Nitaenda moja kwa moja kwenye msingi wa hoja yangu.
Option ya kwanza: CHADEMA ya leo inahitaji viongozi watakaokirudisha chama kwenye misingi yake ya zamani, misingi ya ujasiri, misingi ya hoja, misingi ya uanaharakati. Kuirudisha CHADEMA ya kina Slaa, CHADEMAya kina Heche wakisema tukawatoe viongozi mahabusu vijana wanakwenda.
Leo viongozi na wanachama wanauawa, wanatekwa, wanapotezwa, sijasikia tamko lolote la nguvu la chama zaidi ya press conference. Utawala huu sio wa press conférence, ni utawala wa kutunishiana misuli ni utawala wa UKUTA.
Option ya pili: Ili kukirudisha chama kwenye mstari, anzisheni harakati za kudai katiba mpya na tume huru ya uchaguzi, ikiwezekana tangazeni maandamano ya amani kama yale ya UKUTA kushinikiza katiba mpya ninaimani taasisi mbalimbali na watanzania wengi watawaunga mkono na chama kitarudi kwenye hadhi yake.
Option ya Tatu: Najua hii itaonekana kuwa ngumu kidogo lakini nyepesi. Hakika uchaguzi ujao utakuwa mgumu sana kwa CHADEMA, chama kisipobadili mbinu za ushindi karibu wabunge wote wa CHADEMA hawatarudi bungeni (fact).
Bunge halitakuwa na Msigwa wala Lema wala Mdee wala Mnyika, wala Bulaya. Ili kujiweka salama aidha Chama au wabunge waamue kumuunga mkono Rais Magufuli kama wengine wanavyofanya au wabunge wakae kimya kusubiri mafao yao yawasaidie kuanza maisha mapya ya uraiani baada ya uchaguzi wa 2020.
Ili kubaki salama lazima chama kiamue kuchagua option mojawapo vinginevyo kitaendelea kupukutika na pengine kubaki jina kama vyama vingine.
================
Huu hapa chini ni mchango wa mwanaJF mwenzetu, binafsi nimeona kuna kitu cha kujifunza. Kwanini kina Mbowe wateseke kwa Watanzania waliolala wasioonyesha hata kuguswa na juhudi zao?
Option ya kwanza: CHADEMA ya leo inahitaji viongozi watakaokirudisha chama kwenye misingi yake ya zamani, misingi ya ujasiri, misingi ya hoja, misingi ya uanaharakati. Kuirudisha CHADEMA ya kina Slaa, CHADEMAya kina Heche wakisema tukawatoe viongozi mahabusu vijana wanakwenda.
Leo viongozi na wanachama wanauawa, wanatekwa, wanapotezwa, sijasikia tamko lolote la nguvu la chama zaidi ya press conference. Utawala huu sio wa press conférence, ni utawala wa kutunishiana misuli ni utawala wa UKUTA.
Option ya pili: Ili kukirudisha chama kwenye mstari, anzisheni harakati za kudai katiba mpya na tume huru ya uchaguzi, ikiwezekana tangazeni maandamano ya amani kama yale ya UKUTA kushinikiza katiba mpya ninaimani taasisi mbalimbali na watanzania wengi watawaunga mkono na chama kitarudi kwenye hadhi yake.
Option ya Tatu: Najua hii itaonekana kuwa ngumu kidogo lakini nyepesi. Hakika uchaguzi ujao utakuwa mgumu sana kwa CHADEMA, chama kisipobadili mbinu za ushindi karibu wabunge wote wa CHADEMA hawatarudi bungeni (fact).
Bunge halitakuwa na Msigwa wala Lema wala Mdee wala Mnyika, wala Bulaya. Ili kujiweka salama aidha Chama au wabunge waamue kumuunga mkono Rais Magufuli kama wengine wanavyofanya au wabunge wakae kimya kusubiri mafao yao yawasaidie kuanza maisha mapya ya uraiani baada ya uchaguzi wa 2020.
Ili kubaki salama lazima chama kiamue kuchagua option mojawapo vinginevyo kitaendelea kupukutika na pengine kubaki jina kama vyama vingine.
================
Hakuna option ninayoiunga mkono hata moja hapo! Waendelee kujijenga taratibu japo wanapigwa vibaya mpaka Siku watanzania watakapochoshwa vilivyo na watawala. Haiwezekani wakajiteeesa hku watz wengine wakijilalia makwao kusubiri mafanikio ya wakipiganiacho. Tazama Kenya serikali inajua wananchi sio waoga lkn hapa tunatishwa kama watoto na tunanywea nywiiii. Wapinzani msibebe saaana mzigo nendeni mdogomdogo wananchi nao waamke. Kina mbowe wako jela watu hawapazi sauti unadhani wamejitakia bhana