CHADEMA sukumeni agenda yenu ya kukutana na Rais Samia

Retired

JF-Expert Member
Jul 22, 2016
40,386
73,983
Kwa kuanzia hili ni muhimu na lenye nia njema. Tumetoka kwenye udikteta uliokubuhu na hivyo kuna mwanya wa kufanya reconcilliantion. Push your agenda to meet her.

Na wala hamuendi kujikomba kwake, kujipendekeza, ni kuona kama kunaweza kuwa na mwanzo mpya.
 
Mbona hiyo ipo tayari na kinacho subiriwa ni nafasi tu ya mama.
 
Haya madudu ndiyo yanayowafanya waandike kwamba sasa hivi wana furaha zamani hawakuwa na furaha.

Lakini sauti ya Majaliwa ina mamlaka ndani yake ndiyo maana wako bize kumfundisha rais Samia kuwa amtoe kwenye uwaziri mkuu kwa sababu eti ni masalia ya JPM.

Kwani SAMIA ni masalia ya nani?
 
Chadema ni naive na hawajitambui.

Huyo samia mnakutana nae kwa ajili ya kitu gani?

Mnatafuta huruma zake ama?

Kwahiyo mtakuwa mnaendesha siasa kwa kufuata huruma za Rais aliyeko madarakani?

Hizo huruma zitawasaidia kufikia malengo yenu ya kukamata dola?

Au malengo yenu ni nini hasa?

Kupiga ruzuku tu?
 
Sheria zipo na katiba ipo!

Hiyo reconciliation ni kwa ajili ya kitu gani?

Mnaenda kumbembeleza samia awape ruhusa ya kufanya siasa?

Mnaenda kumbembeleza awape haki yenu ya Kikatiba?

Yaani ninyi ni watu wajinga mno
 
Chadema ni naive na hawajitambui.

Huyo samia mnakutana nae kwa ajili ya kitu gani?...
Usikurupuke, wanasiasa wenye akili uongozi ukibadirika, tena uongozi wa ki-IMLA, basi kunakuwa na nafasi ya kuona/kutafuta the way forward!

Mbowe amesema anataka HAKI na si kujikomba/kupata fadhila za Samia. Lkn kama kuna nafasi ya kusonga mbele kwenye demokrasia, itafute nafasi hiyo. Mkiona ni sawa na Magufuli, maaachana anye.
 
Back
Top Bottom