Nitaenda moja kwa moja kwenye msingi wa hoja yangu.
Option ya kwanza: Chadema ya leo inahitaji viongozi watakaokirudisha chama kwenye misingi yake ya zamani, misingi ya ujasiri, misingi ya hoja, misingi ya uanaharakati. Kuirudisha Chadema ya kina Slaa, Chadema ya kina Heche wakisema tukawatoe viongozi mahabusu vijana wanakwenda. Leo viongozi na wanachama wanauawa, wanatekwa, wanapotezwa, sijasikia tamko lolote la nguvu la chama zaidi ya press conference. Utawala huu sio wa press conférence, ni utawala wa kutunishiana misuli ni utawala wa Ukuta.
Option ya pili: Ili kukirudisha chama kwenye mstari, anzisheni harakati za kudai katiba mpya na tume huru ya uchaguzi, ikiwezekana tangazeni maandamano ya amani kama yale ya Ukuta kushinikiza katiba mpya ninaimani taasisi mbalimbali na watanzania wengi watawaunga mkono na chama kitarudi kwenye hadhi yake.
Option ya tatu: Kupitia kamati kuu, chama kiamue kuunga mkono maandamano ya trh 26/4 yaliyoandaliwa na wananchi, kitendo hiki kitaishitua serikali na kuilazimika kuwaita kwa lengo la kukaa pamoja ili kuzungumza na kumaliza tofauti zilizopo. Hii option ina risk kubwa lakini ina faida nyingi na za haraka, the more the risk the more the profit.
Option ya Nne: Najua hii itaonekana kuwa ngumu kidogo lakini nyepesi. Hakika uchaguzi ujao utakuwa ngumu kwa Chadema, chama kisipobadili mbinu za ushindi karibu wabunge wote wa Chadema hawatarudi bungeni (fact). Bunge halitakuwa na Msigwa wala Lema wala Mdee wala Mnyika, wala Bulaya. Ili kujiweka salama aidha Chama au wabunge wote waamue kumuunga mkono Magufuli kama wenzenu wanavyofanya au wabunge wakae kimya kusubiri mafao yao yawasaidie kuanza maisha mpya ya uraiani baada ya uchaguzi wa 2020.
Ili kubaki salama lazima chama kiamue kuchagua option mojawapo vinginevyo kitaendelea kupukutika na pengine kubaki jina kama vyama vingine.
==========≠=========
Huu hapa chini ni mchango wa mwanaJF mwenzetu, binafsi nimeona kuna kitu cha kujifunza. Kwanini kina Mbowe wateseke kwa Watanzania waliolala wasioonyesha hata kuguswa na juhudi zao?