Na Hemed Kivuyo, Arusha
MUASISI wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema), Edwin Mtei amesema kuwa endapo mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe hatagombea urais mwaka 2010 basi chama hicho kitamsimamisha mgombea mwingine ambaye atakuwa imara kama alivyo Mbowe.
Mtei aliyasema hayo hivi karibuni alipokuwa akizungumza na Mwananchi Jumapili, nyumbani kwake nje kidogo ya Arusha mjini.
Alisema hayo mara baada ya kuulizwa mustakabali wa chama hicho kumpata mgombea wa kiti cha urais huku aliyetarajiwa kugombea kiti hicho, Freeman Mbowe kutaka kugombea ubunge katika moja ya majimbo mkoani Kilimanjaro .
Mtei alisema kuwa kama mwenyekiti huyo ameamua au ataamua kugombea kiti cha ubunge anaamini kuwa ndani ya chama hicho kuna hazina ya viongozi `weledi` ambao hawapatikani katika chama kingine cha siasa hapa nchini.
``Endapo Mbowe atagombea kiti cha ubunge nitamuunga mkono na kwenda kumpigia kampeni kwa kuwa naamini ni kiongozi mwenye uwezo wa kuongoza katika nyanja mbalimbali kutokana na uzoefu alioupata katika siasa nchini,``alisema.
Alisema kuwa kutokana na taarifa hizo, wananchi wasishangae kuona chama hicho kikimsimamisha kiongozi mwingine atayegombea kiti cha urais na kwamba atakuwa na uwezo wa kuongoza nchi na kutekeleza ilani ya chama hicho.
Alisema kuwa pamoja na hayo nia ya chama hicho kwa sasa ni kuongeza nguvu bungeni, kwa kuwa na idadi kubwa ya wabunge ambao watawapigania Watanzania katika kukiondoa chama tawala CCM na kupigania maslahi ya taifa zima.
''Mimi naamini ndani ya Chadema kuna hazina kubwa ya viongozi shupavu na kama Mbowe atagombea ubunge pia tunampa nguvu kwa kuwa ana uwezo mkubwa wa kuongoza na wananchi wasiwe na wasiwasi nia yetu ni moja na tutawapa mgombea urais shupavu,'' alisema Mtei.
NIMESHINDWA KUELEWA KAULI YA MZEE WA CHADEMA MTEI KUWA KAMA MBOWE HATAGOMBEA URAIS 2010,BASI ATATAFUTWA MGOMBEA MWINGINE KWA AJIRI YA NAFASI YA URAIS 2010.
HIVI CHADEMA TAYARI MNA MTU AMBAYE ANA HAKI YA KUWA MGOMBEA URAIS BILA KUPITISHWA NA KIKAO CHOCHOTE CHA WANACHAMA WA CHADEMA, ZAIDI YA RIDHAA YA MZEE MTEI?
MKISOMA MWANACHI MTAONA HABARI YOTE.
http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=16147
MUASISI wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema), Edwin Mtei amesema kuwa endapo mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe hatagombea urais mwaka 2010 basi chama hicho kitamsimamisha mgombea mwingine ambaye atakuwa imara kama alivyo Mbowe.
Mtei aliyasema hayo hivi karibuni alipokuwa akizungumza na Mwananchi Jumapili, nyumbani kwake nje kidogo ya Arusha mjini.
Alisema hayo mara baada ya kuulizwa mustakabali wa chama hicho kumpata mgombea wa kiti cha urais huku aliyetarajiwa kugombea kiti hicho, Freeman Mbowe kutaka kugombea ubunge katika moja ya majimbo mkoani Kilimanjaro .
Mtei alisema kuwa kama mwenyekiti huyo ameamua au ataamua kugombea kiti cha ubunge anaamini kuwa ndani ya chama hicho kuna hazina ya viongozi `weledi` ambao hawapatikani katika chama kingine cha siasa hapa nchini.
``Endapo Mbowe atagombea kiti cha ubunge nitamuunga mkono na kwenda kumpigia kampeni kwa kuwa naamini ni kiongozi mwenye uwezo wa kuongoza katika nyanja mbalimbali kutokana na uzoefu alioupata katika siasa nchini,``alisema.
Alisema kuwa kutokana na taarifa hizo, wananchi wasishangae kuona chama hicho kikimsimamisha kiongozi mwingine atayegombea kiti cha urais na kwamba atakuwa na uwezo wa kuongoza nchi na kutekeleza ilani ya chama hicho.
Alisema kuwa pamoja na hayo nia ya chama hicho kwa sasa ni kuongeza nguvu bungeni, kwa kuwa na idadi kubwa ya wabunge ambao watawapigania Watanzania katika kukiondoa chama tawala CCM na kupigania maslahi ya taifa zima.
''Mimi naamini ndani ya Chadema kuna hazina kubwa ya viongozi shupavu na kama Mbowe atagombea ubunge pia tunampa nguvu kwa kuwa ana uwezo mkubwa wa kuongoza na wananchi wasiwe na wasiwasi nia yetu ni moja na tutawapa mgombea urais shupavu,'' alisema Mtei.
NIMESHINDWA KUELEWA KAULI YA MZEE WA CHADEMA MTEI KUWA KAMA MBOWE HATAGOMBEA URAIS 2010,BASI ATATAFUTWA MGOMBEA MWINGINE KWA AJIRI YA NAFASI YA URAIS 2010.
HIVI CHADEMA TAYARI MNA MTU AMBAYE ANA HAKI YA KUWA MGOMBEA URAIS BILA KUPITISHWA NA KIKAO CHOCHOTE CHA WANACHAMA WA CHADEMA, ZAIDI YA RIDHAA YA MZEE MTEI?
MKISOMA MWANACHI MTAONA HABARI YOTE.
http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=16147