CHADEMA mnataka mteremshiwe gunia la chawa?

well CDM ni chama kikubwa kinaweza kuwa na mtu yeyote anayeweza kufanya kazi hiyo binafsi siko interested na jukumu hilo I could some other things more productive katika kuleta mabadiliko.
"Nimekusoma, ila "strategic communicatins " haifanywi na mtu yoyote, inafanywa na "communicator"!. You can still help by proxy!.
 
Usifananishe maandamano ya Chadema na maandamano ya Waislam, Ponda alikuwa mbele akiongoza maandamano wakati Dr Slaa alikuwa kalala hotel.

yakhe kulala tu ingekuwa nafuu; Slaa akuwa ndani zinaa na janaba kumtopea; baradhuli kamtoa mwana wa watu kikoa tahayuri immejaa mpaka kope za macho
 
Wanadhani maandamano mchezo huyo Mtoi anajisifu eti kashiriki maandamo mengi ya Chadema, maandamano ya Chadema wanaandamana kini Halima Mdee huku wamepaka poda na kasuka rasta, ingia barabarani pambana na polisi.

yakhe debe tupu haliishi mshindo; mtoi anshriki maandamano ya vigori; waume haswa subutu yake! mwana mweupe anyiritika hana kovu uso surubu za polisi aziweza wapi? ataka jifaragua machoni pa waume huyo
 
Hivi kuitisha kikao cha dharura cha kamati kuu au cha Sekretariet ya Chama inachukuwa muda gani? kuna mjumbe ambaye hana simu?

Zitto mbona kwenye mambo kama haya huwa sioni unaibu katibu mkuu wako? hapa ndipo tunapaswa kuona kwa vitendo matakamko na kauli Nzito cha chama na za Viongozi mmoja mmoja. Siasa za kuchekeana Watanzania hatuzihitaji kwa sasa, tunataka misimamo Radical.

Huyo apewe uwaziri au Ukatibu mkuu afanye kazi tu,siasa hawezi tena maana sasa hivi hafanyi siasa,uradical wake anawafanyia viongozi wenzake CDM!
 
Sijaona kosa la chadema. Kimya chao kimeleta funzo kubwa kwa jamii

Mkuu mzitoKabwela,
CHADEMA ni chama makini kwa bahati mbaya Mzee Mwanakijiji , siwezi sema amekurupuka, kwa kuwa chadema ni chama makini,

Kwanza kiliikataa tume ya nchimbi, badae ikawa "kamati" pamoja na kutotoa ushirikiano
Pili waliandikia barua rasmi kwa rais, kumtaka aunde tume kwa muujibu wa sheria ya uchunguzi.
mwisho, M4C isitishwe kwanza, isubiri majibu ya barua yao kwa Rais na majibu ya hiyo kamati ya nchimbi,
kwa muujibu wa JJ Mnyika, ilikuwa na sharti kama JK hatounda hiyo tume, basi watalazimika kufanya alichokisema Mzee Mwanakijiji, ni maandamano ya bila kikomo mpaka tume huru iundwe na waziri Nchimbi, Changonja, IGP,Kamuhanda, Shilogile wajiuzulu. hoja ya MMK inaweka nguvu zaidi kutokana na report ya Jaji Maneto.
 
Last edited by a moderator:
Naunga mkono hoja mkuu wngu ushauri wako kwa CHADEMA siku zote una mazur japokua ww upo upnd wa EL
Mkuu Magesi, mimi sio mshabiki wala mfuasi wa Chadema, mimi wa maslahi ya taifa mbele!. Kwa 2015, mgombea mwenye maslahi ya kupatikana kwa ukombozi wa pili wa kweli kwa Mtanzania ni EL akifuatiwa na J.P. Magufuli!, ndio maana nampigania EL.

P.
 
Mkuu Tukutuku, hii sio dharau ni sifa!, ndio maana mwanamke wa Kafrika anasubiri mpaka apendwe!, na akipendwa kwanza hujifanya hataki huku anataka na ndia maana kwenye ndoa hupigwa, mume hutoka nje na kurudi akimkuta anasubiri tuu!.

Mwanamke wa kizungu, akipenda anakuja staight na kukueleza!, ukimletea za kuleta, off she goes!. Akigundua una cheat, that is the end!.

Chadema inashida sana ya mtu wa full time wa communications. JJ.Mnyika abaki tuu kama mkurugenzi lakini pale panahitajika team na team hiyo iwe na mtu wa "strategic communication"!. Kama Ikulu, Salva ni Mkurugenzi, chini yake yupo Premmy, Michuzi, Minde, Maro, Balua, Kengele kina Kisori etc. Mnyika aendelee kuwepo ila anahitaji watu, wanahitaji team, ndio maana M4C ime invest kwenye ma 4x4 na PA focus ikiwa ni maandamano na mikutano ya hadhara wakati hakuna any investment on "mass communications" kama owning media which costs less reach most!.

Mpaka sasa, all Chadema publicity zinatengemea huruma ya friendly media tuu!. Press realese ni mpaka JJ. Mnyika apate muda!. Watu wako active 24/7 linatokea jambo kubwa kama ripoti ya THBUB Chadema iko kimya 24 hours zimepita!, jana 48 hours zimepita!, leo zinakwenda saa 72!. Japo Chadema haisemi kuwa inashinda, kiukweli inashida na inahitaji sana kusaidiwa kwenye hili!. Watu wa kusaidia wapo!, nimewashauri, sasa wasiisubiri Chadema iseme inashida, nimewashaiuri wajitoe tuu kusaidia!.
P.
Mkuu nashukuru sana kwa uchambuzi mzuri na maelezo ya kutosha.kuna mtu anaitwa Tumaini Makene ingawa sijui sana anafanyinini pale chadema ambaye ni yupo idara ya habari kwenye secretariat ya chadema nadhani anao uwezo wa kufanya haya yote,labda anazembea tu.Jana kwenye taarifa ya habari ya saa mbili usiku(ITV) nilimsikia Vicent Nyerere ambaye ni waziri kivuri wa mambo ya ndani alitoa tamko la kumtaka Dr Emmanuel Nchimbi ajiuzuru,nadhani hili ni tamko zito la chama na huu ni mwanzo mzuri wa kuelekea kwenyo shinikizo kubwa zaidi la kufanya maandamano ya amani.
 
Tatizo haishi Tanzania, ni mtu wakuamrisha mambo kwa remote. Huwa hashiriki kwa vitendo

yakhe mmjaa vigori humu hamna lolote yaani wataka sema hamfiki watu 10 mkaanza haya maandanamano?weye mwanakijiji na balaa lako kusanya vigori wenzio 10 au 20 mwafika hiyo namba mkaanza hayo maandamano? Maanake ambiwa mna uchungu sana kuliko huyo aliyembeba tumboni miezi 9; mwapoteza muda usiku kucha kuteta unafiki kesho andamaneni kama nyie waume mmetimia haswa mmetolewa ngozi za mbele tuone haya maandamano kelele za chura za chosa watu taka lala sasa.
 
hakuna kuogopa wala kuchelewa, suala hapo ni kujipanga, wote mnajua kuna kampeni za madiwani katika kata 28 tanzania nzima, kuna kesi za kupinga matokeo ua uchaguzi wa ubunge, kunakazi kwa CHADEMA tofauti na CCM, CHADEMA inapambana na Serekali pamoja na CCM, ili hali serekali ina watendaji wengi tu waajiriwa ambao wengi wao wa kada ya kati na chini ni CHADEMA.
 
Mkuu Magesi, mimi sio mshabiki wala mfuasi wa Chadema, mimi wa maslahi ya taifa mbele!. Kwa 2015, mgombea mwenye maslahi ya kupatikana kwa ukombozi wa pili wa kweli kwa Mtanzania ni EL akifuatiwa na Membe!, ndio maana nampigania EL.

P.

yakhe vibaya hivyo maslahi ya taifa yapi? ankosa nini wewe? kelele nyingi wantia shaka; wallwah wataka kabidhi paka shume alinde kitoweo? ashavimbiwa kwa ulafi chunga asijetapika
 
nadhani CDM wameshaona mafanikio ya M4C zao na wamelewa ushindi - ambao bado hawajaupata anyway. hizihang overs ndo zetu waswahili. tunaona tushashinda kwa vile tunaongoza mbio, kumbe hatujafika mwisho wa mbio zenyewe. wangekuwa macho na makini zaidi lazima by now wangeshachukua hatua. haiyumkiniki kudai kuwa bado wanajipanga au wanasubiri vikao vya chama. kwa dunia ya leo, sio lazima kukutana physically kufikia position ya chama. na sidhani kama kutoa kauli kuhusianana ripoti hizi kunahitaji chama 'kukaa' kitako. kwa kweli ni mapungufu ya watendaji wakuu wa CDM kuwa kimya mpaka hii leo.
 
kama ulikuwa unaoga mtoni kichaa akachukua nguo zako na kukimbia nazo hauwajibiki kutoka uchi majini na kuanza kumkimbiza kwani ww utaonekana ni kichaa kuliko yeye.

mm ninachoamini ni kuwa CDM wanajaribu kusubiri ili ccm na serikali yake wamalize kusema pumba
zao ndipo wao wajumuishe. mambo mazuri hayataki haraka
 
yakhe vibaya hivyo maslahi ya taifa yapi? ankosa nini wewe? kelele nyingi wantia shaka; wallwah wataka kabidhi paka shume alinde kitoweo? ashavimbiwa kwa ulafi chunga asijetapika
Maslahi ya taifa mbele si nimeyataja?!. Au nirudie tena?. Masllahi ya taifa ni kuhakikisha katika uchaguzi wa 2015, Tanzania tunapata ukombozi wa pili wa kweli wa Mtanzania!.
 
Hiyo tume ni mawakala wa cdm, hawana jipya kwani ukizuiwa kinyume na sheria na wewe ndi unavunja sheria si unatakiwa uende mahakamani basi kupigana isingekuwa kosa ingekuwa mtu akikupiga na wewe mpige kisha kesi imeisha
 
Ili wengine ambao hawajapata kuona kipande cha ripoti wafaidi; hapa chini ni muhtasari wa ripoti yenyewe.
http://chragg.go.tz/?p=313

MUHTASARI WA TAARIFA YA TUME YA UCHUNGUZI WA TUKIO LILILOPELEKEA KIFO CHA DAUDI MWANGOSI
Posted on October 10, 2012 by admin
TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA
(THBUB)
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
MUHTASARI WA TAARIFA YA TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA YA UCHUNGUZI WA TUKIO LILILOPELEKEA KIFO CHA DAUDI MWANGOSI KILICHOTOKEA SEPTEMBA 2, 2012 KIJIJINI NYOLOLO
1.0 UTANGULIZI
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) ni idara huru ya serikali iliyoundwa kwa mujibu wa Kifungu cha 129(1)(c) cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 na Sheria ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Na. 7 ya mwaka 2001. Jukumu kubwa la Tume ni kulinda, kutetea na kuhifadhi haki za binadamu nchini. Katika kutekeleza jukumu hilo Tume imepewa mamlaka ya kupokea malalamiko (kwa njia mbalimbali) kutoka kwa mtu yeyote au kuanzisha uchunguzi wake yenyewe endapo itaona kuna uvunjifu wa haki za binadamu na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora. Kwa kuzingatia majukumu hayo, Tume ilianzisha uchunguzi wake yenyewe baada ya vyombo vya habari kutoa taarifa ya tukio la kifo cha Daudi Mwangosi. Tume iliunda timu ya watu watatu iliyoongozwa na Mhe. Kamishna Bernadeta Gambishi akisaidiwa na maafisa wawili, Bwana Gabriel Lubyagila na Bwana Yohana Mcharo. Timu hiyo ilifanya uchunguzi wake kuanzia tarehe 13-19 Septemba, 2012. Katika uchunguzi uliofanywa, Tume ilizingatia zaidi masuala ya uvunjwaji wa haki za binadamu na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora. Hivyo basi, Tume ilitilia maanani Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, sheria mbalimbali za nchi na mikataba ya kimataifa na ya kikanda inayohusu haki za binadamu ambayo Tanzania imeridhia.
Kwa kuzingatia matakwa ya sheria ya Tume Na. 7 ya mwaka 2001, baada ya uchunguzi huo kukamilika, Tume imeandaa taarifa yake na kuiwasilisha kwenye mamlaka husika kwa hatua zaidi.
Taarifa ya uchunguzi wa Tume imegawanyika katika sehemu kuu nne, ambazo ni:
a) Maelezo ya viongozi, watendaji na wananchi waliohojiwa
b) Uchambuzi wa taarifa/vielelezo vilivyopokelewa kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu mbalimbali zinazohusiana na masuala ya haki za binadamu
c) Matokeo ya uchunguzi
d) Maoni na mapendekezo.
Kwa kuwa tukio la kifo cha Daudi Mwangosi liligusa hisia za jamii, Tume imeona ni vyema kukutana na wawakilishi wa vyombo vya habari ili kutoa taarifa yake.

2.0 MATOKEO YA UCHUNGUZI
Katika uchunguzi wake Tume imebaini kuwa:
a) Tarehe 02/09/2012 Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kiliruhusiwa na Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Mufindi (OCD) kufanya mikutano ya ndani na kuzindua matawi mapya. Lakini jioni ya tarehe 01/09/2012 Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa (RPC), alizuia CHADEMA kufanya mikutano iliyoruhusiwa na OCD ambaye ni “Officer In-charge” wa polisi wa eneo husika kama sheria inavyotaka.
b) Viongozi wa CHADEMA walikuwa na mazungumzo na Mkuu wa Polisi Mkoa Upelelezi (RCO) na kuruhusiwa kufungua matawi yao bila ya kuwa na mikutano ya hadhara. c) Msajili wa vyama vya siasa aliwaandikia barua viongozi wa vyama vya siasa kuwataka kusitisha shughuli zao kwa sababu ya sensa. d) Wakati shughuli za uzinduzi wa tawi la Nyololo ukiendelea, RPC alifika katika eneo hilo na kuamuru viongozi wa CHADEMA wakamatwe; na kuwa wafuasi wa CHADEMA walipinga kukamatwa kwa viongozi wao. e) RPC aliamuru kupigwa kwa mabomu ya machozi ili kuwatawanya wananchi waliokusanyika katika ofisi za tawi hilo la CHADEMA. f) Baada ya mabomu ya machozi kupigwa, wananchi walitawanyika na kukimbia ovyo; na kuwa marehemu Daudi Mwangosi alizingirwa na askari, aliteswa na hatimaye inadaiwa alipigwa bomu na kufa hapo hapo. g) Daudi Mwangosi aliuwawa umbali wa takriban mita 100 kutoka ilipo Ofisi ya CHADEMA tawi la Nyololo. h) Katika tukio hilo wananchi kadhaa walijeruhiwa kwa mabomu, wakiwemo Mwandishi wa Habari wa Nipashe, Bwana Godfrey Mushi, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake CHADEMA Wilaya ya Mufindi, Bibi Winnie Sanga na Mkuu wa Kituo cha Polisi Mufindi, Asseli Mwampamba aliyekuwa akifanya jitihada za kumuokoa marehemu Daudi Mwangosi. Kutokana na hayo yote, Tume imejiridhisha kuwa tukio lililopelekea kifo cha Daudi Mwangosi limegubikwa na uvunjwaji wa haki za binadamu na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora. 2.1 Uvunjwaji wa Haki za Binadamu
Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977, sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, Azimio la Kimataifa la Haki za Binadamu (Universal Declaration of Human Rights of 1948), Mkataba wa Kimataifa kuhusu haki za kiraia na kisiasa (International Covenant on Civil and Political Rights of 1966) na Mkataba wa mataifa ya Afrika kuhusu Haki za Binadamu na Watu (African Charter on Human and Peoples Rights of 1981), Tume imejiridhisha kuwa Jeshi la Polisi limevunja haki zifuatazo:
§ Haki ya kuishi,
§ Haki ya kutoteswa na kupigwa,
§ Haki ya usawa mbele ya sheria na
§ Haki ya kukusanyika na kutoa maoni. CHADEMA ni chama cha siasa ambacho kina usajili wa kudumu. Chini ya sheria ya vyama vya siasa (Cap. 258 RE. 2002), vyama vya siasa vyenye usajili vimeruhusiwa kufanya maandamano na kuwa na mikutano ya kujitangaza baada ya kutoa taarifa kwa “Afisa wa Polisi” wa eneo husika. Baada ya taarifa kutolewa chama husika kinatakiwa kipewe ulinzi na “security agencies” (mawakala wa usalama). 2.2 Ukiukwaji wa Misingi ya Utawala Bora
Ili pawepo utawala bora mamlaka zote za serikali ni lazima zifuate utawala wa sheria. Uchunguzi umebaini kuwa kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Michael Kamuhanda tarehe 02/09/2012 katika utekelezaji wa majukumu yake alikiuka Sheria ya vyama vya siasa (Cap 258 RE. 2002) kifungu cha 11(a) na (b) na sheria ya Polisi (Sura ya 322) kwa kuingilia kazi za OCD wa Mufindi na kutoa amri ya kuzuia shughuli za CHADEMA wakati yeye hakuwa “Officer In-charge” wa polisi wa eneo husika. Kwa maana hiyo amri aliyoitoa haikuwa halali kwa kuwa ilitolewa na mtu ambaye hakuwa na mamlaka kisheria kutoa amri hiyo. Haya ni matumizi mabaya ya mamlaka, hivyo ni ukiukwaji wa misingi ya utawala bora.
Aidha, hatua ya Msajili wa vyama vya siasa, Mhe. John Tendwa kuwaandikia barua viongozi wa vyama vya siasa kuwataka kusitisha shughuli zao kwa sababu ya sensa ilikiuka misingi ya utawala bora kwani maelekezo yaliyotolewa ndani ya barua hizo yanakinzana na sheria ya takwimu Na. 1 ya mwaka 2002 inayotoa fursa kwa wananchi kuendelea na kazi zao wakati wa sensa pia ni kinyume na sheria ya vyama vya siasa (Cap 258 RE. 2002) Kifungu cha 11(a) na (b) inayotoa fursa kwa vyama vya siasa kufanya shughuli zake bila ya kuingiliwa. Ibara ya 8(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaelezea kwamba Tanzania ni nchi inayofuata misingi ya demokrasia na Haki ya Kijamii, aidha ibara 18(b) na (c) ya Katiba inaeleza kuwa kila mtu anayo haki ya kufanya mawasiliano (kutoa maoni/habari) na haki ya kutoingiliwa katika mawasiliano yake. Haki hii imekiukwa kwa kiasi kikubwa na Jeshi la Polisi katika tukio la Nyololo Mufindi kwa kuwa waandishi wa habari na wafuasi wa CHADEMA walizuiwa na Polisi kufanya shughuli zao za kupata habari na za kisiasa. Huu ni ukiukwaji wa misingi ya utawala bora kwa kuwa hali hiyo inazorotesha au inafifisha uhuru wa habari.

3.0 MAONI NA MAPENDEKEZO

Kwa kuzingatia Sheria ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Na. 7 ya mwaka 2001 Kifungu cha 15(2)(c) na 28 Tume inapendekeza yafuatayo:
1. Kamati za ulinzi na usalama za Mkoa na Wilaya ziwe makini na vitendo vya uvunjwaji wa haki za binadamu na ukiukwaji wa misingi ya utalawa bora vinavyofanywa na mamlaka mbalimbali kwenye maeneo yao. Aidha, kamati hizo zihusike moja kwa moja na usalama wa wananchi na mali zao kwa kujadili masuala yote ya kiusalama kabla hatua hazijachukuliwa na vyombo vinavyotekeleza sheria.
2. Viongozi wa CHADEMA na wafuasi wao waepuke malumbano na vyombo vya dola kwa kutii maagizo yanayotolewa na vyombo hivyo bila shuruti. Pale wanapogundua kuwa pana uonevu au upendeleo ni vyema busara ikatumika ili kuepusha madhara makubwa yanayoweza kutokea. 3. Jeshi la Polisi na Msajili wa Vyama vya Siasa waepuke kufanya maamuzi au matendo yanayoibua hisia za ubaguzi au upendeleo miongoni mwa jamii wakati wanapotekeleza majukumu yao ya kisheria. Mfano, Jeshi la Polisi lilizuia mikutano ya CHADEMA kwa sababu ya sensa wakati huo huo Chama cha Mapinduzi (CCM) walikuwa wakifanya uzinduzi wa Kampeni huko Zanzibar. Aidha, rai ya Msajili wa vyama vya siasa haikuzingatiwa kwa upande wa CCM Zanzibar huku CHADEMA walishurutishwa na Polisi kutii rai hiyo. 4. Demokrasia ya mfumo vya vyama vingi iheshimiwe na kulindwa. 5. Elimu ya vyama vya siasa na sheria ya Polisi kuhusu vyama vya siasa itolewe kwa askari polisi ambao wanaonekana kutozifahamu kabisa.

4.0 HITIMISHO
Jukumu la kulinda amani na utulivu ni wajibu wa kila mtanzania, mkulima na mfanyakazi, viongozi wa serikali na watumishi wa umma wote wanapaswa kuwa wazalendo wa kweli wakati wanapotekeleza majukumu yao ya kila siku. Tume inatoa wito kwa watanzania wote kuheshimu haki za binadamu na kutekeleza kwa vitendo misingi ya utalawa bora. Kwa kufanya hivi Taifa letu litaendelea kuwa na amani na utulivu. Tume inatoa rai kwa jeshi la polisi kutekeleza wajibu wake mkuu wa ulinzi na usalama wa raia bila kutumia jazba.
Kuwepo kwa vyama vya siasa ionekane kuwa ni kukuwa kwa demokrasia na sio kuwa ni upinzani kwa chama tawala.
Jaji Kiongozi (Mstaafu) Amiri R. Manento
MWENYEKITI
TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA
OKTOBA 10, 2012
 
Nakushukuru Mwanakijiji tena Mzee wa busara nyingi kwa fikra hii yenye nguvu na uhai wa kiharakati. Mawazo chanya kama haya yanahitajika sana katika kusukuma harakati za ukombozi wa nchi yetu, na yanatakiwa sana hasa nyakati hizi ambapo kuna harakati nyingi zenye lengo moja zinaendelea.

Tunashukuru sana kwa wazo lako; natumaini litafanyiwa kazi mapema na wahusika maana hiyo ndiyo kazi iliyopo barabarani. Natumaini ule msemo wa wahenga usemao: Mwanzo ni mwanzo, hakuna mwanzo mbaya ina maana kubwa sana kwa hoja yako. Ingawa CHADEMA imechelewa kutoa tamko, lakini kauli yako imewasaidia watanzania wengine kuona umuhimu wa CHADEMA kutoa matamko haya nyakati kama hizi; na hivyo kujiandaa kuchukua hatua pindi yanaposhindwa kutekelezwa na serikali hii ya chama cha kifisadi.
 
Ningetaka kuandika kwa kirefu sana kuelezea jambo ambalo labda kwa kifupi lingetosha kuelezewa. Sijaelewa kwanini hadi leo hii masaa zaidi ya 24 tangu Jaji Manento atoe muhtasari wa ripoti yake ya Tume ya Kudumu ya Haki za Binadamu na Utawala Bora iliyonyoshea kidole serikali (Polisi na Msajili wa Vyama vya Siasa) kuwa ndio walioingilia kati uhuru wa CDM kufanya mikutano yake na kusababisha uvunjwaji wa amani, kupigwa kwa wananchi na kuuawa kwa mwandishi wa habari Daud Mwangosi.

Inashangaza kuwa CDM ambao siku mbili nyuma walilaumiwa na Kamati ya Nchimbi kuwa ndio chanzo hasa cha vurugu wamejikuta wakisafishwa na chombo cha juu zaidi na chenye nguvu zaidi za kisheria na badala ya wao kutumia nafasi hiyo wameamua kukaa kimya kana kwamba lililosemwa ni dogo. Ikumbukwe kuwa tangu tukio lile la Iringa litokee ni CDM ambao walikuwa wanafanywa mashetani wa tukio hilo huku viongozi mbalimbali wakikituhumu kuwa ndiyo kilichosababisha tukio hilo baya kwa kutotii amri 'halali' ya serikali.

Tume imeweka wazi kuwa amri iliyotolewa haikutolewa kihalali na hivyo CDM hawakutakiwa kutii isipokuwa kwa busara tu lakini hakukuwa na legal basis ya wao kutii amri isiyo halali. Kumbe tukio zima linawaangukia Msajili wa Vyama vya Siasa John Tendwa na Kamishna Kamuhanda pamoja na viongozi wa juu wa jeshi la Polisi waliohalalisha uvunjivu wa haki za binadamu na matumizi mabaya ya madaraka.

Yale maandamano ambayo wamekuwa wakiyanfay kwa M4C hadi hivi sasa hayajabadilisha mfumo wowote, hayajamuondoa mtu yeyote madarakani na kwa hakika yamekuwa ni maandamano ya kuhubiria waumini tayari! Sielewi kwanini Kamuhanda bado yupo, Kagonja bado yupo na Tendwa bado yupo?

I mean najua sehemu ya jibu - wanasubiri kukaa kama kikao cha kamati kuu ili waamue kwa pamoja bla bla bla bla bala... well.. ukivumilia ujinga utatendewa kijinga! CDM needs to seize this opportunity to force the resignations of those who were implicated! Vinginevyo kama nilivyowahi kuwaambia huko nyuma.. wasubiri kuendelea kubeba majeneza na kutoa hutuba za uchungu hadi qiyama.

Mkuu MM, Wakuu JF

Kwa mtazamo wa haraka mtu anaweza kufikia hitimisho alilonalo MM na wengine wanaoungana mkono naye. Bahati nzuri ni kwamba kwa mtazamo makini kabisa utaweza kuona kuwa kama ilivyo kawaida ya CHADEMA na bila shaka kila mtu angependa umakini huo uendelezwe kwa gharama yoyote, katika suala hili pia CHADEMA imehakikisha ina-maintain Hilo. Kitu gani kisemwe, wakati gani, kwa nini, mahali gani na nani. Maana muhimu pia si kusema tu.

Mathalani ukifanya tafakuri jadidi ndogo tu hivi, utaona kuwa THBUB/CHRAGG wametoa muhtasari wa ripoti ya uchunguzi wao Oktoba 9, 2012. Ikatoka kwenye mainstream media kwa ajili ya mass consumption Oktoba 10, 2012, kwa lugha rahisi ni jana. Hapa JF ni mashahidi kuwa ndani ya masaa 24 tangu kutoka kwa ripoti hiyo ya CHRAGG Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani, Vincent Nyerere akatoa kauli yake ya awali juu ya suala hili.

Kutokana na chama kuwa na network imara ya mawasiliano ikiratibiwa kwa kiasi kikubwa na Kurugenzi ya Habari na Uenezi, hasa kupitia Idara ya Habari, tulijua Waziri Kivuli atazungumza jana, hivyo tuliona umuhimu wa waziri kivuli na chama kutosema kwa siku hiyo hiyo moja ambayo MM na wengine wanataka kuwa CHADEMA ilipaswa iwe imeshasema neno, kauli au tamko, call it any how, lakini iwe imesema.

Lakini kuonesha kuwa tuko in touch na hili suala, leo hii asubuhi hii, wakati hapa mjadala huu umeshika kasi, wengine tulikuwa 'kazini' kuhakikisha kuwa chama Kinabo kauli. Tayari tumetuma kwa Vyombo vya Habari, kauli ya Mkurugenzi wa Habari na Uenezi, juu ya suala hili hili, ikielezea mpaka sasa chama kiko kwenye position gani na ufafanuzi aw masuala kadhaa, hasa kutokana na mjadala wa muhtasari wa ripoti hizo tatu.

Kwa hiyo kesho kutakuwa na taarifa hiyo kwenye Vyombo vya Habari au kuanzia leo asubuhi, mchana, jioni, usiku na kesho kwa maana ya electronic and print media coverage. Tamko limetoa ufafanuzi wa masuala mengi tu ya msingi, bila shaka bila kuathiri masharti ya Ibara yoyote hapa, mara litakapowekwa hapa JF, Mods wanaweza kuunganisha kwenye mjadala huu.

Kwa sasa suala is kusema tu

Wakuu kama nilivyosema hapo juu, kila mmoja wetu hapa angependa kuona CHADEMA ikieendeleza umakini ule ule ambao siku zote umefanya wananchi wakiamini, hivyo kwa hatua iliyofikia wananchi wangependa kuona hatua zinazochukuliwa, hivyo kitakachosemwa kiendane na hatua zinazopangwa kuchukuliwa, hivyo suala si kusema tu for the sake ya kusema. Watu wanataka kuona hatua...Hilo ndilo litakalofanywa na viongozi wakuu wa CHADEMA ndani ya muda mfupi kwa sababu tunajua kwa hakika umma una hamu ya kusikia CHADEMA inasema nini. Na hili linapaswa kufanyika baada ya kufanya analysis ya ripoti zote tatu.

Ni kutokana na hamu hiyo ndiyo maana hata Mhariri wa moja ya magazeti makubwa nchini leo akaandika 'CHADEMA yasema...'

Mpaka sasa ukiangalia kwa makini hakuna timu ya uchunguzi kati ya hizo tatu, iliyotoa taarifa ya uchunguzi katika ukamilifu wake, achilia mbali ile timu nyingine ambayo 'wamechimba' kwa kusingizia kuingilia Uhuru wa mahakama, ni vyema sana kufanya uchambuzi wa ripoti za uchunguzi katika ukamilifu wake, si muhtasari. Hili linaeleweka vyema kwa mtu yeyote makini.

Otherwise watumishi wenu ambao mnawategemea kuhakikisha kila kitu kiko under control, hasa katika mawasiliano ya ndani na nje ya chama, kwa umma, wako full swing. Kwa mfano naweza kusema hapa, juzi kabla ya THBUB hawajazungumza tulikuwa tunapanga namna gani ya kushughulika na ripoti zile mbili za mwanzo, lakini tulipong'amua kuwa tume itatoa ripoti yake (kitu ambacho hata baadhi ya waandishi/Vyombo vya habari havikuwa na habari), tukaamua kuacha kwanza. Jana pia tukaacha baada ya Waziri Kivuli kuzungumza.

Lakini pia kama mjuavyo CHADEMA walifanywa kuwa kondoo wa kafara katika sakata zima, mtuhumiwa mkubwa wa baadhi ya mamlaka za serikali na viongozi wa kiserikali na vyama vibaraka, ingawa ukweli tuliousema ndiyo huo huo baadhi ya timu zimeuweka hadharani baada ya uchunguzi, hivyo ilikuwa wakati mwafaka we wadau wengine kutoa maoni yao juu ya suala hilo kutokana na ripoti hizo.

Nawahakikishia Watanzania wote makini na wapenda nchi yao, waliochoshwa na status quo, wanaopigania kwa dhati mabadiliko ya kweli ya kimfumo na kiutawala na uhuru wa kweli kwa Watz wote kunufaika na rasilimali zao, huku nchi yao ikisimamiwa kwa falsafa ya nguvu ya umma, ambao tunajua kutoka vijijini hadi mijini, vitongoji mpaka mitaa, wanasubiri kwa hamu kusikia CHADEMA inasema na kuelekeza hatua gani za kuchukuliwa, juu ya matukio ya serikali ya CCM kuanza kuteka, kutesa na kuua, kama njia ya kukabili vuguvugu na harakati za kudai haki na uwajibikaji, kwa ajili ya amani na mustakabali mwema wa nchi, HAWATASUBIRI MUDA MREFU kuanzia Leo, kabla hawajasikia chama chao kimesema nini.

Wala hatalazimika kusubiri kikao kikuuuuuubwa, kwa sababu mamlaka ya juu katika uendeshaji wa chama chao, CC tayari ilishatoa maazimio katika masuala yote yanayozungumzwa sasa kuhusu mauaji ya raia wasiokuwa na hatia yanayofanywa na Vyombo vya dola, kwa maslahi ya kisiasa.

Wasalaam
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom