CHADEMA na polisi katika mtifuano mkali

CHADEMA na polisi katika mtifuano mkali

Elimu ya mwanangu ndio my foremost priority. Ujio wa rais wa China is least of my concerns. Ndugu watanzania maandamano palepale,elimu kwanza.
 
Chris Lukosi acha kuji-nafkisha, wachina wakariakoo wanawekeza kwenye nini? Kuuza vitu vya rejareja nao ni uwekezaji?
 
Hivi unadhania nchi inaweza kuendelea bila wawekezaji?
Tatizo lenu nyie mnataka attention sana na mnaitafuta hii attention bila kujali waathirika wa haya maandamano na vurugu zenu, Wakipoteza maisha mnachofanya ni kuzunguka na picha zao kuonyesha huko waliko wawekezaji. mnataka nchi ionekane ina machafuko. Wewe unadhani nani mjinga atawekeza kwenye nchi yenye machafuko?
Hebu tafuteni kazi za kufanya manake sasa mmeanza kuwa kero kwa jamii


1. Jamii ni nani? Au unadhani jamii ni wewe na familia yako?

2. Kama wamekuwa kero si hao unaowaita jamii wasingejitokeza?

3. Uwekezaji umetufikisha wapi so far?

4. Machafuko yapi Yaliyosababiswa na CDM?
 
Mwita Maranya

Mambo ni vipi Mkuu? Bila shaka kwa uwezo wa MUNGU u mzima kama ninavyokuona jamvini Mkuu!

Nimeipenda sana post yako ni ngoja nizungukie kitufe cha LIKE na upate haki yako Mkuu!
Hakuna kulala mpaka kieleweke hakimungu!


Nani kakudanganya kuwa ujio wa raisi wa China una manufaa kwa vizazi vijavyo achilia mbali kizazi cha sasa? Hata sielewi kwanini baadhi ya watu mnakuwa wepesi kurubunika kwa hadaa za ccm na serikali yake.
Kama wewe ni muoga bora ubaki kesho nyumbani ulale tu na mkeo kuliko kuongea vitu visivyo na maana yoyote.
 
Last edited by a moderator:
Maandamano yako palepale.
Wachina wamepewa elimu bora ndio maana ccm inawatukuza.
Nasisi ni lazima tuipiganie elimu ya vizazi vyetu tusije tukaishia kuwa manamba kwenye nchi yetu.
VIONGOZI WA CDM MSIBATILISHE MAANDAMANO. TUPO PAMOJA NANYI.

usilolijuwa ni kama usiku wa kiza
kwa mfano kama tungebadili ada wanayolipa wazazi wa kichina ktk shue zao ndio walipe wazazi wetu kwa Tanzania hakuna ambae angekwenda shule.
na kama watoto wa kitanzania wangekuwa wanasoma kama watoto wa kichina basi Tanzania tungekuwa mbali sana,hawa wachina wanajituma bwana,mtoto hakuna kupumnzika kuanzia saa 12 asubuhi hadi 11 jioni,
bongo watu hamtaki kusoma,msitupie lawama serikali
 
Hii nchi hata wakichukuwa vyama vingine,hakuna ujanja ni lazima tufungue milango ili tuweze kupata wawekezaji ambao watasimamiwa vyema na kuifanya Tanzania isonge mbele.kwa dunia ya sasa bila kufungua milango huwezi kwenda mahali,bila kuwa na ushirikiano na nchi nyingine huwezi kusonga mbele,ufike wakati tukubali kuwa maendeleo ya sasa yanahitaji wawekezaji wawe wa ndani ama wa nje.
Nakubaliana na maandamano hayo,lakini ni vyema tuelewe kuwa Tanzania inahitaji wawekezaji wa kweli na kwa sasa wawekezaji wa kweli ni kutoka uchina na si ujerumani wala uingereza wala USA.
Cha msingi hapa ni kuwa makini ktk kile tukifanyacho,ktk swala la utaifa tusimame kwa pamoja na ktk maswala ya uvyama hainashida mkipambana maana kila chama kinataka kushika dola na hii ni kwa kila chama cha siasa ktk nchi yeyote ile.

Aliewadanganya kuna nchi inakuja kuwekeza hapa ili Tanzania inufaike ni nani? Naona na wewe umeathirika na kile kiza cha 'mikataba' kufungiwa ili isijadiliwe. Tafuta undani wa mikataba hyo uone. For your information, rais wa china anakuja kuendeleza maslahi ya nchi yake,sio ya Tanzania. Chochote Tanzania mtakachokipata ni by-product ya operesheni na maslahi ya wachina. Tanzania should be bold enough to stand up na kupitia hali ngumu ili kuufikia mwisho mwema. Sio hawa viongozi wa nchi hii walio 'trip-happy' na kufurahia vya dezo ilhali wakishiriki kuwapumbaza wananchi kwa mahubiri ya uwekezaji toka nje! Waulize sasa waseme kinagaubaga watanzania watanufaika vipi ndipo utazimia kwa jinsi watakavyoanza kubabaika! Mara ooh ajira,waulize ajira ngapi na za aina gani na hadhi gani uone aibu itakayowakumba. Utasikia vibarua ktk ujenzi! Shame on you CCM na serikali yenu na vibaraka wenu wanaowatetea! Laana hii ya watanzania itawatafuna hadi vizazi vya tano na sita. Halafu watanzania wanaposimama kudai mambo ya msingi kwa maandamano chini ya CHADEMA mnataka eti waache kisa mabwana zenu toka ughaibuni wanakuja! Pumbavu kabisa!
 
Mkuu Korosho,

Hata mimi ningelishauri hivvyo lakini kiuzoefu magamba wamezidisha ubabe. Hata kwa vitu vya msingi wanapinga kwa jeuri tu.

Ebu niambie maccm wanatakaaandamana Arusha kwa sababu zipi? Lini walipata wazo hilo na kwa nini polisi watumie kigezo hicho kusitisha maandamano.

Chadema walipanga hayo maandamano wiki tatu kabla, yamkini uyo jamaa alikuwa hajawa rais.

Polisi wafanye kazi yao kwa mjibu wa katiba sio kubeba mafisadi.
 
Huo ugeni unaathiri nini?Rais wa China anakuja kwa maslahi ya Taifa lake.Hapa CHADEMA wanaongelea maslahi ya taifa letu na vizazi vijavyo

Watoto wamefeli na hatuwezi kuandaa mazingira ya wadogo Zetu na kuwa manamba ndani ya nchi yao watakapowekeza wageni anaokuja kuwatetea kwenye hiyo mikataba ya kinyonyaji watakayosaini na rais wa China

Ukipita Kariakoo utakutana na wamachinga wa kichina ambao wanaziba hata fursa kwa wamachinga na wadogo zetu waliofeli kidato cha nne kujipatia riziki yao.

Tuendeleze vuguvugu bila kurudi nyuma

yaani baada ya maandamano wanafunzi watafaulu au mnapinga mitihani migumu? vizazi gani vijavyo sasa hivi mtoto hata soma tena anajua aki fail chadema wataandamana! tatizo ni chadema kila siku busara wanaziacha nyumbani! ni nchi gani uliwahi kusikia watu wanabaguana wakati wa tatizo ambazo ni cross cutting kama hili! hivi huyo mtei ni wakati gani ana toa busara zake kuwashauri hawa watoto? maana nahisi katika chadema baada ya Bob amebaki yeye tu mzee chadema na ana busara tele at least that is what I belive!
 
Back
Top Bottom