Chalinze: Mabosi watatu wa Tanzania Investment Centre, wafariki ajalini

View attachment 783211 View attachment 783214 View attachment 783211 View attachment 783214
Habari za usiku wadau kuna ajali mbaya iliyotokea leo usiku maeneo ya Chalinze na kugharimu maisha ya Mabosi watatu wa TANZANIA INVESTMENT CENTRE.

Mabosi hao walikuwa wanaelekea Dodoma kwenye mkutano/Kikao muhimu kilichokua kifanyike Kesho Jijini Dodoma.

Waliofariki ni Saidi Amiri Moshi (Kaimu Mkurugenzi wa Research zamani Corporate Affairs), Zacharia Kingu (Kaimu Mkurugenzi wa Corporate Affairs zamani Investment Promotion) na Martin Masalu (Meneja Research).

Waliopata majeraha ni wawili yaani Godfrey Kilolo (Meneja wa Sheria) na dereva wa gari hilo aliyejulikana kwa jina moja tu la Priscus.

Mwenyezi Mungu aziweke roho za Marehemu mahali pema peponi na awaponye majeruhi wa ajali hii mbaya.
Tatizo unakuta watu wote wako dar wanafanya safari kwenda kufanya kikao dodoma ili kuwafurahisha walevi wa udodoma, hizi ajali zitakuwa nyingi tu kwa ujinga huu
 
Kuna mwendo ukipiga mzinga airbags hazikusaidii chochote. Hakuna ajali mbaya kama head-on collision nakushauri epuka head-on siku zote.
Wangepiga head-on hapo asingetoka mtu. Hapo ni wazi wamepona waliokaa kulia.

Mkuu hujui unachosema. Kuumia hivyo kwa V8 kwa sisi tunaozitumia ni kuwa driver baada ya kulikoroga akaamua kuipitisha kando kuwa spidi ili ipigwe ubavuni upande usio wake. Asingepindisha maana yake ingekuwa head-on collision. V8 zina break nzuri sana. Gari inasimama instantly. Labda itaseleleka tu. Hivyo impact ya head-on collision inakuwa ndogo, airbags zinafunguka, na abiria wataathirika kidogo. Kama ulikuwa hujui hili angalia ajali zote za V8 zilizopigwa mbele kisha njoo tena hapa utoe ushuhuda.
 
Mkuu hujui unachosema. Kuumia hivyo kwa V8 kwa sisi tunaozitumia ni kuwa driver baada ya kulikoroga akaamua kuipitisha kando kuwa spidi ili ipigwe ubavuni upande usio wake. Asingepindisha maana yake ingekuwa head-on collision. V8 zina break nzuri sana. Gari inasimama instantly. Labda itaseleleka tu. Hivyo impact ya head-on collision inakuwa ndogo, airbags zinafunguka, na abiria wataathirika kidogo. Kama ulikuwa hujui hili angalia ajali zote za V8 zilizopigwa mbele kisha njoo tena hapa utoe ushuhuda.
Haya mkuu, endelea na ujuaji wako. Ila nikwambie kitu kimoja Land Cruiser is just another Toyota. Tafakari.
 
Mkuu hujui unachosema. Kuumia hivyo kwa V8 kwa sisi tunaozitumia ni kuwa driver baada ya kulikoroga akaamua kuipitisha kando kuwa spidi ili ipigwe ubavuni upande usio wake. Asingepindisha maana yake ingekuwa head-on collision. V8 zina break nzuri sana. Gari inasimama instantly. Labda itaseleleka tu. Hivyo impact ya head-on collision inakuwa ndogo, airbags zinafunguka, na abiria wataathirika kidogo. Kama ulikuwa hujui hili angalia ajali zote za V8 zilizopigwa mbele kisha njoo tena hapa utoe ushuhuda.
head on collision ukutane na gari kubwa lory au bus ina maana engine yote inakuja kwenye dashboard hapo airbag inazidiwa!!
break ni sawa V8 ipo vuzur je vip kwa gari itayogongana nayo kama ilifail break?
 
Barabara ya Dar - Chalinze... hasa karibu na Chalinze ina corrugations & mawimbi mno mnooo dereva inafaa ajue vema barabara hiyo. Ni hatari sana kuendesha speed ktk hiyo road.
 
Kwakweli nimeshitushwa na umri wa huyo Dereva, miaka 23 hata kama alipata leseni na miaka 16 bado ana uzoefu mdogo sana kuendesha viongozi. Atleast watu wakuanzia 35 to 45 wanafaa hizo kazi. Kwanza kichwa kimetulia show za kijinga hakuna, unampa miaka 23 VX V8 kamuaga demu wake na masela kuwa nipeni masaa matano nitakuwa Dodoma.

Dah walale kwa amani. Ila hizi gari nazo zinajifanyaga zenyewe ndio king of Roads, kwenye 50 kph wao wapo 170kph, wanaona baby walker kama kobe wana overtake gari hadi nane, wataacha kuua kweli? Serikali inapaswa kuliangalia hili juzi tu wabunge wa Zanzibar wamenusurika.
akifika chalinze anatext chalinze hapa akifika moro utasikia Moro hiyo!
Masela wanampa nusu saa aingie Gairo wakati ni mwendo wa saa 1 na n usu au saa2
unategemea nn?
 
head on collision ukutane na gari kubwa lory au bus ina maana engine yote inakuja kwenye dashboard hapo airbag inazidiwa!!
break ni sawa V8 ipo vuzur je vip kwa gari itayogongana nayo kama ilifail break?
Huyo jamaa anaona wenzie hawajui kitu yeye ndio anajua kwa sababu 'anatumia' hizo gari.
 
Hili nalo ni msingi kuzingatia. Niliwahi kuongea na dereva wa DC flani, yaani madereva wanachukuliwa kama mashine.

Saa 11 anafata gari, kutwa anampeleka bosi huku na kule afu ghafla jioni anaambiwa fata mizigo yako twende safari.
kuna shida hapo!! dereva kupumzika ni majaliwa!
 
Mmewaondoa madereva wazoefu na makini eti tu sababu hawana cheti cha Form IV. Hayo ndiyo matokeo ya kuajiri vijana wa Form IV. Hana uzoefu, alikuwa amezoea kumuendesha mzazi wake kutoka Kimara kwenda mjini basi. Leo unampa V8 aende Dodoma. Wengi sana walioajiriwa baada ya kufukuza wazoefu ni majanga matupu.
Uko sahihi kabisa! Umri wa dereva unaonyesha kijana hakuwa na ukomavu katika udereva. Ni ajali ya kilimbukeni kutaka kuonyesha kuwa anaendesha V8
 
When will the job vacancy announced. Coz am sure now the vacancies are open
Kiongozi sikufahamu ila unisamehe kidogo nikuambie hili.

Ni upuuzi kuleta mizaha ya namna hii wakati watu wana uchungu na msiba. Wengine wamepoteza ndugu, wengine waume zao, marafiki, classmates na hata wafanyakazi wenzao waliowapenda sana.

Usingojee msiba ukuguse wewe binafsi ndipo uhisi uchungu wa msiba.

Take it or leave it; the choice is yours!
 
Magari ya serikali barabarni ni wafalme wao tochi huwa haziwahusu. Madereva darasa la saba wametolewa kwenye ajira kisa ni std 7, unampa v8 mtu ana miaka 23, huyo NIT kaenda lini? Anyways RIP marehemu na poleni wote mlioguswa na msiba huu
 
Back
Top Bottom