King Kong III
JF-Expert Member
- Oct 15, 2010
- 51,603
- 68,509
Hivi kumbe kuna watu mpaka leo wanaamini kutokujua kingereza ni ishara ya ujinga! Kweli safari ni ndefu ,watu wanaongea kiswahili lugha waliyozaliwa nayo wanachapia ndio ije kingereza lugha ya kujifunzia ukubwani.Tuache uvivu wa kufikiri.Chalz Baba kipaji chake na kutokujua lugha ya kingereza vinamahusiano gani? Ama mnataka kutuambia akiwa anajua kingereza ndio atakuwa anaimba zaidi kama kina Kofi Olomide ama R.Kelly!?. Wiki 2 zilizopita nilikuwa naangalia mahojiano ya fally Ipupa -BET.Fally aliongea kingereza kibovu sana ,ila hiyo haimpunguzii kipaji chake sababu anajitambua na kujikubali.Hata washabiki wake wana mkubali kwa hicho kingereza chake kibovu.Hao kina Wema mnaowasifia wanajua kingereza kimewapeleka Holiwood? Ama wamepata tunzo za kimataifa kwenye uigizaji/filamu?. Ushabiki wa kimawazo ni mbaya sana na ndio unatufanya tushindwe kuendelea kwa kuwa hatujitambui na kujikubali .Huwezi kajikubali kama hukubali wenzako kwa machache mazuri wanayofanya.Tufunguke tuache ulimbukeni na ufinyu wa mawazo.
Kingereza hakina dili sana ila ni mbaya kutumia lugha ambayo hauijui unaweza kuchanganya watu,hiv anavyosema hana contact(akimaanisha mkataba) kweli yupo sahihi?