CHADEMA, uislam na waislam!

CHADEMA, uislam na waislam!

Status
Not open for further replies.
Ndg zangu waislam, islam nduguye islam chadema ni adui mkubwa wa islam tanzania kumbuka walivyo mtendea dada yetu kule igunga walimnyanyasa sana walimfedhehesha sana lakini hawakuomba msamaha hivyo nakuombeni wewe uliye mwislam adui ya mwislam ni adui ya waislam wote.

hivi mkubwa unakumbuka uamuzi wa mahakama ullisema vipi kuhusu hili shauri au umekurupuka tu?
 
Kampeni za wazi za kuwafanya waislamu wachukie chadema kama hizi:

attachment.php
 
Hata mimi bado naamini kwamba CUF ni cha waislam maana mpaka sasa hawajatuambia kilichomfukuzisha uongozi na uanachama bwana Mapalala, Lwakatare sijaona wa dini nyingine wakiondolewa uanachama bila kutolewa sababu kwa umma. Nitaamini vinginevyo kama CUF watakuwa wawazi kuhusu haya, lakini pia ndo chama cha kwanza kupigiwa debe katika nyumba za ibada hasa misikitini mfumo wa vyama vingi ulipoanza nchini bila kukemewa na viongozi wa chama husika sasa kwa nini tusiamini ni chama kwa ajili ya waislam na wa dini nyingine waliopo huko ni wasindikizaji?

Hapa na mimi naweza kusaidia,issue ya mapalala pia imemkumba muasisi mungine hivi majuzi,nadhani kama utakumbuka utaona ya kwamba Hamad Rashid mtu mkubwa na muhimu kabisa cuf nae yalimkuta yalimkua mapalala,hayo ni mambo ya kawaida sana kwenye vyama vyetu hivi vya kiafrika,wakubwa mara nyingi hawapendi mtu mwenye mawazo mbadala,anakua adui,ni kama issue ya kafulila na kina mbatia pale nccr,chacha wangwe na mbowe pale chadema,zitto na wakubwa zake japo zitto kidogo ameonyesha kuwa ngangari ndani ya chama,yah kiufupi ni mambo ya kawaida tu katika siasa zetu hayana uhusiano na dini.

kuhusu cuf na siasa za misikitini,hayo mara nyingi nadhani yanakua ni mapenzi ya viongozi wa dini wenuewe wala sidhani kama huwa wanatumwa na mtu,hutokezea tu wakijifeel wako connected zaidi na chama fulani basi huzitumia madhabahu za kidini kufanya siasa binafsi,na hili ni kwa pande zote,hizi kelele unazozisikia sasa toka kwa waislam dhidi ya chadema na mfumo kristo kama wanavyopenda kuita wenyewe ni kutokana na baadhi sio wote ya viongozi wa kikristo kurudia mchezo ule ule uliokua ukifanywa na baadhi ya masheikh in favour of cuf,yapo makanisa wala sio siri yalikua yakiwaelekeza waumini wake wakipigie kura chadema,lakini kama nilivyosema hayo yote yanatokana na mapenzi binafsi ya kiongozi wa dini husika ambae huamua kutumia joho lake la dini kuwaburuza kondoo wake,kama mtakumbuka mzee mkapa akizindua ama kufunga kampeni za ccm pale jangwani sikumbuki sawasawa aliwakemea baadhi ya viongozi hao wa kikristo kwa kuwataka kama wanapenda siasa wavue majoho ya dini zao kwanza then waje wapambane kwenye majukwaa ya kisiasa badala ya kufanya siasa za madhabahuni
 
Wewe utashi wako uko vipi katika hili?

aah mi najaribu kuwa fair tu kwa kuwa ndio nimeanzisha mjadala wa kitaifa kwa ajili ya kupata suluhu baina ya chadema kama chama cha siasa na waislam,sasa siwezi kuwa refa na mchezaji mimi mwenyewe kaka ndio mana unaona naingia kila upande na kutoka leo,kitu ambacho sio kawaida yangu kwa wanaonifahamu jinsi ninavyokuaga kwa chadema,ccm na uislam
 
Nimewakejeli waislam wapi? Mkuu hizo ni propaganda mnazotumia nyinyi CCM nafikiri umeona ofisi zenu zinavyochomwa huko kusini lakini za CUF na CHADEMA hazijaguswa watu wameshawashtukia

Je wale mapadre wa Sumbawanga waliokuwa wakifukuza waumini wanaoishabikia CCM ni maajenti wa CCM? Mbona Chadema haikutoa tamko kukanusha hilo. Huku kwetu Musoma kila Jumapili ukienda Kanisani Padre anahamasisha tuchague Chadema na Dr Silaa. Hata pale Dodoma kuna kanisa moja Padre alikuwa kabla ya Misa anahubiri siasa waumini wa kweli wasimpigie kura Kikwete wampigie Silaa na Chadema. Na ukitazama ukweli unajidhihirisha sehemu zenye Wakatoliki wengi ndiyo Chadema ilikopata ushindi. Hili linatupa wasiwasi sisi wapiga kura.
 
Aliyeandika hapa huu upuuzi ni nani kama sio wewe!? Acha kukejeli dini za watu kwa maslahi yenu ya kisiasa, tena jiangalieni kwani hatutawavumilia tena kwa kauli zenu watu kama wewe Ritz, wewe kaa na dini yako tuache na dini yetu, uccm wako usiutumie kukashifu dini za watu, wananchi tumeshawajua kuwa mlikuja kwa gia ya kujifanya marafiki zetu katika dini na mkatutangazia uadui na vyama vingine, mmeingia madarakani tumewagundua ninyi ndo maadui wetu wakubwa na mlitutumia kama daraja la kuvukia uchaguzi wa 2010 leo yote mliyotuahidi hakuna zaidi ya vipigo, manyanyaso, kuwekwa selo n.k. hatudanganywi tena kwa sera zenu hzo, TUMESHAJUA MBIVU NA MBICHI. UAMUZI NI WETU. TUMESHAWAFAHAMU MARAFIKI NA MADUI ZETU. UAMUZI NI WETU


Tulizana usipende kukurupuka aliyoandika hayo amekaa kimya.
 
Last edited by a moderator:
Mimi nadhani tuingalie zaidi CCM na uhusiano wake na waislam hasa tukianzia TANU ilivyoanzishwa, viongozi wake, na wanachama wake alafu tuangalie ilivyobadilishwa kutoka TANU mpaka kuwa CCM na uongozi wa CCM ilipoanzishwa mpaka sasa, majibu yote utayapata hapo ndani ya TANU mpaka kuzaliwa kwa CCM. Someni HISTORIA kwa makini.

Mpole

Kama lilivo jina lako naamini utakuwa mpole wa amani bali si kwa kikundi cha watu kupora haki yako. (wanasiasa walio madarakani)

Tunasoma historia ili kujiepusha na kurudia makosa ya awali na pia kudumisha yaliyo mema.

Huku nyuma tulikuwa maskini nchi kibao duniani, lakin wenzetu wanabadilika na wametuacha tunalia na historia.

Mfano, katika kipindi kifupi cha Paul kagame wa Rwanda madarakani, nchi imebadilika na inakimbia kimaendeleo.

Tunatakiwa kubadilika kulingana na wakati badala ya kugeuka nyuma na kuilalamikia historia dunia inasonga mbele, angalia malysia, china nk

Tunapokuwa na serikali inayoongoza kwa hisia na kushindwa kuwajibika kwa watu wake kwa visingizio kila asubuhi hatuwezi kuendelea, Watakwambia majambia ya CUF, watakwambia, Ukristo wa Dr slaa, watakwambia, sheria za uswis ngum kurejesha fedha, watakwambia, Richmond sio ufisadi, watakwambia, ukabila wa wanasiasa, watakwambia ushahida rushwa rada hawana nk

Cha ajabu hao watu wanatuibia haki zetu wazi wazi, ukiiba kuku au mbuzi unafungwa fasta lakini wezi wa Rada, EPA, Meremeta, usafirshaji wa pembe za ndovu wote hao hawafungwi zaidi ya kupandishana vyeo.

Mikataba mibovu ambayo inatughalim fedha nyingi watanzania IPTL, Net group solution nk

Ni jukum letu watanzania kufaham kwamba wanasiasa wanatumia njia mbalimbali kuhakikisha wanabakia madarakani kama vile

- kuchonganisha wananchi kwa maana ya din zao tunapogawanyika wanapata nafasi ya kutuibia kura na hatimae .........

-Kuchonganisha wananchi kwa maana ya makabila yao na kanda wanazo toka, tukigawanyika kwao neema maana wamefanikiwa nk

Bila sisi raia kujitambua tutaishia kupigana na kuwacha wao na familia zao wanajaza matumbo kwa amani sisi tukitekete. Hatuwezi kuirudisha tanganyika ya TAA na TANU.
 
Kim Kardash

Tulipoanzisha mfumo wa vyama vingi, tulikubaliana mambo ya msingi ya kuzingatiwa na vyama vyote, mojawapo ni kuwa na wanachama pande zote za muungano. Lakini la muhimu ni kutokuwa au kuonyesha ubaguzi wa kidini, jinsia au ukabila. Haya yalitakiwa kuzingatiwa na hata katiba za vyama. Msajili wa vyama hasingeweza kukisajili Chama kinachoonyesha muelekeo wa udini na ni sababu tosha kukifuta.

Kwa maoni yangu pia ingekuwa marufuku kwa mtu au taasisi yoyote kuipaka metope taasisi ingine na hasa vyama vya siasa kwamba kina mlengo wa ubaguzi bila kuthibitisha. Nafikiri ni udhaifu wa msajili wa vyama vya siasa kuruhusu vyama kutumia kete hii kuchafuana wakati akijua kuwa hii inathibitisha alivyo dhaifu.
 
Kim Kardash

Tulipoanzisha mfumo wa vyama vingi, tulikubaliana mambo ya msingi ya kuzingatiwa na vyama vyote, mojawapo ni kuwa na wanachama pande zote za muungano. Lakini la muhimu ni kutokuwa au kuonyesha ubaguzi wa kidini, jinsia au ukabila. Haya yalitakiwa kuzingatiwa na hata katiba za vyama. Msajili wa vyama hasingeweza kukisajili Chama kinachoonyesha muelekeo wa udini na ni sababu tosha kukifuta.

Kwa maoni yangu pia ingekuwa marufuku kwa mtu au taasisi yoyote kuipaka metope taasisi ingine na hasa vyama vya siasa kwamba kina mlengo wa ubaguzi bila kuthibitisha. Nafikiri ni udhaifu wa msajili wa vyama vya siasa kuruhusu vyama kutumia kete hii kuchafuana wakati akijua kuwa hii inathibitisha alivyo dhaifu.


Mkuu hapo kwenye blue, hayo yakitendeka tutaishi kwa amani na umoja wetu utatukuka kama hapo awali tulijukana kama Ndugu Rajabu, Ndugu Edward, Ndugu Mwanaisha, Ndugu joyce nk.

Anayetoa tamko ovu lolote bila kuthibitisha, alipaswa kuchukuliwa hatua kali, lakini hili haliwezekani kwa sababu ndiyo mtaji wa serikali iliyoka madarakani kupitia ukimya wa msajiri.
 
Kwa mtazamo wangu
Waislamu waumini wa kawaida wala hawana tatizo na Chadema na Chadema
haina tatizo na waislamu, wakristo au dini yoyote ile. Tatizo ni wale
vocal muslims, akina Sheikh Ponda na wenzake wa Annuur na Radio Iman.

Hawa wangependa chama cha siasa kitangaze from day one kwamba chama
kitafanya hivi kitafanya vile kwa manufaa ya waislam ndipo wakiunge
chama mkono. Sasa kwa chama cha siasa ni makosa makubwa kupandikiza
mbegu za udini kwa namna hiyo.

Waislam yapaswa wakiunge mkono Chadema si kwa vile wao ni waislam, bali
kwa kuwa ni Watanzania kwanza. Wakristo yapaswa wakiunge mkono Chadema
si kwa vile wao ni wakristo, bali kwa kuwa ni watanzania kwanza.

Chadema wanalijua hilo na ndio maana namna zao za kujenga mahusiano na
makundi mbalimbali zinawabeba wote kama watanzania. Kama wadini
hawaitaki Chadema, basi ni tatizo la wadini. Si la Chama.
gud gud guuud! asante kwa uchambuzi mzuri
 
Wewe na kundi lako ndiyo mnawachafua Chadema kwa kuwakejeli Waislam.

If you real mean what you have said Ritz I real liked your comment. Hii nchi yetu sote tuwe wakweli nafsini mwetu
 
hili lipo la kumezeshwa propaganda, cdm haingwi mkono na waislam walio wengi,hasa wenye msimamomao mkali na wale wakada yachini kielimu,wengi wame beba sumu kuwa cdm in ya wakristo,hili linatiashaka kwa cdm kushika dola 2015 kama wanavyo dai cdm.Niwakati wa cdm kuziba ufa huu kwa kujipambanua kuwa sio chama cha wakristo ili kiungwe mkono na watanzania wote bila kujali itikadi ya dini zao. Kwa mtazomo wangu na uhalisia niliona hili swala la udini ndilo linaweza kukwamisha cdm kushindwa kuingia madalakani.
 
Kwa nn iwe ni jambo la ajabu kwa Rufiji kuwa na diwani wa Chadema? Kwa vile ni waislamu wengi? Then, ni kwa nini iwe ni Jambo la kustaajabisha kwa Zitto Kabwe kuwa Muislamu? Kauli za hovyo kama hizo ndio zinaongeza kuwaaminisha waislamu kuwa kumbe muislamu kupata nyadhifa chadema ni Jambo la kushangaza na kustaajabisha ila kwa wengine ni jambo la kawaida kwa vile ni chama chao sio ndio? shame on you!

Nimeipenda hii!
 
[Hakuna kitu kama hicho cha mgogoro kati ya chadema na uislamu ]

mkuu wewe upo maeneo yawapi? watu wana ichukia ccm lakini hawakotayari kuiunga mkono cdm kwasabubu tu ya udini. hili alihitaji uchunguzi kuliona.
 
Je wale mapadre wa Sumbawanga waliokuwa wakifukuza waumini wanaoishabikia CCM ni maajenti wa CCM? Mbona Chadema haikutoa tamko kukanusha hilo. Huku kwetu Musoma kila Jumapili ukienda Kanisani Padre anahamasisha tuchague Chadema na Dr Silaa. Hata pale Dodoma kuna kanisa moja Padre alikuwa kabla ya Misa anahubiri siasa waumini wa kweli wasimpigie kura Kikwete wampigie Silaa na Chadema. Na ukitazama ukweli unajidhihirisha sehemu zenye Wakatoliki wengi ndiyo Chadema ilikopata ushindi. Hili linatupa wasiwasi sisi wapiga kura.

Huu ndio ukweli halisi wa hali ilivyo kua mwaka 2010,pale Bariadi Padre wa Kizungu wa Kanisa Katoliki alisema wazi kuwa waumini wamchague mtu wa dini yao! Kuna haja ya Chadema kukubalia tatizo hili na waangalie namna ya kujipambanua kua wao sasa sio chama cha kidini tena!
 
[Hakuna kitu kama hicho cha mgogoro kati ya chadema na uislamu ]

mkuu wewe upo maeneo yawapi? watu wana ichukia ccm lakini hawakotayari kuiunga mkono cdm kwasabubu tu ya udini. hili alihitaji uchunguzi kuliona.

kama yupo dar kwa mfano ajaribu kupita maeneo yenye waislam wengi kama kariakoo aone kama kuna mtu ana habari na chadema,hata kuizungumzia ni tabu,sasa hiyo sio dalili nzuri kwa chama kikubwa kama chadema
 
CHADEMA ITAMKE WAZIWAZI JINSI ITAKAVYO TATUA TATIZO LA WAISLAM HAPA TANZANIA KUJIONA KUWA NI JAMII ILIYOBAGULIWA KATIKA ELIMU,AJIRA ZA UMMA,HUDUMA ZA AFYA,UMASIKINI KATIKA UKANDA WA PWANI WENYE WAISLAM WENGI,ITAMKE KUIVUNJA BAKWATA NA KUUNDA CHOMBO CHENYE TIJA KWA TAASISI ZOTE ZA KIISLAM,KUZIPA RUHUSA NA USALAMA KWA TAASISI ZA KIMATAIFA ZINAZOSAIDIA JAMII ZA WAISLAM DUNIANI KWANI KWA SASA HAZIPO TENA TANZANIA KWA KIGEZO CHA PROPOGANDA ZA UGAIDI ZINAZOENEZWA NA MAREKANI.hayo yakifanyika nina uhakika CHADEMA itakonga nyoyo za waislam kwani kwa sasa hawana wa kuwasikiliza
 
Hata Nyerere alipohamia Daru ssalam na kukaribishwa na Waislam, aliacha kuvaa kaptura yaani suruali fupi na kuanza kuvaa kibaraka shehe na hata kufunga swaumu siku nzima mpaka kichwa kikamuuma na kuomba apewe aspirini lakini alinyimwa dawa na kuombwa asubiri mpaka futari na baada ya kufuturu na Waislamu Nyerere hakusikia maumivu ya kichwa tena!

Sasa viongozi wa chadema wanachotakiwa kufanya sio kula pilau na Waislamu bali kuingia mkataba na Waislamu kuwa wakishika dola basi watashughulikia kero na madai ya msingi ya Waislamu kuwa...

1. Elimu itakuwa haki ya msingi kwa kila raia na hakutakuwa na ubaguzi wa rangi, dini, jinsia au jiografia kama ilivyo sasa!
2. Shule zote za Waislamu zilizotaifishwa na Nyerere wakati wa azimio la Arusha 1967 wanarudishiwa wenyewe!
3. Mgawo sawa wa madaraka ya nchi na sio dini moja tu kuhodhi kila sehemu!
4. Waislamu wawe huru ndani ya nchi yao kutangaza dini yao bila kuingiliwa na Serikali au Kanisa! mradi wanafuata sheria!
5. na mengine mengi yatakayochangiwa!

Chadema wasijidanganye kuwa watarudisha imani ya Waislamu kwa kula nao Pilau au biriani bali wanatakiwa kutumia mbinu muafaka na mbinu kama hizi hutumiwa hata Marekani na nchi nyingi duniani! hata Kenya Odinga na ODM aliingia Mkataba na Waislamu wa Kenya ktk uchaguzi uliovurugika wa 2007!
 
Mkuu hapo kwenye blue, hayo yakitendeka tutaishi kwa amani na umoja wetu utatukuka kama hapo awali tulijukana kama Ndugu Rajabu, Ndugu Edward, Ndugu Mwanaisha, Ndugu joyce nk.

Anayetoa tamko ovu lolote bila kuthibitisha, alipaswa kuchukuliwa hatua kali, lakini hili haliwezekani kwa sababu ndiyo mtaji wa serikali iliyoka madarakani kupitia ukimya wa msajiri.

Mkuu linawezekana kabisa. Tuykubaliane katika maadili yatakayowekwa na Katiba Mpya liermo. Kinyume chake tutaliangamiza taifa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom