Mkuu, kuna kitu kinaitwa falsafa ya vita ambayo inaongozwa na two schools of thoughts, falsafa ya kwanza ni falsafa ya ushujaa, inayowatumia wapiganaji mashujaa, hawa motoo yao ni "fight, fight, fight", inaamini katika kupambana tuu, Mapambano!, yaani pigana, pigana, pigana, na hata kama unapigwa, "no retreat no surrender", endelea tuu kupigana mpaka mwisho, mpaka risasi ya mwisho na tone la mwisho la damu limwagike, hata mkifa wote na kuwa wiped out, mtakumbukwa kama mashujaa mlioipigania na kuifia nchi yenu, ila mmeshindwa vita na sasa wote ni mateka, wake zenu wanabakwa, na Watoto wenu wanafanywa watumwa!.
Falsafa ya pili ni falsafa ya umakini, inayowatumia wapiganaji makini, hawa hawapeleki jeshi vitani hadi kwanza waijue nguvu ya adui, kwa Imani kuwa "never fight a loosing battle", usipigane vita ambayo unajua hutashinda. Na ukiwa vitani, ukiona dalili za kushindwa vita, ama una surrender ili msiuawawe wote, au una retreat kwa kurudisha nyuma majeshi yako, kwenda kujipanga upya.
Kundi hili la wapiganaji makini, baada ya kujaribu kupigana na kushindana na kushindwa mara kadhaa kwa sababu adui yuko vizuri Zaidi yao, huamua kutumia kanuni inayoitwa, "If you can't beat them, join them". kama huwezi kuwashinda, jiunge nao, jifunze siri zao, jijenge upya na pigana nao kutokea ndani kwao!, yaani " fight from within". Hiki ndicho wanachokifanya baadhi ya wana CCM ambao wanajiunga CCM akiwemo Dr. Slaa. Hili nimelizungumzia hapa.
Tuko Vitani Tuna Wapiganaji Shupavu, Wapiganaji Makini na Watazamaji, Je! Wewe Uko Kundi Gani ?
Katika mazingira ya Tanzania, kati ya Dr. Slaa na MBOWE, ni nani shujaa wa kweli?. Kwa sisi tuliomsikiliza Dr. Slaa akizungumza kutoka moyoni mwake, huwezi amini amejiunga CCM kwa sababu anaipenda au anamuamini Magufuli, bali amejiunga CCM because he has to, its the only way!.
If you can't beat them, join them! He is the worst dictator. Let's pray for him!
P.