Uchaguzi 2020 Hata CHADEMA wasiposhirikiana na ACT-Wazalendo, bado CCM itapigwa chini. Membe na Lissu “watakula vichwa vingi” vya wanachama wa CCM

jmushi1

Platinum Member
Nov 2, 2007
24,989
22,521
Wanajamvi,

Kama heading ya uzi huu inavyojieleza, ni kwamba hakuna haja ya upinzani ku panic kabisa! Hayo ni ya wana ccm kuyafanya, na kamwe siyo upinzani. Wao ccm, kwani wamezuiwa kufanya siasa? Wamekuwa wakifanya kampeni toka awamu hii iingie madarakani. Wakati vyama vingine vikizuiwa kufanya hata vikao vya ndani! Sasahivi, wananchi kama ni kuona na kusikia, basi wameshasikia na kuona vya kutosha kupitia kwa wakuu wa mikoa, wilaya, wakurugenzi, mameneja wa miradi, makatibu uenezi na katibu mkuu wa ccm, ndo wamekuwa wakitamba siyo tu kwenye vyombo vya habari vya binafsi ambavyo viliingiwa na hofu na woga, haswa baada ya tukio ka clouds media pale studio walipovamiwa na kikosi kazi maalum na kunaswa kwenye camera live! Lakini hata Tv yetu ya Taifa TBC, ambayo inaendeshwa kwa kodi zetu wote bila kujali vyama vyetu, wala itikadi zetu, imekuwa ni kama chombo cha propaganda cha ccm. Kwahiyo wao ccm ndo wanaotakiwa kupanic maana wanarudia yale yale ambayo wananchi wamelazimika baada ya kulazimishwa, wameshayaona na kuyasikia kwa miaka minne mfululizo!

Ni wazi sauti nyingine zikija na kumwaga sera zao na kuonyesha madhaifu yaliyopo kwa utawala huu wa ccm, basi watakuwa na shauku kubwa ya kuwasikia bila chembe ya shaka! Hiyo ni kawaida kwa hulka ya mwanadamu. Ni kiumbe mwenye kutafuta habari kila uchao! It is a human psychology. Tunataka tusikie pande zote, kisha tuchague!

Sasa nimeona watu wanasumbuka sana kuhusiana na suala la nani atakuwa mgombea kwa upande wa upinzani. Vyama vya ACT-Wazalendo, pamoja na kile chama kikuu cha upinzani nchini, yani CHADEMA vikizungumziwa na kuhusishwa na wagombea wawili maarufu sana, yani Tundu Antipas Lissu, sambamba na Bernard Membe, ambaye inasemekana yumo ACT-Wazalendo.

yangu rahisi ya ki “layman”, inaonyesha wazi kabisa kuwa ACT-Wazalendo, ni chama mbadala cha CUF. Na ndiyo kinategemewa kumsimamisha mgombea kule Zanzibar. Na kama sikosei, mgombea huyo ni Maalim Seif Sharif Hamad. Kwahiyo kwa upande huo wa kushirikiana inapokuja kwa upande wa Zanzibar, ni suala la kawaida tu na ni utamaduni ulio kuwepo wa kushirikiana. Na ndiyo maana halitabadilika, kwasababu ACT-Wazalendo wameisha wafuta CUF.

Na kwa upande wa bara, mambo yalikuwa ni kati ya Lipumba, na mgombea wa CHADEMA, ambapo CHADEMA walikuwa ndo wanaotoa mgombea wa urais kwa upande wa bara. Last time Lowassa, kabla ya hapo Slaa nk.

Lakini tofauti iliyoko kwa sasa, ni Bernard Kamilius Membe. Huyu yeye ndiye anayeleta mjadala mkali. Ni mjadala ambao unachochewa sana na wana ccm wenyewe! Nadhani kisaikolojia, ni umbea kwasababu yao wenyewe, yamewashinda! Wanatafuta wa kujifananisha nao nje ya chama, na wakati wenzao bado wako kwenye utaratibu wa kupata wagombea urais. Lakini kwasababu ccm wao wameshamaliza upande wao, na watu kunyimwa hata nafasi ya kuchukuwa fomu za kugombea kwenye nafasi ya urais, yani fomu zikafichwa na katibu mkuu akasema wazi kabisa kuwa hawatatoa fomu kwa mtia nia mwingine yoyote yule zaidi ya mwenyekiti aliyeko! Na ndiyo matokeo yake Bernard Membe kujitoa. Huyu tayari ana watu wengi tu ndani ya ccm wanaoona ameonewa na ccm. Jambo lilokuwa ni kinyume hata na katiba yao ya chama. Pia woga unaonyesha udhaifu mkubwa! Hata JK mwenyewe tuliyemuita “dhaifu”, yeye alikubali kina Shibuda wakajitosa na kuchukuwa fomu! Woga wa sasa, unaonyesha kutokukubalika ndani ya chama!

Kwa maoni yangu, hata kama vyama hivi vikiamuwa kuwasimamisha wagombea wao, bado idadi ya kura watakazozipata, zitawazidi ccm. Huu ni ukweli mchungu kwa ccm na ndiyo maana wanahaha sana kuleta mijadala ya kuwachanganya na kutaka kuleta migawanyiko! Lakini hili halitafanya kazi wala kufanikiwa, maana siku ya kufa nyani, miti yote huteleza! Kwanza kuna kura nyingi sana za wana ccm ambao hawakuona umuhimu wa Lissu kutaka kuuwawa! Kura za huruma, ama “sympathy”, na sisi waafrika, siyo tu kwamba tuna sifa hizo, bali pia wengi wana sifa ya “empathy”, ambapo ni “uwezo wa kujiweka kwenye nafasi ya mtu mwingine”.

Na hata matendo ya serikali na bunge kupitia kwa spika Ndugai, yameonyesha wazi kabisa, wananchi wanajuwa kwasababu kwa miaka hiyo minne, wamekuwa wakilishwa propaganda za upande mmoja!, na sasa mahakama nayo inaweza kutupiwa macho pamoja na polisi. Bunge lilishafanya kazi yake kwa wale “wasumbufu”, mara baada ya kusitishwa kurushwa mubashara! Na kweli wengi wameshighulikiwa nje ya bunge! Wengine kutishwa na wengine inasemekana “kununuliwa”

Kule Kenya, hili liliwahi kutokea pia, na ndipo hapo chama cha KANU kilipoanguka chali! Kama sikosei, mara ya pili, ilibidi upinzani wafanye muungano, kwasababu mara ya kwanza, kura zao zote, ziliwashinda KANU, lakini wao walikuwa hawajaungana, na hivyo KANU kubakia madarakani. Sisi hapo tunaweza kurekebisha.

Kwa upande wa Tanzania, siasa zetu ni za tofauti kidogo na zile za Taifa la Kenya. Sisi kwanza siasa za ukabila siyo kivile hata kidogo! Pamoja na kwamba ccm wamejitahidi sana kuzitumia dhidi ya upinzani, Lakini hazijafanikiwa, na ndiyo maana upinzani ulipata nguvu na kuongeza wabunge wengi, pamoja na madiwani!, na umaarufu mkubwa, sana hadi ccm kutishika! Na hata wengine wakisema uchaguzi uliopita, kama siyo kwa “goli la mkono”, ambalo Nape, January pamoja na Kinana, walifanya kazi ya ziada, basi leo hii ccm ingekuwa ndo upinzani.

Sasa miaka mitano ndo hiyo imeshakata, Kinana ni juzi tu kaomba msamaha, ni baada ya Nape na January kufanya hivyo! Lakini nao walifanya kwa shingo upande tu. Kwasababu, nguvu za mwenyekiti ni kubwa mnoo, na pia mara baada ya kuingia, alifanya mabadiliko ambayo wengi waliyaona ni kama dalili za kuji “dhatiti” zaidi ndani ya chama! Na ukizingatia yeye ndo mkuu wa serikali, wengi wanasikilizia kupata nafasi, huku wengine wa “jalalani”, nao wakipiga jaramba! Lakini pia, ni wazi kuwa hao kina Nape na January, wamekulia humo ccm, hivyo hawana ujanja, siasa ndo maisha yao! Na hivyo wamekuwa kama “mateka” wa kifikra na hata kimwili! Wakitoka ccm, wanajuwa hawana lao tena! Kwasababu wanafahamu raha za kubakia humo! Wanafahamu kwa mfumo uliopo, mathalan tume ya uchaguzi, ni vigumu kuwatoa ccm madarakani! Hao nao sura zao halisi zingeonekana kama wengine wangeruhusiwa kuchukuwa fomu ya kugombea urais ndani ya ccm. Hata mzee Makamba naye ni hivyo hivyo tu, wengi tulimsikia kwenye zile tape walizodukuliwa wakati wakimsema mwenyekiti wao! Mzee Mkapa yeye hata kama alidukuliwa, hawakutuhubutu kuweka wazi kama hao wengine, lakini naye alizungumzia umuhimu wa kuwa na tume huru ya uchaguzi nchini! Hilo tu, linaonyesha wazi kabisa kuwa wenye busara, wanatambuwa hitaji kuu la wananchi na Taifa kwa sasa! Siyo kauli ya bahati mbaya tu.

Kura za ccm ndizo zitakazogawanywa, cha msingi, kuwepo na makubaliano baina ya wapinzani mapema iwezekanavyo! Ninayo imani kwamba, uchaguzi huu, kama haki na ushauri na maoni yakizingatiwa, walau kwa kuanzia na mabadiliko kwenye uchaguzi, kuelekea kwenye katiba mpya na tume huru, basi utatuletea viongozi wanaowakilisha kada zote za wananchi pamoja na masilahi yao! Yale ya moja kwa moja kwenye jamii, na pia yale ya watanzania wote kwa ujumla! Hili amelizungumzia vyema sana Sheick Ponda kwenye ule waraka wa “Shura ya Maimamu”, ambapo walizungumzia kuhusu upatikanaji wa katiba mpya baada ya uchaguzi mkuu! Lakini pia umuhimu wa kuweka kanuni za kipindi cha mpito, ili tupate serikali itakayotuongoza kuelekea kwenye katiba mpya ya wananchi kutoka kwa wananchi.

Hapa ina maana kwamba kuna mengi yanayowaunganisha watanzania dhidi ya ccm kuliko yale yanayowatenganisha! Hayo ya kututenganisha, ni machache sana ambayo siyo lazima kupewa kipaumbele! Maana yenyewe ni ya kuwagawanya wapinzani ili kuwadhibiti! Kuwagawanya watanzania, ili kuwaondolea sauti na umoja wa kudai haki, uhuru na maendeleo ya nchi! Yani “devide and rule”. Kwetu ni tofauti kabisa na kule Kenya ambapo siasa za ukabila ndizo zinawaumbuwa na zimekuwa zikifanya hivyo kwa muda mrefu.

“Coalitions”, ama miungano yao, ni ya misingi ya kikabila. Mfano Kaleinjin na Wakikuyu, Vs Waluo na makabila mengine madogo nk. Na Kwahiyo sisi tuna nafasi nzuri zaidi kwa wapinzani kuiangusha ccm, na bado tukapata serikali iliyopatikana kutokana na ridhaa ya wananchi...serikali itakayowatumikia wananchi vyema, na kwa mujibu wa katiba ya nchi! Na hao wakifanya uzembe, tuwe na nafasi na uwezo wa kuwandoa madarakani kwa kupitia sanduku la kura kwa mujibu wa katiba.

Siyo siri, chama cha CUF, kilikuwa na wanachama wengi wa maeneo ya mwambao wa Pwani! Na hivyo wengi kuwa waislam. Majimbo mengi ya waislam, ni hao CUF waliyabeba, lakini mengine machache, ccm wamekuwa wakitumia ujinga na umasikini kuendelea ku watawala. Mifano mingi ipo hai! Ni tofauti na baadhi ya sehemu na mikoa ambako wameshaifuta kabisa ccm kwenye misamiati yao. Hata hivyo, kama nilivyosema hapo awali, ACT-Wazalendo ndiyo ambao sasa wameichukuwa nafasi hiyo ya chama cha CUF. “CUF has simply been replaced”, haswa baada ya Maalim Seif kuondoka huko, na Zitto kuitumia nafasi hiyo kumsajili.

Sasa endapo ACT-Wazalendo watamsimamisha Membe, nadhani siyo mbaya hata kidogo kwa upande wa CHADEMA na upinzani kwa ujumla!Kwanza kuna malalamiko mengi sana ya uwepo wa udini. Malalamiko ambayo yanaelekezwa kwa utawa wa ccm! Na wala siyo mara ya kwanza! Na ndiyo maana hata CUF ilipata nguvu sana! Malalamiko yao hayajaanza leo chini ya utawala wa ccm! Hawa watu sauti zao lazima zitakuwa zinataka mwakilishi. Hata waislam wale ambao walikuwa hawaipigii CUF kura, na wakawa wanaipigia ccm, basi sasa wataipigia kura ACT-Wazalendo.

Hata wale ccm wasioipenda CHADEMA baada ya kulishwa sumu mbaya na chama chao, wataipigia kura ACT-Wazalendo kumfuata Membe...Maana tunafahamu propaganda za ccm inapokuja kwenye udini na ukabila! Na kujidai kwamba wao siyo mafisadi! Tuhuma zao wenyewe, lakini wamekuwa wakiwasingizia upinzani. Sasa ccm mmetawala toka uhuru, upinzani ndo umeleta shida za waislam toka lini? Ufisadi umeanza wapi? Kauli ya “kujivua gamba”, ilikuwaje? Hili huwa najiuliza sana wakati ccm inapokuja na mgombea wao huku wakitutajia maendeleo waliyoyaleta, na kujifananisha na upinzani ambao hawajawahi kuongoza nchi. Mbona hawakubaliani na ukweli pia hata umasikini na unyonge ni wao waliowasababishia watanzania? Hili lenyewe, lilitakiwa liwe kama nguzo ya sababu nzuri kabisa ya kuwa na uchaguzi huru tuone kama hawajaondolewa madarajani! Maana nani mwingine ambaye ameshafanya “mazuri” zaidi yao tokea December 31st 1961? Nani mwingine ameshawahi kufanya “mabaya” zaidi ya ccm kwenye taifa letu?

Hivyo kwa maoni yangu, ni kweli kabisa kuwa uchaguzi wa huru na haki, utawaondoa ccm madarakani, upinzani uungane, ama usiungane, moto ni ule ule! Membe atakula vichwa vya wana ccm, chadema nao watakula vichwa vya wana ccm. Hata yule Sipunda anaweza kula vichwa!

Cha msingi, ni makubaliano yafanyike mapema! Makubaliano ambayo yatahusisha nia ya dhati kabisa ya pande zote mbili! Nia za kuwa na tume huru ya uchaguzi pamoja na katiba mpya ya wananchi kutoka kwa wananchi! Na siyo hii ya mkoloni yenye viraka vya ccm, ambayo inaendelea kutushikia chini kiasi cha kwamba uhuru wetu ukawa mashakani! Waliotufanya wanyonge, ndo hao hao wanaoendelea kuutetea unyonge wetu ili tubakie nao eti na kuendelea kuwachaguwa na kukatazwa kuhoji lolote kuhusu raslimali zao! Unyonge wa watanzania ndiyo sababu kubwa ya wao ccm kuendelea kuwepo madarakani pamoja na umasikini wetu.

Sababu ziko nyingi sana, ila nimeamuwa kuanzia na hizi!

cc Nguruvi3
****Maoni ya Nguruvi3

“Mkuu nilikaa kimya kuhusu haya mambo, naona umeamua 'kunichokoza''
Mkuu, kwanza, sina taarifa za Joka na ni muda sasa sijamuona jamvini, natumai yu bukheri aliko.

Pili, nianze na Zanzibar. Kama kuna fyongo iliyochezwa na CCM ni hii ya Hussein. Huyu bwana hakubaliki na kwamba aligombea ''nyumbani'' mkurunga kunamuondolea sifa ya ''uzanzibar'' hata kwa wana CCM a.k.a mapinduzi daima

Hii ilikuwa fursa ya Shamsa Vuai, lakini kamati maalumu Znz ilichezewa akili kwa kuaminishwa ni Mbarawa.
Hussein akaiangizwa katika kundi la Shamsi, Khalidi akisindikiza bila kujua huku bara ilikuwa Bw Hussein.

Kura za CCM 35 kutoka Znz zilikwenda kwa machaguo yao, huku mwana mpendwa akikomba 129 za Bara

Hili limepeleka ganzi visiwani, kwamba, CCM hawana uthubutu wa kunyanyua nyuso, wameuza ''ghala la silaha''. Zanzibar hakuna raha kwa CCM.

Wale wa Maalimu Seif alipo wapo, wakipata CCM kidogo tu hata mbinu ya kupunguza majimbo haifanyi kazi

Tegemeo la CCM Zanzibar ni moja , kupitia sera za 'Jecharism'' .
Tatizo la sera hiyo ni moja, umma ukiamua basi maji yatazidi unga kama si tui kuingia maji.
Shah wa Iran na Nicole Ceuasescu wa Romani wanatambua somo la nguvu ya umma vizuri.

Kuhusu Bara, kuna tatizo kubwa sana. Baada ya Lowassa na Sumaye wengi wanawaangalia wahamiaji kwa jicho la shaka sana.

Ni kwa msingi huo Chadema hawafikirii kurudia makosa yaliyowagharimu muda mwingi sana.
Mwaka 2015 CDM walitumia muda mwingi kwa mtu, kitu ambacho kingewapa wabunge wengi.

Kwa upande wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe amekomaa na nia yake si uongozi kama yeye bali uongozi wa kuiondoa CCM kwanza. Mtazamo huu umemfanya awe 'muumini' mzuri wa ushirika kwa Wapinzani.

Zitto amegundua tatizo si yeye kuwa kiongozi bali yeye na wenzake kuongoza kuiondoa CCM.
Hii ni ''maturity'' nzuri sana na nampa big up

Pamoja na hayo, kumpokea Membe kuna maswali kama yale tuliyouliza wakati wa Lowassa.
Je, uwekezaji kwa Membe kuna manufaa? Je, kwanini ajiunge dakika za mwisho?
Lengo ni kugombea au kuamini katika demokrasia?

Je, akiwa Kachero anaweza kuleta mabadiliko gani tofauti na yale ya Waziri mkuu Lowassa?
Membe ana dhima ya kuwahahikishia Wapinzani, ana kitu tofauti vinginevyo itakuwa hadithi ile ile.

Kwa upande mwingine najiuliza sana, nini mkakati wa Wapinzani? Suala hapa si kushinda, wana uwezo huo.

Tatizo ni mfumo uliosukwa ambao sasa unahusisha vyombo vingi. Chaguzi zote za marudio zinathibitisha

Hivi Mkurugenzi anakimbia vipi ofisini kupokea fomu na hakuna kinachotokea kwa kosa hilo?

Hivi hatuoni Polisi wakikamata Wapinzani wakati CCM wakisaidiwa na Magereza kupandisha bendera.

Msajili yupo kimya kama vile ofisi yake ipo likizo, huku tume ya uchaguzi na nakala za matokeo ikifanya yake.

Wengi wanadhani Takukuru kuwakamata CCM ni kupambana na rushwa.

Siku kibao kitakapogeuka Wapinzani ''watakamatwa siku moja kabla ya kurudisha fomu''.

Wakurugenzi wataugua masaa machache kabla ya kurudisha fomu.

Mwaka huu CCM itashinda majimbo zaidi ya 50 bila kupingwa kwa namna. Haya hayajulikani?

Kukokesekana kwa tume huru na kushindwa kuidai ni kosa kubwa sana kwa wapinzani

Uchaguzi wa Afrika hauamuliwi na namba bali namna, na ni kwa wale tu wanaoweza kama Malawi , matokeo mengine hayatakuwa tofauti na zama zile”- Nguruvi3
 
Nyie jamaa ni watu wazima Ila ni WAPUMBAVU, kwa tume hii ya uchaguzi itakayojazwa TISS na wajeda tupu vituoni mnaamini mtaiondoa CCM madarakani!?, humu JF upande wa upinzani kuna jamaa anaitwa tindo ndo huwa anaongea uhalisia wengine mmegeuka wajinga kutokana na ushabiki.

Kuna jamaa alikuwa anadai mgombea wa uraisi kupitia CCM ni Membe ni suala la muda tu., Ni mtu mzima na aliamini hivyo, ni type ya watu ninaowaitaga malofa humu.
 
Nyie jamaa ni watu wazima Ila ni WAPUMBAVU, kwa tume hii ya uchaguzi itakayojazwa TISS na wajeda tupu vituoni mnaamini mtaiondoa CCM madarakani!?, humu JF upande wa upinzani kuna jamaa anaitwa tindo ndo huwa anaongea uhalisia wengine mmegeuka wajinga kutokana na ushabiki. Kuna jamaa alikuwa anadai mgombea wa uraisi kupitia CCM ni Membe ni suala la muda tu., Ni mtu mzima na aliamini hivyo, ni type ya watu ninaowaitaga malofa humu.
Kama wewe siyo mpumbavu, niambie ni kwanini Sheick Ponda mumemkamata? Kama unatumia muda wako kusoma na kuelewa zaidi ya upumbavu, je umeusoma waraka ule?

Yani wewe ni mpumbavu nambari wani kabisa!

Ni sawa na kusema “kwasababu kuna majambazi kila mahali, basi watu wasilinde vyao na kujilinda!

Yani unataka nisizungumzie ccm kushindwa kwenye sanduku la kura, kwasababu ya wanajeshi na usalama wa Taifa! Sasa hata nikikuita mpumbavu siyo halali.
 
Kama wewe siyo mpumbavu, niambie ni kwanini Sheick Ponda mumemkamata? Kama unatumia muda wako kusoma na kuelewa zaidi ya upumbavu, je umeusoma waraka ule?

Yani wewe ni mpumbavu nambari wani kabisa!

Ni sawa na kusema “kwasababu kuna majambazi kila mahali, basi watu wasilinde vyao na kujilinda!

Yani unataka nisizungumzie ccm kushindwa kwenye sanduku la kura, kwasababu ya wanajeshi na usalama wa Taifa! Sasa hata nikikuita mpumbavu siyo halali.
Umemjibu vema...japo kasema ukweli ila kashindwa kuongea kistaarabu
 
CCM itapata pigo kuuuuubwa sana pigo moja tu pigo takatifu pigo lililonyooka kabla ya uchaguzi mkuu ujao
Haya maneno nimeyasikia yanazungumzwa sana mtaani na maofisini na watu makini. Lakini nimejaribu kuunganisha dots nimeshindwa kupata maana, jee ni nini kinategemewa na wengi kutokea kabla ya uchaguzi?
 
Wewe ndiye mjinga, pengine labda mgonjwa wa akili vile vile. Umetoa sababu zozote za kupinga kuwa hawatashindwa?

Yani wetu wengine mna akili za “kimbuni mbuni” tuu!🤦🏾‍♂️
Kutoa sababu za hisia kulingana na fikra zako zilizofunikwa na ujinga hakuwezi kuzifanya kuwa ni hali halisi!

Eti CCM itapigwa chini! Uko Tanzania ya wapi?

Are you living in cloud cuckoo land?

Wake up!
 
Ccm na garasa letu litashika nafasi ya tatu ila Bahati nzuri mwenyekiti wa NEC aliteuliwa na garasa letu itabidi alitangaze hivyohivyo
 
Nyie jamaa ni watu wazima Ila ni WAPUMBAVU, kwa tume hii ya uchaguzi itakayojazwa TISS na wajeda tupu vituoni mnaamini mtaiondoa CCM madarakani!?, humu JF upande wa upinzani kuna jamaa anaitwa tindo ndo huwa anaongea uhalisia wengine mmegeuka wajinga kutokana na ushabiki. Kuna jamaa alikuwa anadai mgombea wa uraisi kupitia CCM ni Membe ni suala la muda tu., Ni mtu mzima na aliamini hivyo, ni type ya watu ninaowaitaga malofa humu.
Halafu nimegundua wengi ni watoto sana humu, hata hawaelewi kwamba tume siyo huru
 
Kutoa sababu za hisia kulingana na fikra zako zilizofunikwa na ujinga hakuwezi kuzifanya kuwa ni hali halisi!

Eti CCM itapigwa chini! Uko Tanzania ya wapi?

Are you living in cloud cuckoo land?

Wake up!
ushafikia “ad hominem” very quickly towards the bottom! You have actually bypassed a lot. Who is dumb?🤦🏾‍♂️
EAD353F8-046F-4173-A31F-1E24D56B3985.png
 
Haya maneno nimeyasikia yanazungumzwa sana mtaani na maofisini na watu makini. Lakini nimejaribu kuunganisha dots nimeshindwa kupata maana, jee ni nini kinategemewa na wengi kutokea kabla ya uchaguzi?
Mkuu wengi wakiwa na uhakika wa uchaguzi fair, hawabaki ccm! Wanaopiga kelele ni wanufaika wachache sana. Hata wale masheick si waliukataa waraka? Unadhani mioyo yao iliukataa ama ni woga tu?

Woga ukipungua kidogo tu, ccm chalii mapema mnoo! Na hili ndo maana kura huwa ni siri ya mtu!
 
Halafu nimegundua wengi ni watoto sana humu, hata hawaelewi kwamba tume siyo huru
Hivi unadhani anapoongea hivyo ndo kwamba anataka tume huru? Hapo anatisha tu watu kuwa tume siyo huru, na kwamba usalama na wanajeshi ndo wanahakikisha kuwa ccm wanashinda. Na huyu ni mwana ccm humu nguli! Ambaye hadhani kwamba tume huru ni jambo la maana.

Sasa wewe labda ndo mtoto, maana haumfahamu huyu member kama mimi humu ndani. Kama na wewe ni ccm, wote ni kundi moja la akili za kitoto.
 
Wanajamvi,

Kama heading ya uzi huu inavyojieleza, ni kwamba hakuna haja ya upinzani ku panic! Hayo ni ya wana ccm na kamwe siyo upinzani. Wao Kwani wamezuiwa siasa? Wamekuwa wakifanya kampeni toka awamu hii iingie madarakani, sasa wananchi kama ni kuona na kusikia, wameshasikia na kuona vya kutosha. Ni wazi sauti nyingine zikija watakuwa na shauku kubwa. Hiyo ni kawaida kwa hulka ya mwanadamu. Ni kiumbe mwenye kutafuta habari kila uchao!

Sasa nimeona watu wanasumbuka sana kuhusiana na suala la nani atakuwa mgombea kwa upande wa upinzani. Vyama vya ACT-Wazalendo na CHADEMA vikizungumziwa na kuhusishwa na wagombea wawili, yani Tundu Antipas Lissu, sambamba na Bernard Membe ambaye inasemekana yumo ACT-Wazalendo.

Tathimini rahisi, inaonyesha wazi kabisa kuwa ACT-Wazalendo, ni chama mbadala cha CUF. Na ndiyo kinategemewa kumsimamisha mgombea kule Zanzibar, kama sikosei, ni Maalim Seif. Kwahiyo kwa upande huo wa kushirikiana inapokuja kwa upande wa Zanzibar, ni kawaida tu.

Na kwa upande wa bara, mambo yalikuwa ni kati ya Lipumba, na mgombea wa CHADEMA, ambapo CHADEMA walikuwa ndo wanaotoa mgombea wa urais kwa upande wa bara.

Lakini tofauti iliyoko kwa sasa, ni Bernard Membe. Huyu yeye ndiye anayeleta mjadala mkali, na mjadala ambao unachochewa sana na wana ccm, kwasababu wao wameshamaliza upande wao na watu kuzimwa hata nafasi ya kuchukuwa fomu za kugombea kwenye nafasi ya urais. Na ndiyo matokeo yake Bernard Membe kujitoa. Huyu tayari ana watu wengi tu ndani ya ccm wanaoona ameonewa na ccm. Jambo lilokuwa ni kinyume hata na katiba ya chama.

Kwa maoni yangu, hata kama vyama hivi vikiamuwa kuwasimamisha wagombea wao, bado idadi ya kura watakazozipata, zitawazidi ccm. Huu ni ukweli mchungu kwa ccm na ndiyo maana wanahaha sana kuleta mijadala ya kuwachanganya na kutaka kuleta migawanyiko! Lakini hili halitafanya kazi.

Kule Kenya, hili liliwahi kutokea pia, na ndipo hapo chama cha KANU kilipoanguka chali! Kama sikosei, mara ya pili ilibidi wafanye muungano, kwasababu kura zao zote, zliwashinda KANU, lakini wao walikuwa hawajaungana, na hivyo KANU kubakia madarakani.

Kwa upande wa Tanzania, siasa zetu ni za tofauti kidogo na zile za Taifa la Kenya. Sisi kwanza siasa za ukabila siyo kivile! Pamoja na kwamba ccm wamejitahidi sana kuzitumia. Lakini hazijafanikiwa, na ndiyo maana upinzani ulipata nguvu sana hadi ccm kutishika! Na hata wengine wakisema uchaguzi uliopita, kama siyo kwa “goli la mkono”, ambalo Nape, January pamoja na Kinana, walifanya kazi ya ziada!

Sasa miaka mitano ndo hiyo imeshakata, Kinana ni juzi tu kaomba msamaha, ni baada ya Nape na January kufanya hivyo! Lakini nao walifanya kwa shingo upande, kwasababu nguvu za mwenyekiti ni kubwa mnoo! Hao nao sura zao halisi zingeonekana kama wengine wangeruhusiwa kuchukuwa fomu ya kugombea urais ndani ya ccm. Hata mzee Makamba naye ni hivyo hivyo tu. Mzee Mkapa naye alizungumzia umuhimu wa kuwa na tume huru ya uchaguzi nchini!

Kura za ccm ndizo zitakazogawanywa, cha msingi, kuwepo na makubaliano baina yao mapema iwezekanavyo, ninaamini uchaguzi huu utatuletea viongozi wanaowakilisha kada zote za wananchi pamoja na masilahi yao ya moja kwa moja jamii, na pia kama watanzania. Hili amelizungumzia vyema sana Sheick Ponda kwenye ule waraka wa Shura ya Maimamu, ambapo walizungumzia kuhusu upatikanaji wa katiba mpya baada ya uchaguzi.

Hapa ina maana kwamba kuna mengi yanayowaunganisha watanzania dhidi ya ccm kuliko yale yanayowatenganisha! Hayo ni machache sana ambayo siyo lazima kupewa kipaumbele! Maana yenyewe ni ya kuwagawanya wapinzani ili kuwadhibiti! Yani “devide and rule”. Kwetu ni tofauti kabisa na kule Kenya ambapo siasa za ukabila ndizo zinawaumbuwa. “Coalitions”, ama miungano yao, ni ya misingi ya kikabila. Na Kwahiyo tuna nafasi nzuri zaidi kwa wapinzani kuiangusha ccm, na bado tukapata serikali itakayowatumikia wananchi vyema, na kwa mujibu wa katiba ya nchi! Na hao wakifanya uzembe, tuwe na nafasi na uwezo wa kuwandoa madarakani kwa sanduku la kura!

Siyo siri, chama cha CUF, kilikuwa na wanachama wengi wa maeneo ya mwambao wa Pwani! Na hivyo wengi kuwa waislam. Majimbo mengi ya waislam, ni hao CUF waliyabeba, lakini mengine ni ccm. Hata hivyo, kama nilivyosema hapo awali, ACT-Wazalendo ndiyo ambao sasa wameichukuwa nafasi hiyo ya chama cha CUF. “It has simply been replaced”, haswa baada ya Maalim Seif kuondoka huko, na Zitto kuitumia nafasi hiyo kumsajili.

Sasa endapo ACT-Wazalendo watamsimamisha Membe, nadhani siyo mbaya hata kidogo kwa upande wa CHADEMA na upinzani kwa ujumla!Kwanza kuna malalamiko mengi sana ya uwepo wa udini. Malalamiko ambayo yanaelekezwa kwa utawa wa ccm! Na wala siyo mara ya kwanza! Na ndiyo maana hata CUF ilipata nguvu sana! Malalamiko yao hayajaanza leo chini ya utawala wa ccm! Hawa watu sauti zao lazima zitakuwa zinataka mwakilishi. Hata waislam wale ambao walikuwa hawaipigii CUF kura, na wakawa wanaipigia ccm, basi sasa wataipigia kura ACT-Wazalendo.

Hata wale ccm wasioipenda CHADEMA, wataipigia kura ACT-Wazalendo. Maana tunafahamu propaganda za ccm inapokuja kwenye udini na ukabila! Tuhuma zao wenyewe, lakini wamekuwa wakiwasingizia upinzani. Sasa ccm mmetawala toka uhuru, upinzani ndo umeleta shida za waislam toka lini? Hili huwa najiuliza sana wakati ccm inapokuja na mgombea wao huku wakitutajia maendeleo waliyoyaleta, na kujifananisha na upinzani ambao hawajawahi kuongoza nchi. Hili lenyewe, lilitakiwa liwe sababu nzuri kabisa ya kuwa na uchaguzi huru! Maana nani mwingine ambaye ameshafanya “mazuri” zaidi yao tokea December 31st 1961?

Hivyo ni kweli kabisa kuwa uchaguzi wa huru na haki, utawaondoa ccm madarakani, upinzani uungane, ama usiungane, moto ni ule ule! Membe atakula vichwa vya ccm, chadema nao watakula vichwa vya ccm. Hata yule Sipunda anaweza kula vichwa!

Cha msingi, ni makubaliano yafanyike mapema! Makubaliano ambayo yatahusisha nia ya dhati kabisa ya pande zote mbili! Ni za kuwa na tume huru ya uchaguzi pamoja na katiba mpya ya wananchi kutoka kwa wananchi! Na siyo hii ya mkoloni yenye viraka vya ccm ambayo inaendelea kutushikia chini kiasi cha kwamba uhuru wetu ukawa mashakani!

Sababu ziko nyingi sana, ila nimeamuwa kuanzia na hizi!

Nguruvi3
Kuna dalili za watu kuwa akili zimeyumba. Baada ya kuona upinzani hauna mwelekeo.
 
Jamani huyu mwanzishaji uzi anaumwa tena kichaa kimekuwa sugu, amekuwa akiandika mara Kiingereza mara nne na mada ndefu sana lakini ndani upupu tu. Mnaomjibu mnapoteza time na mnafail sana
 
Back
Top Bottom