CHADEMA, uislam na waislam!

CHADEMA, uislam na waislam!

Status
Not open for further replies.
Takuwekea hapa mabandiko yako ya kejeli dhidi ya Waislam bahati nzuri JF kuna kumbukumbu ya maandishi kila member.

Wewe si ndiyo unaandika humu Waislam wavaa mateneti, wavaa pedo, wanavizia wali wa itima, wanatembea na shanga mkononi huku wanahesabu. Kejeli nyingi tu umeandika humu.

Badilika hakuna mshindi kwenye vita vya dini.
Mmmmhhhh haya bana
 
Wadau

kama mngetumia walau chembe ndogo ya hekima na busara mjadala huu ungekuwa na maana.

Kila mmoja wetu shulti aheshim imani ya mwingine pia kuheshim uwepo wa wasiomin (wapagani)

Watanzania wana dini na iman zao. Lazima uislam uheshimiwe, lazima ukristu uheshimiwe, lazima imani zingine pia waheshimiwe.

Kuchangia mjadala kwa kejeli kwa iman yoyote ni kumkosea mungu na kuwakosea adabu watanzania wanaoamin na wasiomini.

Utu wa mtu ni kauli na matendo yake, hivyo nidham na utulivu unahitajika katika kujadili mambo yanayohusu imani za watanzania.
 
Ndg zangu waislam, islam nduguye islam chadema ni adui mkubwa wa islam tanzania kumbuka walivyo mtendea dada yetu kule igunga walimnyanyasa sana walimfedhehesha sana lakini hawakuomba msamaha hivyo nakuombeni wewe uliye mwislam adui ya mwislam ni adui ya waislam wote.

ahaa ha haaa! yule mama mkuu wa wilaya mfuga kitimoto maarufu pale mbezi beach!! kumtetea bi fatuma kimario hapo watu wazima mlichambia steelwire...lol!
 
Katika uchaguzi wa 2010 zilichapishwa fulana kwa kuandikwa VOTE FOR PEDRO na watu kuzivaa makanisani. Kuvaa barghashia na kula nao futari pamoja haitoshi! kuna jambo zaidi la kufanywa nalo ni sera itakayozingatia mawazo yao.

"Sera itakayozingatia mawazo yao" safi sana kwa kuanzia unaweza kutupa mawazo mawili matatu labda ili wenyewe wayaone maana viongozi wa chadema wapo humu,so ni wakati muafaka wa kusema nini waislam wanahitaji ambacho pengine cdm ikikifanya hali ya kuaminiana itarudi na kukiona cdm kama ni chama cha siasa tu na si vinginevyo

Nitawatolea mfano,hapo kwa jirani zetu kenya,kuelekea uchaguzi mkuu wao ule uliozaa vurugu na mauaji makubwa,waislam wa kenya walipanga mikakati kabambe ya kuhakikisha kura zao kwa umoja wao wanazitumia vizuri,walichofanya waliorodhesha madai yao yote ambayo wanayataka na kuyaweka hadharani huku wakitoa tamko kwamba wao hawana mgombea kwenye uchaguzi mkuu wa rais ila wanayo madai yao ambayo wangependa yatekelezwe hivyo mgombea yeyote atakaekua tayari kutekeleza madai yao wao ndio watakaempigia kura bila kujali dini yake,mwai kibaki akaenda mombasa akakutana na masheikh akakubaliana nao masheikh wakamwambia hatutaki makubaliano ya maneno tunataka makubaliano yetu tuyasajili kisheria mahamani ili ukitugeuke tujue pa kuanzia,kibaki maji yalikua shingoni laila alikua anaelekea kuishika pwani kwa kuwa alikua sambamba na na najib balala ambae ni mwenyeji wa pwani na mtoto wa sheikh maarufu huko,hivyo ili kuikabili nguvu ya Raila pwani kibaki akaingia agreement na waislam kupitia masheikh!hii ni changamoto kwa chadema na waislam wa tanzania ili kuondoa sintofahamu baina yenu tumieni mfano huo,hakuna linaloshindikana pakiwepo nia njema mioyoni
 
Tofauti ni kubwa CHADEMA NI CHAMA CHA KIKROSTO na kikanda pia ni wanafiki waislamu hawapendi unafiki na ukanda hivyo basi chadema hawawezi kukaa meza moja na waislamu wakaaminiana.

Mwenye busara na kuitakia mema nchi ni yule anayeona kosa na akasema kosa ni hili hapa bila kumung'unya maneno, badala ya kusema ukanda, ukristo nadhani tungesema ukanda wenu unatokana na moja mbili tau, badala ya kusema udini kijumlajumla tuainishe matendo yanayoashiria kukumbatia dini moja na kuitenga nyingine, vilevile tutofautishe mtu mmoja mmoja na msimamo wa chama
 
Matusi hayo wewe unafuga naye kiti moto. Chadema nasema tena mwislam yeyote atakae ichagua atakuwa ameusaliti uwislam na hakika hastahili msamaha mbele ya mola wake.
 
Hayo yaliletwa na sultani kikwete kuitenganisha chadema na Uislamu lakini sasa yameanza kumtokea puani Waislamu wa Mtwara wameshaligundua sasa wanampa za USO

chadema haiwezi kuingia misikitini na makanisani kuomba waumini waiunge mkono. Kila mtu ana utashi wake na kutambua lipi jema na lipi baya. Propaganda wote tunazisikia lakini wengine tunafia nafsi zetu na sio dini. Kwa hiyo kila watakachongea viongozi wa dini tunalinganisha na hali halisi na kufanya maamuzi. Hatuwezi kufuata upuuzi wa wachache wanaotetea matumbo yao!
 
Jambo lingine ambalo linaonesha waislamu kuwa mbali kidogo na chadema ni nafasi ya Dr. Slaa ktk kanisa. Yeye ni Padri. Unadhani kwa nafac hiyo waislamu watachukulia poa hivyo? Chukulia Sheikh Alhadi Musa Salum wa Mkoa wa DSM anayekubalika na Waislam wengi agombee urais halafu padri fulani yupo chama kingine ww mkristo bila unafki utamchagua nani? Mm ni mwanachadema ila tukubalitukatae udini hivi sasa umetawala sn ktk nchi yetu. chanzo cha tatizo hili ilikuwa ni uchaguzi wa 2010 hasa ktk kampeni chafu za CCM

Wakati mwingine waislam yabidi wawe consistent katika hoja zao. Kuna wakati wanamwita Dr. Slaa padre hivyo ni mdini, na kuna wakati wanamtuhumu kwamba alilisaliti kanisa hivyo haaminiki. Kipi ni kipi sasa kwa Dr. Slaa?

Mimi bado nasisitiza kwamba ni makosa kwa mwanasiasa yoyote kujipeleka kimbele mbele kwenye mambo ya dini ili kukubalika na watu wa dini hiyo. After all -- kukubalika kwa watu hakumaanishi kukubalika kwa Mungu.

Taifa letu ni kubwa, yatosha tu kumtambua Kikwete kwamba ni Mtanzania aliyetokea kuwa mwislam kwa kuzaliwa na sasa ni rais wa Tanzania. Dr. Slaa ni mtanzania aliyetokea kuwa mkristo kwa kuzaliwa, akawa padre, akastaafu upadre, akaamua kuwatumikia watanzania kwa njia ya siasa.

Kama ilivyokuwa kwa Mkapa mkristo, itawashangaza sana waislam nadhani iwapo Dr. Slaa atatokea kuwa Rais halafu maisha yao nchini yakaneemeka chini ya uongozi wa Dr. Slaa. Na nadhani inawashangaza pia kwamba Kikwete ni mwislam, na makamu wake, lakini maisha ya waislam kama ilivyo kwa wakristo bado ni mpigiko tu.

Somo kubwa hapa ni kwamba dini ya rais haviusiahani kabisa na maisha ya kawaida ya mtanzania.
 
ahaa ha haaa! yule mama mkuu wa wilaya mfuga kitimoto maarufu pale mbezi beach!! kumtetea bi fatuma kimario hapo watu wazima mlichambia steelwire...lol!

yah pia lipo tatizo la kutafsiri na kutofautisha kati ya muislam na mtu mwenye jina la kiislam!
 
Mimi nadhani tuingalie zaidi CCM na uhusiano wake na waislam hasa tukianzia TANU ilivyoanzishwa, viongozi wake, na wanachama wake alafu tuangalie ilivyobadilishwa kutoka TANU mpaka kuwa CCM na uongozi wa CCM ilipoanzishwa mpaka sasa, majibu yote utayapata hapo ndani ya TANU mpaka kuzaliwa kwa CCM. Someni HISTORIA kwa makini.
 
Udini mnaousema upo kwenye Media tu, kwetu bado tunazikana waislam na wakristu, kuoana ndio kama kawa na mambo mbalimbali tunasidiana... Udini upo wap!? Mitandaoni? Mapovu ya nini!
 
Tatizo hapa si Chadema wala uislamu wala ukristo; tatizo ni CCM
 
Nakubaliana na wewe kabisa. Lakini kosa lingine kubwa lililofanyika ni ule waraka wa kanisa kuelekea uchaguzi wa 2010 na hata pale kanisa jijini Arusha lilipojiingiza kutomtambua meya wa Arusha ilijipambanua wazi kuwa kanisa linaiunga mkono chadema na hilo huwezi kulikanusha. Hivyo, CCM wanatumia kosa hilo kwa faida yao na hiyo ndio Siasa.
 
yah lakini hiyo strategy inaonekana kuisaidia ccm kwa kuwa hata kipindi cuf imeshika hatamu za upinzani hapa nchini hii kitu pia ilitumika kuichafua cuf mpaka ikakosa umaarufu miongoni mwa wakristo wakiaminishwa kwamba cuf ni chama cha waislam,chama cha wapenda n.k. lakini ukweli ni kwamba cuf ni chama cha siasa tu na kimeendelea kuwa hivyo,ndio mana nasema viongozi wa cdm wasilikalie kimya hili,they have to do something kuondosha propaganda hii,wakikaa kimya na kujifanya eti hamna kitu kama hicho waislam zaidi watazidi kujiunga katika kuichukia cdm bila sababu

Hata mimi bado naamini kwamba CUF ni cha waislam maana mpaka sasa hawajatuambia kilichomfukuzisha uongozi na uanachama bwana Mapalala, Lwakatare sijaona wa dini nyingine wakiondolewa uanachama bila kutolewa sababu kwa umma. Nitaamini vinginevyo kama CUF watakuwa wawazi kuhusu haya, lakini pia ndo chama cha kwanza kupigiwa debe katika nyumba za ibada hasa misikitini mfumo wa vyama vingi ulipoanza nchini bila kukemewa na viongozi wa chama husika sasa kwa nini tusiamini ni chama kwa ajili ya waislam na wa dini nyingine waliopo huko ni wasindikizaji?
 
.......Mimi naona sera za CDM zijikite kuwapa elimu waislamu hata kwa upendeleo maalum. Hii itakuwa na manufaa kwa taifa letu. Nchi zenye waislamu walioenda shule kama Singapore na Malaysia wameondokana na siasa hizi za maslahi ya kidini kuliko uarabuni kuliko na waislamu wasiojali elimu.
Mkuu naomba nitoe mtazamo tofauti na huo wako, waislamu pia wameenda shule wala hawaitaji upendeleo maalum kwa sababu ikiwa hivyo itafanyika kwa gharama ya nani kama sio ya upande wa pili na kuleta kitu chenye sura ilieile ya gharama za kuendesha mahakama ya kadhi, isipokuwa wale wachache wasioenda elimu dunia ndio wako na sauti sana na pia wana nyadhifa za juu kwenye taasisi za dini. nashauri walioenda shule waingie kwenye taasisi zao na kuwaelimisha wenzao wachache ambao wanachafua sura nzuri ya dini yao.
 
je chadema imehusika kwa namna yeyote ile kufanya dhulma kwa waislam na uislam kiasi cha waislam kuhisi na kuamini ushirikishwaji na utambulikaji wao kama kundi lenye mahitaji uko na utazidi kuwa mashakani kama cdm itapewa ridhaa ya kuongoza taifa hili?je chadema pengine imeonesha dalili zozote za kutotaka kuona watu wenye itikikadi au imani ya dini ya kiislam wanajumuika pamoja kwenye harakati za kisiasa na kisera ndani ya chadema?
Wewe utashi wako uko vipi katika hili?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom