CHADEMA Special Thread

CHADEMA Special Thread

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinawataarifu wanachama wake na umma kwa ujumla kuwa wanawake wa BAWACHA kutoka Mkoa wa Kichama wa Kinondoni wamezuiwa na Jeshi la Polisi katika eneo la Mlandizi na kupelekwa katika Kituo cha Polisi Mlandizi.

Wanawake hao walikuwa katika msafara ulioanza safari leo jioni ukielekea Musoma, Mkoa wa Mara, kwa ajili ya kushiriki Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mwanamke Duniani yatakayofanyika tarehe 8 Machi 2026.

Katika tukio hilo, Jeshi la Polisi limewazuia madereva wa magari hayo na kuchukua vibali vya safari. Askari pia walifanya upekuzi katika magari ya msafara huo na kuchukua sare za maadhimisho ya wanawake pamoja na vifaa vinavyohusiana na CHADEMA ikiwemo mabango na fulana (T-shirts).

Wanawake hao wa BAWACHA wanaendelea kushikiliwa mpaka usiku huu katika Kituo cha Polisi Mlandizi. CHADEMA itaendelea kutoa taarifa kadri zitakavyopatikana.
1772859186893.jpg
 
Bunda Part 01.

Naomba part 01 tuanzie katika mwendelezo huu.

Anasimama Wakili Aloyce Osewe akimhoji shahidi wa Wasila.

Aloyce; je Ulitumia Utaalamu Upi Kutambua Hiyo Petroli?.

Shahidi; Kwa Kunusa.

Aloyce; Nisahihi Hujasema Gari La Mkuu Wa Wilaya Iliwachukua Wapi?

Shahidi; Kituo Cha Polisi.

Aloyce; Umesema Hapa Mahakamani Kwamba Magari Hayakwepo Ndiyomaana Mlitumia Gari La Mkuu Wa Wilaya

Shahidi; Sijasema.

Anapelekewa Maelezo Yake Ili ayaone na Kusoma.

Kuna Bonge La Tusi Shahidi analisema Hapa Lakini Kwenye Maelezo Yake Hilo Tusi Halipo🤣🤣🤣, anaulizwa kulithibitisha lakini anashindwa kwa sababu Hilo Tusi Kaliongeza Yeye mwenyewe😅

Anakaa wakili Aloyce .Anasimama Wakili Massaba.

Massaba; Nataka nikuonyeshe haya Maelezo ili ujue ni ya kwako ama ni mtu mwingine.

Anaendelea Massaba, Hebu ieleze mahakama namba yako ya polisi iko wapi hapa?

Shahidi; haipo.

Massaba; Anamwambia Hebu Soma Haya Maelezo ya Copy na Haya ya original.

Masaba; Hebu Ieleze Mahakama Ni Lini Uliitwa Kwenda Kuedit Tena?

Shahidi; Sijaitwa .

Massaba; Umesema Wewe Ulikua Kwenye Jengo la nini?

Shahidi; Ccm.

Massaba; Ulikua Unamiliki Simu Gani?

Shahidi; Smartphone

Massaba; Kuna Ushahidi Wowote Kwamba Ulileta Ushahidi Wa Kwamba Jengo Lilikua Zima na Sasa Limechomwa?

Shahidi; Sijasema.

Massaba; George Wilson Mauma Unamfahamu?

Shahidi; George Simfahamu, Namfahamu Mauma.

Massaba; Nikweli Kwamba Wakati Unatoa Ushahidi, Hukusema Wamevaa Nini, Husema Rangi Zao?

Shahidi; Sikusema.

Yaani huyu Shahidi Foustina Kila Kitu anajibu Sifahamu, Sijui, Sikusema. Watu wanacheka sana hapa🤣🤣🤣

Anapelekewa Tena Maelezo Yake ayasome.

Massaba; Umesema Jengo la Ccm Liko Sehemu Gani?

Shahidi: SARANGA

Massaba; Hapa Imeandikwa Wapi?

Shahidi; Bunda Store.

Watu wanaangua kicheko🤣🤣🤣

Faustina anachekesha Kwa kweli mpaka naye inabidi acheke tu😅.

Massaba; Kuna Mahali Umeeleza Kua Taarifa Ulizotoa Ndizo Zilisaidia Washtakiwa Kukamatwa.

Shahidi; Sijasema

Massaba; Kuna Mahali Ulieleza Muonekano Wa Watu Hao Ili Iwe Sehemu Ya Kusaidia Ukamataji?

Shahidi; Sikueleza.

Massaba; Kuna Mahali Umeeleza Namna Watu Hao Walivyochoma Jengo ?

Shahidi; Sijasema.

Massaba; Umesema Aliyewasha Moto ni nani?

Shahidi; Sifahamu.

Massaba; Kuna Mahala Umemtaja Jina Mkuu Wa Wilaya?

Shahidi; Hapana

Massaba; Humfahamu Mkuu Wa Wilaya?

Shahidi; Simfahamu.
Kichekoooo🤣🤣

Massaba; Tunakubaliana na Wewe Kwamba Jiwe Haliwashi Moto?

Shahidi; Nikweli.

Massaba; Nikweli Ulishuhudia Moto Unawaka?

Shahidi; Ndiyo

Massaba; Kuna Mahali Umeeleza Mahakama Kua uliwapigia Zima Moto?

Shahidi; Hakuna .

Anaketi wakili Massaba, Anasimama Wakili Dickson Matata..

Part 02 inakuja post inayofuata.

Naomba nisaidie kushare ili watu wengi zaidi wajue kinachoendelea Bunda.

Usisahau kufollow account ya Shija Shibeshi
1772859830208.jpg
 
Bunda Part 4
Anasimama Wakili Mahinyila kumhoji huyo Shahidi wa 4 anayeitwa WP 14298 Faustina Paul ambaye ni mwanadada na ni Askari Polisi.

Mahinyila: Shahidi nitakuuliza maswali na naomba ujibu kama nitakavyokuwa nakuelekeza ili tuokoe muda.

Mahinyila: Shahidi unafahamu washitakiwa wote 21 wanashitakiwa kwa makosa gani?

WP Faustina: Sifahamu.

Mahinyila: Kwahiyo umekuja kutoa ushahidi kwenye kesi ambayo hujui washitakiwa wameshitakiwa kwa kosa gani? Kweli au sio kweli?

WP Faustina: Ndio.

Mahinyila: Ni sahihi katika kazi yako ya Polisi kuna utaratibu wa kuingia kazini na kutoka?

WP Faustina: Ni sahihi upo. Huwa tunasaini kwenye Occurence book.

Mahinyila: Ndio huwa mnaita OB?

WP Faustina: Ndio tunaita hivyo.

Mahinyila: Je wakati wa kutoka pia kazini mnatokaje?

WP Faustina: Tunasaini vile vile kwenye kitabu.

Mahinyila: Na Je kuna utaratibu wowote wa kupangiana zamu za kuingia kazini?

WP Faustina: Upo huo utaratibu anapanga Afande OCS.

Mahinyila: Kwahiyo kuna utaratibu wa muda wa kuingia kazini na kutoka?

WP Faustina: Upo ndio.

Mahinyila: Kuna watu huwa wanaingia mchana au asubuhi au jioni?

WP Faustina: Huwa inakuwa hivyo inategemea na siku husika na majukumu yaliyopo?

Mahinyila: Nitakuwa sahihi nikisema mambo yote hayo yapo kisheria na msahafu wenu polisi yaani PGO katika PGO Na. 287 na 280 imeyasema?

WP Faustina: Ni sahihi PGO imesema hivyo.

Mahinyila: Sasa turudi kwenye ushahidi wako, wakati unatoa ushahidi ulisema kwamba uliingia kazini saa ngapi?

WP Faustina: Sikusema

Mahinyila: Ulitoka saa ngapi ulisema?

WP Faustina: Sikusema.

Mahinyila: Umesema kama ulisaini kwenye OB?

WP Faustina: Sikusema

Mahinyila: Umeileta hiyo occurence book hapa Mahakamani?

WP Faustina: Sijaleta

Mahinyila: Kwahiyo nitakuwa sahihi nikisema kwamba hadi sasa hatujui kwamba ulikuwa kazini au haukuwepo kazini siku hiyo kwasababu hujaleta OB wala hujasema uliingia kazini saa ngapi?

WP Faustina: Mimi niliingia kazini.

Mahinyila: Umeelewa swali kweli?

WP Faustina: Nina akili timamu.

Mahinyila: Huko kwenye una akili timamu au hauna akili timamu tutafika. Jibu swali langu, Je ni sahihi kwamba hadi sasa Mahakama haiwezi kujua ulikuwa kazini siku hiyo ya tar. 30 au haukuwepo au uliingia kazini saa ngapi na saa ngapi ukatoka?

WP Faustina: Haiwezi kujua kwa sababu sijasema.

Mahinyila: Umesema uko kitengo cha General Duty unachofanyia kazi wewe kama askari Polisi?

WP Faustina: Sahihi

Mahinyila: Sasa umeelezea maana ya General Duty kwa maana ya umeifafanulia mahakama?

WP Faustina: Sijaifafanulia.

Mahinyila: Ni sahihi umesema pale kituo cha Polisi ilipigwa filimbi mkakusanyika askari na mkapangiwa kwenda kulinda ofisi ya CCM?

WP Faustina: Sahihi

Mahinyila: Na ulisema gari iliyokuja kuwapeleka kulinda Ofisi ya CCM ni gari ya Mkuu wa Wilaya ya Bunda? Kweli au sio kweli?

WP Faustina: Ni kweli.

Mahinyila: Hivi Polisi hapa Bunda huwa mkiwa mnatekeleza majukumu yenu huwa mnatumia gari ya Mkuu wa Wilaya Bunda kwenda kwenye majukumu yenu?

WP Faustina: Sijui

Mahinyila: Kwani toka uanze kazi ya Polisi umewahi kupanda gari yoyote ya Polisi?

WP Faustina: Sijawahi kupanda

Watu wanacheka. Ni polisi gani ambaye hamjawahi kupanda gari ya polisi?😂😂😂 Ngoja tuone.

Mahinyila: Kwahiyo Mara ya kwanza ulipanda gari ni hiyo ya Mkuu wa Wilaya Tar. 30/10/2025? Kweli au sio kweli.

WP Faustina: Kweli

Mahinyila: Kweli au sio kweli Kwamba hujasema kwanini siku hiyo ilikuja gari ya Mkuu wa Wilaya kuwabeba Polisi na kuwapeleka kulinda ofisi ya CCM?

WP Faustina: Ni kweli sikusema.

Mahinyila: Umesema hapa kuhusu matusi ya hao waandamanaji kwamba walisema Polisi waseng*** na mengine matusi kibao umeyasema mimi sitaki kurudia?

WP Faustina: Nimesema hayo matusi kweli.

Mahinyila: Je washitakiwa wameshitakiwa kwa kosa la kutoa matusi?

WP Faustina: Sifahamu

Mahinyila: Nani anayefahamu?

WP Faustina: Sijui.

Mahinyila: Kwahiyo wewe hujui kama wameshitakiwa kwa kosa hilo na pia hujui nani anayejua jambo hilo?

WP Faustina: Sijui ndio

Mahakama yote kicheko
Part 05 itafuata kwenye post inayokuja.

Share,like, comment kwa wingi na follow Shija Shibeshi
 
Bunda Part 02
Anasimama Wakili Dickson Matata.

Matata; Nikweli Haya ni Maelezo Yako?

Shahidi; Nikweli..

Matata; Haya Majina Ni Yako na Sahihi Ni Yako?

Shahidi; Nikweli.

Matata; Kwahiyo Unakubali Yapokelewe?

Shahidi; Ndiyo.

Matata; Mheshimiwa Hakimu Naomba Maelezo Yapokelewe.

Wakili Wa Serikali Anasimama na Kukataa Yasipokelewe😂😂😂

Nikama Maelezo Ya Shahidi Wao Amejikanyaga Kiasi Cha Wao Kuona Wanaenda Kudhalilika..

Anaendelelea Matata; Mhe hakimu, haya ni maelezo ya Shahidi Aliyeko Hapa,na Maelezo Yake Yanakidhi Kupokelewa hivyo Wakili Wa Serikali Hawezi Kukataa Maana Shahidi Mwenyewe Amekubali Maelezo Yake Yapokelewe..

Matata amekaa na Kumwambia Shahidi naye Akae..
Kimeumana😂😂
Haya ndiyo madhara ya kutengeneza Kesi za Michongo.

Part 03 itafuata kwenye post inayokuja.

Like,share, comment na follow Shija Shibeshi
 
Breaking News;

Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Dar es Salaam imeyatupilia mbali mapingamizi yaliyowekwa na Said Issa Mohammed na wenzake kupinga Lissu kuunganishwa katika Kesi ya Mgawanyo wa Mali inayowakabili Katibu Mkuu wa CHADEMA na Bodi ya Wadhamini.

Uamuzi huo umetolewa na Jaji Hamidu Mwanga leo Machi 03, 2026 baada ya kutupilia mbali mapingamizi mawili yaliyowekwa na Wakili wa walalamikaji(Said Issa Mohammed na Wenzake)

Kwa msingi huu maombi ya msingi ya Lissu yatasikilizwa Ijumaa saa tatu asubuhi mbele ya Jaji Hamidu Mwanga.

Taarifa kamili tutakuletea hivi punde
1772860354339.jpg
 
Huu ni kama uchuro, mkuu 'Mshana Jr' iwapo tayari tunaanza kukubali ya huko 2030.

Ina maana Mzee Butiku na mashetani wenzie tayari wameibuka kidedea?

Hiyo 2030 unayoizungumzia wewe, naina Tanzania ikishatengemaa muda kitambo sana, kiasi kwamba ya 2026 yatakuwa ni historia mbaya iliyopita muda mrefu sana.

Kama CHADEMA na wao wanasubiri 2030, boti wataikuta shang'oa nanga muda kitambo sana.

Hii ni mada mbaya sana, hata sijui imeingiaje ndani ya akili zako.

Nimemaliza kuchangia, sirudi tena kwenye mada mbovu kama hii.
Mkuu wangu Kalamu imeshakaa njema unaweza kurudi sasa😀💪🏿
 
Nchi hii hakuna sheria wala utaratibu wa polisi kupangia mtu aende wapi, au asiende wapi..

Polisi Tanzania hawana mamlaka kisheria wala kikatiba kuingilia uhuru wa watu kwenda wanapotaka wao wenyewe..

Polisi Nchi nzima wameweka barriers wanakamata viongozi na wanachama wa Bawacha waliokua wanaenda Musoma kusherekea Siku ya wanawake Duniani.

Magari yaliyobeba viongozi hawa yanakamatwa na wanashikikiwa maeneo mbalimbali ya Nchi bila sababu… Dakawa, Mlandizi, Geita na maeneo mengine.

Hili jaribio la kuzia watu kufanya movement ndani ya Nchi na kuzia watu kufanya shughuli zao halali, Wengine wanaweza kufikiri litaishia kwa Chadema..

Tukiruhusu madikteta wachache wao ndio waamue, wapi twende wakati gani, tule au tusile, tulale au tukeshe itakua hatari kubwa mno..

Uhuru uliopiganiwa na wazee wetu hauna maana tena katika mazingira haya


View: https://www.facebook.com/share/v/1FixU7YnbC/
 
ASKOFU AANDIKA WARAKA KWA BAWACHA

Mheshimiwa Pamella Massay!
Katibu Mkuu, Baraza la Wanawake CHADEMA

Sisi pia tunafuatilia kwa karibu jinsi ambavyo watawala walivyotumia Jeshi la Polisi ili kuzuia Mkutano wenu wa Siku ya Wanawake Duniani mliopanga kufanya kule Musoma mkoani Mara. Tumeuona pia waraka wa Kanisa Katoliki wa kuwasitisha matumizi ya ukumbi. Waraka huo unaonyesha pia kulikuwa na mashinikizo dhidi yao kuwasitishia ukumbi.

Tunaandika ujumbe huu kwa lengo la kuwatia moyo wanawake wa BAWACHA wanaozuliwa katika vituo vya Polisi nchini kote au ambao pia wamezuiliwa barabarani. Tzmekisikia kilio cha wanawake wa BAWACHA ambao hawajapewa chakula tangu washikiliwe.

Ujumbe wetu ni kuwa mamlaka zote kandamizi duniani zinapokaribia kuporomoka huzidisha kufanya ukatili na unyanyasaji. Hiki sio kipindi cha ninyi kukata tamaa. Bibi Winnie Mandela kule nchini Afrika Kusini hakuwa na Baraza la Wanawake wa ANC lenye nguvu na ari kubwa kama BAWACHA, lakini aliweza kuwatia moyo wanawake wote wa ANC na kuwaunganisha wanawake wote wa Afrika Kusini kupambana na mfumo kandamizi wa Ubaguzi wa Rangi (apatheid) wakati Nelson Mandela na Walter Sisulu wakiwa gerezani.

Giovani Mbeki, Oliver Tambo walipoikimbia nchi na kuongoza mapambano kutokea nje ya nchi, walitegemea sana nguvu ya Bibi Winnie Mandela na wanawake wengi waliokuwa ndani ya Afrika Kusini. Bibi Winnie Mandela alipatiwa kadhia za kila namna kutoka kwa watawala na vikaragosi wao, lakini hakukata tamaa.

Huu sio wakati wa kutegemea nguvu ya taasisi nyingine ili zilete ukombozi katika taifa hili kwa kuwa nyingi ya taasisi hizo zimefinywa na sasa haziwezi kuongea tena. Huu sasa ndio wakati wenu ninyi wanawake mlio mstari wa mbele na ambao mnajitambua kusonga mbele hadi pale mfumo huu kandamizi utakapoporomoka wote.

Kuna kundi kubwa la watu walio nyuma yenu ingawa wanaishi katika woga wa kutekwa na kupotezwa. Ninyi mmekuwa ndio taraja pekee la kwao lililobakia. Ole wenu mkate tamaa sasa wakati huu ambapo mpira wa mnati umetakata na kamba ya manila imetemewa mate ya sumu na mchwa wa Rhotia na Katesh.

Dunia pia unatazama jinsi ambavyo mfumo wa ukandamizaji unavyokandamiza watu wake bila sababu za msingi. Uwongo wao kuwa nchi hii imetulia utaweza kusambaa endapo wanawake wa BAWACHA nao watakata tamaa. Hizo kelele zenu zinawaumiza watawala na pia kuwanyima usingizi. Msiwape usingizi hadi wote wakubali kusikiliza matakwa ya wananchi.

Tunawaombea na tuombeeni na sisi kwani na sisi pia hatuko salama hasa kwa sababu ya sisi kuwatia moyo ninyi na wapambanaji wengine. Ujumbe huu usomwe Mikoa yote ya BAWACHA na katika Wilaya na Majimbo yenu yote na hata katika vituo vya polisi.
Je, nini kimekushangaza? Je, nini maoni yako?

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Itunge, Dar es Salaam; 7 Machi 2026; Saa 6:25 mchana
1772887034523.jpg
 
Baada ya BAWACHA Kibamba na Segerea kuona hakuna dalili ya Polisi wa Gairo kuwaachia waendelee na safari,

Wameamua kuanza kuvaa sare zao, wanasema kwamba watafanya maadhimisho hapo hapo njee ya kituo cha Polisi.
1772887736445.jpg
 
Back
Top Bottom