CHADEMA ndani ya Songea mjini

CHADEMA ndani ya Songea mjini

Mbona kwenye hizo picha nawaona vijana tu,tena wale waliokaa kibange bange!

Inaonyesha we ni juha wa machipuko ya ukombozi dunia ya leo inakombolewa na vijana na si wazee! Ielewe sign yangu hapo chini kiongozi!!
 
Siku Moja kabla kulikuwa na mkutano wa CCM ambao uliwatisha na kuwazuia watu wasiende kwenye mkutano wa chadema,walifanya mkutano katika kata zote nakuwaambia mabomu yatapigwa kwakuwa chadema ni chama cha wahuni na fujo,baada ya kuona hii moyo wangu umekuwa na amani sana.
Mara nyingi nimesikia kwenye hii mikutano wananchi wanasema wameelimika hawatadanganywa tena,wanasema wako tayari kwa lolote au hizo beti CCM hawajasikia wanapoteza wakati hakuna mwananchi asiye jua leo hii kwamba yeye ni mmoja wa wakombozi wa kweli wa nchi hii pamoja tutaweza
 
Kweli watz wameamka sababu ya maisha ya magumu!!!!!
Wakuu hiyo picha ni live naifahamu Songea nimesoma hapo Box 2!!!
 
May 14



2.JPG

1.jpg


KATIKA kile kinachoonekana kuwa ni kumshinikiza Rais Jakaya Kikwete kutekeleza ahadi alizotoa wakati wa kampeni za urais mwaka jana, Chadema kimesema kitatumia kura za maoni kumwajibisha ikiwa atashindwa kuzitekeleza.Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa aliwaambia maelfu ya wakazi wa Mji wa Songea mkoani Ruvuma kuwa wamegundua kwamba katika nchi nyingine, akitolea mfano, Japan, kama waziri mkuu wao akishindwa kutimiza ahadi zake, wananchi hupiga kura za maoni.

Akihutubia mkutano wa hadhara katika Uwanja wa Shule ya Msingi Kibulangoma, Dk Slaa alisema chama chake kilipoanza kuandamana, Rais Kikwete alisema kuwa wanapanga njama za kumwondoa madarakani na kutokana na hilo, kiliamua kuchunguza sababu za Rais kutoa kauli hiyo.

"Serikali ikichaguliwa si lazima akae miaka mitano ikiwa ni kama hajatekeleza ahadi za wananchi na kama hatupi elimu bora na bure kushusha bei ya sukari na mabati. Kama ameshindwa hilo tutamwondoa kwa kura za maoni," alisema Dk Slaa."Tutaandamana na kupiga mchakamchaka ili hoja zetu tulizoahidiwa zitekelezwe kupitia Bunge kwa kuwa nchi itakalika kama wananchi wana amani na maisha mazuri," alisema Dk Slaa.

Alidai kuwa Rais Kikwete amekuwa hawajali wananchi ikiwa ni pamoja na kutokuwashukuru kwa kumpigia kura, akidai kwamba tangu aingie madarakani katika awamu hii, amekuwa akisafiri nje ya nchi badala ya kuwatembelea wananchi wake."Kikwete atueleze alichaguliwa na Ulaya au Tanzania, anasafiri nje kila mwezi badala ya kuwashukuru wananchi waliomchagua," alisema Dk Slaa.

Katika hatua nyingine, Dk Slaa alisema kuwa CCM kimekuwa kikiishambulia Chadema kuwa kinafanya ufisadi kwa kununua magari yaliyotumika, akisema walishasema kwamba watanunua malori ya Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe kwa kuwa wamekuwa wakiyatumia tangu yakiwa mapya
 
Watanzania lazima kieleweke Tanzania. Kila Mtanzania lazima afahamu haki yake na kuidai kwa hawa mafisadi wa ccm. Nia ya hii mikutano lazima kuwaelimisha watanzania na wajue hii nchi ni ya kwao na hawa wanaojiita viongozi wa mikoa, wilaya na vijiji wanatakiwa kufanya kazi. Kila Mtanzania lazima apate nguvu ya kuwauliza hawa makada wa ccm mikoani wakila fedha za wananchi na kusafiri kwa matumizi ya tax payer funds. Nchi nzima lazima ijue kwamba tunaweza kulazimisha ripoti za matumizi na fedha zote zinazoletwa na federal gov mikoani, hii ni haki yako kuuliza maswali tusitegemee kukaa majumbani na kutegemea mkuu wa mkoa atajitolea kuwaeleza wananchi wa mkoa wa Ruvuma kiasi gani anapata kutoka federal gov na jinsi gani wanazitumia.

Waandishi wa habari pia ndio wamekuwa wahujumu wakubwa Taifa letu kama ccm, inawezekana kabisa hawa waandishi wa habari Tanzania hawana uwezo wa kufikiria au wananyimwa haki yao ya kufanya kazi kwa uhuru.

"Tuendelee kuelimisha Taifa na Uhuru wa Ukweli Umefika"
 
Mungu Saidia CHADEMA na watu wake wote katika kuleta ukombozi wa kweli Tanzania
 
Hawa wote ni wachaga? Nakuuliza wewe Nape au tukupe mji?

Gerrard,

Ukimuuliza hawezi kuleta Jibu hapa JF.Hana uwezo mkubwa kiasi hicho hadi aje hapa kujibu hoja.Unamuonea,tafadhali muache upate thawabu.

Is it not shameful that Almost every issue gets the tribalism sickness, even in a POLITICS thread which should be for vigorous, honest and progressive conversation? We need to CHANGE this attitude to make any progress as a Country. For those who won't change but rather foster and accelerate the spread and perpetuity of this Cancer, We are the reason why Tanzania cannot make Any meaningful progress.

Please, let us stop and be mature and let us think and Approach issues as ONE PEOPLE. It is time to rise above the TRIBALISM that has not brought us any meaningful progress. While the host countries we travel to or talk about, often in positive terms, make progress,it is disgraceful that TRIBALISTIC sentiments and topics are What we spend our days talking about.
 
Wakuu... yale maandamano ya CHADEMA ya amani ya kupinga ugumu wa maisha yanayoende mikoa ya kusini. Leo yanafanyika hapa Songea mjini yakiongozwa na m/kiti taifa Mbowe na Katibu mkuu Dr.Slaa. Yataanza saa saba kuanzia Msamara mpaka Lizabon (km4), ambapo kutakuwa na mkutano mkubwa wa hadhara. Makamanda mbalimbali wa chadema wanategemewa kuwasili hapa wakiwa full team...wabunge wote na baadhi ya viongozi wa kitaifa CHM

hapa mjini mambo yameshaanza kupamba moto... watu wana shangwe kubwa na wameshasogea eneo la tukio. Kiufupi Songea ni ngome Kubwa ya Chadema Lakini mara zote CCm wanachakachua kuna madiwani zaidi ya 8kati ya 12. ni jimbo linaloongozwa na Nchimbi, wz michezo na utamaduni

Kuna pikipiki nyingi saana sijapata kuona, vijana wote wana bendera, cap na skaf za CDM
mambo yapo hot... stay tuned

MSIKILIZE ZITTO:

Download or Listen online here ZITTO IN SONGEA

2.JPG

1.jpg

attachment.php

attachment.php




attachment.php


Inafurahisha sana, na inatia moyo watanzania wenzangu kwa mwendo huu tutarajie Tanzania mpya na ya kisasa, tuachane na hao wa magamba. Ninakubali watanzania wanausongo wa kubadilisha nchi yao ili waweze kuiendesha wenyewe kutokana na sehemu husika sio kuendeshwa kama gari bovu. Tupambane tuiondoe mikononi mwa hao mafisadi wasiokuwa na utu hata kidogo. Ombi langu kwenu ndugu zangu watanzani hapa jf na wengine uongozi uliopo hapo chadema usiguswe kabisa mpaka tutoke kwenye makucha yaliyotubana. Mnaona jinsi wamagamba wanavyotupa theard za kumshambulia Mboye. Tunaona Uongozi wa chadema kwa ushirikiano wao kazi wanayoifanya sisi tuwape matumaini. Lengo la watanzania wengi kutokana na katiba ya chadema wanataka nchi yetu iwe kwenye mfumo wa kisheria sio kubahatisha sheria kama CCM wanavyofanya. Tukifanikiwa kuingiza nchi yetu kwenye mfumo wa kisheria tutakuwa tumetoka kwenye utumwa na hata somo la siasa litafundishika mashuleni sio kama kipindi cha CCM.

MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE NA VINGOZI WOTE WA CHADEMA. AMEN
 
hawa jamaa narudia tena wanapumulia mashine siku zao zinahesabika janja yao kwisha inchi yetu tutaikomboa muda si mrefu
 
Wakuu... yale maandamano ya CHADEMA ya amani ya kupinga ugumu wa maisha yanayoende mikoa ya kusini. Leo yanafanyika hapa Songea mjini yakiongozwa na m/kiti taifa Mbowe na Katibu mkuu Dr.Slaa. Yataanza saa saba kuanzia Msamara mpaka Lizabon (km4), ambapo kutakuwa na mkutano mkubwa wa hadhara. Makamanda mbalimbali wa chadema wanategemewa kuwasili hapa wakiwa full team...wabunge wote na baadhi ya viongozi wa kitaifa CHM

hapa mjini mambo yameshaanza kupamba moto... watu wana shangwe kubwa na wameshasogea eneo la tukio. Kiufupi Songea ni ngome Kubwa ya Chadema Lakini mara zote CCm wanachakachua kuna madiwani zaidi ya 8kati ya 12. ni jimbo linaloongozwa na Nchimbi, wz michezo na utamaduni

Kuna pikipiki nyingi saana sijapata kuona, vijana wote wana bendera, cap na skaf za CDM
mambo yapo hot... stay tuned

MSIKILIZE ZITTO:

Download or Listen online here ZITTO IN SONGEA

2.JPG

1.jpg

attachment.php

attachment.php




attachment.php


asante mkuu,REVOLUTION for CHANGES....
 
Ngoja nipige magoti niendelee na sala yangu....

"Mungu baba mtakatifu, uketie mahali pa juu patakatifu..... nakuja mbele zako nalileta taifa lako hili teule, Tazama wanao sisi (watz) kwa namna ya peke tumepata imani ya ukombozi wa taifa letu kupitia watu wako wateule ambao kwa uwezo wako wameweza kumgusa kila mtz mwenye dhiki na aliyekandamizwa na umasikini wa kutisha, ninaomba ukazidi kuwatia nguvu katika mapambano haya ya haki, ukawaepushe na dhuruba zote za mitafaruku ya kisiasa, ukawaimarishe wakaendelee kusimama vyema katika kuendelea kupigania hadhi ya maisha ya heshima ya mtanzania. Sana na zaidi kabisa ukatupe jicho la kimapinduzi kwa kadiri tunavyoikaribia 2015 tukaendelee kuwa na moyo huu wa kufikia mabadiliko tunayoyatamani kwenye nchi yetu.
Kwa jina lako lililokuu, nmeomba.... wote tuseme, Ameeeeeen"

Ameeen......,
 
headline_bullet.jpg
Ukiritimba uliokithiri
headline_bullet.jpg
Ufisadi wa mabilioni
headline_bullet.jpg
Ubovu mitaala ya elimu
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema dawa pekee ya kumaliza tatizo la umaskini uliokithiri miongoni mwa Watanzania wengi nchini ni kuondoa ukiritimba na ufisadi. Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama hicho Taifa, Wilfred Lwakatare, alisema hayo alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Mgazini, Kata ya Kilagano, Wilaya Songea Vijijini, mkoani Ruvuma jana. Mkutano huo ni wa kwanza kati ya mikutano mitatu ya hadhara iliyofanywa na Lwakatare, uliofuatiwa na ule alioufanya katika kituo cha mabasi cha mjini Peramiho na katika Uwanja wa Shule ya Msingi ya Lilambo, Songea mjini.

Lwakatare ni miongoni mwa viongozi waandamizi wa Chadema walioko katika timu sita zinazoendesha operesheni maalum ya chama hicho nchini inayohusisha maandamano na mikutano ya hadhara, kwa lengo la kuishinikiza serikali kusikiliza kilio cha wananchi, ukiwamo umaskini na hali ngumu ya maisha. Operesheni hiyo, ambayo ni muendelezo wa ile iliyofanyika katika mikoa ya Kanda ya Ziwa, inayohusisha mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Kagera na Mara mwezi uliopita, ilianza Mei 6, mwaka huu, katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini, mkoani Mbeya. "Dawa ya umaskini ni ndogo. Ni kuondoa ukiritimba na ufisadi," alisema Lwakatare, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu Taifa na Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Kagera.

Alisema ukiritimba unaonekana katika serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM), ni pamoja na kushindwa kutengeneza barabara nyingi vijijini na hivyo kuwafanya wananchi kupata tabu ya kusafirisha mazao wanayoyalima kuyapeleka kwenye masoko. Pia alisema Sh. bilioni 133 zilizokuwa kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (Epa) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kama zisingeibwa na wajanja wachache, zingeweza kutumika kujenga vyumba 19,000 vya madarasa na kusaidia watoto wa maskini kupata elimu bila tabu.

Alibainisha kuwa, chini ya CCM kamwe umaskini hauwezi kuondoka nchini kwani badala ya kushughulikia tatizo hilo, imekuwa ikiendekeza propaganda kupitia nyimbo za kikundi chake cha burudani cha Tanzania One Theatre (TOT) kuwahadaa Watanzania kwamba, 'wanapendeza', huku wengi wao wakiishia kuusikia mlo wa asubuhi (chai) redioni. Lwakatare alisema chama hicho kimekuwa kikiulea umaskini na imekuwa ikiutumia kama ndoano ya kuvuna kura za wananchi nyakati za uchaguzi.

Alizifananisha shule za sekondari za kata sawa na vituo vya kukulia watoto kutokana na kukosa nyenzo za kufundishia, kama vile maabara. Lwakatare alisema Mbunge wa Peramiho, Jenista Mhagama, ni miongoni mwa wabunge wa CCM, ambao wamekuwa wakipitisha bajeti za mabilioni ya shilingi bungeni kwa ajili ya kujenga shule za kata lakini zikishajengwa wabunge hao awawapeleki watoto wao kwenda kusoma kwenye shule hizo. "Wanajua shule hizi hazitatoa madaktari na wataalamu wengine. Badala yake wanawapeleka watoto wao kwenda kupata elimu nzuri Ulaya. Matokeo yake imekuwa akiondoka Kawawa anakuja Kawawa, akiondoka Mwinyi anakuja Mwinyi," alisema Lwakatare.

Alisema CCM imekuwa na tabia ya kuwahitaji wananchi wakati wa uchaguzi tu, mithili ya kuku wa kienyeji, ambaye mmiliki wake akihitaji kitoweo, humdanganya kwa mahindi ili amkamate na kumchinja. "Kama Tanzania bila ukimwi inawezekana, basi Tanzania bila CCM pia inawezekana," alisema Lwakatare. Aidha, alisema vijiji vinavyoongozwa na CCM, havina maendeleo, na kuwataja wananchi kujiunga na Chadema kwa sababu inauwezo wa kuleta mabadiliko nchini.

Lwakatare alisema ndani ya CCM kuna makundi matatu; kuna 'CCM tafuta kivuli', 'CCM maslahi' na 'CCM kiherehere'. Alisema miongoni mwa wanaoteseka nchini, ni askari polisi, ambao wengi wao wamekuwa wakiishi katika nyumba za mateso. "Kule kwetu Kagera askari wamejengewa nyumba, juu bati, pembeni bati. Likija jua mnaokwa kama mikate, ikija baridi utadhani mochwari gani sijui.
Sasa haya ni maisha gani?" alihoji Lwakatare.

Kabla ya kuhutubia mkutano huo, Lwakatare akiongozana na viongozi wa Chadema Mkoa wa Ruvuma, alifungua matawi matatu ya chama likiwamo tawi la Mapambano Kata ya Majengo, Londoni na Kichangani, yaliyoko mjini Songea na Songea Vijijini.
IPPMedia
 
smart rwakatare sasa naona kweli rwakatare ni mali chadema kwa kupangilia hoja zake namkubali, wanangeni ccm hatuwataki tulikuwa hatujapata mesenja kufikisha ujumbe vijijini
 
headline_bullet.jpg
Ukiritimba uliokithiri
headline_bullet.jpg
Ufisadi wa mabilioni
headline_bullet.jpg
Ubovu mitaala ya elimu
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema dawa pekee ya kumaliza tatizo la umaskini uliokithiri miongoni mwa Watanzania wengi nchini ni kuondoa ukiritimba na ufisadi.
Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama hicho Taifa, Wilfred Lwakatare, alisema hayo alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Mgazini, Kata ya Kilagano, Wilaya Songea Vijijini, mkoani Ruvuma jana. Mkutano huo ni wa kwanza kati ya mikutano mitatu ya hadhara iliyofanywa na Lwakatare, uliofuatiwa na ule alioufanya katika kituo cha mabasi cha mjini Peramiho na katika Uwanja wa Shule ya Msingi ya Lilambo, Songea mjini.

Lwakatare ni miongoni mwa viongozi waandamizi wa Chadema walioko katika timu sita zinazoendesha operesheni maalum ya chama hicho nchini inayohusisha maandamano na mikutano ya hadhara, kwa lengo la kuishinikiza serikali kusikiliza kilio cha wananchi, ukiwamo umaskini na hali ngumu ya maisha. Operesheni hiyo, ambayo ni muendelezo wa ile iliyofanyika katika mikoa ya Kanda ya Ziwa, inayohusisha mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Kagera na Mara mwezi uliopita, ilianza Mei 6, mwaka huu, katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini, mkoani Mbeya.
"Dawa ya umaskini ni ndogo. Ni kuondoa ukiritimba na ufisadi," alisema Lwakatare, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu Taifa na Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Kagera.

Alisema ukiritimba unaonekana katika serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM), ni pamoja na kushindwa kutengeneza barabara nyingi vijijini na hivyo kuwafanya wananchi kupata tabu ya kusafirisha mazao wanayoyalima kuyapeleka kwenye masoko. Pia alisema Sh. bilioni 133 zilizokuwa kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (Epa) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kama zisingeibwa na wajanja wachache, zingeweza kutumika kujenga vyumba 19,000 vya madarasa na kusaidia watoto wa maskini kupata elimu bila tabu.

Alibainisha kuwa, chini ya CCM kamwe umaskini hauwezi kuondoka nchini kwani badala ya kushughulikia tatizo hilo, imekuwa ikiendekeza propaganda kupitia nyimbo za kikundi chake cha burudani cha Tanzania One Theatre (TOT) kuwahadaa Watanzania kwamba, 'wanapendeza', huku wengi wao wakiishia kuusikia mlo wa asubuhi (chai) redioni. Lwakatare alisema chama hicho kimekuwa kikiulea umaskini na imekuwa ikiutumia kama ndoano ya kuvuna kura za wananchi nyakati za uchaguzi.

Alizifananisha shule za sekondari za kata sawa na vituo vya kukulia watoto kutokana na kukosa nyenzo za kufundishia, kama vile maabara. Lwakatare alisema Mbunge wa Peramiho, Jenista Mhagama, ni miongoni mwa wabunge wa CCM, ambao wamekuwa wakipitisha bajeti za mabilioni ya shilingi bungeni kwa ajili ya kujenga shule za kata lakini zikishajengwa wabunge hao awawapeleki watoto wao kwenda kusoma kwenye shule hizo. "Wanajua shule hizi hazitatoa madaktari na wataalamu wengine. Badala yake wanawapeleka watoto wao kwenda kupata elimu nzuri Ulaya. Matokeo yake imekuwa akiondoka Kawawa anakuja Kawawa, akiondoka Mwinyi anakuja Mwinyi," alisema Lwakatare.

Alisema CCM imekuwa na tabia ya kuwahitaji wananchi wakati wa uchaguzi tu, mithili ya kuku wa kienyeji, ambaye mmiliki wake akihitaji kitoweo, humdanganya kwa mahindi ili amkamate na kumchinja. "Kama Tanzania bila ukimwi inawezekana, basi Tanzania bila CCM pia inawezekana," alisema Lwakatare. Aidha, alisema vijiji vinavyoongozwa na CCM, havina maendeleo, na kuwataja wananchi kujiunga na Chadema kwa sababu inauwezo wa kuleta mabadiliko nchini.

Lwakatare alisema ndani ya CCM kuna makundi matatu; kuna 'CCM tafuta kivuli', 'CCM maslahi' na 'CCM kiherehere'. Alisema miongoni mwa wanaoteseka nchini, ni askari polisi, ambao wengi wao wamekuwa wakiishi katika nyumba za mateso. "Kule kwetu Kagera askari wamejengewa nyumba, juu bati, pembeni bati. Likija jua mnaokwa kama mikate, ikija baridi utadhani mochwari gani sijui.
Sasa haya ni maisha gani?" alihoji Lwakatare.

Kabla ya kuhutubia mkutano huo, Lwakatare akiongozana na viongozi wa Chadema Mkoa wa Ruvuma, alifungua matawi matatu ya chama likiwamo tawi la Mapambano Kata ya Majengo, Londoni na Kichangani, yaliyoko mjini Songea na Songea Vijijini.
IPPMedia

Ahsante kumbe hayo makundi ndio yanayopambana tutayodonoa kama mwewe!!
 
CCM walivua gamba la unyerere na kuvaa lao ambalo linakitesa chama na kwa kweli halivuliki kirahisi. Ukiangalia historia ya familia ya Nyerere hakupenda kuwaingiza watoto wake kwenye siasa au serikalini kwa mgongo wake, na hivyo heshima yake ilisheheni na kupevuka.

CCM ya leo na viongozi wao ni tofauti na itikadi za mtazamo wa Nyerere, na ukiangalia safu ya uongozi utaona ni kile alichokisema Nape chama cha ukoo na viongozi wa ukoo kinyume na alivyoelekeza mashambulizi dhidi ya Chadema. Baba kabla hajang'atuka anamwandaa mwanawe kushika hatamu, na anapong'atuka ameshamtarisha na mwendelezo unakuwa wa mfumo wa kitemi. Haya yapo tunayaona kila siku lakini leo Nape anaelekeza kombora kwa Chadema wakati hakumbuki baba yake Moses Mnauye alikuwa kiongozi mwandamizi huko aliko.

Mwingine ambaye huna mkubwa katika serikali na chama cha CCM vigumu mno kupenya maana huko inategemea jina la mtangulizi wako katika siasa au chama, vinginevyo utaishia kuwa msindikizaji.
 
Back
Top Bottom