Mtumiabusara
JF-Expert Member
- Nov 18, 2009
- 473
- 40
Ndugu wasomaji,
Tumeshuhudia jinsi nchi yetu ilivyokumbwa na vurugu za kisiasa jijini Arusha. Katika vurugu hizo damu ilimwagika. Ni wakati wa masikitiko makubwa kwa nchi yetu na vilevile ni wakati wa tafakuri na mafunzo muhimu. Je, ni nini kilichopelekea vurugu na kumwagika kwa damu?
Kimsingi mgogoro wa kisiasa ulisafirishwa kwenda Arusha. Chanzo chake ni halmashauri ya Hai. Katika halmashauri hiyo CHADEMA kiliwaorodhesha Mh. Lucy Owenya(MB) na Mh. Grace Kihwelu (MB) kuwa wapiga kura katika uchaguzi wa mwenyekiti wa halashauri hiyo. Kuorodheshwa kwao kulikipa CHADEMA nafasi kubwa ya kuweza kushinda uchaguzi huo. Tukumbushane tu, kuwa mwenyekiti wa CHADEMA Mh. Freeman Mbowe (MB) ni mjumbe katika halmashauri hiyo ya Hai. Kwa kutokuelewa sheria ipasavyo wajumbe kutoka CCM walipinga ushiriki wa wabunge hao wa CHADEMA katika uchaguzi wa mwenyekiti wa halmashauri. Hata hivyo wabunge hao wa CHADEMA waliruhusiwa kupiga kura na kumpa ushindi mgombea toka chama hicho. Hivi sasa halmashauri ya Hai inaongozwa na CHADEMA.
Tujifunze katika hili kuwa mwenyekiti wa CHADEMA anatambua kuwa wabunge wa viti maalum wanaweza kusajiliwa katika halmashauri fulani na kukipa chama chao "advantage" katika maamuzi yatakayofanywa katika vikao vya halmashauri hiyo. Katika kufahamu hili ndipo mwenyekiti huyu akawachukua wabunge wake hao wawili ili waweze kushinda uchaguzi. Pingamizi kutoka CCM kisheria halikuwa na nguvu yoyote.
Je, CHADEMA walifanya nini baada ya kukutana na changamoto huko Hai?
Walichokifanya CHADEMA ni kupinga uamuzi wa mkurugenzi wa halmashauri ya jiji la Arusha wa kumruhusu Mh. Mary Chatanda (MB) toka CCM kushiriki katika uchaguzi wa meya wa jiji la Arusha. Kigezo walichokitoa ni kwamba swala hilo si sahihi kisheria.
Tujiulize;
iwapo swala hilo si sahihi kisheria, ni kwanini Mh. Freeman Mbowe (MB) aliwasajiri Mh. Lucy Owenya(MB) na Mh. Grace Kihwelu (MB) toka CHADEMA kwenye uchaguzi wa Hai?
Je Mh. Freeman Mbowe (MB) alikuwa anajaribu kuvunja sheria?
Kwa vile waliopinga ushiriki wa wajumbe hao toka CHADEMA huko Hai ni wajumbe toka CCM, je CHADEMA inawatumia wajumbe wa CCM kuwajulisha sheria ya nchi inaruhusu vitu gani?
Iwapo CHADEMA hawajaridhishwa na maamuzi ya mkurugenzi wa Hai, je, ni sahihi kukataa maamuzi halali ya mkurugenzi wa jiji la Arusha kama majibu kwa mkurugenzi wa Hai?
Kwanini CHADEMA hawakuandamana Hai?
Kimsingi, maamuzi ya mkurugenzi wa jiji la Arusha ni maamuzi sahihi. Na wale wote waliowakatalia Mh. Lucy Owenya(MB) na Mh. Grace Kihwelu (MB) kushiriki uchaguzi wa mwenyekiti wa halmashauri huko Hai hawakuwa sahihi - na kwa vitendo, mwenyekiti wa CHADEMA amedhihirisha kulitambua hili.
Hili ni swali muhimu, Nakumbuka hoja ya Chadema ni kuwa Mary Chitanda ni mbunge wa mkoa wa Tanga, Je Lucy Owenya na Grace Kihwelu ni wabunge kupitia mkoa gani? ni nje ya Kilimanjaro?