Chalz Baba-"Sina Contact na Twanga"

Hivi kumbe kuna watu mpaka leo wanaamini kutokujua kingereza ni ishara ya ujinga! Kweli safari ni ndefu ,watu wanaongea kiswahili lugha waliyozaliwa nayo wanachapia ndio ije kingereza lugha ya kujifunzia ukubwani.Tuache uvivu wa kufikiri.Chalz Baba kipaji chake na kutokujua lugha ya kingereza vinamahusiano gani? Ama mnataka kutuambia akiwa anajua kingereza ndio atakuwa anaimba zaidi kama kina Kofi Olomide ama R.Kelly!?. Wiki 2 zilizopita nilikuwa naangalia mahojiano ya fally Ipupa -BET.Fally aliongea kingereza kibovu sana ,ila hiyo haimpunguzii kipaji chake sababu anajitambua na kujikubali.Hata washabiki wake wana mkubali kwa hicho kingereza chake kibovu.Hao kina Wema mnaowasifia wanajua kingereza kimewapeleka Holiwood? Ama wamepata tunzo za kimataifa kwenye uigizaji/filamu?. Ushabiki wa kimawazo ni mbaya sana na ndio unatufanya tushindwe kuendelea kwa kuwa hatujitambui na kujikubali .Huwezi kajikubali kama hukubali wenzako kwa machache mazuri wanayofanya.Tufunguke tuache ulimbukeni na ufinyu wa mawazo.

Kingereza hakina dili sana ila ni mbaya kutumia lugha ambayo hauijui unaweza kuchanganya watu,hiv anavyosema hana contact(akimaanisha mkataba) kweli yupo sahihi?
 
Bwana Mwakalinga maoni yako yameonyesha ukomavu wa fikra na uelewa wa hali ya juu kwa bahati mbaya sina details zozote kuhusu wewe wala elimu yako ila nimevutiwa sana na ulichokiandika ni kweli kuna watu wenye upeo mdogo wa kufikiri ambao wao kazi yao ni kuangalia makosa ya wenzao kwenye lugha ya kiingereza wakisahau kwamba wao wenyewe wana mapungufu kibao sio kwenye hicho kiingereza tu ambacho ni lugha ya kigeni ila hata kwenye kiswahili lugha yao wenyewe. Hawafahamu kwamba hata wao Waingereza wenyewe wenye lugha yao wanafanya makosa pia itakuwa siye.
Weekend njema.
 
kikaza ndo nini?unamcheka nini wakati we mwenyewe kiazi tu

Dogo naona umeamua kupiga ngumi mkuki mwenyewe... hizo ni spellings tu na sio kama mtu anaeongea lugha kwa kuchapia bikira wewe..
 
hahahahahaha, ya shilole ndo imenimaliza kabisa, kwamba yeye ni 'celebration' bola huyu wa 'contact' huenda alimaanisha mawasiliano na twanga hana, japo na mimi nilimsikiliza alikuwa akimaanisha contract..khe jamani kizungu sio chetu...

bola ndiyo nini? unaonekana na wewe ni kilaza tu. Kila mtu anaweza kukosea na wala siyo suala la kucheka.
 
kikaza ndo nini?unamcheka nini wakati we mwenyewe kiazi tu
Kiazi umempendelea!!Huyo ni Gimbi!!mwenzie kakoxea herufi moja kwa lugha ya kigeni lakini huyo gimbi kakosea herufi moja kwenye lugha yake nani mjinga????
 
Angesema Mkataba na sio Contact... amaaaaa

Na mimi natoa ya kwangu...
To do you do you to say me!... You how?

Maana..
Kufanya ufanye wewe kusema useme mm! wee vipi?
 
Hivi kumbe kuna watu mpaka leo wanaamini kutokujua kingereza ni ishara ya ujinga! Kweli safari ni ndefu ,watu wanaongea kiswahili lugha waliyozaliwa nayo wanachapia ndio ije kingereza lugha ya kujifunzia ukubwani.Tuache uvivu wa kufikiri.Chalz Baba kipaji chake na kutokujua lugha ya kingereza vinamahusiano gani? Ama mnataka kutuambia akiwa anajua kingereza ndio atakuwa anaimba zaidi kama kina Kofi Olomide ama R.Kelly!?. Wiki 2 zilizopita nilikuwa naangalia mahojiano ya fally Ipupa -BET.Fally aliongea kingereza kibovu sana ,ila hiyo haimpunguzii kipaji chake sababu anajitambua na kujikubali.Hata washabiki wake wana mkubali kwa hicho kingereza chake kibovu.Hao kina Wema mnaowasifia wanajua kingereza kimewapeleka Holiwood? Ama wamepata tunzo za kimataifa kwenye uigizaji/filamu?. Ushabiki wa kimawazo ni mbaya sana na ndio unatufanya tushindwe kuendelea kwa kuwa hatujitambui na kujikubali .Huwezi kajikubali kama hukubali wenzako kwa machache mazuri wanayofanya.Tufunguke tuache ulimbukeni na ufinyu wa mawazo.

Nadhani wanakosolewa kwa kuchomekea maneno ya kimombo wasichokijua.
 
Kiazi umempendelea!!Huyo ni Gimbi!!mwenzie kakoxea herufi moja kwa lugha ya kigeni lakini huyo gimbi kakosea herufi moja kwenye lugha yake nani mjinga????

Na wewe hiyo nil lugha ya kwenu kamachumu ?? Kimba wewe... utashikishwa ukuta kwa kujifanya unajua sana mjini hapa...
 
akihojiwa na vyombo vya habari mwanamuziki charles gabriel akisema sina contact na twanga (akimaanisha contract) ndio maana naamua kuondoka.......alirudia neneo hilo mara 3 bila kujistukia kwamba anachapia au huenda hajui kabisa

hhahahhahah,nilicheka sana jana wakati namsikia akiwa anarudiarudia na kusisitiza neno hilo "contact" instead of "contract" tatizo la wasnii wetu wa bongo hawataki kusoma wnaishia kuuza sura tu ndo maana hawajui hata haki zao yaani muda wote aliopo kwa ktk tasnia ya muziki ameshindwa kujua kuwa mkataba unaitwa contract
 
Kingereza hakina dili sana ila ni mbaya kutumia lugha ambayo hauijui unaweza kuchanganya watu,hiv anavyosema hana contact(akimaanisha mkataba) kweli yupo sahihi?

You are very right...mahojiano ya kiswahili "contact" a.k.a mkataba wa nn?????
 
hahahahahaha, ya shilole ndo imenimaliza kabisa, kwamba yeye ni 'celebration' bola huyu wa 'contact' huenda alimaanisha mawasiliano na twanga hana, japo na mimi nilimsikiliza alikuwa akimaanisha contract..khe jamani kizungu sio chetu...
...Na kama kweli Twanga watamshitaki kwa kukanusha kwamba hana Contract yeye anaweza kukomaa kwa kutumia tape kama secondary evidence na kugeuza kibao kwa kudai alisema hana contact na si contract
 
Kiingereza ongea na mwingereza anaetafuta ujumbe,sio mswahili anaetafuta makosa....
 
Back
Top Bottom