Haturudii kosa na wala hatudanganyiki. nyie kuleni umbwabwa wenu na hao mashehena ubwabwa yenu.kumekuwa na upotoshaji au propaganda kwamba chadema hakipikiki chungu kimoja na waislam walio wengi(sio wote),je suala hili ukweli wake ukoje?na je ni wapi hasa kama papo wanapotofautiana na kushindwa kuaminiana?je tatizo kama lipo kweli lipo upande gani,kwa waislam ama kwa jinsi chadema yenyewe ilivyojiweka na kuikalia kimya propaganda hii hatari.
ushauri wangu kama tatizo lipo kwa waislam kutokana na kulishwa tu propaganda basi tuwasaidie na kama tatizo lipo upande wa pili kwa maana ya chadema basi muda upo ijirekebishe na kuondoa sintofahamu hii kwa maslahi yake binafsi kama chama cha siasa chenye hamu ya kushika dola siku moja kwa kuwa ni ukweli ulio wazi bila kura za watanzania wote ambao kwa asilimia kubwa ni waislam na wakristo kwa umoja wao hakuna uwezekano wala njia ya mkato ya kushinda uchaguzi wa rais na kuunda serikali.
Nawasilisha.
![]()
Viongozi wa dini ya kiislamu mkoa wa Kilimanjaro.
![]()
mbunge wa jimbo la Moshi mjini Philemoni Ndesamburo akiteta jambo na viongozi wa dini ya kiislamu,huu ni mfano wa kuigwa
![]()
safi sana hii
![]()
![]()
Hii ni namna bora zaidi ya kujenga mahusiano na kuaminiana,iendelezwe na viongozi wa chadema mikoani na wilayani,kamwe chadema isidhani hii propaganda itaondoka yenyewe tu hapana they have to do something kujionyesha hawako upande wa kanisa na hawawachukii waislam kama waislam wengi wanavyoaminishwa na pia wana chadema mmoja mmoja pia mkisaidie chama kwa kuwa polite kwa waislam na wala msiwakejeli kwa namna yeyote ile bali muwasaidie kukielewa chama chenu,muwe mabalozi wazuri wa chama chenu,waislam watawaelewa na kuwakubali tu
Una ushahidi? Unaweza ukatuwekea hapa hilo tamko la kanisa?Mliji changanya sana kumsimamisha Padri Mstaafu kuwa Mgombea Urais,na makanisa yakawa yanatoa approval kuwa hata kama Padri hajaoa sio tatizo kuongoza nchi! Na matamko ya Roman Catholic nayo kipindi yalizidi,siku hizi wameacha! Naona hapa ndipo mlipo jipambanua!
CHADEMA ITAMKE WAZIWAZI JINSI ITAKAVYO TATUA TATIZO LA WAISLAM HAPA TANZANIA KUJIONA KUWA NI JAMII ILIYOBAGULIWA KATIKA ELIMU,AJIRA ZA UMMA,HUDUMA ZA AFYA,UMASIKINI KATIKA UKANDA WA PWANI WENYE WAISLAM WENGI,ITAMKE KUIVUNJA BAKWATA NA KUUNDA CHOMBO CHENYE TIJA KWA TAASISI ZOTE ZA KIISLAM,KUZIPA RUHUSA NA USALAMA KWA TAASISI ZA KIMATAIFA ZINAZOSAIDIA JAMII ZA WAISLAM DUNIANI KWANI KWA SASA HAZIPO TENA TANZANIA KWA KIGEZO CHA PROPOGANDA ZA UGAIDI ZINAZOENEZWA NA MAREKANI.hayo yakifanyika nina uhakika CHADEMA itakonga nyoyo za waislam kwani kwa sasa hawana wa kuwasikiliza
Hata Nyerere alipohamia Daru ssalam na kukaribishwa na Waislam, aliacha kuvaa kaptura yaani suruali fupi na kuanza kuvaa kibaraka shehe na hata kufunga swaumu siku nzima mpaka kichwa kikamuuma na kuomba apewe aspirini lakini alinyimwa dawa na kuombwa asubiri mpaka futari na baada ya kufuturu na Waislamu Nyerere hakusikia maumivu ya kichwa tena!
Sasa viongozi wa chadema wanachotakiwa kufanya sio kula pilau na Waislamu bali kuingia mkataba na Waislamu kuwa wakishika dola basi watashughulikia kero na madai ya msingi ya Waislamu kuwa...
1. Elimu itakuwa haki ya msingi kwa kila raia na hakutakuwa na ubaguzi wa rangi, dini, jinsia au jiografia kama ilivyo sasa!
2. Shule zote za Waislamu zilizotaifishwa na Nyerere wakati wa azimio la Arusha 1967 wanarudishiwa wenyewe!
3. Mgawo sawa wa madaraka ya nchi na sio dini moja tu kuhodhi kila sehemu!
4. Waislamu wawe huru ndani ya nchi yao kutangaza dini yao bila kuingiliwa na Serikali au Kanisa! mradi wanafuata sheria!
5. na mengine mengi yatakayochangiwa!
Chadema wasijidanganye kuwa watarudisha imani ya Waislamu kwa kula nao Pilau au biriani bali wanatakiwa kutumia mbinu muafaka na mbinu kama hizi hutumiwa hata Marekani na nchi nyingi duniani! hata Kenya Odinga na ODM aliingia Mkataba na Waislamu wa Kenya ktk uchaguzi uliovurugika wa 2007!
Haturudii kosa na wala hatudanganyiki. nyie kuleni umbwabwa wenu na hao mashehena ubwabwa yenu.
halafu nikuulize swali we mleta hii thread, nani kakuambia kuwa uislam ni kanzu na kofia?
Watu wasio na elimu ukiwalisha jambo fulani huwa wanalikariri kweli kweli na kuliondoa inakuwa taabu sana. Hata CDM ingeiwahi CCM na kuwaambia waisilamu kuwa CCM ni ya makafiri, nakwambia leo hii waisilamu wangekuwa wanaichukia CCM bila hata kufanya their own judgemement. Kwa hiyo hapa inategemea nani alianza kuwalisha sumu hawa jamaa!Kuvaa kofia baraghashia na kupiga picha na waislam haitoshi hio cheap propaganda cha muhimu ni muhimu ni kufunguka ki sera na muelekeo
Bado kuna tatizo la kuamini malengo na nia ya CDM. Dhidi ya Waislam na uislam kwani hata zao ni za Mehemko kama ya kilokole so yaliyojificha ndani ya moyo zao ni makubwa kuliko yale wanayoengea wakivaa baraghashia kusanif waislam
Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
Mti wenye matunda ndo unaopigwa mawe,wenye propaganda watashindana sana lakini hawatashinda,Mliji changanya sana kumsimamisha Padri Mstaafu kuwa Mgombea Urais,na makanisa yakawa yanatoa approval kuwa hata kama Padri hajaoa sio tatizo kuongoza nchi! Na matamko ya Roman Catholic nayo kipindi yalizidi,siku hizi wameacha! Naona hapa ndipo mlipo jipambanua!
Mkuu amini usiamini nchi hii haitakaa ishikwe na muislam tena.
Mi nadhani hapa tatizo ni lilelile, Elimu..
Elimu ndogo inazuia uwezo wa kuchanganua mambo kwa upana wa kutosha, na ni hapo ndipo viongozi wa dini wenye hisia za siasa wanapoingia na kutumia ushawishi wao kuweka mambo ya siasa kwa interest zao.
Chukua watu wanaomlaumu dr slaa kama mdini, kikubwa wao wanasema aliwahi kuwa padri, lakini hiki hakiwezi kuwa kigezo cha mtu kutokuwa objective kwenye kazi yake. Rais mstaaf alhaji A.Mwinyi alikuwa rais muislam anaipenda hasa dini yake lakini dhahama inayotolewa sana mfano na waislam kama mfano wa unyanyasaji kwao ya mauaji ya Mwembechai ilitokea kipindi chake,
..
watu wasio na elimu ukiwalisha jambo fulani huwa wanalikariri kweli kweli na kuliondoa inakuwa taabu sana. Hata cdm ingeiwahi ccm na kuwaambia waisilamu kuwa ccm ni ya makafiri, nakwambia leo hii waisilamu wangekuwa wanaichukia ccm bila hata kufanya their own judgemement. Kwa hiyo hapa inategemea nani alianza kuwalisha sumu hawa jamaa!
propaganda dhidi ya cuf na chdm hazijafanywa na ccm peke yake. vyombo vyetu vya habari navyo vimechangia. haviendeshwi kiueledi! kama alivyo sema mchangiaji mmoja kuwa picha za mbowe, slaa na ndesamburo wakiwa na waislamu huwa hazipewi front page coverage. kutokana na propaganda ya ccm na uzembe wa vyombo vya habari, mbowe na slaa huwa wanapewa front page photo wakiwa na maaskofu.
kwa upande mwengine, vyombo vya habari huwa vinaweka picha za wafuasi wa cuf wenye baraghashia, shungi, kanzu na ndevu. wafuasi wa cuf ambao hawana muonekano huu huwa hawaoneshwi. hali hii imewafanya wakristu waamini kuwa lisemwalo kuhusu cuf na waislamu ni kweli. vilevile waislamu huendelea kuamini kuwa lisemwalo kuhusu chdm na wakristu ni kweli.
piga, ua, garagaza, imani hizi haziwezi kufutika. wakristu wengi wataendelea kuamini kuwa cuf ni chama cha waislamu na waislamu wengi wataendelea kuamini kuwa chdm ni chama cha wakristu. mtanzania akisha lishwa imani fulani, kumbadilisha ni kazi ngumu! huo ndiyo ukweli. mtanzania akiamini simba au yanga kumtoa huko ni kazi ngumu.
ukiangalia nchi zilizo tuzunguka, utabaini kuwa vyama vingi vikongwe vya siasa vimeangushwa. vilabu vingi vya mpira vinapanda na kushuka. siyo hapa bongo. timu ni simba na yanga kila mwaka japo azam wanawasumbua kiasi fulani.
siyo kwamba nakukatisheni tamaa watanzania wenzangu. tuendelee kuunga mkono mageuzi lkn kwa hapa kwetu kazi ipo.