CHADEMA na polisi katika mtifuano mkali

CHADEMA na polisi katika mtifuano mkali

bwana Jasusi
Tanzania kinachotusumbua ni kuwa na watu wanaopenda kitu kidogo,hii nchi hata wakipewa chadema,kama hatutakuwa na watu wanaofanya kazi kwa uzarendo itakuwa ni kila siku kuilaumu serikali itakayokuwa serikalini,unadhani ni kwanini viwanda hivyo vimekufa? je hatukuweza kusimamia visife? ni kwanini viwanda vya kurosho toka 25 mpaka hakuna kitu,je korosho hazilimwi tena? je waliopewa kazi ya kusimamia mashirika ya umma hawayaoni hayo? KITU KIDOGO
watendaji tuliowapa mamlaka ya kusimamia mali za umma hawafanyi kama inavyotakiwa,ni lazima tubadili mfumo wetu wa utendaji kazi,narudia hata chadema wakiingia madarakani,kama watu hawatatimiza wajibu wao ktk maneo yao ya kazi itakuwa ni lawama hata ktk hiyo serikali itakayo ongozwa na chama kingine.
Tanzania si masikini,ila watendaji waliopewa mamlaka ndio tatizo.
sheria zetu ni nzuri sana,mipango yetu ni mizuri sana na sera zetu ni nzuri sana,tatizo ni wanaopewa kazi ya kusimamia hayo yote niliyoyataja

Mkuu unayoyasema ni kweli kabisa. Na hapo ndipo tunaona kuwa CDM angalau inaonyesha kuwa sheria zipo nzuri lakini kwa makusudi kabisa hazifuatwi kwa sababu au za kifisadi au uzembe wa kepeana vyeo kirafiki na kichama chama zaidi bila kujali utaalamu na kutukuzana kijinga jinga tu huku ubabe ukitumika kuteketeza wale wazalendo wenye nia thabiti ya kuiendeleza nchi. Sheria ndiyo tunazo nzuri nyingine tuliiga tu lakini kwa maslahi ya CCM hazifuatwi! Umeona hata Bunge linavyoendeshwa, kibabe babe tu! sasa kama mhimili muhimu kwa Taifa unaendeshwa kwa siasa za kibabe namna ile unashauri nini?
Itakuwa busara kabisa Chadema ikaingia nayo ikafanya makosa yake lakini tunaamini yapo watakayoyamudu na wengine tena watafuata na ndiyo maana ya Demokrasia na maendeleo ndivyo yanavyochangiwa katika nchi. Siyo chama kimoja kikae madarakani mika 70 kikituzalishia familia za kifalme zenye ubinafsi zinazojali elimu na afya za familia zao tu.
 
Hivi unadhania nchi inaweza kuendelea bila wawekezaji?Tatizo lenu nyie mnataka attention sana na mnaitafuta hii attention bila kujali waathirika wa haya maandamano na vurugu zenu, Wakipoteza maisha mnachofanya ni kuzunguka na picha zao kuonyesha huko waliko wawekezaji. mnataka nchi ionekane ina machafuko. Wewe unadhani nani mjinga atawekeza kwenye nchi yenye machafuko?Hebu tafuteni kazi za kufanya manake sasa mmeanza kuwa kero kwa jamii
Usijidanganye kuwa maendeleo yanaletwa na wawekezaji kwani ni nani mwekezajie aliyekwenda china au india na singapole? Wao waliwekeza kwenye elimu ya watoto wao kupata wataalam na kisha kujenga viwanda vyao na kuuza utaalam wao kwingine.Magamba yanaua elimu yetu ili wawalete waporaji wa mali zetu na wao wawekewe 10% uswisi.Hadi sasa hatujawa na wawekezaji Tanzania ali waporaji tu ambao wamepora hata mchanga wetu na wanyama wetu wakisaidiwa na viongozi wa serikali sikivu na chama chake mufilisi. Maandamano ni muhimu, lazima kwa ukombozi na tishio kwa magamba.
 
Hivi unadhania nchi inaweza kuendelea bila wawekezaji?
Tatizo lenu nyie mnataka attention sana na mnaitafuta hii attention bila kujali waathirika wa haya maandamano na vurugu zenu, Wakipoteza maisha mnachofanya ni kuzunguka na picha zao kuonyesha huko waliko wawekezaji. mnataka nchi ionekane ina machafuko. Wewe unadhani nani mjinga atawekeza kwenye nchi yenye machafuko?
Hebu tafuteni kazi za kufanya manake sasa mmeanza kuwa kero kwa jamii
Usijidanganye kuwa maendeleo yanaletwa na wawekezaji kwani ni nani mwekezajie aliyekwenda china au india na singapole? Wao waliwekeza kwenye elimu ya watoto wao kupata wataalam na kisha kujenga viwanda vyao na kuuza utaalam wao kwingine.Magamba yanaua elimu yetu ili wawalete waporaji wa mali zetu na wao wawekewe 10% uswisi.
Hadi sasa hatujawa na wawekezaji Tanzania ali waporaji tu ambao wamepora hata mchanga wetu wanyama wetu wakisaidia na viongozi wa serikali sikivu na chama chake mufilisi.
Maandamano ni muhimu, lazima kwa ukombozi na tishio kwa magamba.
 
POLISI legezeni tuu au muamue Kuua na kukamata ovyo!
 
Wote hawa mie nimewazoea,
Nakumbuka hata wakati ule nilipokuwa kamanda wao nilikuwa nikiitisha mikutano wanakupigia simu mpaka inawaka moto..."TUKO PAMOJA KAMANDAA!" lakini siku ya mkutano wote wanaingia mitini unabaki kuhutubia meza na viti.
Ni sawa tu na hawa viongozi wao, wanawafanya vijana wa watu chambo halafu kwenye maandamano hutaona ndugu au familia wanakwenda huko.
Kikinuka utakuta wanaoumia ni masikini tu wakati wao tayari wameisha pata umaarufu wanakula bata tu.
Nakumbuka Osama Bin laden mpaka anapofariki wanae wote na wake zake walikuwa hawana hata jeraha moja, yeye alikuwa anawavalisha mabomu watoto wa mafala anawaambia wakifa wataenda mbinguni na watapata wanawake bikra kumi na nane. kama kweli huko ni kuzuri kwa nini asiwapeleke wanae wakatese?
Hebu jiulize, Hawa wanaojitokeza kukujibu hapa kila mara, ulishawahi kuwaona au kusikia kama wamaumia kwenye maandamano?.

Kila siku wako hapa 17hrs na longo longo na post kibao. Kwani wao wanabahati ya aina gani ambayo katika maandamano mamia kama siyo maelefu ya CHADEMA hawajakumbana na lungu la fanya fujo uone (FFU).

Wao wana dhana isemayo, WAJINGA NDIYO WALIWAO
 
Nitafurah kama Dr Ndalichako ataunganishwa kwenye shinikizo la kujiuzuru maana yeye ndiyo mchakachuaji wa kwanza wa mitihani. Anauza mitihani sana na kuharibu matokeo ya watoto wetu. CHADEMA nafikri mnapaswa kuliona hili maana sije kuwa mtu anayehusika INDIRECT akawa ndo wa kutoa kafara wakati wahusika mnawaacha. We are watching you move! Tendeni haki msibague! Dr Ndalichako = Dr Kawambwa = RESIGN
 
Hivi unadhania nchi inaweza kuendelea bila wawekezaji?
Tatizo lenu nyie mnataka attention sana na mnaitafuta hii attention bila kujali waathirika wa haya maandamano na vurugu zenu, Wakipoteza maisha mnachofanya ni kuzunguka na picha zao kuonyesha huko waliko wawekezaji. mnataka nchi ionekane ina machafuko. Wewe unadhani nani mjinga atawekeza kwenye nchi yenye machafuko?
Hebu tafuteni kazi za kufanya manake sasa mmeanza kuwa kero kwa jamii

Kama upumbavu ni tusi basi ndo nakupa na ban naisubiri. Kama umetembelea maeneo ya ujenzi ambayo wakandarasi ni wachina na ndugu zetu ni casual laborers nadhani hutakuwa na haja ya kumuona huyo raisi wao. Kwa taarifa yako ni bora hata wahindi kuliko hao wachina.
Ila kwa umburula wako wa kupenda barabara za CCM ambazo hukuziona ukiwa UK, najua utakimbilia pale kwenye uwanja wa ndege wa wachina ulioshindwa kujengwa mpaka leo ili ukamuone huyo raisi wao.
wenzio wanatetea maslahi yao na wewe unashangilia wao kutetea maslahi yao.
ni vile tu niko nyuma ya keyboard, ila ungekuwa mbele yangu ningekutwanga japo konde moja tu.
 
Hivi unadhania nchi inaweza kuendelea bila wawekezaji?
Tatizo lenu nyie mnataka attention sana na mnaitafuta hii attention bila kujali waathirika wa haya maandamano na vurugu zenu, Wakipoteza maisha mnachofanya ni kuzunguka na picha zao kuonyesha huko waliko wawekezaji. mnataka nchi ionekane ina machafuko. Wewe unadhani nani mjinga atawekeza kwenye nchi yenye machafuko?
Hebu tafuteni kazi za kufanya manake sasa mmeanza kuwa kero kwa jamii
chris mkosi! mawazo yako ni mkosi ka jina lako!
 
Inaelekea unanifahamu vizuri kuliko hata ninavyojifahamu mimi mwenyewe
Anyway endeleeni kufuata kila analowaambia DJ mfanye, lakini kumbukeni tu kumuuliza kama na familia yake itakuja kwenye hayo maandamano au watakuwa wanawaangalia tu kwenye tv mnavyokula kichapo kwa kutotii amri ya serikali.

acha maneno kanga nyang'au wewe
 
Hebu jiulize, Hawa wanaojitokeza kukujibu hapa kila mara, ulishawahi kuwaona au kusikia kama wamaumia kwenye maandamano?.

Kila siku wako hapa 17hrs na longo longo na post kibao. Kwani wao wanabahati ya aina gani ambayo katika maandamano mamia kama siyo maelefu ya CHADEMA hawajakumbana na lungu la fanya fujo uone (FFU).

Wao wana dhana isemayo, WAJINGA NDIYO WALIWAO

Mwanadiwani umeingia JF mbio mbio kama bao la kwanza. Wewe ndo mtumishi mpya wa Lumumba? wenzio tulishindwa hiyo kazi maana kuitetea CCM inabidi uwe na akili ya maiti. hata wakina Makamba na Kingunge wamechoka kuitetea.
Karibu lakini mkuu
 
Chris Lukosi , Hawa wengi wanaopiga kelele hapa JF huwezi kuwaona ground zero. Kwani hujui mbwa mwoga alivyo na kelele.

Wengi wao humu wao maandamano yao yatakuwa kwa njia ya keyboard/keypad, wao wanapenda kuita digitari kupata updates.

endeleeni kujipa moyo wakati wa kuwaondoa wadhulumati umefika
 
Last edited by a moderator:
Huwezi kuisimamisha Nchi weekend! Nchi inasimamishwa Siku ya kazi!

goodluck then

another political miscalculation... nchi haitasimama, watanzania ni waoga, hawawezi kuacha kwenda kazini, watakaoandamana ni wale wasio na kazi

kila jambo na wakati wake

good luck anyway
 
Inaelekea unanifahamu vizuri kuliko hata ninavyojifahamu mimi mwenyewe
Anyway endeleeni kufuata kila analowaambia DJ mfanye, lakini kumbukeni tu kumuuliza kama na familia yake itakuja kwenye hayo maandamano au watakuwa wanawaangalia tu kwenye tv mnavyokula kichapo kwa kutotii amri ya serikali.

Kwani wakati unachukua uongozi huko UK hukujua CDM mwenyekiti wake ni DJ? ila kumbuka ni bora huyo DJ kuliko hao walioenda china kuuza nyara za serikali. na hao wachina unaoaka kuwapokea ndo wanabeba pembe za ndovu mchana kweupe bila hata vibali. Katibu mkuu wako na hao wachina lao moja
 
Huku Jeshi la polisi nchini likiamua kutumika vibaya na Chama cha Mapinduzi na Serikali yake kwa kupiga marufuku maandamano kwenye mikoa yote yalikopangwa kufanyika, Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimeendelea kusisitiza na kulitaka jeshi la polisi kutambua hivyo kuwa maandamano yako pale pale.

Taarifa iliyotelewa kwa vyombo vya habari na jeshi la polisi kwa jiji la Dar es salaam zinadai kuwa haliwezi kuruhusu maandamano hayo kwa kuwa kuna ugeni wa rais wa China siku hiyo lakini CHADEMA wamedai kuwa Rais wa china yuko hapa nchini kwa maslahi ya nchi yake na wao CHADEMA wako kwenye shughuli zao kwa maslahi ya nchi ambazo hazina mausiano yoyote na rais huyo wa china.


.
It doesnt matter whether policeCcm like or not we are going to demostrate. Chinese president is there for the benefit of his people, but who's ready to be a voice of the voiceless fellow Tanzanias?
So longer U can not convince me to believe that those Chinese merchants in Kariakoo are investors's. They are rather INVADER'S.

.
 
Naona mnafarijiana magamba (Madiwani, Lukosi), tarehe 25 kama ratiba inavyosema kuelekea kwa pinda. Nakuja kesho kutoka Tandahimba
 
Hivi unadhania nchi inaweza kuendelea bila wawekezaji?
Tatizo lenu nyie mnataka attention sana na mnaitafuta hii attention bila kujali waathirika wa haya maandamano na vurugu zenu, Wakipoteza maisha mnachofanya ni kuzunguka na picha zao kuonyesha huko waliko wawekezaji. mnataka nchi ionekane ina machafuko. Wewe unadhani nani mjinga atawekeza kwenye nchi yenye machafuko?
Hebu tafuteni kazi za kufanya manake sasa mmeanza kuwa kero kwa jamii

Wewe kuli endelea kubebea wazungu mabosi huko, tuachie sis ukombozi wa nchi yetu kuli mkubwa wewe.
 
Mwanadiwani umeingia JF mbio mbio kama bao la kwanza. Wewe ndo mtumishi mpya wa Lumumba? wenzio tulishindwa hiyo kazi maana kuitetea CCM inabidi uwe na akili ya maiti. hata wakina Makamba na Kingunge wamechoka kuitetea.
Karibu lakini mkuu
Mimi basi siyo kama wao kwa sababu dhana nzima ya kutetea inafanyika pale ambapo makosa yamefanyika.

Hakuna kosa ambalo limefanyika kwangu mimi kuanza kulitetea.

Nashukuru kwa kunikaribisha mkuu.
 
A word of encouragement during a failure is worth more than an hour of praise after success.
lukosi, kamwene. Pamoja na mapenzi kwa chama chetu cha mapinduzi lakini sometimes tuangalie kumbukumbu ambazo bila shaka zinatupa ukweli. Tumekuwa na wawekezaji hapa nchini kwa muda mrefu sasa, lakini wametusaidia nini cha maana. Sanasana wananchi tumekuwa na maisha magumu kupita kiasi. Wawekezaji wametubana kila sehemu na wanachukua kila kitu. Kibaya zaidi hao wachina mpaka kazi za umachinga wamechukua wao, unategemea wananchi watafurahia ujio wa huyu raisi wa china?.

Mdogo wangu lukosi shukuru mungu uko nje ya nchi ambako unapata mkate na siagi kirahisi sana na bila shaka wanao wanapata elimu safi na iliyo bora kama siyo bure basi kwa gharama nafuu.

Ukweli ni kwamba chadema wanatuamsha kiakili na kutufanya tukumbuke majukumu yetu. Mimi na wewe pamoja na kwamba tumo ndani ya ccm lakini tulikuwa hatujui kwamba tanzania kama nchi hatuna mitaala ya elimu, hicho ni kitu cha kuchekesha kama si cha kusikitisha.

Sababu inayowapelekea chadema pamoja na wananchi wanaowaunga mkono kufanya haya maandamano ninakubaliana nayo kwa 100%. Wabunge wa upinzani wamejaribu kuomba hili suala lijadiliwe bungeni ili litafutiwe ufumbuzi lakini spika na naibu wake wakatumia kiti chao kukataza lisijadiliwe bungeni. Kumbuka kwamba wabunge wanatumwa na waliowapigia kura kupeleka vilio na matatizo yao bungeni, sasa kama bunge linawanyima uhuru huo wabunge unataka wananchi wafanye nini zaidi ya kuandamana na hasa kwenye suala la msingi kama hili?.

Kitu cha maana na cha msingi ambacho kinaweza kufanyika hapa ni kuwaomba chadema kama wanaweza kufanya hayo maandamano siku nyingine na sababu za msingi waelezwe lakini si kutumia nguvu ya polisi ambao wanalipwa kwa kodi za watanzania wote. Sababu ya ujio wa raisi wa china sioni kama inajitosheleza kusimamisha maandamano hayo, raisi huyo wa china amekuja kwa sababu na faida ya nchi yake na watanzania wanataka kufanya maandamano hayo kwa faida ya vizazi vijavyo. Pamoja na hayo pia kuna barabara nyingi sana tanzania ni kiasi cha kupanga hayo maandamano yapite wapi na msafara wa raisi wa china upite wapi.

Wananchi kupoteza maisha wakati wa maandamano ni sababu ya polisi kutumia nguvu zaidi kuliko akili. Bila shaka unalijua vyema jeshi la polisi tokana na ukweli kwamba ulikuwa ndani ya jeshi hilo kabla ya kulikimbia na kutimkia ughaibuni.
 
Back
Top Bottom