CHADEMA Special Thread

CHADEMA Special Thread

‼️🚨SERIKALI HARAMU TANZANIA WAMEKUBALI MASHARTI YA COMMONWEALTH ‼️
Jamani mapichapicha yasiwadanganye 🤣 wala maneno ya kidiplomasia! Someni tamko rasmi! Tumebana kila kona 🔥👊🏽
Kabudi amekuwa mpoleee! Wamekubali timu ya Commonwealth iingie nchini na kufanya uchunguzi ikiwa ni pamoja na kukutana na wadau wote! Angalieni maamuzi ya Dec 2025 mkutano wa mawaziri ilihusu Tanzania na waliweka maazimio mazito hadi kumteua mjumbe maalum Mutharika - ingawa tumemweka kwenye mabano 😅
Sasa jana wameenda kusema “sawa basi njooni” 👊🏽 So tujiandae kuwaonyesha na kuwaeleza @commonwealthsec ukweli wote
Kumbukeni Bi Kizimkazi alimpiga stop Mutharika na msafara wake kuingia nchini na kuchunguza mauaji halaiki wakidai wameanzisha LITUME lao! Sasa wameambiwa wakubali kwanza au watimuliwe Commonwealth 😁. Walivyo wajinga wakajua wataficha ushahidi na mashahidi ila sasa wamefinywaaa 🤣imebidi waachie!
Huu ni ushindi kwetu sasa tuendelee kuibana Commonwealth na @SGCommonwealth wakutane na wahanga wa kweli si wa maCCM wauaji! Pia wakutane na vyama vyote watakavyo lakini CHADEMA isikosekane na Tundu Lissu atembelewe
Nje ya hapo hakuna cha maana!

Thank you @SGCommonwealth for the continued engagement on Tanzania and our hope is that the visit will be truly impartial without govt MINDERS and you will meet all stakeholders including @ChademaTZ2 and ensure the safety of those who will meet you. This is to make you understand that despite their suits and formal ties or maxi dresses, the CCM cabal led by @SuluhuSamia are VICIOUS and BRUTAL! There is not an ounce of kindness or politeness - it is a façade! They even engage in transnational abductions to silence us!
Kindly keep that in mind and stand with the PEOPLE of Tanzania and not the murderous illegitimate govt!
#TanzaniaMassacre #SamiaMustGo
1772953753062.jpg
 
Bawacha wa Mkoa wa Kagera ambao walikuwa wamezuiwa kituo cha Polisi Geita mjini tangu jana asubuhi, wameachiwa huru jioni hii.
1772989655342.jpg
1772989651828.jpg
1772989648456.jpg
 
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Mara, Chacha Heche , ameibuka kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook akijibu wito wa mdahalo wa kisiasa uliotolewa na Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kenani Kihongosi.

Katika ujumbe wake, Chacha Heche amesema mdahalo wa kisiasa unapaswa kuwa na vigezo vinavyoeleweka na kujikita katika masuala muhimu ya kitaifa badala ya kuwa mjadala wa maneno bila hoja zenye tija kwa wananchi.

Amesema iwapo mdahalo huo utaandaliwa kwa kuzingatia misingi hiyo, ni muhimu kujadili masuala yanayogusa maisha ya wananchi ikiwemo utawala bora, usalama wa raia, usimamizi wa rasilimali za nchi, mikataba ya kimkakati kama ile ya bandari pamoja na hali ya uchumi na ugumu wa maisha kwa wananchi.

Aidha, Chacha Heche amegusia pia suala la Tundu Lissu akisema linahitaji kuwekwa wazi kuhusu namna atakavyoshiriki mdahalo huo iwapo utaandaliwa.
Kauli ya Chacha Heche imekuja kufuatia wito wa mdahalo uliotolewa na Kenani Kihongosi wakati akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika wilayani Maswa mkoani Simiyu Machi 7, 2026.

Akizungumza katika mkutano huo, Kihongosi aliwataka viongozi wa upinzani Tundu Lissu na John Heche kujitokeza katika mdahalo wa wazi wa kisiasa ili kujadili hoja zao mbele ya wananchi.

“Nawaambia waje akae mmoja hapa, mwingine hapa kila mmoja aanze kupiga ukweli hapa. Mimi nawatamani wale, kama ni Heche njoo kaa hapa, kama ni Tundu kaa hapa, halafu tujenge hoja tuone watafika wapi, hawatakuwa na hoja watapaniki,” alisema Kihongosi.

Aliongeza kuwa Chama Cha Mapinduzi kinaamini katika kujibu hoja kwa kutumia takwimu na maelezo ya kina badala ya malumbano ya kisiasa.

“Sisi CCM hatufoki, hatugombi tunawapa data, kwa hiyo muwaambie waje tukae kwenye meza tuweke mdahalo halafu tuone hiyo battle ya hoja,” alisema.
1772990069743.jpg
 
Asanteni sana THRDC kwa kusimama nasi kukemea Ukandamizwaji wa Haki unaofanywa na Jeshi la Polisi dhidi ya BAWACHA.✊
1772990161359.jpg
1772990155504.jpg
1772990149944.jpg
 
#Habari_Njema.

Katibu Mkuu wa BAWACHA Taifa Mhe. Pamela Maassay pamoja na Viongozi na Wanachama 50 ambao walikuwa wamekamatwa leo Musoma mjini wakati wanatoka kwenye misa Kanisani, wameachiwa kwa dhama jioni hii.

Mungu awabariki watu wote mliopaza sauti kwa ajili yao.

Giza halijawahi kushinda NURU.
1772990454152.jpg
 
Je, ni uhalifu gani ambao BAWACHA walikuwa wanakwenda kuutekeleza huko Musoma?
1772990683693.jpg
 
Simba wa Tanganyika aliegoma kuwapigia magoti mafisadi wa mali za umma wa Tanganyika akiwa jela hawalali usingizi na akiwa nje ndio balaa kabisa🔥💪🏿🇹🇿
Neno moja kwa kamanda wa vita vyote asie na chembe ya uoga moyoni mwake.♥️♥️♥️♥️
1772993437039.jpg
 
Mkuu wangu Kalamu imeshakaa njema unaweza kurudi sasa😀💪🏿
Hsante mkuu 'Mshana jr'.

Kwanza nataka nitambue jitihada zako nzuri sana za kutoa taarifa juu ya mambo mbalimbali ya chama. Hii ni kazi nzuri sana; ambayo pengine wewe mwenyewe unaweza usijue umuhimu wake, na kwa uhudhuriaji mdogo kwenye mada muhimu kama hii. Hii ni kumbukumbu ya kipekee sana kuhusu maswala mengi ya chama. Kwa hiyo hata kama ushiriki wa uchangiaji hapa siyo mkubwa sana, lakini umuhimu huo wa kuweka kumbukumbu ni jambo muhimu sana.

Swala la pili ninalopenda kugusia, ni majaribu makubwa sana wanayopitia viongozi wa chama, na wanachama kwa ujumla wakati huu.

Kutokana na mambo mengi yanayofanywa dhidi ya chama, ni kama Samia na Genge lake wameamua kukitangazia chama hiki vita.

Ni wakati wa majaribu makubwa sana kwa viongozi wa chama.

Maoni yangu juu ya hili, ni kuwasihi viongozi hawa wawe na uhimilifu na uvumilivu mkubwa sana. Wasikate tamaa. Hiki ndicho kipimo cha juu kabisa cha kuwa mwamini juu ya unachokisimamia.

Hawa viongozi watafunguliwa mashtaka, na misukosuko mbalimbali. Wasishawishike kuingizwa kwenye mtego wa kuvunja sheria; wawe ndani ya sheria stahiki wakati wote. Watashinda tu.

Na ili kutodhoofisha chama kwa viongozi wao wakuu kunyimwa haki ya kutumikia chama, ni muhimu pawepo na ngazi za viongozi watakaochukua majukumu wakati walio juu yao wanapozuiliwa kufanya shughuli za chama.

CHADEMA inao wanachama wengi sana, hapawezi kukosa viongozi wa kuchukua nafasi wakati wenzao wanapokuwa wamezuiliwa kwa njia mbalimbali za kihujuma.

Sasa sijui kama hili la mwisho nimelieleza vizuri ili lieleweke.
Lengo ni kuwa CHADEMA haiwezi kudhoofishwa kwa kuwazuia viongozi wake kufanya shughuli za chama..

Naomba unisaidie kulieleza kwa kifupi kama umelielewa kwa njia yako.

Wanachofanya hili Genge chini ya Samia sasa hivi ni kutengeneza njia zilezile za kuachiana nmadaraka na kulindana katika uhalifu wao.

Inashawishi sana kutafuta njia za kuwaondoa kwa nguvu!
 
Back
Top Bottom