CHADEMA; kwa hili mnastahili maua yenu

CHADEMA; kwa hili mnastahili maua yenu

Neema ya BWANA

Senior Member
Joined
Jun 25, 2023
Posts
129
Reaction score
61
Kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, ninapenda kuzungumzia kipengele kimoja kilichonivutia zaidi katika Ilani ya mwaka 2020-2025 ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA); Sura ya 16, Kifungu namba 16.1 Kipengele b (Ukurasa wa 95) ambacho kinasema:

"Katika kutimiza azma ya kujiendeleza katika sekta ya sayansi na teknolojia, Serikali ya Chadema itaweka mkazo katika kuimarisha mahusiano yanayolenga kuiwezesha Tanzania kuiga na kuchota maendeleo ya kiteknolojia yaliyofikiwa katika nchi za Asia na hasa China."

Kipengele hiki ni muhimu sana kwa taifa letu, kwani tunafahamu sote kuwa China ni taifa lililopiga hatua kubwa katika Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia duniani; yaliyopelekea uchumi wake kukua kwa kasi kubwa na kuwa imara zaidi.

Ingawa lengo hili lilitolewa na CHADEMA kupitia Ilani yake ya uchaguzi ya mwaka 2020-2025, lakini tukiamua kuweka kando vyama vyetu, dini zetu na ubaguzi wa aina yoyote ile tukabaki kuwa Watanzania ambao ni Wazalendo tunaolitakia mema taifa letu; haijalishi Ilani hii inakaribia kumaliza muda wake, lakini lengo hili linaweza kuhuishwa upya na kutekelezwa nasi sote kuanzia Serikali iliyopo madarakani, Chama Tawala (CCM), Mimi, Wewe, Watanzania, Taasisi, Mashirika, Vyama vya Upinzani na CHADEMA wenyewe haijalishi wako ndani au nje ya Serikali; kupitia SEKTA BINAFSI.

Ni uwekezaji wa aina gani unaweza kulifaa lengo hili?

  1. Eneo la kwanza la uwekezaji unaoweza kufanyika kupitia lengo hili ni kuanzisha shule binafsi za kimataifa (International Schools) zenye mitaala (mtaala) ya Kichina inayolenga sanaa, ubunifu, sayansi na teknolojia nchini Tanzania; kuanzia ngazi ya malezi (daycare), awali, msingi, sekondari mpaka elimu ya kati (college) kwani tayari tumekwishaona mitaala kutoka magharibi kama vile Cambridge na International Baccalaureate (IB) ikifanya kazi nchini.
  2. Eneo la pili la uwekezaji unaoweza kufanyika kupitia lengo hili ni kuwekeza katika Uandishi Bunifu na kuandika vitabu vipya kwa Lugha ya Kiswahili vyenye kuelezea na kuvumbua siri za mafanikio ya China pamoja na bunifu mbalimbali zinazofanyika nchini humo kama vitabu vya ziada kwa wanafunzi ambao hawataweza kusoma katika shule zilizoelezewa katika kipengele namba 1 lakini pia vitabu vinavyoweza kusomwa na mtu yeyote kwenye jamii ya Tanzania.
  3. Eneo la tatu la uwekezaji unaoweza kufanyika kupitia lengo hili ni kutafsiri vitabu vya Historia ya China na Vitabu vya Taguchi za Kichina vilivyopo katika lugha ya Kichina ili viwe katika Lugha ya Kiswahili kama vitabu vya ziada kwa wanafunzi ambao hawataweza kusoma katika shule zilizoelezewa katika kipengele namba 1 lakini pia vitabu vinavyoweza kusomwa na mtu yeyote kwenye jamii ya Tanzania.

Taguchi ni nini?

Taguchi ni njia za kitakwimu ambazo zilivumbuliwa na Mjapani aitwaye Genichi Taguchi ili kuongeza thamani ya ubora (quality) wa ubunifu wa bidhaa zinazozalishwa viwandani na katika nyanja mbalimbali kama vile Uhandisi, Bioteknolojia, Masoko, TEHAMA, Mawasiliano, Uchukuzi, n.k.

Sababu ya mimi kuona kuwa maeneo haya matatu yanafaa zaidi katika uwekezaji huu ni kutokana na Elimu, Ujuzi na Maarifa kuwa moja kati ya nyenzo kuu zilizowafanya Wachina wapige hatua kubwa kwenye Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia kisha Uchumi duniani.

Mfano; kupitia Falsafa ya Kichina iitwayo CONFUCIANISM iliyoanzishwa na 'Kong Qiu' au 'Zhong Ni' maarufu kama Master Kong, Kong Fuzi au Confucius (551-479 BCE) inayotumika kwenye nyanja maalum nchini humo ambazo ni Utamaduni, Jamii, Biashara na Siasa.

Confucianism ni nini?
Confucianism ni Falsafa ya Kichina yenye lengo la kurejesha, kujaza, kuhamasisha na kuimarisha tabia njema kwenye jamii ya Kichina; ili kuibua matokeo mema na chanya kwenye jamii za Kichina yatakayojidhihirisha dunia nzima. Hakika leo hii sote tunashuhudia mema haya yaletwayo na taifa la China. Falsafa hii ya Kichina inafundisha kuhusu tabia njema mbalimbali kama ifuatavyo:-

REN Confucian
Upendo, Utu na Huruma

YI Confucian
Haki na Kufanya Matendo ya Haki

LI Confucian
Kuwa na mpangilio mzuri wa jambo unalofanya ikiwemo kufuata kanuni au mfumo. (System or Proper Way)

ZHI Confucian
Kuyatafsiri Maarifa, Hekima, Ujuzi na Elimu uliyonayo haijalishi udogo au ukubwa wake; ili yatumike katika kufanya maamuzi sahihi, kujua lipi ni sahihi na lipi si sahihi, kufanya ubunifu (innovation), kuwaza kwa hekima, kufanya uchambuzi na ku-judge mambo kwa hekima.

Kwa tafsiri rahisi, ZHI ni Hekima kwa Vitendo; ku-apply kile ulichonacho kwa kufanya kitu kipya. Hii imepelekea Wachina kuwa watu wenye uthubutu wa kufanya mambo makubwa zaidi duniani.

XIN Confucian
Katika Falsafa ya Kichina; XIN ni Ukweli, Uaminifu na Kutovunja Ahadi. Maneno yaliyonyooka, matendo yaliyonyooka pasipo kupepesa macho na kufanya kile ulichoahidi kufanya ni sehemu ya Utamaduni wa Kichina.

Xin inajenga urafiki, uhusiano na inasimama kama tabia moyo (muhimu zaidi) kwenye Utamaduni wa Kichina.

Ndiyo iwe Ndiyo!
Hapana iwe Hapana!

XIN Confucian inaibua tamaduni nyingine za Kichina ambazo ni Guanxi pamoja na Mianzi. Guanxi ni ujenzi wa Uhusiano Mzuri (Good Relationship or Friendship) ambao ni binafsi, wa kibiashara, wa kijamii, wa kisiasa, n.k. Namna bora ya kujenga Guanxi kwa Wachina ni kwa njia ya kukutana Uso kwa Uso kupitia vikao, mikutano, kutembeleana, kukaribishana, n.k.

Kutengeneza Guanxi ni mchakato wa muda mrefu; mfano ni ule niliowashauri CHADEMA kurudi kwa jamii kwenye andiko langu lililopita. Kujenga Guanxi kunachochea kuibuka kwa Mianzi (Face) Gaining.

Mianzi (Face) Gaining ni kitendo cha kufanya jitihada za kuleta neema na mambo yaliyo mema kwa mwingine ili kulinda 'Social Image' yake. Unapofanya mabaya kwa mwingine maana yake unaharibu 'Social Image' yake; na kwenye Utamaduni wa Kichina huitwa Mianzi (Face) Loosing; ambapo Mianzi Loosing hupelekea kubomoa Guanxi.

  • Unapomtukana mwingine hii katika Utamaduni wa Kichina ni Mianzi Loosing inayopelekea kubomoka kwa Guanxi.
  • Unapomzungumzia mwingine vizuri awe yupo au hayupo hii katika Utamaduni wa Kichina huitwa Mianzi Giving ambayo hupelekea Kujengeka kwa Guanxi.
  • Kama wewe ni mwanasiasa na hukufanya kile ulichoahidi kwa wanachi wako hii katika Utamaduni wa Kichina huitwa Mianzi Loosing ambayo hupelekea kubomoka kwa Guanxi.
  • Kama una rafiki yako na umeamua kumualika nyumbani kwako aje kula chakula cha jioni hii katika Utamaduni wa Kichina huitwa Mianzi Giving ambayo hupelekea kujengeka kwa Guanxi.

XIAO Confucian
Hii ni namna watoto na vijana wa Kichina wanapaswa kuwahudumia wazazi na wakubwa wengine kwenye familia na jamii zao. Kupitia tabia hii njema ya Xiao Confucian, Wachina hufundishwa kuwasikiliza wakubwa, kutumia lugha laini wazungumzapo na mkubwa, kuwasalimia wakubwa, kuwafariji wakubwa kwa maneno na vitendo hasa pale wanapopitia changamoto mbalimbali, kuwahudumia wakubwa kwa fedha na mahitaji mengine, heshima kwa wakubwa, n.k. katika familia na jamii zao.

WEN Confucian
Hii ni sanaa za amani ambazo hutumiwa ili kuleta maendeleo ya mtu binafsi. Confucius (Kong Fuzi) aliamini kuwa sanaa ina nguvu ya kubadili maisha ya mwanadamu. Katika Wen Confucian; sanaa zilizozungumziwa zaidi ni sanaa za Kiutamaduni za China kama via Calligraphy (Sanaa ya Uandishi wa Mkono kwa kutumia mwandiko mzuri), Music (Muziki), Numeracy (Namba au Hesabu), n.k.

Hitimisho
Mpaka sasa nchini Tanzania ipo Taasisi ya Kichina iitwayo Confucius inayopatikana kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM); iliyojikita katika kufundisha Lugha ya Kichina kwa Watanzania.

Ingawa taasisi hii imeleta nuru kwa kufundisha lugha iliyo katika nafasi za juu sana ulimwenguni kwa sasa; mapungufu ya taasisi hii ni kuwa haijachota elimu nzima-nzima iliyobeba maendeleo ya kiteknolojia yaliyofikiwa katika Nchi ya China na kuileta Tanzania, hivyo suluhu ni vyema kuanzisha Shule Binafsi za Mitaala ya Kichina na kuzalisha vitabu vinavyohusu China kwa Lugha ya Kiswahili nchini Tanzania.
 
Kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, ninapenda kuzungumzia kipengele kimoja kilichonivutia zaidi katika Ilani ya mwaka 2020-2025 ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA); Sura ya 16, Kifungu namba 16.1 Kipengele b (Ukurasa wa 95) ambacho kinasema:

"Katika kutimiza azma ya kujiendeleza katika sekta ya sayansi na teknolojia, Serikali ya Chadema itaweka mkazo katika kuimarisha mahusiano yanayolenga kuiwezesha Tanzania kuiga na kuchota maendeleo ya kiteknolojia yaliyofikiwa katika nchi za Asia na hasa China."

Kipengele hiki ni muhimu sana kwa taifa letu, kwani tunafahamu sote kuwa China ni taifa lililopiga hatua kubwa katika Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia duniani; yaliyopelekea uchumi wake kukua kwa kasi kubwa na kuwa imara zaidi.

Ingawa lengo hili lilitolewa na CHADEMA kupitia Ilani yake ya uchaguzi ya mwaka 2020-2025, lakini tukiamua kuweka kando vyama vyetu, dini zetu na ubaguzi wa aina yoyote ile tukabaki kuwa Watanzania ambao ni Wazalendo tunaolitakia mema taifa letu; haijalishi Ilani hii inakaribia kumaliza muda wake, lakini lengo hili linaweza kuhuishwa upya na kutekelezwa nasi sote kuanzia Serikali iliyopo madarakani, Chama Tawala (CCM), Mimi, Wewe, Watanzania, Taasisi, Mashirika, Vyama vya Upinzani na CHADEMA wenyewe haijalishi wako ndani au nje ya Serikali; kupitia SEKTA BINAFSI.

Ni uwekezaji wa aina gani unaweza kulifaa lengo hili?

  1. Eneo la kwanza la uwekezaji unaoweza kufanyika kupitia lengo hili ni kuanzisha shule binafsi za kimataifa (International Schools) zenye mitaala (mtaala) ya Kichina inayolenga sanaa, ubunifu, sayansi na teknolojia nchini Tanzania; kuanzia ngazi ya awali, msingi, sekondari mpaka elimu ya kati (college) kwani tayari tumekwishaona mitaala kutoka magharibi kama vile Cambridge na International Baccalaureate (IB) ikifanya kazi nchini.
  2. Eneo la pili la uwekezaji unaoweza kufanyika kupitia lengo hili ni kuwekeza katika Uandishi Bunifu na kuandika vitabu vipya kwa Lugha ya Kiswahili vyenye kuelezea na kuvumbua siri za mafanikio ya China pamoja na bunifu mbalimbali zinazofanyika nchini humo kama vitabu vya ziada kwa wanafunzi ambao hawataweza kusoma katika shule zilizoelezewa katika kipengele namba 1 lakini pia vitabu vinavyoweza kusomwa na mtu yeyote kwenye jamii ya Tanzania.
  3. Eneo la tatu la uwekezaji unaoweza kufanyika kupitia lengo hili ni kutafsiri vitabu vya Historia ya China na Vitabu vya Taguchi za Kichina vilivyopo katika lugha ya Kichina ili viwe katika Lugha ya Kiswahili kama vitabu vya ziada kwa wanafunzi ambao hawataweza kusoma katika shule zilizoelezewa katika kipengele namba 1 lakini pia vitabu vinavyoweza kusomwa na mtu yeyote kwenye jamii ya Tanzania.

Taguchi ni nini?

Taguchi ni njia za kitakwimu ambazo zilivumbuliwa na Mjapani aitwaye Genichi Taguchi ili kuongeza thamani ya ubora (quality) wa ubunifu wa bidhaa zinazozalishwa viwandani na katika nyanja mbalimbali kama vile Uhandisi, Bioteknolojia, Masoko, TEHAMA, Mawasiliano, Uchukuzi, n.k.

Sababu ya mimi kuona kuwa maeneo haya matatu yanafaa zaidi katika uwekezaji huu ni kutokana na Elimu, Ujuzi na Maarifa kuwa moja kati ya nyenzo kuu zilizowafanya Wachina wapige hatua kubwa kwenye Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia kisha Uchumi duniani.

Mfano; kupitia Falsafa ya Kichina iitwayo CONFUCIANISM iliyoanzishwa na 'Kong Qiu' au 'Zhong Ni' maarufu kama Master Kong, Kong Fuzi au Confucius (551-479 BCE) inayotumika kwenye nyanja maalum nchini humo ambazo ni Utamaduni, Jamii, Biashara na Siasa.

Confucianism ni nini?
Confucianism ni Falsafa ya Kichina yenye lengo la kurejesha, kujaza, kuhamasisha na kuimarisha tabia njema kwenye jamii ya Kichina; ili kuibua matokeo mema na chanya kwenye jamii za Kichina yatakayojidhihirisha dunia nzima. Hakika leo hii sote tunashuhudia mema haya yaletwayo na taifa la China. Falsafa hii ya Kichina inafundisha kuhusu tabia njema mbalimbali kama ifuatavyo:-

REN Confucian
Upendo, Utu na Huruma

YI Confucian
Haki na Kufanya Matendo ya Haki

LI Confucian
Kuwa na mpangilio mzuri wa jambo unalofanya ikiwemo kufuata kanuni au mfumo. (System or Proper Way)

ZHI Confucian
Kuyatafsiri Maarifa, Hekima, Ujuzi na Elimu uliyonayo haijalishi udogo au ukubwa wake; ili yatumike katika kufanya maamuzi sahihi, kujua lipi ni sahihi na lipi si sahihi, kufanya ubunifa (innovation), kuwaza kwa hekima, kufanya uchambuzi na ku-judge mambo kwa hekima.

Kwa tafsiri rahisi, ZHI ni Hekima kwa Vitendo; ku-apply kile ulichonacho kwa kufanya kitu kipya. Hii imepelekea Wachina kuwa watu wenye uthubutu wa kufanya mambo makubwa zaidi duniani.

XIN Confucian
Katika Falsafa ya Kichina; XIN ni Ukweli, Uaminifu na Kutovunja Ahadi. Maneno yaliyonyooka, matendo yaliyonyooka pasipo kupepesa macho na kufanya kile ulichoahidi kufanya ni sehemu ya Utamaduni wa Kichina.

Xin inajenga urafiki, uhusiano na inasimama kama tabia moyo (muhimu zaidi) kwenye Utamaduni wa Kichina.

Ndiyo iwe Ndiyo!
Hapana iwe Hapana!

XIN Confucian inaibua tamaduni nyingine za Kichina ambazo ni Guanxi pamoja na Mianzi. Guanxi ni ujenzi wa Uhusiano Mzuri (Good Relationship or Friendship) ambao ni binafsi, wa kibiashara, wa kijamii, wa kisiasa, n.k. Namna bora ya kujenga Guanxi kwa Wachina ni kwa njia ya kukutana Uso kwa Uso kupitia vikao, mikutano, kutembeleana, kukaribishana, n.k.

Kutengeneza Guanxi ni mchakato wa muda mrefu; mfano ni ule niliowashauri CHADEMA kurudi kwa jamii kwenye andiko langu lililopita. Kujenga Guanxi kunachochea kuibuka kwa Mianzi (Face) Gaining.

Mianzi (Face) Gaining ni kitendo cha kufanya jitihada za kuleta neema na mambo yaliyo mema kwa mwingine ili kulinda 'Social Image' yake. Unapofanya mabaya kwa mwingine maana yake unaharibu 'Social Image' yake; na kwenye Utamaduni wa Kichina huitwa Mianzi (Face) Loosing; ambapo Mianzi Loosing hupelekea kubomoa Guanxi.

  • Unapomtukana mwingine hii katika Utamaduni wa Kichina ni Mianzi Loosing inayopelekea kubomoka kwa Guanxi.
  • Unapomzungumzia mwingine vizuri awe yupo au hayupo hii katika Utamaduni wa Kichina huitwa Mianzi Giving ambayo huoelekea Kujengeka kwa Guanxi.
  • Kama wewe ni mwanasiasa na hukufanya kile ulichoahidi kwa wanachi wako hii katika Utamaduni wa Kichina huitwa Mianzi Loosing ambayo hupelekea kubomoka kwa Guanxi.
  • Kama una rafiki yako na umeamua kumualika nyumbani kwako aje kula chakula cha jioni hii katika Utamaduni wa Kichina huitwa Mianzi Giving ambayo hupelekea kujengeka kwa Guanxi.

XIAO Confucian
Hii ni namna watoto na vijana wa Kichina napaswa kuwahudumia wazazi na wakubwa wengine kwenye familia na jamii zao. Kupitia tabia hii njema ya Xiao Confucian, Wachina hufundishwa kuwasikiliza wakubwa, kutumia lugha laini wazungumzapo na mkubwa, kuwasalimia wakubwa, kuwafariji wakubwa kwa maneno na vitendo hasa pale wanapopitia changamoto mbalimbali, kuwahudumia wakubwa kwa fedha na mahitaji mengine, heshima kwa wakubwa, n.k. katika familia na jamii zao.

WEN Confucian
Hii ni sanaa za amani ambazo hutumiwa ili kuleta maendeleo ya mtu binafsi. Confucius (Kong Fuzi) aliamini kuwa sanaa ina nguvu ya kubadili maisha ya mwanadamu. Katika Wen Confucian; sanaa zilizozungumziwa zaidi ni sanaa za Kiutamaduni za China kama via Calligraphy (Sanaa ya Uandishi wa Mkono kwa kutumia mwandiko mzuri), Music (Muziki), Numeracy (Namba au Hesabu), n.k.

Hitimisho
Mpaka sasa nchini Tanzania ipo Taasisi ya Kichina iitwayo Confucius inayopatikana kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM); iliyojikita katika kufundisha Lugha ya Kichina kwa Watanzania.
Ingawa taasisi hii imeleta nuru kwa kufundisha lugha iliyo katika nafasi za juu sana ulimwenguni kwa sasa; mapungufu ya taasisi hii ni kuwa haijachota elimu nzima-nzima iliyobeba maendeleo ya kiteknolojia yaliyofikiwa katika Nchi ya China na kuileta Tanzania, hivyo suluhu ni vyema kuanzisha Shule Binafsi za Mitaala yaKichina nchini Tanzan

Kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, ninapenda kuzungumzia kipengele kimoja kilichonivutia zaidi katika Ilani ya mwaka 2020-2025 ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA); Sura ya 16, Kifungu namba 16.1 Kipengele b (Ukurasa wa 95) ambacho kinasema:

"Katika kutimiza azma ya kujiendeleza katika sekta ya sayansi na teknolojia, Serikali ya Chadema itaweka mkazo katika kuimarisha mahusiano yanayolenga kuiwezesha Tanzania kuiga na kuchota maendeleo ya kiteknolojia yaliyofikiwa katika nchi za Asia na hasa China."

Kipengele hiki ni muhimu sana kwa taifa letu, kwani tunafahamu sote kuwa China ni taifa lililopiga hatua kubwa katika Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia duniani; yaliyopelekea uchumi wake kukua kwa kasi kubwa na kuwa imara zaidi.

Ingawa lengo hili lilitolewa na CHADEMA kupitia Ilani yake ya uchaguzi ya mwaka 2020-2025, lakini tukiamua kuweka kando vyama vyetu, dini zetu na ubaguzi wa aina yoyote ile tukabaki kuwa Watanzania ambao ni Wazalendo tunaolitakia mema taifa letu; haijalishi Ilani hii inakaribia kumaliza muda wake, lakini lengo hili linaweza kuhuishwa upya na kutekelezwa nasi sote kuanzia Serikali iliyopo madarakani, Chama Tawala (CCM), Mimi, Wewe, Watanzania, Taasisi, Mashirika, Vyama vya Upinzani na CHADEMA wenyewe haijalishi wako ndani au nje ya Serikali; kupitia SEKTA BINAFSI.

Ni uwekezaji wa aina gani unaweza kulifaa lengo hili?

  1. Eneo la kwanza la uwekezaji unaoweza kufanyika kupitia lengo hili ni kuanzisha shule binafsi za kimataifa (International Schools) zenye mitaala (mtaala) ya Kichina inayolenga sanaa, ubunifu, sayansi na teknolojia nchini Tanzania; kuanzia ngazi ya awali, msingi, sekondari mpaka elimu ya kati (college) kwani tayari tumekwishaona mitaala kutoka magharibi kama vile Cambridge na International Baccalaureate (IB) ikifanya kazi nchini.
  2. Eneo la pili la uwekezaji unaoweza kufanyika kupitia lengo hili ni kuwekeza katika Uandishi Bunifu na kuandika vitabu vipya kwa Lugha ya Kiswahili vyenye kuelezea na kuvumbua siri za mafanikio ya China pamoja na bunifu mbalimbali zinazofanyika nchini humo kama vitabu vya ziada kwa wanafunzi ambao hawataweza kusoma katika shule zilizoelezewa katika kipengele namba 1 lakini pia vitabu vinavyoweza kusomwa na mtu yeyote kwenye jamii ya Tanzania.
  3. Eneo la tatu la uwekezaji unaoweza kufanyika kupitia lengo hili ni kutafsiri vitabu vya Historia ya China na Vitabu vya Taguchi za Kichina vilivyopo katika lugha ya Kichina ili viwe katika Lugha ya Kiswahili kama vitabu vya ziada kwa wanafunzi ambao hawataweza kusoma katika shule zilizoelezewa katika kipengele namba 1 lakini pia vitabu vinavyoweza kusomwa na mtu yeyote kwenye jamii ya Tanzania.

Taguchi ni nini?

Taguchi ni njia za kitakwimu ambazo zilivumbuliwa na Mjapani aitwaye Genichi Taguchi ili kuongeza thamani ya ubora (quality) wa ubunifu wa bidhaa zinazozalishwa viwandani na katika nyanja mbalimbali kama vile Uhandisi, Bioteknolojia, Masoko, TEHAMA, Mawasiliano, Uchukuzi, n.k.

Sababu ya mimi kuona kuwa maeneo haya matatu yanafaa zaidi katika uwekezaji huu ni kutokana na Elimu, Ujuzi na Maarifa kuwa moja kati ya nyenzo kuu zilizowafanya Wachina wapige hatua kubwa kwenye Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia kisha Uchumi duniani.

Mfano; kupitia Falsafa ya Kichina iitwayo CONFUCIANISM iliyoanzishwa na 'Kong Qiu' au 'Zhong Ni' maarufu kama Master Kong, Kong Fuzi au Confucius (551-479 BCE) inayotumika kwenye nyanja maalum nchini humo ambazo ni Utamaduni, Jamii, Biashara na Siasa.

Confucianism ni nini?
Confucianism ni Falsafa ya Kichina yenye lengo la kurejesha, kujaza, kuhamasisha na kuimarisha tabia njema kwenye jamii ya Kichina; ili kuibua matokeo mema na chanya kwenye jamii za Kichina yatakayojidhihirisha dunia nzima. Hakika leo hii sote tunashuhudia mema haya yaletwayo na taifa la China. Falsafa hii ya Kichina inafundisha kuhusu tabia njema mbalimbali kama ifuatavyo:-

REN Confucian
Upendo, Utu na Huruma

YI Confucian
Haki na Kufanya Matendo ya Haki

LI Confucian
Kuwa na mpangilio mzuri wa jambo unalofanya ikiwemo kufuata kanuni au mfumo. (System or Proper Way)

ZHI Confucian
Kuyatafsiri Maarifa, Hekima, Ujuzi na Elimu uliyonayo haijalishi udogo au ukubwa wake; ili yatumike katika kufanya maamuzi sahihi, kujua lipi ni sahihi na lipi si sahihi, kufanya ubunifa (innovation), kuwaza kwa hekima, kufanya uchambuzi na ku-judge mambo kwa hekima.

Kwa tafsiri rahisi, ZHI ni Hekima kwa Vitendo; ku-apply kile ulichonacho kwa kufanya kitu kipya. Hii imepelekea Wachina kuwa watu wenye uthubutu wa kufanya mambo makubwa zaidi duniani.

XIN Confucian
Katika Falsafa ya Kichina; XIN ni Ukweli, Uaminifu na Kutovunja Ahadi. Maneno yaliyonyooka, matendo yaliyonyooka pasipo kupepesa macho na kufanya kile ulichoahidi kufanya ni sehemu ya Utamaduni wa Kichina.

Xin inajenga urafiki, uhusiano na inasimama kama tabia moyo (muhimu zaidi) kwenye Utamaduni wa Kichina.

Ndiyo iwe Ndiyo!
Hapana iwe Hapana!

XIN Confucian inaibua tamaduni nyingine za Kichina ambazo ni Guanxi pamoja na Mianzi. Guanxi ni ujenzi wa Uhusiano Mzuri (Good Relationship or Friendship) ambao ni binafsi, wa kibiashara, wa kijamii, wa kisiasa, n.k. Namna bora ya kujenga Guanxi kwa Wachina ni kwa njia ya kukutana Uso kwa Uso kupitia vikao, mikutano, kutembeleana, kukaribishana, n.k.

Kutengeneza Guanxi ni mchakato wa muda mrefu; mfano ni ule niliowashauri CHADEMA kurudi kwa jamii kwenye andiko langu lililopita. Kujenga Guanxi kunachochea kuibuka kwa Mianzi (Face) Gaining.

Mianzi (Face) Gaining ni kitendo cha kufanya jitihada za kuleta neema na mambo yaliyo mema kwa mwingine ili kulinda 'Social Image' yake. Unapofanya mabaya kwa mwingine maana yake unaharibu 'Social Image' yake; na kwenye Utamaduni wa Kichina huitwa Mianzi (Face) Loosing; ambapo Mianzi Loosing hupelekea kubomoa Guanxi.

  • Unapomtukana mwingine hii katika Utamaduni wa Kichina ni Mianzi Loosing inayopelekea kubomoka kwa Guanxi.
  • Unapomzungumzia mwingine vizuri awe yupo au hayupo hii katika Utamaduni wa Kichina huitwa Mianzi Giving ambayo huoelekea Kujengeka kwa Guanxi.
  • Kama wewe ni mwanasiasa na hukufanya kile ulichoahidi kwa wanachi wako hii katika Utamaduni wa Kichina huitwa Mianzi Loosing ambayo hupelekea kubomoka kwa Guanxi.
  • Kama una rafiki yako na umeamua kumualika nyumbani kwako aje kula chakula cha jioni hii katika Utamaduni wa Kichina huitwa Mianzi Giving ambayo hupelekea kujengeka kwa Guanxi.

XIAO Confucian
Hii ni namna watoto na vijana wa Kichina napaswa kuwahudumia wazazi na wakubwa wengine kwenye familia na jamii zao. Kupitia tabia hii njema ya Xiao Confucian, Wachina hufundishwa kuwasikiliza wakubwa, kutumia lugha laini wazungumzapo na mkubwa, kuwasalimia wakubwa, kuwafariji wakubwa kwa maneno na vitendo hasa pale wanapopitia changamoto mbalimbali, kuwahudumia wakubwa kwa fedha na mahitaji mengine, heshima kwa wakubwa, n.k. katika familia na jamii zao.

WEN Confucian
Hii ni sanaa za amani ambazo hutumiwa ili kuleta maendeleo ya mtu binafsi. Confucius (Kong Fuzi) aliamini kuwa sanaa ina nguvu ya kubadili maisha ya mwanadamu. Katika Wen Confucian; sanaa zilizozungumziwa zaidi ni sanaa za Kiutamaduni za China kama via Calligraphy (Sanaa ya Uandishi wa Mkono kwa kutumia mwandiko mzuri), Music (Muziki), Numeracy (Namba au Hesabu), n.k.

Hitimisho
Mpaka sasa nchini Tanzania ipo Taasisi ya Kichina iitwayo Confucius inayopatikana kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM); iliyojikita katika kufundisha Lugha ya Kichina kwa Watanzania.
Ingawa taasisi hii imeleta nuru kwa kufundisha lugha iliyo katika nafasi za juu sana ulimwenguni kwa sasa; mapungufu ya taasisi hii ni kuwa haijachota elimu nzima-nzima iliyobeba maendeleo ya kiteknolojia yaliyofikiwa katika Nchi ya China na kuileta Tanzania, hivyo suluhu ni vyema kuanzisha Shule Binafsi za Mitaala ya Kichina nchini Tanzania.
No reform no election in Tanzania in 2025
 
Someni na CCM Manifesto 2020 - 2025 sio utaipenda tu, utapata mahaba kabisa na CCM, you will love it, na CCM ndio inafanya yale yote mazuri mno yaliyomo humo..!!

Mungu ibariki CCM idumu milele, Mungu mbariki Mh. Rais wetu, Mama yetu, Samia Suluhu Hassan 🙏🙏
 
Someni na CCM Manifesto 2020 - 2025 sio utaipenda tu, utapata mahaba kabisa na CCM, you will love it, na CCM ndio inafanya yale yaliyomo humo..!!

Mungu ibariki CCM idumu milele, Mungu mbariki Mh. Rais wetu, Mama yetu, Samia Suluhu Hassan 🙏🙏
Ni kweli japo CCM kwa advantage ya kuwa madarakani tayari nyingi zimeshatekelezeka, imenipasa kupitia ya Chama Kikuu cha Upinzani kwa sababu muda wa Ilani hii unakwenda ukingoni ikiwa haijatekelezeka hivyo nimeona niokote madini tusije kujikuta kama taifa tumeyatupa kwenye dustbin.
 
nimerudia maratano ccm hawana hiki kitu
Wanayo kwenye Sura ya Nne: Sayansi, Teknolojia na Ubunifu pia wameelezea haya ila kwa mfano kwenye kipengele cha kuwapeleka watanzania nje ya nchi kusomea masuala haya wametaja tu kwenye vyuo bora duniani hawakuwa specific ni kwenye taifa au mataifa yapi ili tufanye tathmini ya hapa na pale. Lakini pia wamezungumza kuhusu kuweka mazingira wezeshi ya kuwawezesha wataalam wa sayansi na teknolojia kutoka nje ya nchi kuja nchini; lakini hawajaweka wazi hususan kutoka taifa au mataifa gani. CHADEMA wao wamekuwa specific kuwa ni Asia hususan China.
 
Kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, ninapenda kuzungumzia kipengele kimoja kilichonivutia zaidi katika Ilani ya mwaka 2020-2025 ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA); Sura ya 16, Kifungu namba 16.1 Kipengele b (Ukurasa wa 95) ambacho kinasema:

"Katika kutimiza azma ya kujiendeleza katika sekta ya sayansi na teknolojia, Serikali ya Chadema itaweka mkazo katika kuimarisha mahusiano yanayolenga kuiwezesha Tanzania kuiga na kuchota maendeleo ya kiteknolojia yaliyofikiwa katika nchi za Asia na hasa China."

Kipengele hiki ni muhimu sana kwa taifa letu, kwani tunafahamu sote kuwa China ni taifa lililopiga hatua kubwa katika Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia duniani; yaliyopelekea uchumi wake kukua kwa kasi kubwa na kuwa imara zaidi.

Ingawa lengo hili lilitolewa na CHADEMA kupitia Ilani yake ya uchaguzi ya mwaka 2020-2025, lakini tukiamua kuweka kando vyama vyetu, dini zetu na ubaguzi wa aina yoyote ile tukabaki kuwa Watanzania ambao ni Wazalendo tunaolitakia mema taifa letu; haijalishi Ilani hii inakaribia kumaliza muda wake, lakini lengo hili linaweza kuhuishwa upya na kutekelezwa nasi sote kuanzia Serikali iliyopo madarakani, Chama Tawala (CCM), Mimi, Wewe, Watanzania, Taasisi, Mashirika, Vyama vya Upinzani na CHADEMA wenyewe haijalishi wako ndani au nje ya Serikali; kupitia SEKTA BINAFSI.

Ni uwekezaji wa aina gani unaweza kulifaa lengo hili?

  1. Eneo la kwanza la uwekezaji unaoweza kufanyika kupitia lengo hili ni kuanzisha shule binafsi za kimataifa (International Schools) zenye mitaala (mtaala) ya Kichina inayolenga sanaa, ubunifu, sayansi na teknolojia nchini Tanzania; kuanzia ngazi ya malezi (daycare), awali, msingi, sekondari mpaka elimu ya kati (college) kwani tayari tumekwishaona mitaala kutoka magharibi kama vile Cambridge na International Baccalaureate (IB) ikifanya kazi nchini.
  2. Eneo la pili la uwekezaji unaoweza kufanyika kupitia lengo hili ni kuwekeza katika Uandishi Bunifu na kuandika vitabu vipya kwa Lugha ya Kiswahili vyenye kuelezea na kuvumbua siri za mafanikio ya China pamoja na bunifu mbalimbali zinazofanyika nchini humo kama vitabu vya ziada kwa wanafunzi ambao hawataweza kusoma katika shule zilizoelezewa katika kipengele namba 1 lakini pia vitabu vinavyoweza kusomwa na mtu yeyote kwenye jamii ya Tanzania.
  3. Eneo la tatu la uwekezaji unaoweza kufanyika kupitia lengo hili ni kutafsiri vitabu vya Historia ya China na Vitabu vya Taguchi za Kichina vilivyopo katika lugha ya Kichina ili viwe katika Lugha ya Kiswahili kama vitabu vya ziada kwa wanafunzi ambao hawataweza kusoma katika shule zilizoelezewa katika kipengele namba 1 lakini pia vitabu vinavyoweza kusomwa na mtu yeyote kwenye jamii ya Tanzania.

Taguchi ni nini?

Taguchi ni njia za kitakwimu ambazo zilivumbuliwa na Mjapani aitwaye Genichi Taguchi ili kuongeza thamani ya ubora (quality) wa ubunifu wa bidhaa zinazozalishwa viwandani na katika nyanja mbalimbali kama vile Uhandisi, Bioteknolojia, Masoko, TEHAMA, Mawasiliano, Uchukuzi, n.k.

Sababu ya mimi kuona kuwa maeneo haya matatu yanafaa zaidi katika uwekezaji huu ni kutokana na Elimu, Ujuzi na Maarifa kuwa moja kati ya nyenzo kuu zilizowafanya Wachina wapige hatua kubwa kwenye Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia kisha Uchumi duniani.

Mfano; kupitia Falsafa ya Kichina iitwayo CONFUCIANISM iliyoanzishwa na 'Kong Qiu' au 'Zhong Ni' maarufu kama Master Kong, Kong Fuzi au Confucius (551-479 BCE) inayotumika kwenye nyanja maalum nchini humo ambazo ni Utamaduni, Jamii, Biashara na Siasa.

Confucianism ni nini?
Confucianism ni Falsafa ya Kichina yenye lengo la kurejesha, kujaza, kuhamasisha na kuimarisha tabia njema kwenye jamii ya Kichina; ili kuibua matokeo mema na chanya kwenye jamii za Kichina yatakayojidhihirisha dunia nzima. Hakika leo hii sote tunashuhudia mema haya yaletwayo na taifa la China. Falsafa hii ya Kichina inafundisha kuhusu tabia njema mbalimbali kama ifuatavyo:-

REN Confucian
Upendo, Utu na Huruma

YI Confucian
Haki na Kufanya Matendo ya Haki

LI Confucian
Kuwa na mpangilio mzuri wa jambo unalofanya ikiwemo kufuata kanuni au mfumo. (System or Proper Way)

ZHI Confucian
Kuyatafsiri Maarifa, Hekima, Ujuzi na Elimu uliyonayo haijalishi udogo au ukubwa wake; ili yatumike katika kufanya maamuzi sahihi, kujua lipi ni sahihi na lipi si sahihi, kufanya ubunifu (innovation), kuwaza kwa hekima, kufanya uchambuzi na ku-judge mambo kwa hekima.

Kwa tafsiri rahisi, ZHI ni Hekima kwa Vitendo; ku-apply kile ulichonacho kwa kufanya kitu kipya. Hii imepelekea Wachina kuwa watu wenye uthubutu wa kufanya mambo makubwa zaidi duniani.

XIN Confucian
Katika Falsafa ya Kichina; XIN ni Ukweli, Uaminifu na Kutovunja Ahadi. Maneno yaliyonyooka, matendo yaliyonyooka pasipo kupepesa macho na kufanya kile ulichoahidi kufanya ni sehemu ya Utamaduni wa Kichina.

Xin inajenga urafiki, uhusiano na inasimama kama tabia moyo (muhimu zaidi) kwenye Utamaduni wa Kichina.

Ndiyo iwe Ndiyo!
Hapana iwe Hapana!

XIN Confucian inaibua tamaduni nyingine za Kichina ambazo ni Guanxi pamoja na Mianzi. Guanxi ni ujenzi wa Uhusiano Mzuri (Good Relationship or Friendship) ambao ni binafsi, wa kibiashara, wa kijamii, wa kisiasa, n.k. Namna bora ya kujenga Guanxi kwa Wachina ni kwa njia ya kukutana Uso kwa Uso kupitia vikao, mikutano, kutembeleana, kukaribishana, n.k.

Kutengeneza Guanxi ni mchakato wa muda mrefu; mfano ni ule niliowashauri CHADEMA kurudi kwa jamii kwenye andiko langu lililopita. Kujenga Guanxi kunachochea kuibuka kwa Mianzi (Face) Gaining.

Mianzi (Face) Gaining ni kitendo cha kufanya jitihada za kuleta neema na mambo yaliyo mema kwa mwingine ili kulinda 'Social Image' yake. Unapofanya mabaya kwa mwingine maana yake unaharibu 'Social Image' yake; na kwenye Utamaduni wa Kichina huitwa Mianzi (Face) Loosing; ambapo Mianzi Loosing hupelekea kubomoa Guanxi.

  • Unapomtukana mwingine hii katika Utamaduni wa Kichina ni Mianzi Loosing inayopelekea kubomoka kwa Guanxi.
  • Unapomzungumzia mwingine vizuri awe yupo au hayupo hii katika Utamaduni wa Kichina huitwa Mianzi Giving ambayo hupelekea Kujengeka kwa Guanxi.
  • Kama wewe ni mwanasiasa na hukufanya kile ulichoahidi kwa wanachi wako hii katika Utamaduni wa Kichina huitwa Mianzi Loosing ambayo hupelekea kubomoka kwa Guanxi.
  • Kama una rafiki yako na umeamua kumualika nyumbani kwako aje kula chakula cha jioni hii katika Utamaduni wa Kichina huitwa Mianzi Giving ambayo hupelekea kujengeka kwa Guanxi.

XIAO Confucian
Hii ni namna watoto na vijana wa Kichina wanapaswa kuwahudumia wazazi na wakubwa wengine kwenye familia na jamii zao. Kupitia tabia hii njema ya Xiao Confucian, Wachina hufundishwa kuwasikiliza wakubwa, kutumia lugha laini wazungumzapo na mkubwa, kuwasalimia wakubwa, kuwafariji wakubwa kwa maneno na vitendo hasa pale wanapopitia changamoto mbalimbali, kuwahudumia wakubwa kwa fedha na mahitaji mengine, heshima kwa wakubwa, n.k. katika familia na jamii zao.

WEN Confucian
Hii ni sanaa za amani ambazo hutumiwa ili kuleta maendeleo ya mtu binafsi. Confucius (Kong Fuzi) aliamini kuwa sanaa ina nguvu ya kubadili maisha ya mwanadamu. Katika Wen Confucian; sanaa zilizozungumziwa zaidi ni sanaa za Kiutamaduni za China kama via Calligraphy (Sanaa ya Uandishi wa Mkono kwa kutumia mwandiko mzuri), Music (Muziki), Numeracy (Namba au Hesabu), n.k.

Hitimisho
Mpaka sasa nchini Tanzania ipo Taasisi ya Kichina iitwayo Confucius inayopatikana kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM); iliyojikita katika kufundisha Lugha ya Kichina kwa Watanzania.

Ingawa taasisi hii imeleta nuru kwa kufundisha lugha iliyo katika nafasi za juu sana ulimwenguni kwa sasa; mapungufu ya taasisi hii ni kuwa haijachota elimu nzima-nzima iliyobeba maendeleo ya kiteknolojia yaliyofikiwa katika Nchi ya China na kuileta Tanzania, hivyo suluhu ni vyema kuanzisha Shule Binafsi za Mitaala ya Kichina na kuzalisha vitabu vinavyohusu China kwa Lugha ya Kiswahili nchini Tanzania.
Kweli mkuu
 
Hapana ndugu yangu, sote tu watu wa taifa la Tanzania. #uzalendokwanza
Utakuwa wewe ni mgonjwa asee, kama CCM ni watu wangeiba mali za umma huku masikini wanakufa kwa kukosa madawa n.k? leo nimeangalia Star TV mzee mmoja anahangaika(alikuwa analia hana hela) na kipofu cha mkojo tangu 2021 amekosa 3M za upasuaji lakini maza katanga kununua kila goli la Simba kwa milioni 30? kwa hiyo goli ni muhimu kuliko uhai wa walipa kodi? achana na CCM ni mashetani tupu hayana utu, kama na wewe ni CCM ulaaniwe wewe na uzao wako wote
 
Utakuwa wewe ni mgonjwa asee, kama CCM ni watu wangeiba mali za umma huku masikini wanakufa kwa kukosa madawa n.k? leo nimeangalia Star TV mzee mmoja anahangaika(alikuwa analia hana hela) na kipofu cha mkojo tangu 2021 amekosa 3M za upasuaji lakini maza katanga kununua kila goli la Simba kwa milioni 30? kwa hiyo goli ni muhimu kuliko uhai wa walipa kodi? achana na CCM ni mashetani tupu hayana utu, kama na wewe ni CCM ulaaniwe wewe na uzao wako wote
Kwanza, Mimi si mgonjwa ushindwe kwa JINA LA YESU.

Mbili mimi ni mwanajamii siko upande wa chama chochote hivyo usinilazimishe kuwatukana CCM wala CHADEMA.

Tatu, nitoe pole kwa huyo mgonjwa naamini MUNGU Atafanya njia kwa wakati wake.

Nne laana isiyo na sababu haimpati mtu NENO LA MUNGU LINASEMA.

Tano, nikutakie jioni njema.
 
Kwanza, Mimi si mgonjwa ushindwe kwa JINA LA YESU.

Mbili mimi ni mwanajamii siko upande wa chama chochote hivyo usinilazimishe kuwatukana CCM wala CHADEMA.

Tatu, nitoe pole kwa huyo mgonjwa naamini MUNGU Atafanya njia kwa wakati wake.

Nne laana isiyo na sababu haimpati mtu NENO LA MUNGU LINASEMA.

Tano, nikutakie jioni njema.
Usichangie vitu ambavyo huvijui, Mwamposa mama ake alimpeleka kutibiwa Uingereza, why alishindwa kumuombea? acheni kumjaribu MUNGU, lazima tutekeleze wajibu wetu na siyo kumjaribu MUNGU, ni bora kununua goli milioni 30 hata kama zitafungwa 10 badala ya kusaidia mgonjwa ambaye anateseka kwa miaka 5 anatembea na kopo la mkojo tena amekosa milioni 3 tu apone asaidie watoto wake 4? Israel ni taifa takatifu la Mungu lakini linapigana kujilinda na maadui, kwanini wasimuachie MUNGU? MUNGU amekupa akili ikusaidie.
 
Usichangie vitu ambavyo huvijui, Mwamposa mama ake alimpeleka kutibiwa Uingereza, why alishindwa kumuombea? acheni kumjaribu MUNGU, lazima tutekeleze wajibu wetu na siyo kumjaribu MUNGU, ni bora kununua goli milioni 30 hata kama zitafungwa 10 badala ya kusaidia mgonjwa ambaye anateseka kwa miaka 5 anatembea na kopo la mkojo tena amekosa milioni 3 tu apone asaidie watoto wake 4? Israel ni taifa takatifu la Mungu lakini linapigana kujilinda na maadui, kwanini wasimuachie MUNGU? MUNGU amekupa akili ikusaidie.
Sasa ndugu yangu unadhani MUNGU Anashindwa kumsaidia mtu yeyote? Akitaka hata sasa Anaweza kumuinulia mtu wa kumsaidia hata kama si Rais Samia na akapelekwa hata Uingereza, hivyo kumtegemea YEYE Ndiyo point ya msingi kuliko kuwanyooshea watu vidole kwani hata mimi na wewe pia ni wajibu wetu kumsaidia Mtanzania mwenzetu.
 
Back
Top Bottom