Zack Abdul
JF-Expert Member
- Mar 9, 2026
- 753
- 674
Anaandika Mwandishi wa Habari Mwandamizi, Mkazi wa Jijini Mwanza Alloyce Nyanda (Mtozi), akionesha kuunga mkono chapisho la Msanii wa Muziki wa 'HipHop' Nchini, anayeishi Nchini Marekani kwa sasa Roma Mkatoliki (ambalo tumeweka kwenye post iliyopita):
"Ukisoma andiko la Roma, kama utataka kulichambua linaweza kuwa na swali moja kuu je, kinachowafanya CHADEMA mpaka sasa hawajaenda kuhani Kizimkazi ni kipi?"
"Roma anasema kwenye agenda kuu za CHADEMA ndipo kuna tricky kubwa kwamba ukimpinga mtu kwa jambo fulani, basi na wewe unatakiwa usiwe mtu wa kufanya jambo hilohilo"
"Roma anasema wananchi wanapaswa kuelewa kwamba 'CHADEMA wakishika Dola, hawatafanya haya na yale wanayofanya hawa Watawala', Hatutaua (kwahiyo inabidi wasiue hata sasa na wao CHADEMA), Hatutaiba (kwahiyo inabidi wasiibe hata sasa, yaani CHADEMA wasiwe wezi), Hatutafurahia kuona Binadamu amekufa au ameuliwa hata akiwa ni adui (na inabidi waanze kuonyesha hilo sasa), Adui akifa au akifiwa tutaenda kuzika na tutaenda kuhani msibani (Hata sasa CHADEMA waonyeshe hili)..."
"Ukiniuliza hata Mimi Mtozi naweza kuweka swali langu kuu, 'Kipi kinawafanya CHADEMA mpaka sasa hawajaenda kuhani kwa Ndugu Samia wakati amefiwa na Mume wake Hafidh Ameir Hassan?, msiba huo ulitokea Septemba 07.2026...
Je, ni visasi?, na kama ni visasi juu ya nani?, na wakipewa Dola watawalipisha wangapi?
Na kwenye agenda za CHADEMA kuna eneo la visasi?, Kwa sababu kama wanataka wananchi waamini kwamba kesho wakipewa Dola watakuwa tofauti na wale wanaowakosoa leo, basi tofauti hiyo inapaswa kuonekana kabla hawajapewa Dola, hapo ndipo credibility ya agenda yao inapopimwa" -Nyanda
"Ukisoma andiko la Roma, kama utataka kulichambua linaweza kuwa na swali moja kuu je, kinachowafanya CHADEMA mpaka sasa hawajaenda kuhani Kizimkazi ni kipi?"
"Roma anasema kwenye agenda kuu za CHADEMA ndipo kuna tricky kubwa kwamba ukimpinga mtu kwa jambo fulani, basi na wewe unatakiwa usiwe mtu wa kufanya jambo hilohilo"
"Roma anasema wananchi wanapaswa kuelewa kwamba 'CHADEMA wakishika Dola, hawatafanya haya na yale wanayofanya hawa Watawala', Hatutaua (kwahiyo inabidi wasiue hata sasa na wao CHADEMA), Hatutaiba (kwahiyo inabidi wasiibe hata sasa, yaani CHADEMA wasiwe wezi), Hatutafurahia kuona Binadamu amekufa au ameuliwa hata akiwa ni adui (na inabidi waanze kuonyesha hilo sasa), Adui akifa au akifiwa tutaenda kuzika na tutaenda kuhani msibani (Hata sasa CHADEMA waonyeshe hili)..."
"Ukiniuliza hata Mimi Mtozi naweza kuweka swali langu kuu, 'Kipi kinawafanya CHADEMA mpaka sasa hawajaenda kuhani kwa Ndugu Samia wakati amefiwa na Mume wake Hafidh Ameir Hassan?, msiba huo ulitokea Septemba 07.2026...
Je, ni visasi?, na kama ni visasi juu ya nani?, na wakipewa Dola watawalipisha wangapi?
Na kwenye agenda za CHADEMA kuna eneo la visasi?, Kwa sababu kama wanataka wananchi waamini kwamba kesho wakipewa Dola watakuwa tofauti na wale wanaowakosoa leo, basi tofauti hiyo inapaswa kuonekana kabla hawajapewa Dola, hapo ndipo credibility ya agenda yao inapopimwa" -Nyanda