Siku za hivi karibuni kumejitokeza wimbi la wabunge wa cdm kufanya mikutano ya hadhara sehemu nyingi za nchi, nakubaliana na ukweli ya kwamba cdm imepata umaarufa hasa baada ya uchaguzi wa mwaka 2010.
Ninachoaasi viongozi cdm na wafuasi wao ni kwamba binadamu yoyote ana hulka ya kukosa hamasa na kitu chochote hasa baada ya kuwa na mazoe na kitu husika, rai yangu ni kwamba hii mikutano ya hadhara mnayofanya imeanza kuwachosha wananchi na sitashangazwa na cdm kukosa kabisa wasikilizaji ama wahudhuriaji wa mikutano yao 2015.
Ninavyoamini mimi ni kwamba kuna baadhi ya sehemu za nchi hii CHADEMA hawajawahi kufanya mikutano au kama wamefanya basi ni mara chache sana tena wakati wa uchaguzi tu. Wanachotakiwa sasa hivi ni kuweka msisitizo maeneo kama hayo ambayo chama bado hakijajulikana sana badala ya kuwaambia waache kabisa. Kumbuka chama kama CCM kilikuwepo tangu 1977 lakini bado kinafanya mikutano kila kukicha kupitia makada wao sasa iweje kwa vyama vya upinzani vilivyoanza 1992