CHADEMA Kumuondoa Lema Arusha

CHADEMA Kumuondoa Lema Arusha

Soma habari vizuri, LEMA anaondolewa na wana CHADEMA wenzie! CCM haihusiki hapa.

CCM kazi yake ni kuwaletea maendeleo watanzania sio kupiga porojo za kisiasa.
hahaha!!! porojo kama za nape vuvuzela na ashumpter mshama?
 
lema sio riziki

Et hugochavez fyuuuuu!! hugo gani ww una akili za nyuma ya makal.o,acha kutumia majina ya watu wanaojielewa kwa kuwa na akili finyu kama piritoni.

Watanzania tumeichoka nyinyiemu hata mwalimu JK nyerere mzimu wake unatuongoza kuwa tuachane nayo.Kilichobaki ni kulazimisha kutawala,kitu ambacho kina mwisho amini hivo.Mwisho upo tu wa kulazimisha kutawala.
 
[JFMP3][/JFMP3]

Jamani hivi umpigaji ramli si umeshakatazwa na serikali?huyu msalani anapiga ramli mchana kweupe haogopi sheria au sheria zetu zina double standards.
 
Wanajamvi! Amani idumu Tanzania!


Hizi ni habari zenye uhakika 100% nilizozipata kutoka ndani ya CHADEMA na zikathibitishwa na mmoja wa viongozi wakuu hapa mkoani.

CHADEMA kupitia mwenyekiti wao wameongea na Mbunge wa Arusha mjini Bw Godbless J Lema na kumuomba asigombee tena ubunge wa jimbo la Arusha mjini kupitia chama hicho.

Habari zaidi zinasema, CHADEMA wamefikia hatua hiyo baada ya kugundua kuwa wakazi wa Arusha mjini hawana tena Imani na Bw.Lema baada ya LEMA kushindwa kutimiza karibia asilimia 98 ya ahadi zake kwa wana Arusha, Kwahiyo kama angegombea angeshindwa vibaya na hivyo kuwa ni aibu kwa chama hicho, ukichukulia kuwa wameshatangaza kuwa Arusha mjini ni ngome yao.

Suala lingine lililosababisha CHADEMA kumuondoa LEMA ni hili la wanachama wengi wa CHADEMA ambao nao ni viongozi katika ngazi za chini kuonyesha wazi kupingana na uongozi wa Mbunge huyu! Kwa mfano kijana wa CHADEMA siku nyingi Bw.Noel Ole Veroya kutangaza Nia ya kumn'goa LEMA Arusha. Hali hii imechangiwa kwa kiasi kikubwa na siasa za fujo alizosiasisi Ndg.Lema.

Suala la Ukabila nalo Limechukua nafasi yake, kwani Bw.Noel ametajwa kuwa ni mzawa wa Arusha huku Godbless LEMA akishawishiwa akagombee Jimbo la HAI(Nyumbani kwao) kwani Mbowe anatarajiwa kuhamia jimbo la Moshi mjini.

Pia CHADEMA imemtoa wasiwasi Bw.LEMA kwamba iwapo atakosa nafasi ya Ubunge watampa cheo kama kile cha NAPE, kwahiyo hatakufa njaa hapa mjini.

Wapiga Kura wengi wa Arusha mjini wamefurahishwa na habari hizi kwani wengi wao wamechoshwa na vituko vya Mh.LEMA na sasa wanataka maendeleo.

Inaelekea Godbless Lema ni kiboko ya CCM Arusha.Tanzania hatuna UKABILA,hebu iangalie hii hoja yako ilivyojaa UKABILA huna hata AIBU.................Pole sana Lema Godbless ndiyo chaguo letu..............
 
Wanajamvi! Amani idumu Tanzania!


Hizi ni habari zenye uhakika 100% nilizozipata kutoka ndani ya CHADEMA na zikathibitishwa na mmoja wa viongozi wakuu hapa mkoani.

CHADEMA kupitia mwenyekiti wao wameongea na Mbunge wa Arusha mjini Bw Godbless J Lema na kumuomba asigombee tena ubunge wa jimbo la Arusha mjini kupitia chama hicho.

Habari zaidi zinasema, CHADEMA wamefikia hatua hiyo baada ya kugundua kuwa wakazi wa Arusha mjini hawana tena Imani na Bw.Lema baada ya LEMA kushindwa kutimiza karibia asilimia 98 ya ahadi zake kwa wana Arusha, Kwahiyo kama angegombea angeshindwa vibaya na hivyo kuwa ni aibu kwa chama hicho, ukichukulia kuwa wameshatangaza kuwa Arusha mjini ni ngome yao.

Suala lingine lililosababisha CHADEMA kumuondoa LEMA ni hili la wanachama wengi wa CHADEMA ambao nao ni viongozi katika ngazi za chini kuonyesha wazi kupingana na uongozi wa Mbunge huyu! Kwa mfano kijana wa CHADEMA siku nyingi Bw.Noel Ole Veroya kutangaza Nia ya kumn'goa LEMA Arusha. Hali hii imechangiwa kwa kiasi kikubwa na siasa za fujo alizosiasisi Ndg.Lema.

Suala la Ukabila nalo Limechukua nafasi yake, kwani Bw.Noel ametajwa kuwa ni mzawa wa Arusha huku Godbless LEMA akishawishiwa akagombee Jimbo la HAI(Nyumbani kwao) kwani Mbowe anatarajiwa kuhamia jimbo la Moshi mjini.

Pia CHADEMA imemtoa wasiwasi Bw.LEMA kwamba iwapo atakosa nafasi ya Ubunge watampa cheo kama kile cha NAPE, kwahiyo hatakufa njaa hapa mjini.

Wapiga Kura wengi wa Arusha mjini wamefurahishwa na habari hizi kwani wengi wao wamechoshwa na vituko vya Mh.LEMA na sasa wanataka maendeleo.
Sogea karibu na hapo ulipo siku yoyote jioni nikununulie supu ya Makongoro hapa jirani na unapokaaga, kwakua naona unaupungufu wa Bonn marrow!
 
Wanajamvi! Amani idumu Tanzania!


Hizi ni habari zenye uhakika 100% nilizozipata kutoka ndani ya CHADEMA na zikathibitishwa na mmoja wa viongozi wakuu hapa mkoani.

CHADEMA kupitia mwenyekiti wao wameongea na Mbunge wa Arusha mjini Bw Godbless J Lema na kumuomba asigombee tena ubunge wa jimbo la Arusha mjini kupitia chama hicho.

Habari zaidi zinasema, CHADEMA wamefikia hatua hiyo baada ya kugundua kuwa wakazi wa Arusha mjini hawana tena Imani na Bw.Lema baada ya LEMA kushindwa kutimiza karibia asilimia 98 ya ahadi zake kwa wana Arusha, Kwahiyo kama angegombea angeshindwa vibaya na hivyo kuwa ni aibu kwa chama hicho, ukichukulia kuwa wameshatangaza kuwa Arusha mjini ni ngome yao.

Suala lingine lililosababisha CHADEMA kumuondoa LEMA ni hili la wanachama wengi wa CHADEMA ambao nao ni viongozi katika ngazi za chini kuonyesha wazi kupingana na uongozi wa Mbunge huyu! Kwa mfano kijana wa CHADEMA siku nyingi Bw.Noel Ole Veroya kutangaza Nia ya kumn'goa LEMA Arusha. Hali hii imechangiwa kwa kiasi kikubwa na siasa za fujo alizosiasisi Ndg.Lema.

Suala la Ukabila nalo Limechukua nafasi yake, kwani Bw.Noel ametajwa kuwa ni mzawa wa Arusha huku Godbless LEMA akishawishiwa akagombee Jimbo la HAI(Nyumbani kwao) kwani Mbowe anatarajiwa kuhamia jimbo la Moshi mjini.

Pia CHADEMA imemtoa wasiwasi Bw.LEMA kwamba iwapo atakosa nafasi ya Ubunge watampa cheo kama kile cha NAPE, kwahiyo hatakufa njaa hapa mjini.

Wapiga Kura wengi wa Arusha mjini wamefurahishwa na habari hizi kwani wengi wao wamechoshwa na vituko vya Mh.LEMA na sasa wanataka maendeleo.
Nyie kaeni hapo chini mkijidanganya!
 
Wanajamvi! Amani idumu Tanzania!


Hizi ni habari zenye uhakika 100% nilizozipata kutoka ndani ya CHADEMA na zikathibitishwa na mmoja wa viongozi wakuu hapa mkoani.

CHADEMA kupitia mwenyekiti wao wameongea na Mbunge wa Arusha mjini Bw Godbless J Lema na kumuomba asigombee tena ubunge wa jimbo la Arusha mjini kupitia chama hicho.

Habari zaidi zinasema, CHADEMA wamefikia hatua hiyo baada ya kugundua kuwa wakazi wa Arusha mjini hawana tena Imani na Bw.Lema baada ya LEMA kushindwa kutimiza karibia asilimia 98 ya ahadi zake kwa wana Arusha, Kwahiyo kama angegombea angeshindwa vibaya na hivyo kuwa ni aibu kwa chama hicho, ukichukulia kuwa wameshatangaza kuwa Arusha mjini ni ngome yao.

Suala lingine lililosababisha CHADEMA kumuondoa LEMA ni hili la wanachama wengi wa CHADEMA ambao nao ni viongozi katika ngazi za chini kuonyesha wazi kupingana na uongozi wa Mbunge huyu! Kwa mfano kijana wa CHADEMA siku nyingi Bw.Noel Ole Veroya kutangaza Nia ya kumn'goa LEMA Arusha. Hali hii imechangiwa kwa kiasi kikubwa na siasa za fujo alizosiasisi Ndg.Lema.

Suala la Ukabila nalo Limechukua nafasi yake, kwani Bw.Noel ametajwa kuwa ni mzawa wa Arusha huku Godbless LEMA akishawishiwa akagombee Jimbo la HAI(Nyumbani kwao) kwani Mbowe anatarajiwa kuhamia jimbo la Moshi mjini.

Pia CHADEMA imemtoa wasiwasi Bw.LEMA kwamba iwapo atakosa nafasi ya Ubunge watampa cheo kama kile cha NAPE, kwahiyo hatakufa njaa hapa mjini.

Wapiga Kura wengi wa Arusha mjini wamefurahishwa na habari hizi kwani wengi wao wamechoshwa na vituko vya Mh.LEMA na sasa wanataka maendeleo.

[h=3]WARAKA WA TATU WA LEMA KWA RAIS KIKWETE[/h]






Mh Rais Nakusalimu .
Wakati mwingine unapaswa kupewa pole na kuombewa na kufanyiwa dua kwani wewe ndie unatumikia ofisi kubwa kuliko zote Nchini na wakati huo huo unapaswa kupewa hongera kufikia malengo yako hayo ya kutumikia ofisi kubwa na ya Heshima kuliko zote Nchini , nimekuwa nikitafakari sana suala la Udini katika Taifa letu na huko Nyuma mwaka jana nilikuandikia pia waraka kuonya na kukumbusha hatua mathubuti kabla mambo hayajaaribika sijui kama ulisoma lakini naamini Usalama wa Taifa ambao siku hizi wanatumikia CCM watakuwa walisoma na Nape na wenzake pia walipata fursa ya kuusoma .


Mh Rais katika waraka hule nilisema hivi “ Mh Rais Taifa linahitaji Tiba “ siwezi leo kuandika kile nilichosema katika waraka ule ila niliweza kubashiri sumu ya udini inayoendelea katika Taifa lako na
langu, Mh Rais , ukweli nakwambia ukifanya mchezo kidogo sana Taifa hili linapotea likiwa mikononi mwako kwani hali ya Nchi sio nzuri hata kidogo na watu waliokuwa wanaishi kwa umoja na upendo sasa wanaanza kutafuta mbinu za kugombana na kuuwana.


Mh Rais, Siasa ya Udini na Ukanda makusudi yake yalikuwa kudhoofisha vyama vya upinzani na yalifanikiwa kwa baadhi ya vyama kudhoofishwa sana na mkakati huo unaendelea dhidi ya Chadema lakini kinachosikitisha ni kuwa wale waliobuni mkakati huo walishindwa kutafakari au kuona madhara yake mbele .


Mh Rais, mkakati wa kudhoofisha Chama cha Siasa kwa Udini na Ukanda hauishi tu kuangamiza hicho Chama bali kuwagawa Watu na Taifa kwa Ujumla , Mtu anapojaribu kusema Chadema ni Chama cha Wakristo kimsingi matamshi hayo hayaangamizi Chadema tu bali yanagawa Watu kwa matabaka ya Udini wao na na kufanya Dini moja iamini kuwa Dini nyingine ni mbaya na hivyo mpango huo unafanya Watu waanze kutazamana kwa Udini na Ukabila na matokeo yake ndiyo haya tunaanza kuyaona leo .
Mh Rais, Taifa linahitaji tiba , Hivi karibuni Waziri Mkuu alienda Geita kwenye mgogoro wa Waisilamu na Wakristo na niliona mawazo ya Waziri Mkuu kwenye vyombo vya habari na kwa kweli nilisikitika kwa
busara zile zilizokuwa zimejaa hofu kubwa . Tatizo lile lilianza na nani kati ya Mkristo na Muislamu anayepaswa kuchinja?


Mh Rais , Nilipoona jambo hili nilianza kujiuliza maswali mengi sana, kwanza , umakini huu kwa pande zote mbili juu ya jambo hili umeletwa na nini na nani? Kwani yako mambo mengi yaliyokatazwa na Biblia na Msaafu ambayo watu wote wa dini hizi mbili wamekataa kuyatii au kuyafuata , kwa mfano waislamu na wakristo vijana kwa wazee wanakunywa pombe pamoja baadhi yao kujenga mahusiano hata ya kimapenzi yasiyo rasmi bila hata kufuata utaratibu wa Msaafu wala Biblia lakini hapa hutaona ugomvi mkubwa sana japokuwa ni masuala yanayo mkera na kumuudhi mwenyezi Mungu sana.


Mh Rais , ndio maana katika suala hili la nani achinje kati ya Muislamu na Mkristo niliposikia maafa yake nikakumbuka waraka niliokuandikia mwaka jana kuhusu choko choko za Udini ambazo zimeanza
kuleta maafa ambazo Mwanzilishi wake ni CCM .


Mh Rais Chama chako unachokiongoza , Team yako imekuwa ikifanya sana propaganda hizi za, Udini , Ukabila , na Ukanda usiku na mchana , lakini nimekuwa nikikerwa sana na Jinsi kabila la Wachaga
linavyochukuliwa katika propaganda hizi na wanaofanya hivyo asilimia kubwa ni mashemeji wa Wachaga na mimi najiuliza wanaweza vipi kufanya Siasa za Ukanda na Ukabila wakati wao wenyewe ni familia moja ?


Kwa mfano , Mh Mwigulu Nchemba , Mh David Mathayo , Mh January Makamba , Mh Benjamin Mkapa , Mh Fredrik Sumaye , Mh Theo , Mh Dr Faustin Ndungulile , Mh Prof Ibrahimu Lipumba , Pro Mahalu , Mh Dr Hamis Kigwangala , Mh John Mgufuli , Mh Sospeter Muhongo , Mh Jaji Warioba, Idd Simba, Mh Salmin Amour , na wengine wengi wote hawa wameoa Kilimanjaro . Sasa unajiuliza hawa wote ni Viongozi ndani ya CCM na wengine ndio mabingwa wa kufanya Siasa za Udini na Ukanda , je wake
zao ndani ya nyumba wanajisikiaje wanapoona waume zao wanatukana kabila za ndugu zao kwa sababu ya Siasa ? Hii ni hatari kubwa Mh Rais kama kuchinja ni suala zito kiasi hicho katika Imani ya Kiislamu na pia ni neno kutoka katika Kitabu cha Imani yao basi ni haki na kweli kuwa wao wanapaswa kuchinja kwa Imani ya Dini yao na wala wasilazimishwe kumkosea Mungu wao kwani hakuna maarifa na Busara
inayozidi imani, lakini vile vile Wakristo wasilazimishwe kushiriki Ibada ambayo sio yao. Waislamu kama wanaamini kuwa wao kuchinja ndio jambo lililoamrishwa katika vitabu vyao basi sasa Jambo hilo liheshimiwe na kutafutiwa utaratibu na vile vile Wakristo wasipuuzwe kugoma kushiriki jambo ambalo kwa wengine lina sura ya Imani.


Nini Kifanyike?


Kwanza Chama chako na Viongozi wake uwakanye na kuwashauri mara moja kabisa kuacha propaganda za udini na ukanda , kwani katika hili hakuna namna Nchi inaweza kubaki salama , kwani hizo choko choko hazitokani na nia mbaya ya Waislamu na Wakristo bali ni siasa chafu iliyopandikizwa ili kuangamiza vyama vya Siasa na sasa imekwenda zaidi na imeanza kuwatesa wakati ambao Nchi ina matatizo mengi , Kwa mfano Chadema tulipoandama Arusha kupinga Uchaguzi wa Meya feki ,
Kiongozi mmoja wa Mkoa wa CCM hapa Arusha , alinukuliwa na vyombo vya habari akidai tunafanya maandamano hayo kwa sababu za Udini na ndio maana hatumtaki Meya , lakini kitu cha kushangaza huyu Meya Feki ni Mkristo tena Mchaga Kabila langu , lakini niliambiwa na tunampinga na Maaskofu wanampinga kwa sababu Chadema ni Chama cha Udini ‘ sasa najiuliza kama Meya huyu Feki ni Mchaga na ni Mkristo je hayo madai ya kijinga yanatoka wapi ? Kama Ukristo ni ajenda kubwa kwetu kwani
nini tulimpinga sasa ? Huu ni mfano mmoja iko mingi sana inayoashiria mkakati wa makusudi wa kuangamiza Chadema na huku mkisahau kuwa maliangamiza Taifa , na ndio Mkuu wa Mkoa wa Arusha alipokuja tu alidai kuwa amekuja kupambana na Chadema na Wachaga , ila nimuhakikishie hataweza na asijaribu kamwe na mikutano ambayo amekuwa akiifanya aiche mara moja .


Pili, Mh Rais, ninaamini kuwa wewe umesafiri Nchi mbali mbali kuliko mimi , Ukienda Marekani , Spain , Brazil , China , Hong Kong , UK, Italy , Sweden, Botswana , Namibia , South Afrika , Zimbabwe na Nchi
nyiongi utaona Maduka au Mabucha ya Nyama yameandikwa (Halal ) au unanua bidhaa yeyote ya aina ya Nyama na kukuta imeandikwa “Halal” na ni ustarabu kwamba bidhaa hiyo machinjio yake yamezingatia maadili ya Dini ya Kiislamu na Waislamu wenye Imani thabiti na Imani yao hapo ndipo watakapofanya manunuzi yao katika bidhaa hiyo ya aina ya Nyama. Lakini maeneno hayo hayo unaweza kupata nyama katika maduka mbali mbali yasiozingatia utaratibu huo na kwa hivyo watu wasiojali sana
masuala ya Imani wala hawatasumbuka kuuliza na kusoma kama Nyama hiyo imezingatia masuala ya matakwa ya Imani Fulani.


Hivyo, Mh Rais, nafikiri ni vyema utaratibu huu ukaletwa hapa kwetu ili tuonyeshe Kujali Imani ya Waislamu katika Jambo hili ambalo limekuwa kwazo katika Jamii hizi mbili kubwa na kama ufumbuzi wake hautakuwa kuzingatia hili basi tarajia uchungu kuendelea kutembea kwenye vifua vya watu bila kusema na siku moja hali inaweza kuwa mbaya na tukapoteza Taifa.


Mh Rais, naiona hofu isiyokuwa ya kweli ya Mh Waziri Mkuu kuwa tukiruhusu hilo kuwa Wakristo na Waislamu wataweza kutengana kwenye mambo mengine mengi haswa katika Biashara na mambo mengine , kitu ambacho nasema sio kweli kwani , Sukari ,Mchele , Soda na Juisi na bidhaa nyingi hazina makatazo na maelekezo katika Imani , Mfano kila Mkristo anajua kuwa Mwislamu hatumi Nguruwe na Nguruwe kwa mwislamu ni haramu na hivyo Mkristo hawezi kupika Nguruwe na huku akijua kuwa
wageni wake siku hiyo ni Waislamu.


Kwa hiyo hofu ya kuligawa Taifa kwa kurusu jambo hili haliwezi kutokea kwani ni miiko ya Kiimani ambayo pande zote zinapaswa kuheshimiana ili upande mmoja usione umekandamizwa na kupuuzwa , na hofu ya kibiashara inayoweza kutokea katika suala hili inapaswa kupuuzwa kwani IMANI ni zaidi ya Biashara japokuwa sioni jambo hili likitokea .


Mh Rais, nisikuchoshe sana, lakini haya ni maoni yangu na Mke wangu na sio Chama changu tumeamka leo Asubuhi tukasema tukuandikie tena kwani wewe ni Mkuu wa Nchi , Najua unaweza kuwa busy sana kusoma waraka huu mrefu ila najua Mwigulu na Nape lazima wausome na Rizwan pia hivyo niwaombe wakufikishe ujumbe huu kwa niaba ya familia yangu.


Mh Rais , We are pressed on every side by troubles, but not crushed and broken. We are perplexed because we don,t know why things happen as they do . But we don’t give up and quit, we are hunted down BUT God never abandons Us, We get knocked down BUT we get up again and keep going. The root of life need commitment and there’s a lot of suffer to get at the Climax. Don’t Give Up Mr President please, Help our Country now.


Godbless Jonathan Lema



 
Huu uchafu pelekea wakina Makonda pale lumumba[/QUOT

Huu uchafu ni wakwenu na unaotoka UFIPA, kwa hivyo kama umeshikwa na matapishi kamtapikie Slaa, ndiye kiongozi wa kumuondoa LEMA , akijua kuwa lema hatakiwi tena na wana Arusha.

Tusisahau Wachaga na Wamburu ndio wamekuwa wakazi wengi wa Arusha na ni wafanyi biashara wazuri sana, Siasa za Lema simewarudisha nyuma vibaya sana, hawamtaki na hawana imani naye hata kidogo.

Aondoke kesha iharibu ngome ya Chadema , na popote atakapopelekwa huyo ni MZIGO.
 
Wanajamvi! Amani idumu Tanzania!


Hizi ni habari zenye uhakika 100% nilizozipata kutoka ndani ya CHADEMA na zikathibitishwa na mmoja wa viongozi wakuu hapa mkoani.

CHADEMA kupitia mwenyekiti wao wameongea na Mbunge wa Arusha mjini Bw Godbless J Lema na kumuomba asigombee tena ubunge wa jimbo la Arusha mjini kupitia chama hicho.

Habari zaidi zinasema, CHADEMA wamefikia hatua hiyo baada ya kugundua kuwa wakazi wa Arusha mjini hawana tena Imani na Bw.Lema baada ya LEMA kushindwa kutimiza karibia asilimia 98 ya ahadi zake kwa wana Arusha, Kwahiyo kama angegombea angeshindwa vibaya na hivyo kuwa ni aibu kwa chama hicho, ukichukulia kuwa wameshatangaza kuwa Arusha mjini ni ngome yao.

Suala lingine lililosababisha CHADEMA kumuondoa LEMA ni hili la wanachama wengi wa CHADEMA ambao nao ni viongozi katika ngazi za chini kuonyesha wazi kupingana na uongozi wa Mbunge huyu! Kwa mfano kijana wa CHADEMA siku nyingi Bw.Noel Ole Veroya kutangaza Nia ya kumn'goa LEMA Arusha. Hali hii imechangiwa kwa kiasi kikubwa na siasa za fujo alizosiasisi Ndg.Lema.

Suala la Ukabila nalo Limechukua nafasi yake, kwani Bw.Noel ametajwa kuwa ni mzawa wa Arusha huku Godbless LEMA akishawishiwa akagombee Jimbo la HAI(Nyumbani kwao) kwani Mbowe anatarajiwa kuhamia jimbo la Moshi mjini.

Pia CHADEMA imemtoa wasiwasi Bw.LEMA kwamba iwapo atakosa nafasi ya Ubunge watampa cheo kama kile cha NAPE, kwahiyo hatakufa njaa hapa mjini.

Wapiga Kura wengi wa Arusha mjini wamefurahishwa na habari hizi kwani wengi wao wamechoshwa na vituko vya Mh.LEMA na sasa wanataka maendeleo.

JELA NI MAHALI PA KUISHI KAMA SABABU YA KWENDA HUKO NI VITA DHIDI YA UONEVU, UKANDAMIZAJI WA HAKI NA UTU WA BINADAMU.
412052743.jpg
Wapendwa wapiga kura wangu na Watanzania wenzangu. Sina wakati mgumu kuchukua maamuzi haya yanayotokea leo. Upendo huu nilio nao kwa watu wa Arusha na nchi yangu ni sababu ya msingi ya maamuzi haya. Nimetishwa mara nyingi, rafiki zangu wametishwa, jamii ya watu duni imeendelea kuishi kwa mashaka na matisho kwa muda mrefu.

Katika mazingira haya, nikawaza sana kuwa anatakiwa kutokea mtu mmoja jasiri atakayeweza kuona thamani ya watu wengine. Huyo mtu anaweza kuwa wewe lakini kwa wakati huu siwezi kumsubiri tena na nimechagua kuwa mimi nikiamini kuwa utanikuta nikiendelea na safari ya ukombozi.

Tupo wengi sana tunaotaka mabadiliko, haki na ukweli. Hata hivyo hofu, woga na mashaka yamepoteza thamani yetu yote ya maana ya kuishi.

Waliofungwa kwa kuonewa na kuteswa, waliokosa chakula na kulala nje, waliokwenda hospitali na kukosa madawa, waliokosa ajira na kipato mpaka kujikuta wametoroka familia zao, waliopoteza matumaini ya maisha, waliopora utajiri wa nchi yetu kwa manufaa yao binafsi, walionunua haki na sheria dhidi ya wajane na wanyonge na kuwapora vipato vyao vidogo na mashamba yao, USIULIZE SABABU NINI!

Nimetafakari sana na nikatambua kuwa sababu ni mimi pale nilipokuwa kimya wakati wajane na wanyonge wanaonewa.

NIliposikia wengine wanaandamana kupinga uovu, uonevu, wizi, ufisadi na ukandamizaji wa haki nikasema ni hao na wala sio mimi, kumbe nilipaswa kuwa mbele katika harakati hizi.

Nilipoona wenzangu hawawezi kupata matibabu nikasema mimi sio mgonjwa, nilipopata taarifa za rafiki zangu kufungwa kwa makosa yasiyo yao, nilipoona watoto wa mitaani wanaomba chakula, nilipoona wazee
wamepoteza matumaini ya kuishi katika uzee wao, nilipoona vijana hawana ajira, nilipoona mabinti wasichana wadogo wameamua kufanya biashara ya ukahaba, NIKATAFAKARI,TENA NIKATAFAKARI, dhahabu zetu, almasi yetu, Milima na mabonde yetu, Tanzaninte yetu, samaki wetu, Uranium yetu, makaa ya mawe yetu, utalii wetu, ardhi na kilimo chetu na zaidi utu na mahusiano yetu.

Na sasa siwezi kukaa kimya tena. NI afadhali vita inayotafuta haki na usawa kuliko amani inayopumbaza na kudhalilisha utu wa mwanadamu. Na katika msingi huu hofu na mashaka vimekosa thamani kwangu, sitamwogopa mtu yoyote, mwenye silaha yoyote, mwenye cheo chochote na wala sitaogopa jela yoyote katika kupigania haki, utu wa kweli katika jamii yangu.

Wanafikiri wataendelea kutuogopesha kwa sababu wana jela na silaha, wanafikiri tutaendelea kuabudu uoga, wanafikiri wataendela kutunyanyasabila sababu ya msingi LAKINI SISI TUNAJUA TUTASHINDA KWA SABABU HAKI TUNAYOIPIGANIA NI MAKUSUDI YA MWENYEZI MUNGU.

Leo nitakwenda jela kwa hiari yangu binafsi kwa siku kadhaa na si kwa NIA YA KUJITAFUTIA UTUKUFU WANGU bali ," JELA NI MAHALI PA KUISHI KAMA SABABU YA KWENDA HUKO NI VITA DHIDI YA UONEVU, UKANDAMIZAJI WA HAKI NA UTU WA BINADAMU.

Kila mara nilipotishiwa nikagundua wanaonitishia, wananitishia kwa jela na mauti. Na mimi nikagundua na nikatambua ni afadhali kuishi miaka hamsini jela huku sababu ikiwa ni kupinga uonevu na ukandamizaji kuliko maisha ya woga na anasa yasiyo na kusudi katika kutetea utu na heshima ya mwanadamu mwenzangu.

Wale mlionitishia kunipeleka jela sasa nimetangulia kwa hiari yangu na wale mliobaki msiogope jela endeleeni kupigania ukombozi utakaoleta usawa katika nchi yenu.

Watakaotubeza na kututukana wasameheni kwani wanahitaji ukombozi wa fikra, watakaotupongeza na kutuonea huruma wafundisheni ujasiri na waambieni mapambano bado yanaendelea tunahitaji umoja wao. Nitarudi mapema.

MSIOGOPE, MSIOGOPE, MSIOGOPE, MUNGU YUPO UPANDE WETU.

Hata kama sipo arusha, na si mwenyeji wa Arusha I wish we could have ten people like him, Tanzania yenye Neema Ingepatikana kwa vyovyote vile.........

Let him have long life and lets wait if he is going to behave contrary......

 
Wanajamvi! Amani idumu Tanzania!


Hizi ni habari zenye uhakika 100% nilizozipata kutoka ndani ya CHADEMA na zikathibitishwa na mmoja wa viongozi wakuu hapa mkoani.

CHADEMA kupitia mwenyekiti wao wameongea na Mbunge wa Arusha mjini Bw Godbless J Lema na kumuomba asigombee tena ubunge wa jimbo la Arusha mjini kupitia chama hicho.

Habari zaidi zinasema, CHADEMA wamefikia hatua hiyo baada ya kugundua kuwa wakazi wa Arusha mjini hawana tena Imani na Bw.Lema baada ya LEMA kushindwa kutimiza karibia asilimia 98 ya ahadi zake kwa wana Arusha, Kwahiyo kama angegombea angeshindwa vibaya na hivyo kuwa ni aibu kwa chama hicho, ukichukulia kuwa wameshatangaza kuwa Arusha mjini ni ngome yao.

Suala lingine lililosababisha CHADEMA kumuondoa LEMA ni hili la wanachama wengi wa CHADEMA ambao nao ni viongozi katika ngazi za chini kuonyesha wazi kupingana na uongozi wa Mbunge huyu! Kwa mfano kijana wa CHADEMA siku nyingi Bw.Noel Ole Veroya kutangaza Nia ya kumn'goa LEMA Arusha. Hali hii imechangiwa kwa kiasi kikubwa na siasa za fujo alizosiasisi Ndg.Lema.

Suala la Ukabila nalo Limechukua nafasi yake, kwani Bw.Noel ametajwa kuwa ni mzawa wa Arusha huku Godbless LEMA akishawishiwa akagombee Jimbo la HAI(Nyumbani kwao) kwani Mbowe anatarajiwa kuhamia jimbo la Moshi mjini.

Pia CHADEMA imemtoa wasiwasi Bw.LEMA kwamba iwapo atakosa nafasi ya Ubunge watampa cheo kama kile cha NAPE, kwahiyo hatakufa njaa hapa mjini.

Wapiga Kura wengi wa Arusha mjini wamefurahishwa na habari hizi kwani wengi wao wamechoshwa na vituko vya Mh.LEMA na sasa wanataka maendeleo.

wew jamaa utakua na mental blindness kwa kutunga uongo mwepesi kama mtu mwenye elimu ya kaptula!!!!lini umekua msemaji wa chadema?
 
Wanajamvi! Amani idumu Tanzania!


Hizi ni habari zenye uhakika 100% nilizozipata kutoka ndani ya CHADEMA na zikathibitishwa na mmoja wa viongozi wakuu hapa mkoani.

CHADEMA kupitia mwenyekiti wao wameongea na Mbunge wa Arusha mjini Bw Godbless J Lema na kumuomba asigombee tena ubunge wa jimbo la Arusha mjini kupitia chama hicho.

Habari zaidi zinasema, CHADEMA wamefikia hatua hiyo baada ya kugundua kuwa wakazi wa Arusha mjini hawana tena Imani na Bw.Lema baada ya LEMA kushindwa kutimiza karibia asilimia 98 ya ahadi zake kwa wana Arusha, Kwahiyo kama angegombea angeshindwa vibaya na hivyo kuwa ni aibu kwa chama hicho, ukichukulia kuwa wameshatangaza kuwa Arusha mjini ni ngome yao.

Suala lingine lililosababisha CHADEMA kumuondoa LEMA ni hili la wanachama wengi wa CHADEMA ambao nao ni viongozi katika ngazi za chini kuonyesha wazi kupingana na uongozi wa Mbunge huyu! Kwa mfano kijana wa CHADEMA siku nyingi Bw.Noel Ole Veroya kutangaza Nia ya kumn'goa LEMA Arusha. Hali hii imechangiwa kwa kiasi kikubwa na siasa za fujo alizosiasisi Ndg.Lema.

Suala la Ukabila nalo Limechukua nafasi yake, kwani Bw.Noel ametajwa kuwa ni mzawa wa Arusha huku Godbless LEMA akishawishiwa akagombee Jimbo la HAI(Nyumbani kwao) kwani Mbowe anatarajiwa kuhamia jimbo la Moshi mjini.

Pia CHADEMA imemtoa wasiwasi Bw.LEMA kwamba iwapo atakosa nafasi ya Ubunge watampa cheo kama kile cha NAPE, kwahiyo hatakufa njaa hapa mjini.

Wapiga Kura wengi wa Arusha mjini wamefurahishwa na habari hizi kwani wengi wao wamechoshwa na vituko vya Mh.LEMA na sasa wanataka maendeleo.

[h=2] Maswali 7 Ya Godbless Lema Kwa Polisi-Mauaji ya Mtuhumiwa wa Mabomu Arusha[/h]


1.Tobo la risasi katika hiyo picha Linaonekana tumboni. Je hapo ndipo lilipo ---- la kulia? kwanini wadanganje..?? what are they hiding?.

2.Nani mwenye uwezo wa kuthibitisha makosa ya mtuhumiwa na kukiri kwake kuhusika namatukio ya ugaidi?.

3. Hivi mtu anayekimbia anapigwaje risasi ya tumbo? Alikua anakimbia kinyumenyume au? Maana kama kweli alikua anakimbia angepigwa risasi kwa nyuma kwa maana ya mgongoni si tumboni.

4. Hivi unaweza kumkamata mtuhumiwa wa kulipua mabomu tena anayejua kucheza "karate na judo"halafu umsafirishe bila kumfunga pingu?.

5.Kwa jinsi ambavyo nguvu kubwa ilitumika na Polisi wenyewe na hata Serikali nachama tawala kupotosha juu ya tukio lile la milipuko kwenye mkutano wa CHADEMA Arusha, na kwa jinsi ambavyo Rais Kikwete aligomea wito wa Chadema na makundi mbalimbali ya kijamii wa kumtaka aunde tume ya kijaji (Judiciary commission) kuchunguza mauaji yale, kwa nini tuwaamini polisi kuhusu taarifa namaelezo yao kuwa mtuhumiwa alitoroka akiwa chini ya ulinzi kisha akauawa?.

6. Tukumbuke kuanzia mwanzo jeshi la Polisi na hata Rais hawakuonyesha nia njema katika hili leo hii tuwaamini walikuwa wana nia njema ya kumfikisha mtuhumiwa kwenye mikono ya sheria?.

7. Kifo cha mtuhumiwa katika"Mazingira tata" mikononi mwa watuhumiwa wengine (Maana hata polisi walituhumiwa kuhusika) lazima kitaacha maswali mengi bila majibuTunahitaji jeshi linalotoa huduma (PoliceService). nitakuwa wa mwisho kuamini tukio hili....... (Godbless Lema).

 
JELA NI MAHALI PA KUISHI KAMA SABABU YA KWENDA HUKO NI VITA DHIDI YA UONEVU, UKANDAMIZAJI WA HAKI NA UTU WA BINADAMU.
412052743.jpg
Wapendwa wapiga kura wangu na Watanzania wenzangu. Sina wakati mgumu kuchukua maamuzi haya yanayotokea leo. Upendo huu nilio nao kwa watu wa Arusha na nchi yangu ni sababu ya msingi ya maamuzi haya. Nimetishwa mara nyingi, rafiki zangu wametishwa, jamii ya watu duni imeendelea kuishi kwa mashaka na matisho kwa muda mrefu.

Katika mazingira haya, nikawaza sana kuwa anatakiwa kutokea mtu mmoja jasiri atakayeweza kuona thamani ya watu wengine. Huyo mtu anaweza kuwa wewe lakini kwa wakati huu siwezi kumsubiri tena na nimechagua kuwa mimi nikiamini kuwa utanikuta nikiendelea na safari ya ukombozi.

Tupo wengi sana tunaotaka mabadiliko, haki na ukweli. Hata hivyo hofu, woga na mashaka yamepoteza thamani yetu yote ya maana ya kuishi.

Waliofungwa kwa kuonewa na kuteswa, waliokosa chakula na kulala nje, waliokwenda hospitali na kukosa madawa, waliokosa ajira na kipato mpaka kujikuta wametoroka familia zao, waliopoteza matumaini ya maisha, waliopora utajiri wa nchi yetu kwa manufaa yao binafsi, walionunua haki na sheria dhidi ya wajane na wanyonge na kuwapora vipato vyao vidogo na mashamba yao, USIULIZE SABABU NINI!

Nimetafakari sana na nikatambua kuwa sababu ni mimi pale nilipokuwa kimya wakati wajane na wanyonge wanaonewa.

NIliposikia wengine wanaandamana kupinga uovu, uonevu, wizi, ufisadi na ukandamizaji wa haki nikasema ni hao na wala sio mimi, kumbe nilipaswa kuwa mbele katika harakati hizi.

Nilipoona wenzangu hawawezi kupata matibabu nikasema mimi sio mgonjwa, nilipopata taarifa za rafiki zangu kufungwa kwa makosa yasiyo yao, nilipoona watoto wa mitaani wanaomba chakula, nilipoona wazee
wamepoteza matumaini ya kuishi katika uzee wao, nilipoona vijana hawana ajira, nilipoona mabinti wasichana wadogo wameamua kufanya biashara ya ukahaba, NIKATAFAKARI,TENA NIKATAFAKARI, dhahabu zetu, almasi yetu, Milima na mabonde yetu, Tanzaninte yetu, samaki wetu, Uranium yetu, makaa ya mawe yetu, utalii wetu, ardhi na kilimo chetu na zaidi utu na mahusiano yetu.

Na sasa siwezi kukaa kimya tena. NI afadhali vita inayotafuta haki na usawa kuliko amani inayopumbaza na kudhalilisha utu wa mwanadamu. Na katika msingi huu hofu na mashaka vimekosa thamani kwangu, sitamwogopa mtu yoyote, mwenye silaha yoyote, mwenye cheo chochote na wala sitaogopa jela yoyote katika kupigania haki, utu wa kweli katika jamii yangu.

Wanafikiri wataendelea kutuogopesha kwa sababu wana jela na silaha, wanafikiri tutaendelea kuabudu uoga, wanafikiri wataendela kutunyanyasabila sababu ya msingi LAKINI SISI TUNAJUA TUTASHINDA KWA SABABU HAKI TUNAYOIPIGANIA NI MAKUSUDI YA MWENYEZI MUNGU.

Leo nitakwenda jela kwa hiari yangu binafsi kwa siku kadhaa na si kwa NIA YA KUJITAFUTIA UTUKUFU WANGU bali ," JELA NI MAHALI PA KUISHI KAMA SABABU YA KWENDA HUKO NI VITA DHIDI YA UONEVU, UKANDAMIZAJI WA HAKI NA UTU WA BINADAMU.

Kila mara nilipotishiwa nikagundua wanaonitishia, wananitishia kwa jela na mauti. Na mimi nikagundua na nikatambua ni afadhali kuishi miaka hamsini jela huku sababu ikiwa ni kupinga uonevu na ukandamizaji kuliko maisha ya woga na anasa yasiyo na kusudi katika kutetea utu na heshima ya mwanadamu mwenzangu.

Wale mlionitishia kunipeleka jela sasa nimetangulia kwa hiari yangu na wale mliobaki msiogope jela endeleeni kupigania ukombozi utakaoleta usawa katika nchi yenu.

Watakaotubeza na kututukana wasameheni kwani wanahitaji ukombozi wa fikra, watakaotupongeza na kutuonea huruma wafundisheni ujasiri na waambieni mapambano bado yanaendelea tunahitaji umoja wao. Nitarudi mapema.

MSIOGOPE, MSIOGOPE, MSIOGOPE, MUNGU YUPO UPANDE WETU.

Hata kama sipo arusha, na si mwenyeji wa Arusha I wish we could have ten people like him, Tanzania yenye Neema Ingepatikana kwa vyovyote vile.........

Let him have long life and lets wait if he is going to behave contrary......


Sasa mtu anayejipeleka Jela ana akili timamu huyo?
 
Wanajamvi! Amani idumu Tanzania!


Hizi ni habari zenye uhakika 100% nilizozipata kutoka ndani ya CHADEMA na zikathibitishwa na mmoja wa viongozi wakuu hapa mkoani.

CHADEMA kupitia mwenyekiti wao wameongea na Mbunge wa Arusha mjini Bw Godbless J Lema na kumuomba asigombee tena ubunge wa jimbo la Arusha mjini kupitia chama hicho.

Habari zaidi zinasema, CHADEMA wamefikia hatua hiyo baada ya kugundua kuwa wakazi wa Arusha mjini hawana tena Imani na Bw.Lema baada ya LEMA kushindwa kutimiza karibia asilimia 98 ya ahadi zake kwa wana Arusha, Kwahiyo kama angegombea angeshindwa vibaya na hivyo kuwa ni aibu kwa chama hicho, ukichukulia kuwa wameshatangaza kuwa Arusha mjini ni ngome yao.

Suala lingine lililosababisha CHADEMA kumuondoa LEMA ni hili la wanachama wengi wa CHADEMA ambao nao ni viongozi katika ngazi za chini kuonyesha wazi kupingana na uongozi wa Mbunge huyu! Kwa mfano kijana wa CHADEMA siku nyingi Bw.Noel Ole Veroya kutangaza Nia ya kumn'goa LEMA Arusha. Hali hii imechangiwa kwa kiasi kikubwa na siasa za fujo alizosiasisi Ndg.Lema.

Suala la Ukabila nalo Limechukua nafasi yake, kwani Bw.Noel ametajwa kuwa ni mzawa wa Arusha huku Godbless LEMA akishawishiwa akagombee Jimbo la HAI(Nyumbani kwao) kwani Mbowe anatarajiwa kuhamia jimbo la Moshi mjini.

Pia CHADEMA imemtoa wasiwasi Bw.LEMA kwamba iwapo atakosa nafasi ya Ubunge watampa cheo kama kile cha NAPE, kwahiyo hatakufa njaa hapa mjini.

Wapiga Kura wengi wa Arusha mjini wamefurahishwa na habari hizi kwani wengi wao wamechoshwa na vituko vya Mh.LEMA na sasa wanataka maendeleo.

[h=1]SERIKALI KANDAMIZI HUSABABISHA UASI NDANI YA NCHI - Waraka wa Godbless Lema[/h]
[h=5]Na: SeriaJr on Wednesday, December 12, 2012 / maoni : 1[/h]
[h=6]
Nimetazama habari za vyombo za habari leo asubuhi na kutafakari nafikiri napaswa kuweka kumbukumbu vyema na sahihi bila kumumunya maneno hata kidogo.
[/h][h=6]Nimekuwa Bunda na Musoma katika ujenzi wa Chama na jana tarehe 10/12/2012 nilifanya mkutano Arusha Mjini wenye ujumbe unaofanana na nilioutoa Bunda na Musoma na ambao nitaupeleka Nchi nzima kuanzia January bila kupumzika wala kuchoka mimi na makamanda wengine ambao sasa tumeamua ni " DIE or LIVE .[/h][h=6]Nimeamua kusema na nitaendelea kusema popote nitakupokuwa kuwa " Ni afadhali vita inayotafuta haki na usawa kuliko amani inayopumbaza na kudhalilisha utu wa Mwanadamu , nilipokuwa Musoma na Bunda niliwaambia Wananchi hao kuwa wakati wakuendelea sisi Watanzania kuwa wajinga umekwisha na lazima tuhufikishe mwisho.[/h][h=6]Maisha yameendelea kuwa Magumu sana kila siku , hakuna haki wa usawa katika mambo muhimu ya maisha , wezi wakubwa wanaohujumu pesa za umma wanaendelea kuwa na neema kubwa na ya kupindukia huku watu katika Taifa hili wanaendelea kuwa Masikini wakupindukia na kuishi maisha ya aibu kubwa katika jamii huku dada zetu wakiishia kuuza miili yao na marafiki zetu wakiishia jela kwa udokozi unaotafuta kushinda njaa zao tu za kila siku.[/h][h=6]Ni mpaka lini tutaendelea kukaa kimya tunaposikia wezi na wabadhirifu wa mali ya Umma wameibia na kuipotezea Taifa bilioni elfu tisa ( 9000,000,000,000) wakipewa adhabu ya kujiuzulu uwaziri na huku mwizi wa simu Manzese anafungwa miaka kumi jela ? huko wapi usawa na Amani katika Taifa hili ?[/h][h=6]Hivi karibuni tumesikia kutoka Bungeni pesa nyingine nyingi zimefichwa huko New Jersey , Dubai , Uswisi na kwingine kwingi na haya ni mabilioni ya Walipa kodi wa Watanzania na Wabunge wanasema wawajua lakini hawawezi kuwataja , hiki ni kichekesho kwani kutaja mwizi na kwenyewe kunataka itifaki ? na sisi tunapata huzuni eti wanaposwa kusimamia sheria na utawala wa Serikali wanahitaji itifaki kuwataja Majambazi na Majangili wanaoendelea kuangamiza maisha ya Nchi yetu na mimi niombe Nipewe hayo majina ninajua kwa sasa sina kinga ya Bunge lakini nitawataja bila kumuogopa Mtu yeyote wa cheo chochote.[/h][h=6]Ushauri wangu kwa wabunge wa vyama vyote sio kila jambo unahitaji mwongozo wa Spika wakati mwingine unahitaji mwongozo wa haki na ukweli hata kama Spika hataki , hatuwezi kusema eti Spika hakunipa nafasi ikawa ni sababu ya kuficha majambazi na majangili wa pesa zetu , kuvunja utaratibu au sheria kwa kupigania haki na ukweli ni jambo linalokubalika Mbinguni na Duniani , kama Mwl Nyerere , ,Nelson Mandela na Martin Luther Jr walipovunja sheria za wakandamizaji ili kupigania uhuru wa msingi na haki za watu wao.[/h][h=6]CCM na Serikali yake Dhaifu wamekuwa wakifanya mzaha na amani ya Nchi yetu kwa kuendelea kupuuza utawala bora katika Taifa letu , dharau wanayoonyesha kwa Watanzania ni kubwa sana , na msaada wao katika kutekeleza mambo machafu ya ufisadi unatokana na namana walivyoweza kuthibiti vyombo vya usalama, sasa swali je tutaendelea kuona Nchi inaporwa na kuishia eti kwa sababu CCM na serikali yake wanaongoza polisi na Majeshi ? Mimi siwezi kuishi nyakati hizi nikitazama mambo haya Nelsom Mandela alisema "Serikali au utawala unapotumia mabavu kumkandamiza mtu mnyonge kimsingi haimfundishi mtu huyo kuwa dhaifu bali humfundisha mtu huyo kutafuta njia za kujitetea dhidi ya uonevu "[/h][h=6]Nchi yetu ilipoingia vitani na Uganda mwaka 1978 , Nyerere alisema " tunakwenda kumpiga Idd Amin , kwani Sababu tunazo , Nia Tunayo na Uwezo tunao .
Sababu ya vita ilikuwa ni kupinga uvamizi wa Nduli Idd Amin na nia ilikuwa ni kutetea dhamira njema na masilahi ya wananchi ,rasilimali na mipaka ya Nchi yetu hivyo basi hata kama hatukuwa na uwezo ilitupasa kutafuta uwezo ili kutetea Nchi yetu na watu wetu.
[/h][h=6]Kuna uchaguzi mwaka 2015 na haya nimesema Musoma na sasa naandika kama kumbukumbu muhimu ambayo niko radhi kwenda nayo popote hata kunyongwa, Watanzania watachagua Rais , Wabunge na Madiwani tunataka uchaguzi huru na wa haki Chadema au Chama chochote cha siasa kikishinda kwa haki kitangazwe mara moja kuwa mshindi , lakini jaribio lolote lakutaka kupindisha haki katika uchaguzi linaleta moja kwa moja tafsiri kuwa uchaguzi wa kura hauwezi kuleta mfumo mpya wa utawala Tanzania na mimi ndipo najiuliza sasa unataka tukiibiwa kura kwa nguvu sisi tufanyeje ? twende Bar tukacheze Darts ? Mabadiliko katika Taifa letu sio ombi ni lazima na kama tutakuwa na sababu , na nia , basi uwezo wa kupigania uhuru wa pili kati Taifa letu kwanini tusitafute ? Maisha ya Watanzania lazima yabadilike ,. Rasilimali lazima zitumike kwa manufaa ya wote na sio viongozi na familia zao ,naniliposema Tanzania isipokuwa makini watazaliwa M23 wengine kwani siku zote vikundi vya waasi vinazaliwa na Serikali na utawala Kandamizi.[/h][h=6]January Makamba alisema " Upinzani kamwe usitarajie kamwe kuwa kuna siku watapewa Nchi hii kuongoza " Na mimi ni mjibu hii Nchi sio ya baba yake , hii Nchi ni mali ya Watanzania wote na yeyote atakayeshinda uchaguzi kwa haki na kweli ataongoza Nchi na wakifikiri wanaweza kupora ushindi kwa nguvu basi watu wema pia watakuwa na sababu na nia ya kutafuta haki ambayo kimsingi huwa aiombwi .[/h][h=6]Ni lazima sana tunapoelekea kwenye uchaguzi Mkuu watawala wajue vita na ghasia mara zote zinasababishwa na mfumo mbaya wa utawala na kwa hali ya maisha ilivyo kinachoifanya Tanzania kuwa na utulivu sio sera nzuri za CCM kama Chama Tawala bali ni uungwana wa Watanzania ambao na hakika wamekaribia kuchoka na ni hatari kubwa mtu mpole akichoka na kusema sasa basi.[/h][h=6]Kwa hiyo katika kipindi hiki tunachoangahika kutafuta usawa katika mambo ya msingi katika jamii , Maneno yetu kwa Watanzania ni kuwafundisha ujasiri na utiyari wa kuokoa Nchi yao ambayo imekwishateketezwa na kikundi cha wahuni wachache ambao hawaoni Aibu kuiba wala kuua kila siku . Tukatae kwa nguvu zote kuburuzwa . kuonewa , na Taifa letu kuibiwa kila kitu na ukitazama Sekretarieti Mpya ya CCM utaona mafisadi wa zamani wenye uzoefu tofauti wa wizi wamerudi tena katika madaraka ya Chama Tawala[/h][h=6]Kila mtu anawajibu wa kukekemea uozo katika Taifa letu na kupinga vikali kikundi cha uasi kilichoko Tanzania kinachoitwa CCM kwani kazi yake ni kuiba , kupora , kutaifisha na kuua .[/h][h=6]Hivyo basi ujasiri ni kipimo sahihi , tusirudi Nyuma , tusonge mbele kila mtu kwa nafasi yake na uwezo wake katika kunusuru Taifa hili.[/h][h=6]Mwisho nimesikia pia propaganda nyingine nyingi kuhusu mimi zimesomwa kwenye magazeti ya kufungia vitumbua , kwa sasa sina muda wa upuuzi huo kwani wakati na ukimya mara nyingi ni nguvu kubwa katika kujibu habari za kidaku na umbeya .[/h][h=6]"Ni kheri Mwanadamu akaishi miaka michache duniani jina lake likabaki linaishi kwa haki na wema kuliko miaka mingi na ukatoweka kama mzoga " STEVEN BIKO[/h][h=6]GODBLESS J LEMA[/h]11 Disemba 2012


 
Kwa arusha hata kama tukipata jiwe la cdm tutalipigia kura. Huyu bwana Allan anaacha kusemeya ya ccm anakimbilia ya chadema, hahaha, wameishiwa na sera. Kwa hiyo ccm mmekata tamaa kabisa na arusha??????????? !!!!!!!!!!!
 
mbona unamuogopa sana lema?kipigo alichokupiga 2010 kilikuwa kipigo kitakatifu,na ndicho hichohicho atakupa mwezi wa kumi
 
Back
Top Bottom