Chalinze: Mabosi watatu wa Tanzania Investment Centre, wafariki ajalini

Tanzania hatuelewi tofauti ya ajari na crush nyingi ni crush na si ajari
ajari hutokea pale ambapo dereva nina maana dereva aliyesomea udereva na sio kuchukua gari nyumbani na kuliendesha amechukua tahadhali zoote za barabarani na kufuata sheria lkn bado ikatokea hiyo senerio hii ni ajari.
Tofauti na hayo itakuwa crush

Sure na hapo ndipo ule msemo wa "Ajali haina kinga" ndio unapaswa ku-apply. Kuna mahali niliwahi kusema ajali nyingi Tanzania kwa maana halisi ya accident si ajali ila ni uzembe bahati mbaya sikueleweka. Matokeo ya uzembe wa wazi wazi hatupaswi kuita ajali ninakubaliana na wewe 100 kwa 100 .
 
CHAL/TR/AR/11/2018 ILANI YA KWANZA:KOSA AJALI YA MAGARI MAWILI KUGONGANA NA KUSABABISHA VIFO,MAJERUHI NA UHALIBIFU WA MAGARI HAYO: Mnamo tarehe 21/05/2018 majira ya saa 15:30hrs huko maeneo ya kijiji cha Msoga-chalinze ,barabara ya Msoga/Msolwa wilaya ya kipolisi Chalinze Mkoa wa Pwani, gari no STK.5923 aina TOYOTA LANDCRUISER mali ya Wizara ya viwanda,biashara na uwekezaji ikiendeshwa na dereva aitwae PRISCUS s/o PETER,23yrs,mchaga,mkristo,mkazi wa Dsm, aligongana na gari no. T. 620AQV/ T.407DBY aina ya SCANIA ikiendeshwa na dereva asiyefahamika jina, jinsia ya kiume kwani alitoroka mara tu baada ya ajali
na kusababisha vifo vya watu wawili ambao ni MARTIN s/o LAURENCE@ MASALU,39yrs,msukuma,manajor wa kanda,mkazi wa Dsm na ZACHARIA s/o NALIGIA@ KINGU,49yrs,mnyiramba,mkazi wa Dsm

Poleni sana TIC na familia za Marehemu.Kuna taarifa zinasema waliofariki ni watatu.Kuna jina jingine siwezi kulitaja hapa wanadai naye kafariki (nimeambiwa na mtu wa karibu na TIC).Kuna haja ya kurudi kwenye mfumo wa zamani wa UMRI wa kazi ya udereva.
 
Gari la serikali mwendo wa serikali moto bati likitokea la kutokea eti wanasema AJALI HAINA KINGA nyoooo Angeendesha spidi ya 80 yote haya yasingetokea. TUSIMLAUMU SHETANI WAKATI UJINGA TWAFANYA SIE.......
Upo sawa. Spidi yote hiyo kuwahi vikao Dodoma. Pengine ni vyema ofisi na watendaji wote Wakuu kuhamishiwa huko Dodoma na hivyo kupunguza safari hizi za mwendokasi za kuwahi kufika huko na pengine hata usifike kama ilivyotokea kwa hawa wenzetu. RIP.
 
poleni wafiwa japo hapo inaonekana kua tatizo la safety,hizo v8 ukifunga mkanda na maputo hayo pengine wangejeruhiwa tu kama alivyojeruhiwa dereva
 
Tanzania hatuelewi tofauti ya ajari na crush nyingi ni crush na si ajari
ajari hutokea pale ambapo dereva nina maana dereva aliyesomea udereva na sio kuchukua gari nyumbani na kuliendesha amechukua tahadhali zoote za barabarani na kufuata sheria lkn bado ikatokea hiyo senerio hii ni ajari.
Tofauti na hayo itakuwa crush
Ajari - Ajali
 
Kwakweli nimeshitushwa na umri wa huyo Dereva, miaka 23 hata kama alipata leseni na miaka 16 bado ana uzoefu mdogo sana kuendesha viongozi. Atleast watu wakuanzia 35 to 45 wanafaa hizo kazi. Kwanza kichwa kimetulia show za kijinga hakuna, unampa miaka 23 VX V8 kamuaga demu wake na masela kuwa nipeni masaa matano nitakuwa Dodoma.

Dah walale kwa amani. Ila hizi gari nazo zinajifanyaga zenyewe ndio king of Roads, kwenye 50 kph wao wapo 170kph, wanaona baby walker kama kobe wana overtake gari hadi nane, wataacha kuua kweli? Serikali inapaswa kuliangalia hili juzi tu wabunge wa Zanzibar wamenusurika.
 
Kwakweli nimeshitushwa na umri wa huyo Dereva, miaka 23 hata kama alipata leseni na miaka 16 bado ana uzoefu mdogo sana kuendesha viongozi. Atleast watu wakuanzia 35 to 45 wanafaa hizo kazi. Kwanza kichwa kimetulia show za kijinga hakuna, unampa miaka 23 VX V8 kamuaga demu wake na masela kuwa nipeni masaa matano nitakuwa Dodoma.

Dah walale kwa amani. Ila hizi gari nazo zinajifanyaga zenyewe ndio king of Roads, kwenye 50 kph wao wapo 170kph, wanaona baby walker kama kobe wana overtake gari hadi nane, wataacha kuua kweli? Serikali inapaswa kuliangalia hili juzi tu wabunge wa Zanzibar wamenusurika.
Neno
 
MABOSI WANAOENDESHWA KWENYE HAYO MA V8 MARA NYINGI HAWAVAAGI MKANDA....
GARI ZAO ZINAKWENDA MWENDOKASI PIA...
VIFOO VINGINE TUNAJITAKIA

OVA
 
duh poleni wafiwa!
ajali haina kinga ila kuna vitu bado vinatia ukakasi...
trafiki polisi aliyepitisha hiyo Leseni class C kwa kijana wa miaka 23 awe mtuhumiwa wa kwanza,mimi najua class c hutolewa kwa dereva mwenye 24 kuendelea WITH 6 years experience in driving awe amaepitia NIT au VETA
LESENI zinatolewa kama njugu mjini mamalaka husika zipo tu
 
Back
Top Bottom