CHADEMA mna chaguo za kubaki salama

CHADEMA mna chaguo za kubaki salama

Mkuu, heading yangu inazungumzia Chadema sio kwamba matatizo mengine ya kitaifa siyajui, karibu tuzungumuzie options.
Unfortunately, there are no options for CHADEMA or any credible opposition in Tanzania where state tyranny prevails and the citizenry is cowed into total submission. All that you've put forward are NON-OPTIONS:

Kama wananchi wanafurahia serikali yao inavyoenenda na hawakubali au hawako tayari kwa mapambano dhidi ya udikteta uliopo unaodaiwa na CHADEMA, basi waarifu CHADEMA wafunge virago na kutoweka. HAKUNA NAMNA NYINGINE.

CHADEMA ya Dk. Slaa HAIWEZEKANI. Sijui kwa nini watu wanapenda kudanganyana kwenye hili. HII SIO ENZI YA KIKWETE. Siku hizi Polisi na dola wanapiga risasi waandamanaji mchana kweupe na kuua wanasiasa bila kificho. Dk. Slaa ashukuru Mungu kuwa aliachana na upinzani mapema na kufikia bei muafaka na utawala huu. Angekuwa bado huko angekuwa target number one badala ya Lissu. Yaani angeshakuwa R.I.P. na tungekuwa tumeshamsahau kama Ben Saanane alivyosahaulika.

Maandamano ya kudai Tume huru na Katiba mpya? Ni siku wananchi watakapokuwa tayari kujitoa mhanga mbele ya risasi za dola ndipo itakapowezekana kama ilivyokuwa Kenya na kwingineko. Wananchi wasipoona umuhimu huo, hakuna haja ya vitu hivyo.

CHADEMA kuunga mkono maandamano ya Mange? A gift on a golden plate for the State! Leo hii serikali inavyohangaika kutafuta namna ya kubandika sura ya CHADEMA (kama sio ya Mbowe kabisa) kwenye maandamano hayo na kwenye waraka wa KKKT halafu ikute sura hizo zimejibandika zenyewe, sio sherehe hiyo! Itakuwa ni mwendokasi wa mahakamani, jela na vipondo vya uhakika hadi watu wa R.I.P. kwa uhaini!

CHADEMA imuunge mkono Magufuli? Well, that's a sarcastic mode of ridiculing the defeated chaps. Inawezekana kweli ndio wamefikia mwisho wao wa safari. Wanachotaka kufanya hakiwezekani Tanzania. Watanzania ni watu wa amani na utulivu; hawataki shida na serikali yao. Basi, waambie CHADEMA waamue tu kukaa kimya, watulie na kujilia vijisenti vyao kimyakimya kama Kinana na joka la makengeza walivyoamua. Inatosha.
 
Nakunaliana na option ya pili japo nayo ni ngumi vile vile.Kwa serikali hii SIKIVU,tutarajei,vifo,vilema na kila aina ya mateso yatakayowapata CHADEMA na wote watakaounga mkono harakati hizo.Naamini uungwaji mkono katika kudai Katiba mpya na tume huru utakuwa mkubwa na utahusisha hata wasiokuwa vyama.

Nafikiri option ya tatu siyo nzuri kwa CHADEMA,naamini hata hili linalotokea sasa kwa uongozi wa juu wa chama Kikuu cha Upinzani wakati huu linamaksudi ya kuijaza hasira CHADEMA ILI ijihusishe kwenye maandano hao,ili wapate sababu sahihi isiyo na mawaa ya kuifuta CHADEMA.Wasiingie kwenye huo mtego.

ILA CHADEMA wana kila sababu sasa ya kupinga uonevu,unyanyasaji na kila aina ya mateso ambayo wanafanyiwa na serikali hii YA MAENDELEO YASISYO NA CHAMA.WAANDAMANE KWA HAYO.
 
Nitaenda moja kwa moja kwenye msingi wa hoja yangu.

Option ya kwanza: Chadema ya leo inahitaji viongozi watakaokirudisha chama kwenye misingi yake ya zamani, misingi ya ujasiri, misingi ya hoja, misingi ya uanaharakati. Kuirudisha Chadema ya kina Slaa, Chadema ya kina Heche wakisema tukawatoe viongozi mahabusu vijana wanakwenda. Leo viongozi na wanachama wanauawa, wanatekwa, wanapotezwa, sijasikia tamko lolote la nguvu la chama zaidi ya press conference. Utawala huu sio wa press conférence, ni utawala wa kutunishiana misuli ni utawala wa Ukuta.

Option ya pili: Ili kukirudisha chama kwenye mstari, anzisheni harakati za kudai katiba mpya na tume huru ya uchaguzi, ikiwezekana tangazeni maandamano ya amani kama yale ya Ukuta kushinikiza katiba mpya ninaimani taasisi mbalimbali na watanzania wengi watawaunga mkono na chama kitarudi kwenye hadhi yake.

Option ya tatu: Kupitia kamati kuu, chama kiamue kuunga mkono maandamano ya trh 26/4 yaliyoandaliwa na wananchi, kitendo hiki kitaishitua serikali na kuilazimika kuwaita kwa lengo la kukaa pamoja ili kuzungumza na kumaliza tofauti zilizopo. Hii option ina risk kubwa lakini ina faida nyingi na za haraka, the more the risk the more the profit.

Option ya Nne: Najua hii itaonekana kuwa ngumu kidogo lakini nyepesi. Hakika uchaguzi ujao utakuwa mgumu sana kwa Chadema, chama kisipobadili mbinu za ushindi karibu wabunge wote wa Chadema hawatarudi bungeni (fact). Bunge halitakuwa na Msigwa wala Lema wala Mdee wala Mnyika, wala Bulaya. Ili kujiweka salama aidha Chama au wabunge waamue kumuunga mkono Magufuli kama wengine wanavyofanya au wabunge wakae kimya kusubiri mafao yao yawasaidie kuanza maisha mapya ya uraiani baada ya uchaguzi wa 2020.

Ili kubaki salama lazima chama kiamue kuchagua option mojawapo vinginevyo kitaendelea kupukutika na pengine kubaki jina kama vyama vingine.
==========≠=========
Huu hapa chini ni mchango wa mwanaJF mwenzetu, binafsi nimeona kuna kitu cha kujifunza. Kwanini kina Mbowe wateseke kwa Watanzania waliolala wasioonyesha hata kuguswa na juhudi zao?
Quinine......kwangu Mimi naona unania nzuri lakini I guarantee you that you have uttered no option for CHADEMA to go against the current group of leadership and the incumbent symbol...nasikitika hata hao wanaounga jitihada hawajui wanafanya hivyo kwa maslahi hayo mpaka lini.....is it for tomorrow and next year or just for two or three decades????
On my own view nafikiri ni Wananchi wenyewe tu bila agent yeyote waamue kama Sierra Leone, Cameroon, Gambia or Zimbabwe na South Africa....
But numekuelewa na hasa kiu yako...
 
Kwa kweli, ikitokea come back kali ya upinzani, nitanyanyua mikono kuwaheshimu milele.
Maana tuache utani, upinzani una hali ngumu sana.
 
Ukweli ni kwamba tunawalaumu sana wapinzani lakini ukweli utabaki pale kuwa dola inawanyanyasa na sasa Magufuli ameamua kucheza mchezo wa siasa mwenyewe. Hivyo hakuna LA kusema zaidi ya kuamua kati ya kifo au kusalimika. Huyu bwana hajui siasa ya kiustaatabu ya kujibizana hivyo ataendelea kua na mwishoe wengi watarudi nyuma sana.
 
Mkuu, kuna kitu kinaitwa falsafa ya vita ambayo inaongozwa na two schools of thoughts, falsafa ya kwanza ni falsafa ya ushujaa, inayowatumia wapiganaji mashujaa, hawa motoo yao ni "fight, fight, fight", inaamini katika kupambana tuu, Mapambano!, yaani pigana, pigana, pigana, na hata kama unapigwa, "no retreat no surrender", endelea tuu kupigana mpaka mwisho, mpaka risasi ya mwisho na tone la mwisho la damu limwagike, hata mkifa wote na kuwa wiped out, mtakumbukwa kama mashujaa mlioipigania na kuifia nchi yenu, ila mmeshindwa vita na sasa wote ni mateka, wake zenu wanabakwa, na Watoto wenu wanafanywa watumwa!.

Falsafa ya pili ni falsafa ya umakini, inayowatumia wapiganaji makini, hawa hawapeleki jeshi vitani hadi kwanza waijue nguvu ya adui, kwa Imani kuwa "never fight a loosing battle", usipigane vita ambayo unajua hutashinda. Na ukiwa vitani, ukiona dalili za kushindwa vita, ama una surrender ili msiuawawe wote, au una retreat kwa kurudisha nyuma majeshi yako, kwenda kujipanga upya.

Kundi hili la wapiganaji makini, baada ya kujaribu kupigana na kushindana na kushindwa mara kadhaa kwa sababu adui yuko vizuri Zaidi yao, huamua kutumia kanuni inayoitwa, "If you can't beat them, join them". kama huwezi kuwashinda, jiunge nao, jifunze siri zao, jijenge upya na pigana nao kutokea ndani kwao!, yaani " fight from within". Hiki ndicho wanachokifanya baadhi ya wana CCM ambao wanajiunga CCM akiwemo Dr. Slaa. Hili nimelizungumzia hapa.
Tuko Vitani Tuna Wapiganaji Shupavu, Wapiganaji Makini na Watazamaji, Je! Wewe Uko Kundi Gani ?
Katika mazingira ya Tanzania, kati ya Dr. Slaa na MBOWE, ni nani shujaa wa kweli?. Kwa sisi tuliomsikiliza Dr. Slaa akizungumza kutoka moyoni mwake, huwezi amini amejiunga CCM kwa sababu anaipenda au anamuamini Magufuli, bali amejiunga CCM because he has to, its the only way!.
If you can't beat them, join them! He is the worst dictator. Let's pray for him!

P.
Mkuu hiyo falsafa ya umakini ni mbaya sana sababu inabidi ukubaliane na lolote ilimradi tu usife. Kama ni wake zenu au nyie wenyewe kubakwa inabidi ushuhudie na ukubali ili upate mda wa kujijenga upya. Fight till death ni nzuri Lakini angalia pia unapigania nn. Mfano, kufungwa kwa ajili ya watu ambao hawaoni umuhimu wa unachopigania hadi ufungwe hapo ujue haupo vitani Ila Una mihemko tu. Vita Tamu ni Ile vita ambayo mm nauwawa/nafungwa kwa ajili yenu na nyinyi mnapata nguvu ya mapambano Mara kumi zaidi sababu ya yaliyonikuta. Siyo mm nafungwa/kufa nyinyi ndo kwanza mpo nyuma ya keyboard. Wananchi wa aina hii wameridhika hawaitaji kuchochewa.
 
Tema mate chini...kwa sababu hakuna binadamu yoyote mwenye gurantee!, kwa maana hamjui siku wala saa!, Lema sio Mungu na wewe sio Mungu kumpangia Mungu, mambo ya Mungu, mwachie Mungu, unachoweza kufanya ni kumuombea tuu, lakini huwezi kuzuia lolote kama limepangwa!. Mungu huongea na binadamu kupitia ndoto, nyingine za kweli, nyingine za uongo.

Time will tell!.
P.
Mkuu Mungu haongei na binadamu kwa ndoto alafu ikawa ya uongo maana Mungu si binadamu mpaka aseme uongo
 
Ninapoona mabandiko kama hili hapa moyo wangu unanyong'onyea sana naililia Tanzania yangu. Hapa watu wanaongea kana kwamba hii ni vita ya CHADEMA real? Kwamba CHADEMA wafanye hivi, vile au kile? Wewe unayeshauri hayakuhusu? Unafanya nini kwa yanayoendelea kwenye nchi yako? Takwimu zinasema CHADEMA wapo wangapi? Wanafika hata milioni mbili hao wanachama? Yaani kati ya raia milioni 55 wanaotakiwa wafanye vile au hivi ni CHADEMA ambao wapo millioni 2 au tuseme kamati kuu ya CHADEMA maana ndiyo chombo cha maamuzi ya CDM hata arobaini sina hakika kama wanafika?
Ni lazima watanzania mioyo yetu ituume then tufanye kitu kwa ajili ya nchi yetu, lazima tujisikie uchungu kwa nchi yetu na tuubebe huu msalaba wote ili tujitwalie heshima na utu wetu kama wazawa wa nchi hii na raia wazalendo
 
Ninapoona mabandiko kama hili hapa moyo wangu unanyong'onyea sana naililia Tanzania yangu. Hapa watu wanaongea kana kwamba hii ni vita ya CHADEMA real? Kwamba CHADEMA wafanye hivi, vile au kile? Wewe unayeshauri hayakuhusu? Unafanya nini kwa yanayoendelea kwenye nchi yako? Takwimu zinasema CHADEMA wapo wangapi? Wanafika hata milioni mbili hao wanachama? Yaani kati ya raia milioni 55 wanaotakiwa wafanye vile au hivi ni CHADEMA ambao wapo millioni 2 au tuseme kamati kuu ya CHADEMA maana ndiyo chombo cha maamuzi ya CDM hata arobaini sina hakika kama wanafika?
Ni lazima watanzania mioyo yetu ituume then tufanye kitu kwa ajili ya nchi yetu, lazima tujisikie uchungu kwa nchi yetu na tuubebe huu msalaba wote ili tujitwalie heshima na utu wetu kama wazawa wa nchi hii na raia wazalendo
Nimekuelewa, hii vita ni yetu sote ila tambua si wote huenda vitani front, kuna wanaopanga, washauri, financers, nk nk, jambo lolote lazima liwe na chanzo liwe na kiongozi hatuwezi siku moja watanzania wote tukaamuka tuko sehemu moja tunajadili kitu kimoja, ndiyo maana kuna bunge, wabunge wako 300 tu kuwakilisha watanzania mil60 ndio tunaowatuma, sijui ulikuwa unataka hadi niwe ndani ya kamati kuu ya Chadema ndio nitoe ushauri?
 
Kila option ni suicide mission.
Angalau kurudi kwenye siasa za hoja itapunguza madhara mabaya kwa upinzani.

"Siasa za hoja" kivipi wakati serikali hii haitaki kusikia hoja? Ukiwabana sana kwa hoja unaishia kutekwa, kupigwa risasi, na mengineyo. Mifano ipo na sina haja ya kuirudia....
Dawa ya hawa wababe ni kuwachanganyia hoja na vitendo. Kwa mfano, kama UKUTA unaitishwa basi ni kuhakikisha unafanyika kweli, hata kama mapolisi na wanajeshi watatumwa waanze kufanya mazoezi ya vitisho hadharani wiki kadhaa kabla...
Asanteni.
 
"Siasa za hoja" kivipi wakati serikali hii haitaki kusikia hoja? Ukiwabana sana kwa hoja unaishia kutekwa, kupigwa risasi, na mengineyo. Mifano ipo na sina haja ya kuirudia....
Dawa ya hawa wababe ni kuwachanganyia hoja na vitendo. Kwa mfano, kama UKUTA unaitishwa basi ni kuhakikisha unafanyika kweli, hata kama mapolisi na wanajeshi watatumwa waanze kufanya mazoezi ya vitisho hadharani wiki kadhaa kabla...
Asanteni.
Kila la heri.
Mimi siamini ktk siasa za kupoteza maisha ya ya watu.
Mimi ni muumini wa siasa za J.K. Nyerere.
 
Ni option ya 4 tu ndiyo inayoweza kutufanya na sisi wananchi tuone kama tunaweza kuuchagua upinzani.wananchi tunaona wazi jinsi Rais wetu anavyotupigania kwa moyo mmoja na kwa kukemea mabaya.leo hii tunaanza kuona nidhamu ya watendaji wa serikali inarudi,watu walioanza kua miungu watu hapo nyakati za nyuma.leo unaibuka eti upinzani wa kumponda mtu kama huyu kweli?yaani upinzani umesahau miaka kidigo ya nyuma ulisema nini na leo unasema nini.hawajielewi hata kidogo,wananchi tunaona kwa macho yetu na masikio yetu yanasikia pia,kumuunga mkono Rais wala siyo aibu maana juhudi zae tunaziona.badala yake upinzani umekua wa kupinga kila kitu,yaani eti ni kama serikali hii hakuna ilichofanya kwetu,sijui hawa watu wanadhani sisi ni watoto! leo wanaishia aibu ya kupelekwa mahabusu wakidhani ndiyo sifa ya upambanaji kisiasa ili vyombo vya habari viandike habari za kiumbea.badilikeni tutawaelewa

JAH RASTAFARI MORNING AFRICA

Hakuna ukweli katika madai ya kua Upinzani WANAPINGA KILA KITU.

Wananchi wengi wana uwezo mdogo wa kupambanua mambo, ya Siasa, Uchumi, nk. Hii inachangiwa zaidi na Uwezo wa Elimu zao.

Hivyo Kusema kua wananchi wanaona. Sio Kweli.

Wananchi kama wewe na wengine wanahitaji wataalamu wa chambuzi za Siasa, wachumi, wanasheria nk waweze kuwaeleza hali halisia kwa lugha nyepesi ya ki layman

Kwa kawaida, Serikali inawaonyesha kile mnachotakiwa kukiona. Ili iweze kua Imara katika shughuli zake za kuwanyonya.

Tundu lisu aliporipoti kuhusu kukamatwa kwa Bombadier ilimgharimu, kwasababu alitaarifu kile ambacho wananchi hawakupaswa kufahamu kuhusu Serikali yao.

THE GREAT MASSES OF THE PEOPLE WILL MORE EASILY FALL VICTIMS TO A BIG LIE THAN A SMALL ONE. - By Adolph Hitler.
 
Chama credible?, ccm ni nini Mkuu hadi iwe imara kiasi hicho. Siasa si mchezo tu ambao waweza badilika. Tupe siri
 
Mkuu Mungu haongei na binadamu kwa ndoto alafu ikawa ya uongo maana Mungu si binadamu mpaka aseme uongo
Ni kweli Mungu hawezi kuongea uongo, tatizo ni shetani naye kila siku anapenda kuji pretend ndie Mungu, na ana pose kama Mungu, hivyo wengi wanamwabudu shetani bila kujijua kuwa ni shetani, wao wanaabudi, wakiamini wamamwabudu Mungu, hivyo ndoto nyingine, sio ndoto za Mungu ni za shetani.

P.
 
Ni kweli Mungu hawezi kuongea uongo, tatizo ni shetani naye kila siku anapenda kuji pretend ndie Mungu, na ana pose kama Mungu, hivyo wengi wanamwabudu shetani bila kujijua kuwa ni shetani, wao wanaabudi, wakiamini wamamwabudu Mungu, hivyo ndoto nyingine, sio ndoto za Mungu ni za shetani.

P.
Jiran yngu wa zamani naomba unijibu kwa utulivu sna swali langu ndugu yngu unaweza kupitia historia za nchi nyingine pia niambie ukweli unaona kuna uwezekano kweli mbunge yyote wa upinzani kurudi bungeni mwaka 2021 kwa aina ya siasa yetu hii tulio nayo kuwa mkweli na muwazi km taifa tunaelekea wapi...
 
Jiran yngu wa zamani naomba unijibu kwa utulivu sna swali langu ndugu yngu unaweza kupitia historia za nchi nyingine pia niambie ukweli unaona kuna uwezekano kweli mbunge yyote wa upinzani kurudi bungeni mwaka 2021 kwa aina ya siasa yetu hii tulio nayo kuwa mkweli na muwazi km taifa tunaelekea wapi...
Kwa hali ilivyo sasa, na kata hali hii itaendelea hivi, kwa huku bara, mbunge wa upinzani, ikitokea akarudi bungeni, then ni mmoja tuu, ZZK.

Hili nimelizungumza hapa
Trend Reading: Wanaohamia CCM wasibezwe! Wanaona mbali, 2020 Majimbo yote kurejeshwa. Je tunarejea nchi ya Chama kimoja?
Swali la Ukweli Mchungu: Je, 2020 Magufuli ana mpinzani au mshindani, au Ni Magufuli tu?!.
Kwa Kasi hii ya Magufuli, kuna haja Kufanya Uchaguzi wa Rais 2020?
In 2015 Election, Tanzania had A Choice To Choose From. Jee Kwa 2020, Do We Still Have A Choice?.
Je, CHADEMA inaweza kushinda 2020? Is it serious, credible & mature enough opposition?!.
P
 
Nikweli 2020 wabunge wengi wa Chadema wanaweza wasirudi kama hali itaendelea kuwa hivi,pia nina wasiwasi na voters turn out itakuwa ndogo sana cos waTZ wengi wamekata tamaa,wamechoka,hawajui kesho yao,ajira hakuna,biashara ngumu.So upinzani lazima watafute mbinu mbadala ya kubaki salama.Wakitegemea hizi siasa za kiharakati kama alizowakataza mzee Lowassa watapotea zaid
 
Kifupi 2020 itakuwa na wapiga kura wachache sana , I bEt for whole tz milioni mbili hawatafika
 
Tema mate chini...kwa sababu hakuna binadamu yoyote mwenye gurantee!, kwa maana hamjui siku wala saa!, Lema sio Mungu na wewe sio Mungu kumpangia Mungu, mambo ya Mungu, mwachie Mungu, unachoweza kufanya ni kumuombea tuu, lakini huwezi kuzuia lolote kama limepangwa!. Mungu huongea na binadamu kupitia ndoto, nyingine za kweli, nyingine za uongo.

Time will tell!.
P.
Nimuombee Nani, Faru?!. Aisee[emoji23] [emoji23]
 
Back
Top Bottom