Kenneth Nollo
Member
- Dec 20, 2012
- 98
- 18
Chadema kujifanya wako karibu na Waislamu wakamtetea Sheikh Ponda eti serikali inatumia nguvu nyingi na Kusema Bakwata haifai!
hata akina ponda hawana tatizo na chadema wasiwasi yao ni pale wanapoona ccm pamoja na mwenyekiti wake kuwa muislam wananyanyaswa, hivyo wanadhani kwamba kwa kuwa chadema mwenyekiti wake ni mkristo watanyanyaswa zaid. lakini chadema haina udini na kama watachukua nchi watakaofaidika zaidi ni waislam.kwani ndio itakuwa mwanzo wa utawala wa haki na sheriaKwa mtazamo wangu Waislamu waumini wa kawaida wala hawana tatizo na Chadema na Chadema haina tatizo na waislamu, wakristo au dini yoyote ile. Tatizo ni wale vocal muslims, akina Sheikh Ponda na wenzake wa Annuur na Radio Iman.
Hawa wangependa chama cha siasa kitangaze from day one kwamba chama kitafanya hivi kitafanya vile kwa manufaa ya waislam ndipo wakiunge chama mkono. Sasa kwa chama cha siasa ni makosa makubwa kupandikiza mbegu za udini kwa namna hiyo.
Waislam yapaswa wakiunge mkono Chadema si kwa vile wao ni waislam, bali kwa kuwa ni Watanzania kwanza. Wakristo yapaswa wakiunge mkono Chadema si kwa vile wao ni wakristo, bali kwa kuwa ni watanzania kwanza.
Chadema wanalijua hilo na ndio maana namna zao za kujenga mahusiano na makundi mbalimbali zinawabeba wote kama watanzania. Kama wadini hawaitaki Chadema, basi ni tatizo la wadini. Si la Chama.
Hata Nyerere alipohamia Daru ssalam na kukaribishwa na Waislam, aliacha kuvaa kaptura yaani suruali fupi na kuanza kuvaa kibaraka shehe na hata kufunga swaumu siku nzima mpaka kichwa kikamuuma na kuomba apewe aspirini lakini alinyimwa dawa na kuombwa asubiri mpaka futari na baada ya kufuturu na Waislamu Nyerere hakusikia maumivu ya kichwa tena!
Sasa viongozi wa chadema wanachotakiwa kufanya sio kula pilau na Waislamu bali kuingia mkataba na Waislamu kuwa wakishika dola basi watashughulikia kero na madai ya msingi ya Waislamu kuwa...
1. Elimu itakuwa haki ya msingi kwa kila raia na hakutakuwa na ubaguzi wa rangi, dini, jinsia au jiografia kama ilivyo sasa!
2. Shule zote za Waislamu zilizotaifishwa na Nyerere wakati wa azimio la Arusha 1967 wanarudishiwa wenyewe!
3. Mgawo sawa wa madaraka ya nchi na sio dini moja tu kuhodhi kila sehemu!
4. Waislamu wawe huru ndani ya nchi yao kutangaza dini yao bila kuingiliwa na Serikali au Kanisa! mradi wanafuata sheria!
5. na mengine mengi yatakayochangiwa!
Chadema wasijidanganye kuwa watarudisha imani ya Waislamu kwa kula nao Pilau au biriani bali wanatakiwa kutumia mbinu muafaka na mbinu kama hizi hutumiwa hata Marekani na nchi nyingi duniani! hata Kenya Odinga na ODM aliingia Mkataba na Waislamu wa Kenya ktk uchaguzi uliovurugika wa 2007!
Na ni ukweli ulio wazi kuwa vikaratasi hivi vilikuwa vinasambazwa misikitini kumpigia kampeni Kikwete.Huu ndio ukweli halisi wa hali ilivyo kua mwaka 2010,pale Bariadi Padre wa Kizungu wa Kanisa Katoliki alisema wazi kuwa waumini wamchague mtu wa dini yao! Kuna haja ya Chadema kukubalia tatizo hili na waangalie namna ya kujipambanua kua wao sasa sio chama cha kidini tena!
Zubeda
hayo madai uliorodhesha umeyatowa wapi? ninamaana hizo kasoro kama zipo nani alizisababisha? japokuwa kwa mtaamo wangu hazipo.
1. umeongelea ubaguzi wa rangi fafanua kidogo hili linfanyika wapi hapa tanzania na kwa misingigani?
2. Aliyetaifisha mashule alikuwa na lengo zuri tu kwa maslah ya watanzania wote, wakirudishiwa na wakristo warudishiwe? Je tunajenga umoja wa watanzania kama taifa au tunabomoa vipande vipande kama unavyopingana katika hoja yako no 1?
3. mgao sawa wa madaraka kwa maana ya Din? vipi kuhusu makabila nayo tutafanya hivyo maana wasukuma ni wengi sana.
b) Je tutafanya usaili wetu kwa maana ya dini zetu, kama ndivyo nafasi ya taaluma ya kila mmoja wetu itakuwa wapi?
c) Endapo tutajipanga kwa maana ya uwiano wa imani zetu, unataka kuniambia Pengo atafanya operation za matumbo na Idd Simba atafanya operation za wagonjwa wa moyo? je hiyo ndiyo maana halisi ya Taaluma na ufanisi kwa fani husika?
4. Nani kakwambia waislam wa tanzania hawapo huru?, Je wapagani wa tanzania wanauhuru gani na kwanini?
5. Chadema haijawahi kushika dola hata siku moja, ccm na serikali yake ndiyo wametutawala tangia uhuru, Je kasoro unazozisema zimesababishwa na
a) chadema kwasababu ndiyo ipo, madarakani na hivyo imewagawa watanzania nakusababisha mapungufu tuliyonayo-Ilaumiwe!
b) CCM ambayo ipo madarakani na hivyo imewagawa watanzania na kutufikisha hapa tulipo na mapungufu tuliyonayo-Ilaumiwe
c) Cuf kwasababu haijawaunganisha watanzania kudai haki zao za msingi kutoka serikali na hivyo itupiwe lawama
d) ...........
Nimeonelea nikuulize haya maswali kidogo ili kuanzia hapa tuone utata upo wapi, kwa watawala wa ccm, CUF, Cdm au NCCR.
Wewe unaoneka ulikuwa unaishi ughaibuni maana huna habari yoyote kuhusu Waislamu! nitakujibu fanya subira!
Mliji changanya sana kumsimamisha Padri Mstaafu kuwa Mgombea Urais,na makanisa yakawa yanatoa approval kuwa hata kama Padri hajaoa sio tatizo kuongoza nchi! Na matamko ya Roman Catholic nayo kipindi yalizidi,siku hizi wameacha! Naona hapa ndipo mlipo jipambanua!
Ni kweli udini ulioasisiwa na CCM dhidi ya CUF na kisha kuujenga ipasavyo dhidi ya CDM . Udini huu umewageukia, CCM wanamjadala mkubwa na mkali kweli kweli;wamegawanyika, kuna wanaosema rais ajaye kupitia CCM lazima awe MUISLAM. Upande mwingine, kuna wale wanaotaka rais ajaye lazima awe MKRISTO.
CCM wana kazi kweli kweli safari hii kuliko wakati mwingine wowote ule.
Zubeda
Hata la ubaguzi wa rangi walau tuambie unafanyika wapi hapa tanzania?
Mkuu amini usiamini nchi hii haitakaa ishikwe na muislam tena.
Zubeda
hayo madai uliorodhesha umeyatowa wapi? ninamaana hizo kasoro kama zipo nani alizisababisha? japokuwa kwa mtaamo wangu hazipo.
1. umeongelea ubaguzi wa rangi fafanua kidogo hili linfanyika wapi hapa tanzania na kwa misingigani?
2. Aliyetaifisha mashule alikuwa na lengo zuri tu kwa maslah ya watanzania wote, wakirudishiwa na wakristo warudishiwe? Je tunajenga umoja wa watanzania kama taifa au tunabomoa vipande vipande kama unavyopingana katika hoja yako no 1?
3. mgao sawa wa madaraka kwa maana ya Din? vipi kuhusu makabila nayo tutafanya hivyo maana wasukuma ni wengi sana.
b) Je tutafanya usaili wetu kwa maana ya dini zetu, kama ndivyo nafasi ya taaluma ya kila mmoja wetu itakuwa wapi?
c) Endapo tutajipanga kwa maana ya uwiano wa imani zetu, unataka kuniambia Pengo atafanya operation za matumbo na Idd Simba atafanya operation za wagonjwa wa moyo? je hiyo ndiyo maana halisi ya Taaluma na ufanisi kwa fani husika?
4. Nani kakwambia waislam wa tanzania hawapo huru?, Je wapagani wa tanzania wanauhuru gani na kwanini?
5. Chadema haijawahi kushika dola hata siku moja, ccm na serikali yake ndiyo wametutawala tangia uhuru, Je kasoro unazozisema zimesababishwa na
a) chadema kwasababu ndiyo ipo, madarakani na hivyo imewagawa watanzania nakusababisha mapungufu tuliyonayo-Ilaumiwe!
b) CCM ambayo ipo madarakani na hivyo imewagawa watanzania na kutufikisha hapa tulipo na mapungufu tuliyonayo-Ilaumiwe
c) Cuf kwasababu haijawaunganisha watanzania kudai haki zao za msingi kutoka serikali na hivyo itupiwe lawama
d) ...........
Nimeonelea nikuulize haya maswali kidogo ili kuanzia hapa tuone utata upo wapi, kwa watawala wa ccm, CUF, Cdm au NCCR.
Ni kweli udini ulioasisiwa na CCM dhidi ya CUF na kisha kuujenga ipasavyo dhidi ya CDM . Udini huu umewageukia, CCM wanamjadala mkubwa na mkali kweli kweli;wamegawanyika, kuna wanaosema rais ajaye kupitia CCM lazima
awe MUISLAM. Upande mwingine, kuna wale
wanaotaka rais ajaye lazima awe MKRISTO.
CDM hamna KAZI maana mgombea wenu ni BABU na tayari ni Padri......CCM hajulikani hadi
CCM mda ukifika. Hongereni kwa democracy yanu maana mwenyekiti kashaweka bayani sasa hakuna uchaguzi hapo ndani ya chama
Wake up Kama ni hivyo wakristo tuanze kudai mapema cdm ikishika dola lazima ifanye mambo maalum kwa wakristo maana sasa tumeshatukanwa vya kutosha na hiyo chadema. Kama ni kweli ni wakristo pekee waliopa chadema kura basi ijulikane kuwa hata bila kura za waislamu chadema itashinda maana hata 2010 ilishinda!!!
Ndio maana wanafanya kampeni kama hizi:CDM wanajua wazi bila kuungwa mkono na waislam hawawezi kuingia Ikulu ukweli ndio huo. WAISLAM ndio wanaipiga kura sana kuliko wengine.Pia wengi wao wapo katika informal sector hivyo wanamuda kwa kujiandikisha na kusimama kwa mda mrefu kusubiri kupiga kura.
Waislamu huwa hakuna utenganishi kati ya dini na siasa, kwao siasa ni dini pia. Maana religion is the way of life ( Mfumo kamili wa maisha).