CHADEMA, mchukueni HAMADI RASHID

CHADEMA, mchukueni HAMADI RASHID

mi sioni huyu jamaa kama anafaa sana kwa cdm because huyu jamaa ana uchu sana wa madaraka so asipochaguliwa atahama sio mtu mzuri kwa msimamo wa chama
Akihama sawa,lakini kwa vyovyote vile ataacha cdm imeeleweka znz na hivyo atatuacha na wanachama wa kutosha.
 
Wakati umefika wa CDM kutafuta namna ya kujiimarisha kule Zanzibar,kwangu mimi Hamad Rashid atakuwa ni kete nzuri sana kwa cdm katika kukijenga chama kule Zanzibar, hivyo nashauri cdm tumchukue huyu jamaa,maana sijaona dhambi kubwa aliyofanya.Critical /Great thinkers watatoa maoni ya kujenga na si matusi.


Wana jf mnasemaje?
Bahati mbaya Hamad RASHID HATAKIWI TENA ZANZIBAR ,ukitaka kujua kama kweli Hamad Rashid alijisahau katika uwongozi wake ndani ya maika 15 ya ubunge wa jimbo lae,nenda Wawi Pemba ukajionee mwenyewe.

Mvuto hana tena, kama muna pesa za kuchezea na muda mpeni hamadi rashid hiyo kaziii,acheni ujinga huo, zanzibar itakombolewa na wazanzibari wenyewe na sio chadema. Ikiwa watanzania munasubiri chadema iwaletee maendeleo au munasubiri chadema iitoe ccm madarakani yagujuuu,wananchi ndio watakao weza kuitoa ccm madarakani, lakini sio chadema peke yake.
 
Mkuu, Hamad ni mwanasiasa mzuri lakini ni moto wa kuotea mbali.

kuna taarifa zenye uhakika wa asilimia kubwa kwamba anatumika kudhoofisha nguvu ya upinzani nchini.

Hata hivyo kuna wazanzibari wengi waadilifu na wazalendo wanaweza kuwa recruited na kuwa maarufu kuliko kutafuta watu maarufu ambao wengi wao ni hatari
 
Si sahihi kumchukua Hamad!!
Mtu aliyeshindikana kwenye chama chake kama mnafiki,mroho wa madaraka na mbinafsi.
Tukumbuke jasiri haachi asili.
 
Chadema fanyeni usajili dirisha dogo mchukueni Hamadi Rashid.
 
SAGANKA Tunasema kwamba, Chadema hawana chao Zanzibar! wamesahau kura za maruhani?
wao wazidi kujiimarisha huku Kaskazini na kanda ya Magharibi! ndiko wanakokubalika kidogo na ili upinzani ushinde CDM hawana budi kuzungumza kwa adabu na heshima na CUF!
 
Last edited by a moderator:
sikubaliani na wale wanaosema kuwa chadema haihitaji watu kutoka vyama vingine. nauliza;
i- muasisi wa chdm mzee mtei hakutokea ccm?
ii- dk slaa alikua mbunge wa ccm kwa muda mrefu. alipotemwa kura za maoni akakimbilia chadema.
iii- mbowe alikua ccm kabla ya kujiunga chdm.

akina zitto, mnyika..... ndiyo damu changa ambazo zimeanzia chadema.
 
Chadema ni failure Hamad haezi kwenda ht kwa dawa anarudi ccm chama chny mafanikio
 
Alivyokuwa cuf alishiriki kikamilifu kuishambulia cdm badala ya ccm kana kwamba cdm ndiyo chama tawala. Watz hawawezi kumsahau hamad hasa kwa kitendo chake cha kinafiki na uchu wa madaraka kutaka sheria za bunge zipindishwe ili cdm kisiwe chama kikuu cha upinzani au kipokwe nafasi muhimu. Aendelee tu na mahakama. Naamini 2015 atakuwa muuza kahawa na kashata maarufu pale visiwani
 
sikubaliani na wale wanaosema kuwa chadema haihitaji watu kutoka vyama vingine. nauliza;
i- muasisi wa chdm mzee mtei hakutokea ccm?
ii- dk slaa alikua mbunge wa ccm kwa muda mrefu. alipotemwa kura za maoni akakimbilia chadema.
iii- mbowe alikua ccm kabla ya kujiunga chdm.

akina zitto, mnyika..... ndiyo damu changa ambazo zimeanzia chadema.

Kwa kipindi hiko kulikua na mfumo wa chama kimoja huwezi laumu lakini sasa tuna vijana wengi ambao hatujui chama kimoja tumekua na mfumo wa vyama vingi kwa uhai huu wa miaka 20 wa vyama vingi huwezi sasa kutumia watu wale wale waliokaaa ccm baada ya kupigwa chini ndo wanakumbukua chadema.hapana
 
Huyu ndiye mwanzilishi wa chama cha adc. Nadhani kwa sasa atashughulika kuimarisha chama chake. Forget about him!!!
 
Hatutaki mtu asiyekubalika nyumbani.Kumbuka tunajenga chama,hivyo labda akijiunga tu kwa hiari yake lakini si kuombwa kujiunga.Sijafika znz na hivyo siwezi kuzungumzia mvuto wa hamad huko,ninachoelewa ni kuwa ni kati ya wabunge wenye ushawishi na ni miongoni mwa walioshinda kwa ushindi mnono.Lakini pia ukimlinganisha na waznz wengi anaoneka kuwa walau ana hoja.

Wewe hujawahi kusikia kama katika uchaguzi mkuu wa 2010 Hamad Rashid alikua 'KASHABWAGWA' (ameshaangushwa) na wananchi jimboni kwake lakini Maalim akenda akamuokota na kumpangusa mavumbi ndipo akakubalika na kupata huo ushindi uliousema! Nachotaka kukwambia panapohusika SIASA ndani ya Zanzibar kwa sasa Hamad Rashid hata ukimpeleka katika mnada kuamua kumuuza kwa bei ya shilingi 10 ya Kitanzania basi hatakiwi!
 
kwa kipindi hiko kulikua na mfumo wa chama kimoja huwezi laumu lakini sasa tuna vijana wengi ambao hatujui chama kimoja tumekua na mfumo wa vyama vingi kwa uhai huu wa miaka 20 wa vyama vingi huwezi sasa kutumia watu wale wale waliokaaa ccm baada ya kupigwa chini ndo wanakumbukua chadema.hapana


inaelekea hujanielewa. Slaa alipigwa chini ccm ndiyo akakimbilia chadema. Kama wewe siyo mtafiti wa mambo ya kisiasa, nyamaza. Slaa aliangushwa kwenye kura ya maoni ccm ndiyo akakimbilia chadema.
 
Hana tofauti na Shibuda huyo.. hafai hata kua mshabiki wacha uanachama
 
inaelekea hujanielewa. Slaa alipigwa chini ccm ndiyo akakimbilia chadema. Kama wewe siyo mtafiti wa mambo ya kisiasa, nyamaza. Slaa aliangushwa kwenye kura ya maoni ccm ndiyo akakimbilia chadema.

Najua aliangusha lakini kwa kipindi hiko muamko wa vyama vya upinzani ulikua mdogo sana hivi kulikua na vijana waliogombea kweli
 
Back
Top Bottom