CHADEMA mnataka mteremshiwe gunia la chawa?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
Ningetaka kuandika kwa kirefu sana kuelezea jambo ambalo labda kwa kifupi lingetosha kuelezewa. Sijaelewa kwanini hadi leo hii masaa zaidi ya 24 tangu Jaji Manento atoe muhtasari wa ripoti yake ya Tume ya Kudumu ya Haki za Binadamu na Utawala Bora iliyonyoshea kidole serikali (Polisi na Msajili wa Vyama vya Siasa) kuwa ndio walioingilia kati uhuru wa CDM kufanya mikutano yake na kusababisha uvunjwaji wa amani, kupigwa kwa wananchi na kuuawa kwa mwandishi wa habari Daud Mwangosi.

Inashangaza kuwa CDM ambao siku mbili nyuma walilaumiwa na Kamati ya Nchimbi kuwa ndio chanzo hasa cha vurugu wamejikuta wakisafishwa na chombo cha juu zaidi na chenye nguvu zaidi za kisheria na badala ya wao kutumia nafasi hiyo wameamua kukaa kimya kana kwamba lililosemwa ni dogo. Ikumbukwe kuwa tangu tukio lile la Iringa litokee ni CDM ambao walikuwa wanafanywa mashetani wa tukio hilo huku viongozi mbalimbali wakikituhumu kuwa ndiyo kilichosababisha tukio hilo baya kwa kutotii amri 'halali' ya serikali.

Tume imeweka wazi kuwa amri iliyotolewa haikutolewa kihalali na hivyo CDM hawakutakiwa kutii isipokuwa kwa busara tu lakini hakukuwa na legal basis ya wao kutii amri isiyo halali. Kumbe tukio zima linawaangukia Msajili wa Vyama vya Siasa John Tendwa na Kamishna Kamuhanda pamoja na viongozi wa juu wa jeshi la Polisi waliohalalisha uvunjivu wa haki za binadamu na matumizi mabaya ya madaraka.

Yale maandamano ambayo wamekuwa wakiyanfay kwa M4C hadi hivi sasa hayajabadilisha mfumo wowote, hayajamuondoa mtu yeyote madarakani na kwa hakika yamekuwa ni maandamano ya kuhubiria waumini tayari! Sielewi kwanini Kamuhanda bado yupo, Kagonja bado yupo na Tendwa bado yupo?

I mean najua sehemu ya jibu - wanasubiri kukaa kama kikao cha kamati kuu ili waamue kwa pamoja bla bla bla bla bala... well.. ukivumilia ujinga utatendewa kijinga! CDM needs to seize this opportunity to force the resignations of those who were implicated! Vinginevyo kama nilivyowahi kuwaambia huko nyuma.. wasubiri kuendelea kubeba majeneza na kutoa hutuba za uchungu hadi qiyama.

Mkuu MM, Wakuu JF

Kwa mtazamo wa haraka mtu anaweza kufikia hitimisho alilonalo MM na wengine wanaoungana mkono naye. Bahati nzuri ni kwamba kwa mtazamo makini kabisa utaweza kuona kuwa kama ilivyo kawaida ya CHADEMA na bila shaka kila mtu angependa umakini huo uendelezwe kwa gharama yoyote, katika suala hili pia CHADEMA imehakikisha ina-maintain Hilo. Kitu gani kisemwe, wakati gani, kwa nini, mahali gani na nani. Maana muhimu pia si kusema tu.

Mathalani ukifanya tafakuri jadidi ndogo tu hivi, utaona kuwa THBUB/CHRAGG wametoa muhtasari wa ripoti ya uchunguzi wao Oktoba 9, 2012. Ikatoka kwenye mainstream media kwa ajili ya mass consumption Oktoba 10, 2012, kwa lugha rahisi ni jana. Hapa JF ni mashahidi kuwa ndani ya masaa 24 tangu kutoka kwa ripoti hiyo ya CHRAGG Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani, Vincent Nyerere akatoa kauli yake ya awali juu ya suala hili.

Kutokana na chama kuwa na network imara ya mawasiliano ikiratibiwa kwa kiasi kikubwa na Kurugenzi ya Habari na Uenezi, hasa kupitia Idara ya Habari, tulijua Waziri Kivuli atazungumza jana, hivyo tuliona umuhimu wa waziri kivuli na chama kutosema kwa siku hiyo hiyo moja ambayo MM na wengine wanataka kuwa CHADEMA ilipaswa iwe imeshasema neno, kauli au tamko, call it any how, lakini iwe imesema.

Lakini kuonesha kuwa tuko in touch na hili suala, leo hii asubuhi hii, wakati hapa mjadala huu umeshika kasi, wengine tulikuwa 'kazini' kuhakikisha kuwa chama Kinabo kauli. Tayari tumetuma kwa Vyombo vya Habari, kauli ya Mkurugenzi wa Habari na Uenezi, juu ya suala hili hili, ikielezea mpaka sasa chama kiko kwenye position gani na ufafanuzi aw masuala kadhaa, hasa kutokana na mjadala wa muhtasari wa ripoti hizo tatu.

Kwa hiyo kesho kutakuwa na taarifa hiyo kwenye Vyombo vya Habari au kuanzia leo asubuhi, mchana, jioni, usiku na kesho kwa maana ya electronic and print media coverage. Tamko limetoa ufafanuzi wa masuala mengi tu ya msingi, bila shaka bila kuathiri masharti ya Ibara yoyote hapa, mara litakapowekwa hapa JF, Mods wanaweza kuunganisha kwenye mjadala huu.

Kwa sasa suala si kusema tu.

Wakuu kama nilivyosema hapo juu, kila mmoja wetu hapa angependa kuona CHADEMA ikieendeleza umakini ule ule ambao siku zote umefanya wananchi wakiamini, hivyo kwa hatua iliyofikia wananchi wangependa kuona hatua zinazochukuliwa, hivyo kitakachosemwa kiendane na hatua zinazopangwa kuchukuliwa, hivyo suala si kusema tu for the sake ya kusema. Watu wanataka kuona hatua...Hilo ndilo litakalofanywa na viongozi wakuu wa CHADEMA ndani ya muda mfupi kwa sababu tunajua kwa hakika umma una hamu ya kusikia CHADEMA inasema nini. Na hili linapaswa kufanyika baada ya kufanya analysis ya ripoti zote tatu.

Ni kutokana na hamu hiyo ndiyo maana hata Mhariri wa moja ya magazeti makubwa nchini leo akaandika 'CHADEMA yasema...'

Mpaka sasa ukiangalia kwa makini hakuna timu ya uchunguzi kati ya hizo tatu, iliyotoa taarifa ya uchunguzi katika ukamilifu wake, achilia mbali ile timu nyingine ambayo 'wamechimba' kwa kusingizia kuingilia Uhuru wa mahakama, ni vyema sana kufanya uchambuzi wa ripoti za uchunguzi katika ukamilifu wake, si muhtasari. Hili linaeleweka vyema kwa mtu yeyote makini.

Otherwise watumishi wenu ambao mnawategemea kuhakikisha kila kitu kiko under control, hasa katika mawasiliano ya ndani na nje ya chama, kwa umma, wako full swing. Kwa mfano naweza kusema hapa, juzi kabla ya THBUB hawajazungumza tulikuwa tunapanga namna gani ya kushughulika na ripoti zile mbili za mwanzo, lakini tulipong'amua kuwa tume itatoa ripoti yake (kitu ambacho hata baadhi ya waandishi/Vyombo vya habari havikuwa na habari), tukaamua kuacha kwanza. Jana pia tukaacha baada ya Waziri Kivuli kuzungumza.

Lakini pia kama mjuavyo CHADEMA walifanywa kuwa kondoo wa kafara katika sakata zima, mtuhumiwa mkubwa wa baadhi ya mamlaka za serikali na viongozi wa kiserikali na vyama vibaraka, ingawa ukweli tuliousema ndiyo huo huo baadhi ya timu zimeuweka hadharani baada ya uchunguzi, hivyo ilikuwa wakati mwafaka we wadau wengine kutoa maoni yao juu ya suala hilo kutokana na ripoti hizo.

Nawahakikishia Watanzania wote makini na wapenda nchi yao, waliochoshwa na status quo, wanaopigania kwa dhati mabadiliko ya kweli ya kimfumo na kiutawala na uhuru wa kweli kwa Watz wote kunufaika na rasilimali zao, huku nchi yao ikisimamiwa kwa falsafa ya nguvu ya umma, ambao tunajua kutoka vijijini hadi mijini, vitongoji mpaka mitaa, wanasubiri kwa hamu kusikia CHADEMA inasema na kuelekeza hatua gani za kuchukuliwa, juu ya matukio ya serikali ya CCM kuanza kuteka, kutesa na kuua, kama njia ya kukabili vuguvugu na harakati za kudai haki na uwajibikaji, kwa ajili ya amani na mustakabali mwema wa nchi, HAWATASUBIRI MUDA MREFU kuanzia Leo, kabla hawajasikia chama chao kimesema nini.

Wala hatalazimika kusubiri kikao kikuuuuuubwa, kwa sababu mamlaka ya juu katika uendeshaji wa chama chao, CC tayari ilishatoa maazimio katika masuala yote yanayozungumzwa sasa kuhusu mauaji ya raia wasiokuwa na hatia yanayofanywa na Vyombo vya dola, kwa maslahi ya kisiasa.

Wasalaam
 
Niliwahi kusema maneno ambayo si matamu kwa baadhi ya watu kwamba Chadema wanaachezezea shilingi chooni na kuna mambo ambayo wanafanya kwa mazoea hadi kufikia mahali watu makini wanashindwa kuwatofautisha na vyama vingine ikiwamo CCM.

Tuwe wakweli kwamba kuna mambo ambayo yanawasaidia sana CDM ambayo yanatokana na udhaifu wa CCM na baaadhi watendaji serikalini mambo ambayo wahusika wakiyafanyia kazi (japo nu ndoto) Cdm watakua na kazi ngumu zaidi ya kufikia malengo yao ya kisiasa ikiwa ni pamoja na kushika dola. kuhusu Ripoti yaJaji Amiri Manento, naungana na Mwanakijiji kwamba CDM walipaswa kufanya siasa mapema tena mara tu tume mbili zilipowasilisha taarifa zake kwani Tundu Lissu alishazikataa mapema na hapo ndipo palikua mahali pa kuanzia.
 
mimi mwenyewe nna vibrate kila dk watanzania tumelala jamani kwa nini tusiingie mtaani tukamtimue yule mpangaji fedhuli pale magogoni? aaaaaaaaargh
 
Mzee Mwanakijiji kwa mambo kama haya yanayofanywa ni nahakika waathirika wa watukio hayo sio CDM bali ni ukandamizaji na uonevu dhidi ya uma.
Watanzania wanatakiwa waamke na uchukua hatua kukomesha ubaladhuli huu na sio kua na Taasisi, vyama na mashirika ya kutoa kauli tu bila kuonyesha vitendo
 
Last edited by a moderator:
Kwa kweli katika hili viongozi wangu wamechelewa, mimi nilitarajia hata baada ya ripoti za MCT na ile ya Nchimbi mara moja lingetolewa tamko zito sana, bahati nzuri tume ya haki za binadamu na utawala bora inekuja kumaliza kazi.

Kama alivyosema mdau hapo juu VUTA-NKUVUTE, tumepata penalty dakika ya mwisho ya muda wa nyongeza. Natarajia hadi kesho tutakuwa tumesikia kauli rasmi ya chama juu ya hizi ripoti.
 
Last edited by a moderator:
Hatahivyo nikubali chadema walipaswa kutoa tamko la nguvu zaidi ambalo lingepaswa kutolewa na ama slaa au mbowe ili lipate heading za kutosha kwenye vyombo vya habari ili kufukia mashimo yaliyochimbwa na wenzao
kusema kweli ni Golden chance!
 
Baada ya ripoti ya tume ya jaji Manento ambayo ndio tume halali yenye mamlaka ya kisheria yanatakiwa yafanyike maandamano ya yasiyo kuwa na kikomo mkoani Iringa kuhakikisha kuwa Kamanda Kamuhanda,Mwema, chagonja na Nchimbi wanang'oka kwenye nafasi zao. Kuna mambo viongozi wetu wa chama wanatakiwa kuongozwa na busara lakini sio hili ambalo mara baada ya tukio chama kikapakwa matope kupitia vipindi vya kupika kwenye runinga.

1. Dr slaa.
2. Mbowe
3. Lissu
4. Zitto
Popote mlipo, amkeni mhamasishe umma wa wana Iringa ili kumtendea haki marehemu Daudi Mwangosi,ally zona na wengine wengi walio uwawa mikononi mwa Polisi, ile kauli ya hakuna kulala mpaka kieleweke ndio inatakiwa kutumika hapa kuwaondoa mabaradhuri walio sababisha vifo vya watanzania wenzetu! Chama kitatuangusha kama kitanyamaza baada ya kutolewa ripoti yenye nguvu za kisheria.

Tusisubiri kesho, tuanze sasa maana ukimya wetu ni mauti kwa wengine, 'hakuna kulala mpaka haki ipatikane, na ikipatikana wahusika wawe wameshapoteza nafasi zao'
 
Kwa kweli katika hili viongozi wangu wamechelewa, mimi nilitarajia hata baada ya ripoti za MCT na ile ya Nchimbi mara moja lingetolewa tamko zito sana, bahati nzuri tume ya haki za binadamu na utawala bora inekuja kumaliza kazi.

Kama alivyosema mdau hapo juu VUTA-NKUVUTE, tumepata penalty dakika ya mwisho ya muda wa nyongeza. Natarajia hadi kesho tutakuwa tumesikia kauli rasmi ya chama juu ya hizi ripoti.

Tujadili tukitambua kwamba Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora ni chombo cha serikali na kwa kweli huu ni mfanomhai kwamba kuna mambo hayahitaji tume wqla kamati bali tunahitaji uwajibikaji wa vyombo vilivyopo. Kama ni suala la haki za binadamu kuna chomo, kama ni rushwa kuna chombo kama ni jinai kuna chombo, tatizo kubwa ni hajuna uwajibikaji kila eneo na hapo ndipo zinaibuka tume kufunika kombe na kuwapa watu ulaji na kudhulumu haki za wengine. Watu ama vyombo visivyowajibika viwajibishwe na watawala kwani na wao wwtawajibishwa na umma kupitia kura. Tutengeneze mfumo wa uwajibikaji na Chadema kama chama mbadala kifanye kazi ya kutoa mawazo mbadala ya kubadili mfumo na si kujiandaa kuongoza kwa mazoea.
 
Last edited by a moderator:
Mbona mnakuwa waoga kiasi hicho wakati nyie mnataka kuwakomboa watanzania.

Hapo anamtahadharisha tu kwakuwa serikali yenu dhaifu inajua kuonea wananchi wanyonge, hao polisi wakipigiwa simu kwamba majambazi wamevamia sehemu hawfiki hadi wajiridhishe kwamba wameshaondoka.

Chadema si waoga na ndio maana pamoja na vitisho, mateso na mauaji bado tu tunaendelea na movement zetu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom