewe juha unajua unachosema, I guess hujawahi kutoka nje ya Tanzania. Unajua maana ya
conservative? Vyama ambavyo viko pro-homesexual Ulaya na Marekani ni liberal parties hata republican
ya USA, members wake wengi including W Bush ni ma-conservative na wanapinga ushoga.

Cameroon kwenye commonwealth alikuwa anawakilisha Uingereza as head of States na sio chama cha
Conservatives, no wonder alisema NCHI read again NCHI zote ambazo hazitatambua haki ya mashoga
... na sio VYAMA read again vyama.

Eti Katiba ya Uingereza haitambui mashoga, you real look like a laughing stock, mambo ya ushoga sio
Uingerza tu bali Ulaya yote yanatambuliwa na yako kwenye katiba ya nchi hizo. Acha kuonesha upumbavu
wako hapo. Kabebe mabengi ya Nape wakati anapokwenda Ulaya ili ufunguke akili na macho unasumbuliwa
na UPORINI.
 
ubatili mtupu, kwani ni kwa nini jamii yetu inachukia ushoga?-hata mmi nachukia sana tena sana na nikiona shoga au hata nikisikia uwepo wao napata kichefuchefu.
Lakini huwa najiuliza na naomba wan jf tujiulize, hivi ni nini hasa msingi wa sisi kuuchukia ushoga?
Ni mafundisho ya dini zetu? Ni maagizo ya vitabu vyetu vitakatifu?
Kwamba tunaogopa dhambi?
Tunaogopa kumkosea mungu wetu mkuu?
Na ufisadi je?
Uzinzi je?
Uwongo je?
Wizi je?
Udikteta?
Ubinafsi je?
U sisi tu je?

Yeye aliye msafi na awe wa kwanza kurusha jiwe.

Ushoga si haramu zaidi kuliko hayo mengine,
ccm na serikali yake haina haki ya kupinga ushoga kwa nguvu zake zote.

Ukichukia dhambi moja na ukakumbatia zingine inakuwaje?

Nadhani hizo nchi za magharibi zilijiuliza sana maswali haya kabla ya kutoa huo uhuru wa mashoga.

Naomba nieleweke kwamba mimi siungi mkono na wala sitaunga mkono ushoga.

Hivi kwa mfano shoga akikuuliza swali hili, ipi ni haramu zaidi kwa jamii ushoga na uzinzi utajibu vipi?
Ufisadi na ushoga?
Mbona mafisadi na wazinzi serikali zetu zinawapenda?
Jamii zinawafanyia sherehe mafisadi na akina membe hawasemi?

Serikali na wananchi wengi wayatendayo kila siku hayana tofauti na ushoga.
Kwanini mashoga wanyimwe haki wakati mafisadi wananyenyekew na kuheshimiwa?
Ni ubatili mtupu.
Hapa hujanena kitu...okay...chukulia mfano. Una mwanao mpendwa wa kiume, first born. Mara ghafla anaanza mambo ya kishoga, na anakwambia ana mume wake na anataka kuolewa, Kweli kuna dhambi kama hiyo? Ndugu yangu ushoga usikie kwa jirani tu! Ni aibu kubwa sana!
 
Kaka umeshajibiwa vizuri sana lakini inaonekana una asili ya ubishi usio na msingi hata kwa mambo yaliyo wazi. Hapo kwenye red; hivi Cameroon alikuwa anaongea kama kiongozi wa chama chake ama kama Mkuu wa Serikali ya Uingereza? Hivi alikuwa anaongelea sera za chama au sheria za nchi kutambua haki za mashoga? Hebu tumia akili bro.

Well, hebu tuliangalie suala hilo kwa mtazamo tofauti: ANC cha Afrika ya Kusini ni chama rafiki (wa damu, kufa na kuzikana) wa CCM na vyote ni vyama tawala na tena vikiwa na udhibiti wa mabunge ya nchi zao. Miaka michache iliyopita, Afrika Kusini ilitambua na kuingiza katika sheria zao "Haki za Mashoga" likiwa taifa la kwanza na pekee Afrika kufanya hivyo! Mbona hatujasikia CCM ikitangaza kuvunja "urafiki" na ANC? Tafadhali, hebu tumia akili kidogo.

Mimi naamini kabisa, kwa mtiririko wa mambo unavyoenda, CCM (CCM kama taasisi) ndicho chama kitakachoingiza nchi hii katika ushoga na si vinginevyo.

Kaka hakuna ubishi tunawekana sawa tu, labda na mimi nikuulize swali langu..

Hivi hii mikataba serikali inayongia kama mikataba ya madini kule Geita, Kahama, Nyamongo, Nyarugusu, pamoja na kuuza mali za umma. Ubinafsishaji wa makampuni, CCM hawamo wamo?
Nijibu mkuu wangu
 
Kwa ufahamu mdogo nilionao, vyama vikiwa marafiki kabla ya kuingia madaraka, uhusiano unakoma chama kimoja kinapoingia madarakani, kwani vinginevyo mahusiano ya kibalozi lazima yatakuwa na matatizo, sasa hapa chadema wato tamko la nini wakati wao hawapo serikari?

Complitely right,kama conservative wanaiongoza serkali ya UK na bado UK inaipa miasaada serikari ya Tz tunaipokea hapa ni nani wa kujibu Serikali ya CCM au CDM?
 
Cameroun ni PM alitoa kauli ya serikali na siyo chama. Kama sheria hiyo ipo katika katiba yao hata angekuwa wa chama kingine angesema hivyo kukidhi matakwa ya nchi yao.
..........Ndugu yangu umenena uwezo wa wananchi kuelewa ukochini sana tizama sisi tunaodhani twaelewa hatujui tofauti ya chama na serekali MEMBE BENARD hajatoa msimamo wa CCM ametoa msimamo wa serekali DAVID CAMERON ametoa msimamomo UK. haya ya chama ni USHAMBA wetu.
 
Hapa hujanena kitu...okay...chukulia mfano. Una mwanao mpendwa wa kiume, first born. Mara ghafla anaanza mambo ya kishoga, na anakwambia ana mume wake na anataka kuolewa, Kweli kuna dhambi kama hiyo? Ndugu yangu ushoga usikie kwa jirani tu! Ni aibu kubwa sana!

Hapo kwenye red; tunapotea kwa kukosa maarifa. Ukishatamka neno dhambi maana yake unazungumzia masuala ya rohoni na kiroho dhambi zote ni sawa mbele za Mungu. Usitake kupoza UFISADI kwa kutisha watu na USHOGA; tena jana nilionya kwenye thread nyingine kwamba makuwadi wa kisiasa hapa nchini wamepata hoja ya kudandia ili kuwasahaulisha wananchi taabu walizo nazo likiwepo suala la UFISADI, KUTOWAJIBIKA, UPENDELEO serikalini, na mengineyo chungu nzima kwa kushadidia hoja mpya ya ushoga.

Kijamii UFISADI ni mbaya kuliko USHOGA ila kimaadili USHOGA ni mbaya kuliko UFISADI. Kiroho (yaani kidini) UFISADI ni sawa na USHOGA. Natumaini umepata mwanga. Sasa pima mwenyewe unatazama suala lipi kwa "angle" ipi!
 
Kaka hakuna ubishi tunawekana sawa tu, labda na mimi nikuulize swali langu..

Hivi hii mikataba serikali inayongia kama mikataba ya madini kule Geita, Kahama, Nyamongo, Nyarugusu, pamoja na kuuza mali za umma. Ubinafsishaji wa makampuni, CCM hawamo wamo?
Nijibu mkuu wangu

Mkuu unatoka nje ya mada. Mada kuu ni USHOGA. Sasa kuuliza swali au hoja isiyobeba neno kuu la mada nitashindwa kukujibu.
 
..........Ndugu yangu umenena uwezo wa wananchi kuelewa ukochini sana tizama sisi tunaodhani twaelewa hatujui tofauti ya chama na serekali MEMBE BENARD hajatoa msimamo wa CCM ametoa msimamo wa serekali DAVID CAMERON ametoa msimamomo UK. haya ya chama ni USHAMBA wetu.

Mkuu, JF sio sehemu ya porojo Great Thinkers wanataka uweke pandiko kutoka kwenye katiba ya Uingereza inaonyesha hayo maneno yako..

Ushoga upo kwenye katiba ya Uingereza..

Tuwekee mkuu
 
Hivi wewe juha unajua unachosema, I guess hujawahi kutoka nje ya Tanzania. Unajua maana ya
conservative? Vyama ambavyo viko pro-homesexual Ulaya na Marekani ni liberal parties hata republican
ya USA, members wake wengi including W Bush ni ma-conservative na wanapinga ushoga.

Cameroon kwenye commonwealth alikuwa anawakilisha Uingereza as head of States na sio chama cha
Conservatives, no wonder alisema NCHI read again NCHI zote ambazo hazitatambua haki ya mashoga
... na sio VYAMA read again vyama.

Eti Katiba ya Uingereza haitambui mashoga, you real look like a laughing stock, mambo ya ushoga sio
Uingerza tu bali Ulaya yote yanatambuliwa na yako kwenye katiba ya nchi hizo. Acha kuonesha upumbavu
wako hapo. Kabebe mabengi ya Nape wakati anapokwenda Ulaya ili ufunguke akili na macho unasumbuliwa
na UPORINI.

Naona umekuja kwa jazba maneno kibao nani kakuambia katiba ya Uingereza inawatambua mashoga? Usikasirike ukikasirika akili inahama,

Ni kweli sijawahi kutoka nje ya nchi..
Labda na mimi nikuulize wewe kati yako wewe na JK nani katembea sana nje ya nchi? Kwa hiyo JK akikuambia kitu lazima ukubali...duu!

Huyu jamaa ndio debe tupu kabisa mtu hatakae kwenda sana nje ya nchi ndio anamkubali
 
Cameroun ni PM alitoa kauli ya serikali na siyo chama. Kama sheria hiyo ipo katika katiba yao hata angekuwa wa chama kingine angesema hivyo kukidhi matakwa ya nchi yao.

Kweli we haki bin aman. Ile ni kauli ya serikali ya uingereza na sio kauli ya conservative party. Sioni kwa nini CDM watoe maelezo. Membe ameshatoa majibu as muwakilishi wa serikali imetosha. Hakuna mjadala hapa.
 
Hapo kwenye red; tunapotea kwa kukosa maarifa. Ukishatamka neno dhambi maana yake unazungumzia masuala ya rohoni na kiroho dhambi zote ni sawa mbele za Mungu. Usitake kupoza UFISADI kwa kutisha watu na USHOGA; tena jana nilionya kwenye thread nyingine kwamba makuwadi wa kisiasa hapa nchini wamepata hoja ya kudandia ili kuwasahaulisha wananchi taabu walizo nazo likiwepo suala la UFISADI, KUTOWAJIBIKA, UPENDELEO serikalini, na mengineyo chungu nzima kwa kushadidia hoja mpya ya ushoga.

Kijamii UFISADI ni mbaya kuliko USHOGA ila kimaadili USHOGA ni mbaya kuliko UFISADI. Kiroho (yaani kidini)
UFISADI ni sawa na USHOGA. Natumaini umepata mwanga. Sasa pima mwenyewe unatazama suala lipi kwa "angle" ipi!
Hapo kwenye red ..Acha kunidanganya ww, biblia inaniambia mfira.ji na mfirwa.ji hawatauona ufalme wa mbingu!..
Ww unapata wapi ujasiri wa kuona ufisadi na ushoga ni sawa?
 
Cameroon angesema tunazidisha misaada kwa serikali za kifisadi, mngesema kuwa hayo ni matokeo ya utekelezaji wa sera za ccm, lakini kwa kuwa amesema anataka mashoga watambuliwe mnataka msimamo wa chadema. Kwani cameroon alipokuwa anazungumza australia chadema walikuwepo? Unadhani alikuwa hajui kuwa hawapo? Unapotaja kuhusu mou ya chadema na conservative na haki za binadamu je suala la ushoga ni suala la haki za binadamu? Unataka kusema kwa kuwa misikiti yote na makanisa yote yanayopinga ushoga ndo yanapinga suala la haki za binadamu? Tunahusiana katika siasa, dini na kijamii lakini kasoro za serikali na sera za serikali za marekani nauingereza ni tofauti na sera za maadili za chadema, ambazo ni za kiafrika, tena zinazokubalika hata kwa ccm. Kuhusisha chadema na tamko la cameroon ni ujinga
 
Hapo kwenye red ..Acha kunidanganya ww, biblia inaniambia mfira.ji na mfirwa.ji hawatauona ufalme wa mbingu!..
Ww unapata wapi ujasiri wa kuona ufisadi na ushoga ni sawa?

Ila Biblia inasema FISADI atauona ufalme wa Mbinguni! Hii ni dini mpya!!!
 
Back
Top Bottom