CHADEMA na polisi katika mtifuano mkali

CHADEMA na polisi katika mtifuano mkali

Hii nchi hata wakichukuwa vyama vingine,hakuna ujanja ni lazima tufungue milango ili tuweze kupata wawekezaji ambao watasimamiwa vyema na kuifanya Tanzania isonge mbele.kwa dunia ya sasa bila kufungua milango huwezi kwenda mahali,bila kuwa na ushirikiano na nchi nyingine huwezi kusonga mbele,ufike wakati tukubali kuwa maendeleo ya sasa yanahitaji wawekezaji wawe wa ndani ama wa nje.
Nakubaliana na maandamano hayo,lakini ni vyema tuelewe kuwa Tanzania inahitaji wawekezaji wa kweli na kwa sasa wawekezaji wa kweli ni kutoka uchina na si ujerumani wala uingereza wala USA.
Cha msingi hapa ni kuwa makini ktk kile tukifanyacho,ktk swala la utaifa tusimame kwa pamoja na ktk maswala ya uvyama hainashida mkipambana maana kila chama kinataka kushika dola na hii ni kwa kila chama cha siasa ktk nchi yeyote ile.

Nyie waswahili ubongo wenu umelala sana, yani mawazo yenu yote ni wawekezaji? Kwanza nadharia ya uwekezaji unaijua? Hivi unajua ni nani wamejanga au kuleta maendeleo nchi za ulaya, marekani au asia pacific?

Acheni uduanzi! Nchi hii tutaipigania sisi wenyewe na familia zetu!!
 
Safi sana makamanda, maandamano lazima yafanyike,wakiwaletea za kuleta waonyesheni ukamanda wenu, mawe kwa kwenda mbele, tafuteni jamaa mmoja ajiwashe moto kama yule mwarabu. Sasa ni wakati wa ukombozi,ni kupigana mpaka kufa.mkuu wa majeshi ya anga ndio atakua mbele na tofali lake.....wapuuzi nyie.
 
Uchi wa serikali ya CCM utaanikwa Jumatatu kwa kuwa dunia nzima itkuwa Tanzania. Maandamano kuelekea ofisi ya waziri mkuu ni sawasawa na kuelekea Ikulu kwa kuwa ofisi ya waziri mkuu iko Ikulu. Rais wa China na vyombo vyote wa habari vya kimataifa vitakua maeneo hayo. Hapa kazi ipo!
 
Th right attitude!!


Hapa ndo napo ipa CDM salute. Inajua kumake its case stand out of the crowd at the right time, yaani hakuna ubishi hapa!


Siku CDM itapoteza hii attitudes, basi mi nitahama hichi chama!!
 
Nitoe ushauri kwa serikali na jeshi la polisi. Wawasiliane na CHADEMA kujua wanaandamana mikoa gani na muda gani, na kwa kila mkoa/mji ambapo kuna maandamano basi wawaambie wakuu wa mikoa au Wilaya husika wapokee hayo maandamano. (Wakuu wa mikoa na Wilaya wanawakilisha executive branch).

Sijui ni kwanini serikali na polis huwa wanajipa tabu ya kuzuia maandamano. Waache uwoga, na siasa za kizamani. Watu wanaandama wapokee na kusikiliza wanasema nini. Very easy na hakutakuwa na gharama za mabomu wa vitu vizito.
 
m 23 ; pole sana mkuu naona leo upo zamu, masalia wenzako wameenda wapi au ndo mambo ya weekend?
 
Hakuna mtu mwenye akili zake timamu, na ambaye anajali muda na kazi zake, anayejua wajibu kwenye familia yake, na anayetekeleza majukumu yake vinzuri, atashiriki maandamano hayo. Wapuuzi, wenye akili finyu, wasiokuwa na plan za kazi, wanaoamka wasijue nini cha kufanya ndio watakuwa mstari wa mbele kwenda kuwa chambo kwenda kutetea ulaji wa viongozi wa Chadema.
 
Boss,
I hope hilo jina la Mkwawa unajua maana yake.
Pili unatakiwa ujue sababu zilizowafanya wanafunzi wafeli na baada ya hapo hata ukiandamana mie nitakuunga mkono kwani tutajua nani au nini kilisababisha wanafunzi kufeli, sio kuandamana kila kukicha kama vile hakuna kazi nyingine ya kufanya.
KESHO MVUA ZISIPONYESHA NA MAZAO YAKAHARIBIKA UTAANDAMANA WAZIRI WA KILIMO AJIUZURU?

Chris Lazima ujue wewe unasimamia nini, Je unasimamia tumbo au unasiamamia sera na wananchi.
Hakuna nchi duniani iliyoendelea inamchekea mtendani mbovu hasa pale wizara au taasisi yake inaposhindwa ispokuwa kwa masikini kama wewe.

Nionyeshe ni nchi gani makini duniani pamoja na hiyo ambayo wewe ni mkimbizi wa kiuchumi na kielimu baada ya serikali ya CCM kukunyima elimu na ajira ikabidi ukimbie kama ina viongozi ambao hawawajibiki pale wanapoharibu.

Kila waziri au kiongozi anayeshindwa kuongoza taasisi au wizara yake lazima aondoke.

Sisi hatuko tayari kuona tena watoto wanakosa elimu kwa ajili ya Maccm kuwagawana fedha za elimu. Ndio maanadamo yataongeza bajeti ya wizara, ndio maandamano yatawafanya watawala kutekeleza wajibu wao, ndio maandamao wajibishi ndio silaha iliyotumiwa duninani na wote waliodai haki na ilipatikana. Ndio maandamono hata leo yanatumika hata huko ulipo kudai haki.

Njia za mazungumzo zikishindikana njia nyingine zitatumika. Hatuna muda wa kubembeleza wazembe, wezi, mafisadi, na wavivu. wewe subiria ninaamini siku moja utaona matunda ya hawa wanaojitoa kwa ajili ya ndugu, watoto na kizazi hiki na cha kesho.

Hata afrika ya kusini kulikuwa na wasaliti ila leo wanashangilia uhuru haki na usawa. Hata kwenye kudai uhuru tulikuwa na watu walituuza kwa kutetea wakoloni, hata kwenye harakati za Martin luther king baadhi ya weusi walisaliti leo wanashangilia Mweusi kuwa raisi. Hata Yesu alisalitiwa na mwanafuzi wake hivyo hujaanza wewe kuwasaliti watanzania.

Kwa sababu unatetea chama huoni, mateso ya Watanzania, kwa sababu unajikomba huoni madhara ya elimu mbovu Tanzania, Kwasababu hujawahi kupimwa malaria na kupewa majibu fake kwasababu ya ukosefu wa ujuzi, Kwasababu hujawahi kuona uzembe wa kujenga barabara chini ya kiwango na kusababisha hasara kwa walipa kodi.

Huna uchungu na kodi zetu wala hujui mwananchi ni nani?

Na nisikusikie ukilalalmikia huduma bora za jamii. wewe tuache sisi na Tanzania yetu na lazima tumwajibishe yeyote mzende, mvivu, mwizi, fisadi kwa gharama zozote zile.

Maandamano ni kilele cha serikali kuwa kikteta.

Siku moja tutakuona ukiyakubali haya kwa aibu.
 
Nitoe ushauri kwa serikali na jeshi la polisi. Wawasiliane na CHADEMA kujua wanaandamana mikoa gani na muda gani, na kwa kila mkoa/mji ambapo kuna maandamano basi wawaambie wakuu wa mikoa au Wilaya husika wapokee hayo maandamano. (Wakuu wa mikoa na Wilaya wanawakilisha executive branch).

Sijui ni kwanini serikali na polis huwa wanajipa tabu ya kuzuia maandamano. Waache uwoga, na siasa za kizamani. Watu wanaandama wapokee na kusikiliza wanasema nini. Very easy na hakutakuwa na gharama za mabomu wa vitu vizito.

Wana kazi muhimu za kufanya kuliko kusikiliza upuuzi wa CDM
 
hayo maandamano yangefanyika wikendi

watanzania ni waoga kuacha kazi zao
 
Nitoe ushauri kwa serikali na jeshi la polisi. Wawasiliane na CHADEMA kujua wanaandamana mikoa gani na muda gani, na kwa kila mkoa/mji ambapo kuna maandamano basi wawaambie wakuu wa mikoa au Wilaya husika wapokee hayo maandamano. (Wakuu wa mikoa na Wilaya wanawakilisha executive branch).

Sijui ni kwanini serikali na polis huwa wanajipa tabu ya kuzuia maandamano. Waache uwoga, na siasa za kizamani. Watu wanaandama wapokee na kusikiliza wanasema nini. Very easy na hakutakuwa na gharama za mabomu wa vitu vizito.
Na CHADEMA washasema tofauti na Dar ambako maandamano yapelekwa kwenye ofisi za Waziri Mkuu, Mwanza, Mbeya na Arusha yatapelekwa Kwa wakuu wa Mikoa. Kwa hiyo ni juu yao kutumia hiyo busara unayopa ambayo kimsingi italiepushia taifa jili kadhia isiyo ya lazima.

Serikali hapa inahaha kwa kuwa wanajua wanavuliwa nguo mchana kweupeeeeeeee!
 
Uchi wa serikali ya CCM utaanikwa Jumatatu kwa kuwa dunia nzima itkuwa Tanzania. Maandamano kuelekea ofisi ya waziri mkuu ni sawasawa na kuelekea Ikulu kwa kuwa ofisi ya waziri mkuu iko Ikulu. Rais wa China na vyombo vyote wa habari vya kimataifa vitakua maeneo hayo. Hapa kazi ipo!

Ni kujidanganya mkuu.
 
Chris Lazima ujue wewe unasimamia nini, Je unasimamia tumbo au unasiamamia sera na wananchi.
Hakuna nchi duniani iliyoendelea inamchekea mtendani mbovu hasa pale wizara au taasisi yake inaposhindwa ispokuwa kwa masikini kama wewe.

Nionyeshe ni nchi gani makini duniani pamoja na hiyo ambayo wewe ni mkimbizi wa kiuchumi na kielimu baada ya serikali ya CCM kukunyima elimu na ajira ikabidi ukimbie kama ina viongozi ambao hawawajibiki pale wanapoharibu.

Kila waziri au kiongozi anayeshindwa kuongoza taasisi au wizara yake lazima aondoke.

Sisi hatuko tayari kuona tena watoto wanakosa elimu kwa ajili ya Maccm kuwagawana fedha za elimu. Ndio maanadamo yataongeza bajeti ya wizara, ndio maandamano yatawafanya watawala kutekeleza wajibu wao, ndio maandamao wajibishi ndio silaha iliyotumiwa duninani na wote waliodai haki na ilipatikana. Ndio maandamono hata leo yanatumika hata huko ulipo kudai haki.

Njia za mazungumzo zikishindikana njia nyingine zitatumika. Hatuna muda wa kubembeleza wazembe, wezi, mafisadi, na wavivu. wewe subiria ninaamini siku moja utaona matunda ya hawa wanaojitoa kwa ajili ya ndugu, watoto na kizazi hiki na cha kesho.

Hata afrika ya kusini kulikuwa na wasaliti ila leo wanashangilia uhuru haki na usawa. Hata kwenye kudai uhuru tulikuwa na watu walituuza kwa kutetea wakoloni, hata kwenye harakati za Martin luther king baadhi ya weusi walisaliti leo wanashangilia Mweusi kuwa raisi. Hata Yesu alisalitiwa na mwanafuzi wake hivyo hujaanza wewe kuwasaliti watanzania.

Kwa sababu unatetea chama huoni, mateso ya Watanzania, kwa sababu unajikomba huoni madhara ya elimu mbovu Tanzania, Kwasababu hujawahi kupimwa malaria na kupewa majibu fake kwasababu ya ukosefu wa ujuzi, Kwasababu hujawahi kuona uzembe wa kujenga barabara chini ya kiwango na kusababisha hasara kwa walipa kodi.

Huna uchungu na kodi zetu wala hujui mwananchi ni nani?

Na nisikusikie ukilalalmikia huduma bora za jamii. wewe tuache sisi na Tanzania yetu na lazima tumwajibishe yeyote mzende, mvivu, mwizi, fisadi kwa gharama zozote zile.

Maandamano ni kilele cha serikali kuwa kikteta.

Siku moja tutakuona ukiyakubali haya kwa aibu.

maneno yako yanaingia kama msumari wa moto kwa kweli nchi yetu imeoza.
 
Lakini safari hii msitoe mtu kafara.uzuri yule muuaji yuko jela lasivyo tutasikia kafa mtu kwenye maandamano
 
Chris msaliti, katiba haisimami kufanya kazi yake kisa mgeni kaja.
 
Lakini safari hii msitoe mtu kafara.uzuri yule muuaji yuko jela lasivyo tutasikia kafa mtu kwenye maandamano
kama wiki hii jakaya kikwete alipomtoa mama traffic polisi kafara pale shekilango
 
Hivi unadhania nchi inaweza kuendelea bila wawekezaji?
Tatizo lenu nyie mnataka attention sana na mnaitafuta hii attention bila kujali waathirika wa haya maandamano na vurugu zenu, Wakipoteza maisha mnachofanya ni kuzunguka na picha zao kuonyesha huko waliko wawekezaji. mnataka nchi ionekane ina machafuko. Wewe unadhani nani mjinga atawekeza kwenye nchi yenye machafuko?
Hebu tafuteni kazi za kufanya manake sasa mmeanza kuwa kero kwa jamii

Lukosi, kamwene. Pamoja na mapenzi kwa chama chetu cha mapinduzi lakini sometimes tuangalie kumbukumbu ambazo bila shaka zinatupa ukweli. Tumekuwa na wawekezaji hapa nchini kwa muda mrefu sasa, lakini wametusaidia nini cha maana. Sanasana wananchi tumekuwa na maisha magumu kupita kiasi. Wawekezaji wametubana kila sehemu na wanachukua kila kitu. Kibaya zaidi hao wachina mpaka kazi za umachinga wamechukua wao, unategemea wananchi watafurahia ujio wa huyu Raisi wa china?.

Mdogo wangu Lukosi shukuru mungu uko nje ya nchi ambako unapata mkate na siagi kirahisi sana na bila shaka wanao wanapata elimu safi na iliyo bora kama siyo bure basi kwa gharama nafuu.

Ukweli ni kwamba Chadema wanatuamsha kiakili na kutufanya tukumbuke majukumu yetu. Mimi na wewe pamoja na kwamba tumo ndani ya CCM lakini tulikuwa hatujui kwamba Tanzania kama nchi hatuna mitaala ya elimu, hicho ni kitu cha kuchekesha kama si cha kusikitisha.

Sababu inayowapelekea Chadema pamoja na wananchi wanaowaunga mkono kufanya haya maandamano ninakubaliana nayo kwa 100%. Wabunge wa upinzani wamejaribu kuomba hili suala lijadiliwe bungeni ili litafutiwe ufumbuzi lakini spika na naibu wake wakatumia kiti chao kukataza lisijadiliwe bungeni. Kumbuka kwamba wabunge wanatumwa na waliowapigia kura kupeleka vilio na matatizo yao bungeni, sasa kama bunge linawanyima uhuru huo wabunge unataka wananchi wafanye nini zaidi ya kuandamana na hasa kwenye suala la msingi kama hili?.

Kitu cha maana na cha msingi ambacho kinaweza kufanyika hapa ni kuwaomba Chadema kama wanaweza kufanya hayo maandamano siku nyingine na sababu za msingi waelezwe lakini si kutumia nguvu ya polisi ambao wanalipwa kwa kodi za watanzania wote. Sababu ya ujio wa Raisi wa China sioni kama inajitosheleza kusimamisha maandamano hayo, Raisi huyo wa China amekuja kwa sababu na faida ya nchi yake na watanzania wanataka kufanya maandamano hayo kwa faida ya vizazi vijavyo. Pamoja na hayo pia kuna barabara nyingi sana Tanzania ni kiasi cha kupanga hayo maandamano yapite wapi na msafara wa Raisi wa China upite wapi.

Wananchi kupoteza maisha wakati wa maandamano ni sababu ya polisi kutumia nguvu zaidi kuliko akili. Bila shaka unalijua vyema jeshi la polisi tokana na ukweli kwamba ulikuwa ndani ya jeshi hilo kabla ya kulikimbia na kutimkia ughaibuni.
 
Hakuna mtu mwenye akili zake timamu, na ambaye anajali muda na kazi zake, anayejua wajibu kwenye familia yake, na anayetekeleza majukumu yake vinzuri, atashiriki maandamano hayo. Wapuuzi, wenye akili finyu, wasiokuwa na plan za kazi, wanaoamka wasijue nini cha kufanya ndio watakuwa mstari wa mbele kwenda kuwa chambo kwenda kutetea ulaji wa viongozi wa Chadema.

Tatizo la viongozi ni kudhani kuwa wapuuzi ndo wanaandama bila kujua kuwa MWENYE NJAA HANA CHA KUPOTEZA. Mkuu ni kweli kuwa wanaodai haki hawana cha kufanya kwa sababu wameshanyang'anywa. TUNA HALI NGUMU SANA MKUU KAMA TAIFA
 
watanzania mtajionea maajabu jumatatu la jeshi la polisi, wamezoea kupakia polisi na kuwasafirisha mikoa mbalimbali kudhibiti maandamano sasa jumatatu je wataweza kudhibiti maandamano hayo nchi nzima ? mtashangaa watanzania kuwa jeshi la polisi halina uwezo kama wananchi wengi wanavyodhania. wananchi wakiamua hakuna jeshi linaloweza kukabiliana nao.
 
Hivi unadhania nchi inaweza kuendelea bila wawekezaji?
Tatizo lenu nyie mnataka attention sana na mnaitafuta hii attention bila kujali waathirika wa haya maandamano na vurugu zenu, Wakipoteza maisha mnachofanya ni kuzunguka na picha zao kuonyesha huko waliko wawekezaji. mnataka nchi ionekane ina machafuko. Wewe unadhani nani mjinga atawekeza kwenye nchi yenye machafuko?
Hebu tafuteni kazi za kufanya manake sasa mmeanza kuwa kero kwa jamii

Kero kwako Mlowezi, sio jamii...Jamii ipi unayoongelea wewe? Kama ni kweli CDM imekuwa kero kwa jamii basi polisi waruhusu maandamano then wananchi wenyewe wachague kushiriki ama laa!. Naona unawahusudu wageni/wawekezaji mpaka unasahau maslahi ya nchi yako.
 
Back
Top Bottom