CHADEMA kuikabili Sheria ya kulinda mashahidi

CHADEMA kuikabili Sheria ya kulinda mashahidi

Elias Msuya

Senior Member
Joined
Dec 23, 2011
Posts
173
Reaction score
671
Baada ya Mahakama Kuu ya Masijala ya Dar es Salaam kukubali ombi la upande wa Jamhuri la kuficha majina na taarifa nyingine za mashahidi raia wa upande wa Mashitaka katika kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, chama hicho kimesema kinaipinga Sheria hiyo ya iliyopitishwa kama Mabadiliko ya Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Namba 2 ya 2018.

Agosti 4, 2025, Jaji Hussein Mtembwa alisema kutokana na uzito wa kosa la uhaini na hofu ya mashahidi kutishiwa, ni haki kwa mashahidi raia kulindwa kwa kutotajwa majina yao, anuani wala mahali walipo katika hatua ya committal, Preliminary Inquiry (PI) na hata wakati wa kusikilizwa kwa kesi hiyo.

Hata hivyo, Kaimu Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, Dk Rugemeleza Nshala amesema leo Agosti 6 kuwa sharia hiyo japo ilipitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano, haikufuata utaratibu wa kutumika.

“Bunge lilipitisha ila liliitaka Serikali kuweka utarratibu wa kuitumia, lakini haikufanya hivyo. Tumefuatilia na tumegundua kuwa sheria hiyo haikutangazwa kwenye gazeti la Serikali jambo ambalo ni kinyume cha Katiba na tumegundua kuna wafungwa 27 wamehukumiwa kunyongwa kwa sharia hiyo,” amedai Dk Nshala.

Lissu anatarajia kufikishwa tena mahakamani Agosti 13, ambapo anatarajiwa kusomewa mashitaka yake (comital) ili ahamishiwe mahakama kuu kusikiliza kesi hiyo ya uhaini.



“Bado hatujachelewa, tutamweleza jaji haya mambo yote, mambo ndiyo yameanza,” amesema Dk Nshala.
 
Baada ya Mahakama Kuu ya Masijala ya Dar es Salaam kukubali ombi la upande wa Jamhuri la kuficha majina na taarifa nyingine za mashahidi raia wa upande wa Mashitaka katika kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, chama hicho kimesema kinaipinga Sheria hiyo ya iliyopitishwa kama Mabadiliko ya Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Namba 2 ya 2018.

Agosti 4, 2025, Jaji Hussein Mtembwa alisema kutokana na uzito wa kosa la uhaini na hofu ya mashahidi kutishiwa, ni haki kwa mashahidi raia kulindwa kwa kutotajwa majina yao, anuani wala mahali walipo katika hatua ya committal, Preliminary Inquiry (PI) na hata wakati wa kusikilizwa kwa kesi hiyo.

Hata hivyo, Kaimu Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, Dk Rugemeleza Nshala amesema leo Agosti 6 kuwa sharia hiyo japo ilipitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano, haikufuata utaratibu wa kutumika.

“Bunge lilipitisha ila liliitaka Serikali kuweka utarratibu wa kuitumia, lakini haikufanya hivyo. Tumefuatilia na tumegundua kuwa sheria hiyo haikutangazwa kwenye gazeti la Serikali jambo ambalo ni kinyume cha Katiba na tumegundua kuna wafungwa 27 wamehukumiwa kunyongwa kwa sharia hiyo,” amedai Dk Nshala.

Lissu anatarajia kufikishwa tena mahakamani Agosti 13, ambapo anatarajiwa kusomewa mashitaka yake (comital) ili ahamishiwe mahakama kuu kusikiliza kesi hiyo ya uhaini.



“Bado hatujachelewa, tutamweleza jaji haya mambo yote, mambo ndiyo yameanza,” amesema Dk Nshala.
maskini chadema, dah!

hadi huruma 🐒
 
Aisee Kwaio Ukishitakiwa Kwa Sheria Hii Ya Kuficha Mashahidi Ni Hakuna Kupona ? Dah
Kwaheri Jemedari Lissu.
Ccm Wamekupenda Zaidi.
 
Kwa mahakama hizi za Rostam wasahau kupata haki, hapa dawa ni kutafuta waganga wa kienyeji wawashughulikie hawa wapumbavu.
 
Freeman Mbowe hapo roho yake kwatuuuuu, anajua Lissu anaenda kunyongwa ili arudi kuwa mwenyekiti tena Chadema
1000046826.jpg
 
Kwa mahakama hizi za Rostam wasahau kupata haki, hapa dawa ni kutafuta waganga wa kienyeji wawashughulikie hawa wapumbavu.
Waganga wa nini mkuu? Unaweza kukuta mganga ana kadi ya CCM kama walivyo jaa kule Gamboshi. Hapa ni kuwaibua kina "Traoure" wa bongo ambao ninao uhakika wapo na kuwauliza jee hiyo dozi ya "ubumbuwazi" waluonyweshwa haijawaisha mwilini?
Wakiamua kuchukua, baada ya miezi sita watakuwa wamewafyeka mafisadi wote, katiba mpya (ya Warioba inarekebishwa kidogo) inawekwa na uchaguzi huru na wa kweli unafanyika.
Au unaonaje?
 
Waganga wa nini mkuu? Unaweza kukuta mganga ana kadi ya CCM kama walivyo jaa kule Gamboshi. Hapa ni kuwaibua kina "Traoure" wa bongo ambao ninao uhakika wapo na kuwauliza jee hiyo dozi ya "ubumbuwazi" waluonyweshwa haijawaisha mwilini?
Wakiamua kuchukua, baada ya miezi sita watakuwa wamewafyeka mafisadi wote, katiba mpya (ya Warioba inarekebishwa kidogo) inawekwa na uchaguzi huru na wa kweli unafanyika.
Au unaonaje?
Jeshi limejaa makada tupu
 
Baada ya Mahakama Kuu ya Masijala ya Dar es Salaam kukubali ombi la upande wa Jamhuri la kuficha majina na taarifa nyingine za mashahidi raia wa upande wa Mashitaka katika kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, chama hicho kimesema kinaipinga Sheria hiyo ya iliyopitishwa kama Mabadiliko ya Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Namba 2 ya 2018.

Agosti 4, 2025, Jaji Hussein Mtembwa alisema kutokana na uzito wa kosa la uhaini na hofu ya mashahidi kutishiwa, ni haki kwa mashahidi raia kulindwa kwa kutotajwa majina yao, anuani wala mahali walipo katika hatua ya committal, Preliminary Inquiry (PI) na hata wakati wa kusikilizwa kwa kesi hiyo.

Hata hivyo, Kaimu Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, Dk Rugemeleza Nshala amesema leo Agosti 6 kuwa sharia hiyo japo ilipitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano, haikufuata utaratibu wa kutumika.

“Bunge lilipitisha ila liliitaka Serikali kuweka utarratibu wa kuitumia, lakini haikufanya hivyo. Tumefuatilia na tumegundua kuwa sheria hiyo haikutangazwa kwenye gazeti la Serikali jambo ambalo ni kinyume cha Katiba na tumegundua kuna wafungwa 27 wamehukumiwa kunyongwa kwa sharia hiyo,” amedai Dk Nshala.

Lissu anatarajia kufikishwa tena mahakamani Agosti 13, ambapo anatarajiwa kusomewa mashitaka yake (comital) ili ahamishiwe mahakama kuu kusikiliza kesi hiyo ya uhaini.



“Bado hatujachelewa, tutamweleza jaji haya mambo yote, mambo ndiyo yameanza,” amesema Dk Nshala.
Mnamdanganya mwenzenu, mnajua kabisa Lissu kesi hii hatoboi!! Alidhani ana watu wa kumsaidia kujifanya jeuri, eti analeta dharau, na kujifanya kutegemea wazungu, haya sasa, kiko wapi!! Wamfyekelee mbali huko!
 
Back
Top Bottom