Kwa mtazamo wangu Waislamu waumini wa kawaida wala hawana tatizo na Chadema na Chadema haina tatizo na waislamu, wakristo au dini yoyote ile. Tatizo ni wale vocal muslims, akina Sheikh Ponda na wenzake wa Annuur na Radio Iman.
Hawa wangependa chama cha siasa kitangaze from day one kwamba chama kitafanya hivi kitafanya vile kwa manufaa ya waislam ndipo wakiunge chama mkono. Sasa kwa chama cha siasa ni makosa makubwa kupandikiza mbegu za udini kwa namna hiyo.
Waislam yapaswa wakiunge mkono Chadema si kwa vile wao ni waislam, bali kwa kuwa ni Watanzania kwanza. Wakristo yapaswa wakiunge mkono Chadema si kwa vile wao ni wakristo, bali kwa kuwa ni watanzania kwanza.
Chadema wanalijua hilo na ndio maana namna zao za kujenga mahusiano na makundi mbalimbali zinawabeba wote kama watanzania. Kama wadini hawaitaki Chadema, basi ni tatizo la wadini. Si la Chama.