CHADEMA, mchukueni HAMADI RASHID

CHADEMA, mchukueni HAMADI RASHID

Kwa hadhi yake ni kujimaliza kwenda kwenye chama cha ukanda badala ya chama cha kitaifa.Mna wasiwasi gani cdm mbona mne safari
 
CHADEMA kinajengwa kwa kujenga sera zake,kuelimisha watz na kuwafanya watz kuona chama ni mali yao.Chadema hakihitaji watu wanaotoka ktk vyama vyao kwa vurugu ili kujijenga.Chadema ni zaidi ya viongozi,wao wanapewa jukumu kla kuongoza wala si kwamba chama ni mali yao.Hamad Rashid hatumuhitaji ili kujijenga Zanzibar,kwa chadema ni busara kuwaacha wazanzibar kuwapa fursa ya kuelewa sera za chama na itikadi za chadema na wao kuchagua kujiunga kwa ridhaa yao na si kwa kulazimishwa na Mtu,maana akiondoka ataondoka nao.

So chama hakijengwi kwa majina ya watu bali kwa uzalendo wa wanachama.Nadhani hoja hii inakosa uzito wa kimjadala kwa manufaa ya chama na Tanzania tuitakayo!

Great!!! hayo ndo maneno watu waelewe msingi wa Chadema si kutafuta viongozi au wanachama waliokufa / achwa nd io wajiunge la hasha .Inapendeza mtu avutike mwenyewe na sera za chama
 
Great!!! hayo ndo maneno watu waelewe msingi wa Chadema si kutafuta viongozi au wanachama waliokufa / achwa nd io wajiunge la hasha .Inapendeza mtu avutike mwenyewe na sera za chama
Chama hakiwezi kuwa na maisha marefu kama kinategemea majina ya watu,lazima chama kiwe mstari wa mbele kuandaa viongozi wanaokipa chama nafasi ya kukubalika na si chama kuegemea kwenye umaarufu wa watu.Ni kweli chama hutegemea wanachama na viongozi wao kujenga sera na kuzinadi kwa wanchi lakini lazima chama kiheshimike kama taasisi na kijulikane hivyo.Jina lazima liwe chadema then muhusika ndo afuate.Lkn hatumuhitaji Hamad rashid Ili kujijenga Zanzibar,Bali watz wa Zanzibar wakikubalina na sera na itikadi za chama hakuna wa kuwaforce kujiunga.
 
hamaad amekuwa against na cdm toka siku nyingi aliunda kambi ya upinzani bila kushirikisha cdm na hakuwa na sababu za msingi pengine ni mtu wa kutumika
 
Tumchukue tumpeleke wapi huyo mtu jamani? Kumchukua huyo ni sawa na kujitwika gunia la misumari
 
Majanikv Nakuunga mkono mdogo wangu,ndugu yangu.

Mimi niseme kitu kimoja, suala la zanzibar waachieni wazanzibari wenyewe, cuf ina nguvu kubwa kulete mageuzi na kuindoa ccm madarakani, na vijana tunao waunga uwamsho,lakini kuna kitu kimoja ambacho ndicho kinachotuuumiza wazanzibar,sisi tuko wachache, wakati wa uchaguzi serikali ya muungano hutumia nguvu kubwa kuhakikisha ccm inakuwepo madarakani,iwe kwa kuwauwa wazanzibari au kuwavunja vunja viungo,au kwa mabomu ya machozi,na haya wanawafanyia wazanzibari tu kwa vile ni wachache na wanaweza kutudhibiti.

Lakini hawafahamu kuwa wazanzibari hatujawa tayari kufanya mapinduzi lakini na uchache wetu tukiamua,tutapiga mambomu wote wanafiki na office yote ile ya kisiwandui,najua tutakufa wengi sana mpaka kuitoa ccm,lakini iko siku tutakifika.

Upande wa bara tunaaamini wazanzibari ccm 2015 itakuwa mpinzani na chadema itachukua, na bara nyinyi vijana muko wengi kabisa, sisi tunawetegemea nyinyi muipindue ccm,kwa kwa uchaguzi pili kwa nguvu za umma,mana ccm haitatoka madarakani kama munavyofikiria nyinyi.

Pili serikali tanganyika huko kwenu wanaogopa nguvu za umma kwa sababu wananchi ni wengi zaidi ya hilo jesho la police,na pale moto chedema watakapo uwasha ccm hawataweza kuuzima abadani na itaondoka madarakani,kwa nguvu zenu,tuangalie misri na libya ? Umoja ni nguvu, cha msingi kama ni lengo kuiyondoa ccm madarakani basi sio lazima chedema kuwepo zanzibar cha msingi tuangalie jee wako ambao wanao unga mkono hoja ya kuiondoa ccm ? tupoo.

Wazanzibari tunaamini kuwa kuiyondoa ccm zanzibar ni muungano,ukivunjika ccm bye bye, na huko bara pia ccm itakuwa haina nguvu tena.,uaminimusiamini zanzibar hakuna tena ccm,tuna wahuni tu,ccm haina mvuto tena,pemba ishasahauliwa ccm, badu unguja sasa,ndio ambao kumepamba moto, hata ikifika 2015 ccm tushaizika na muungano.

Mungu ibariki Tanganyika na watu wake, NA Zanzibar na watu wake.

Zanzibar kwanza
 
Last edited by a moderator:
Huyu mtu alimkashifu sana Kamanda wetu mpendwa LISSU, Bungeni wakati wa mjadala wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba wakati CDM walipotoka nje ya Bunge kwamba ni LISSU ni Mwanasheria Bandia na kwamba asikanyage Zanzibar. Jamani, mmeshasahau?
 
Mtoa hoja ametoa maoni kwa mtazamo wake.Yanaweza kukubaliwa ama kukataliwa.Binafsi ninamashaka na wazo hilo.Hamad Rashid hana mahaba na CDM.Kama ataombwa wakati yeye hakuwa na wazo hilo,akikubali atajiunga CDM kwa maslahi ya tumbo lake tu.Mifano ipo mingi, kisiasa, Shibuda ni mfano mzuri kimwili CDM kimoyo CCM. Katika soka, Ngassa yupo Simba kimwili,kimoyo anafurahia ushindi wa Yanga.Tafakari na chukua hatua.
 
Majanikv Mkuu cdm imeanzishwa mwaka gani na hadi sasa imeshindwa kupenya vilivyo kule zanzibar.Wakati mwingine tuangalie hasara iliyo ndogo.

Na CUF imeanza mwaka gani na imepenya kiasi gani bara?
 
Last edited by a moderator:
Haina haja ya kumuomba mtu ajiunge na chama atawasumbua sana yeye mwenyewe aridhike na sera za chama aingie mwenyewe kwa kuomba na sio kumwita.
 
Majanikv Mkuu cdm imeanzishwa mwaka gani na hadi sasa imeshindwa kupenya vilivyo kule zanzibar.Wakati mwingine tuangalie hasara iliyo ndogo.

Zanzibar haina umuhimu sana kisiasa kwa maana mbili kwanza ina wapiga kura wachache sana pamoja na kuwa na majimbo mengi sana ya uchaguzi lakini pia sooner than later muungano au utavunjika au utakuwa na sura tofauti hivo kuwekeza sana kisiasa zanzibar ni kupoteza muda!
 
hatuna haja naye naye asiwe haja na sie, wabaki huko huko, mbona vijana wasomi wengi tu huko.
 
Kwa mtizamo wangu hamad rashid ana faida zaidi kwa chadema kuliko hasara, ni mtu anayeziweza siasa za kibongo na ana ushawishi mzuri kwa watu, tatizo letu wabongo ni kutoaminiana utadhani tumerogwa hivi, nna uhakika ccm wanaomba hamad asiende chadema kwa sababu kwao hili linaweza kuwa tishio jingine 2015, na hasa kama atasimama kama mgombea mwenza..hebu imagine Slaa yupo mwanza hamad anapiga tanga, hamad mtwara slaa mby, ccm lazima wakae!!
 
Wakati umefika wa CDM kutafuta namna ya kujiimarisha kule Zanzibar,kwangu mimi Hamad Rashid atakuwa ni kete nzuri sana kwa cdm katika kukijenga chama kule Zanzibar, hivyo nashauri cdm tumchukue huyu jamaa,maana sijaona dhambi kubwa aliyofanya.Critical /Great thinkers watatoa maoni ya kujenga na si matusi.
Wana jf mnasemaje?

Kama kumbukumbu yangu bado iko vizuri Hamad Rashid amewahi kukaririwa mara kadhaa na vyombo vya habari kwamba yeye si mtu wa kuhama hama vyama, na kwamba kama atafukuzwa na chama cha cuf hawezi kuhamia chama kingine chochote zaidi ya kuanzisha chama chake kipya.

Na kwakuwa anasemekana kuwa mlezi wa chama cha ADC ambacho anahusishwa katika kukianzisha hiyo ni dhahiri kwamba ametimiza azma yake ya kuanzisha chama chake na si kuhama hama kama alivyokwisha sema.

Muhimu ni viongozi wetu kuendelea kujipanga tu, ili kama yeye mwenyewe HR anavutiwa ama kushawishika basi ajiunge kwa hiari yake badala ya kutaka aombwe.
 
Back
Top Bottom