Chadema kusimamisha mgombea wa Urais 2010; si lazima Mbowe!

Huu ni unafiki wa hali ya juu toka kwa Mzee Mtei. Hivi kweli Mzee Mtei anaweza kutuambia kuwa hajui kuwa Mbowe hatagombea urais 2010? Ina maana yote yaliyoandikwa magazetini, JF n.k, ya Mbowe kurudi kwenye ubunge hakuyaona na kumfanya amuulize mkwe wake niaje?

Mtei anafahamu wazi kuwa mgombea uraisi haibuki tu bila kuwa amejijengea umaarufu. Walio maarufu CHADEMA either wanapigwa vita au hawagombei kwa sababu zisizojulikana.

Mbowe si maarufu tena ukiachilia kwa baadhi tu ya mashabiki wa CHADEMA. Kwa hiyo ni wazi kuwa kwenye ligi ya uraisi Mbowe hayumo tena na ndio maana ameamua kukimbilia kwenye ubunge ili ajijenge kwa ajili ya 2015.

Ni wazi pia kuwa, yeyote atakayewekwa kugombea 2010, atakuwa msindikizaji tu au mtu wa kupasha moto hicho kiti kinachoandaliwa na Mtei 2015 kwa ajili ya mkwe wake Mbowe.

Ndio maana wale vijana wengine wote ambao 2015 watakuwa tayari kwa uraisi na hivi sasa wanataka nafasi za uongozi ndani ya CHADEMA, k.m. Kafulila na Zitto, ambazo zingeweza kuwajenga ndani na nje ya chama kwa ajili ya kugombea uraisi, wanapigwa vita na Mzee Mtei na mkwe wake. Kwa Mzee Mtei uraisi ni wa Mbowe tu na atafanya lolote kumlinda mkwewe kwenye hilo. Hii ndiyo demokrasia ya sera ya majimbo.
Duh,kumbe kafulila ni presidential material kwako?
 
KubwaJinga,

Wewe jinga kubwa kweli, kum rate aliyekuwa ofisa habari, mtovu wa nidhamu eti ni presidential material.
 
Mkuu I don't like it but that is the fact. Niambie vyama vingapi vya upinzani vimewahi kusimamisha mgombea wa uraisi ambae siyo mwenyekiti wap. Niambie ni mara ngapi CCM raisi akawa mtu mmoja na mwenyekiti wa chama akawa mtu mwingine. Sasa kama kila mtu anafanya hivyo si vyema kuisolate chama kimoja kwa kufanya kitu hicho hicho. Kama hatupendi tabia ya mwenyekiti kuwa mgombea uraisi basi tukemee kwa vyama vyote.
Nachokumbuka mimi mwaka 2005 Mbowe akiwa mwenyekiti aliingia ktk uchaguzi wa mgombea Urais na kama sikosei mpinzani wake ktk uchaguzi wa ndani Chadema alikuwa mwanamke.
Nakumbuka sana nilikemea kitendo cha viongozi wengine kujichimbia au kupangwa matokeo kwa Mbowe kutokuwa na Mshindani wa nguvu hivyo kuto onyesha demokrasia ndani ya Chama. Na mwana JF, Eric Ongara tulipekana kichizi ktk mada hiyo..that was then..
Kwa hiyo ulinipa mshangao kusikia kwamba Chadema husimamisha mwenyekiti wake kama mgombea wa Urais wakati majuzi tu Zitto kasema Mgombea wa kiti cha Urais Chadema sii lazima awe mwenyekiti na kwamba yeye hata kama angechukua wenyekiti asingeweza kugombea Urais kutokana na umri wake..
Sasa sielewi nani anazungumza ukweli!
 
Swali! :mzee kuna taarifa kwamba binadamu hufa je wewe nawe unatarajia kufa.
Jibu! :Ndio, ni wajibu na itakapokuwa kwangu sina budi kuurudia udongo.
Kichwa cha habari front page :MZEE KUURUDIA UDONGO!!!
-Asema pia atakufa...
 
Our political culture is that of a chairman of a party running for president. Usually it is the party chairman who runs for president unless otherwise stated. So sioni ajabu hapa. Hata kwa CCM mgombea wao wa uraisi eventually anakua mwenyekiti wa chama.
Mzee Mwinyi, Mkapa,JK hawakuwa wenyeviti wa chama wakati wanagombea Urais.

Lipumba wakati anagombea 1995 hakuwa mwenyekiti wa CUF.
Seif Sharif Hamad mara zote anagombea sio mwenyekiti wa CUF.

Barack Obama sio Mwenyekiti wa Democratic.
David Cameroon sio Mwenyekiti wa Conservative.
Gordon Brown sio Mwenyekiti wa Labour Party.
Tony Blair hakuwa Mwenyekiti wa Labour Party.
ujinga huu uko Chadema tu.
 
NIMESHINDWA KUELEWA KAULI YA MZEE WA CHADEMA MTEI KUWA KAMA MBOWE HATAGOMBEA URAIS 2010,BASI ATATAFUTWA MGOMBEA MWINGINE KWA AJIRI YA NAFASI YA URAIS 2010.

HIVI CHADEMA TAYARI MNA MTU AMBAYE ANA HAKI YA KUWA MGOMBEA URAIS BILA KUPITISHWA NA KIKAO CHOCHOTE CHA WANACHAMA WA CHADEMA, ZAIDI YA RIDHAA YA MZEE MTEI?

MKISOMA MWANACHI MTAONA HABARI YOTE.
http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=16147
Kanda2
kweli wewe kichwa maji.
Mzee Mtei hajasema kwamba Mbowe ana haki ya kugombea Urais mwakani na wengine hawana.Wote tunafahamu kwamba Mbowe ndiye aliyegombea 2005 na tulitarajiandiye angegombea 2010 na ndio maana hata humu JF hili limekuwa likijadiliwa sana na hata wengine kushauri Dk Slaa ndio agombee 2010 kwani yeye ana haki peke yake? Na hata kwa upande wa chama chako CCM tunafahamu JK ndiye atakayegombea 2010 kwani yeye ana haki?Acha uvivu wa kufikiri Bwana Mkubwa.
Kila mmoja ana haki ilimradi tu atimize matakwa ya kikatiba ya chama husika na ya nchi pia.[/QUOTE]
CCM ATAGOMBEA JOHN SHIBUDA AMESHATANGAZA.HUO USULTAN WA MTU KUOGOPWA UKO CHADEMA TU.
 
Mzee Mtei ametamka kwamba Chadema kuna wanachama wanaoweza kugombea urais endapo Freeman Mbowe hatataka kusimama. Mbona wanaJF wengine mnafadhaishwa na kudhani huyu mzee ndiye analazimisha mambo? Anapenda chama alichoasisi kishinde, na hiyo ndiyo sababu ya kumheshimu.

Kila Mtanzania ana haki ya kuwa na jina la kiongozi anayem rate kuwa ataweza kuongoza nchi. Hata Kanda2 ana haki hiyo. Kwa hiyo Mzee Mtei ana mtu au watu katika Chadema anaowa rate ni presidential material hata kama mkwewe Freeman hatasimama.
kweli kabisa Mzee huyu anamchezo wa kulazimisha na kuwazuia wagombea wenye uwezo.
kamzuia Zitto Kabwe.
kalazimisha Kafulila afukuzwe.
 
Mzee Mwinyi, Mkapa,JK hawakuwa wenyeviti wa chama wakati wanagombea Urais.

Lipumba wakati anagombea 1995 hakuwa mwenyekiti wa CUF.
Seif Sharif Hamad mara zote anagombea sio mwenyekiti wa CUF.

Barack Obama sio Mwenyekiti wa Democratic.
David Cameroon sio Mwenyekiti wa Conservative.
Gordon Brown sio Mwenyekiti wa Labour Party.
Tony Blair hakuwa Mwenyekiti wa Labour Party.
ujinga huu uko Chadema tu.

Mkuu soma vizuri post yangu. Kuhusu CCM nilisema wagombea wao wanaishia kuwa wenyekiti. Au sija sema hivyo? Na hao wagombea wa nje ya nchi hawana nafasi kwa sababu mimi naongelea kwa tanzania.
 
Back
Top Bottom