utaipigania kwa vitendea kazi vipi? Hiyo usa yenyewe inategemea wawekezaji toka nchi mbalimbali,wewe utaipigania nchi ya tanzania kwa kuifanyia nini zaidi,watu wanahitaji ajira,serikali pekee haiwezi kuwaajiri watanzania wote,siasa haiwezi kuajili watanzania wote,ni lazima tuwe na njia mbadala za kutengeneza ajira na hizo si nyingine ni kuwa na wawekezaji ambao watatengeza ajira kupitia kile watakacho wekeza na hii inawezekana kama tutaweza kuwasimamia na si kuwaacha wafanye watakavto.
Wewe utaipigania tanzania kwa kiwango kipi na mpaka lini utafikia kikomo? Maana dunia nzima kwa sasa maendeleo yanategemea wawekezaji wa ndani na wa nje.ajira ktk kilimo haiwezi kuwa ajira ya kudumu kama tutaendelea na kilimo cha jembe la mkono ni lazima tuingie ubia na nchi marafiki ili kuweza kupata zana za kilimo,kilimo cha kutegemea mvua kimepitwa na wakati,ujengaji wa mifereji ya umwagiliaji inahitaji pesa nyingi na ktk hili hatuwezi kama tanzania kusimama bila kuingia ubia na wawekezaji wa ndani na wa nje
sasa unaposema utaipigania tanzania kwa kusema tu bila kutenda sioni kama hiyo itafanya kazi.
Dunia inakimbia,nyie mnalala tu,amkeni wabongo,acheni kulalama.